Habari za Punde

Katiba Mpya kumaliza malalamiko ya pande zote za Muungano

Spika  wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar Mhe Pandu Ameir Kificho amesema  zowezi linaoendelea la  ukusanyaji wa maoni kuhusiana na Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  linalenga kupata Muungano mzuri zaidi  utakaomaliza  malalamiko ya pande zote za Muungano huo.
Spika Kificho amesema hayo leo wakati akizungumza na Balozi wa Canada hapa nchini Bw. Alexandre Leveque huko  Ofisini kwake Chukwani  nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
Amesema  zowezi hilo linaendelea vizuri  ambapo wananchi na makundi mbali mbali  yanaendelea kutoa maoni yao  kuhusiana na Katiba Mpya  pamoja na mwelekeo wa Muunndo wa Muungano wanautarajia  ambao wanahisi utaleta maslahi zaidi kati ya Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.

Amesema  Muungano wa Tanzania ni wa pekee ambao unahitaji  kutunzwa na kuendelezwa  ingawa wananchi wamekuwa na mawazo tofauti juu ya mfumo wanaouhitaji .
 Mhe Kificho amesema katika  kuudumisha Muungano huo ni vyema    kuyapatia ufumbuzi malalamiko ya kila upande  ikiwa ni pamoja na kufahamika vyema mambo ya muungano na yale yasiyokuwa ya Muungano.
Amefahamisha kwamba zowezi la uchukuaji wa maoni ni muhimu  kwa wananchi na kutokana na umuhimu  huo Baraza la Wawakilishi la Zanzibar chini ya ufadhili wa Serikali ya Norway  limechukua  juhudi ya kutoa elimu ya katiba pamoja na kutayarisha kitabu maalum cha Elimu ya Katiba ili  kuwapamwangaza wananchi hao kuhusiana na Katiba yao.
Kwa  upande wake Balozi  Alexandre  Leveque amesema  mpango wa kukusanya maoni ya wananchi wakati wa kuunda katiba ni jambo zuri lenye kuonyesha kukomaa kwa demokrasia hapa nchini.
Amesema  nchi yake inatarajia kuona Watanzania wanapata katiba yenye mafanikio ambapo Canada itafuatilia kwa karibu mwenendo wa mchakato wa Upatikanaji wa katiba mpya na nchi hiyo itatoa kila aina ya ushirikiano  ili kuhakikisha kwamba zowezi hilo linafanikiwa.

5 comments:

  1. Uzuri wa Muungano na ubaya wa Muungano wanaujuwa Wananchi wenyewe, ikiwa Upande moja unahisi hauna benefit kwao Basi viongozi wanyamaze kimya wananchi ndio sauti ya mwicho sio kuonekana mbumbubu wasio fahamu shida na raha.

    Kificho yeye ni mtumichi tu wa wananchi sio Master wa kuwa lazimisha Muungano.

    Kwake una Benefit alikwisha zitaja kuwa kaekeza vitega uchumi Tanganyika na kuwa na majumba , ndio akaulazimisha uweko kwa Maslahi yake sio ya wazanzibar walio wengi ndani ya Zanzibar yenyewe.

    ReplyDelete
  2. wewe mwandishi hii nchi yetu inaitwa zanzibar wala sio tanzania zanzibar. kificho wewe unafaidika lakini raia wa kawaida wanateseka. ukifika wakati wa kuamua watatoa msimamo wao kuhusu nchi yao.

    ReplyDelete
  3. Kwa anaeijua Zanzibar inavyoendeshwa, hawezi kusema kua inaonewa bali atasema kua inajionea au tunajionea wenyewe.

    Mtu yeyote naesema Zanzibar inaonewa aidha ni mgeni hapa au anajipumbaza.

    ReplyDelete
  4. This comment has been removed by a blog administrator.

    ReplyDelete
  5. sasa unategemea nini kutoka kwa kificho mtu mwenye elimu ya kuunga

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.