Habari za Punde

Ligi Kuu ya Zanzibar Bandari na Mafunzo timu hizo zimetoka sare ya 1-1

MSHAMBULIAJI WA timu ya Mafunzo Jaku Joma akimpita beki wa timu ya Bandari Kassim Hariri, katika mchezo wa ligi Kuu ya Zanzibar uliofanyika katika uwanja wa Amaan, timu hizo zimetoka sare ya manao 1—1
Beki wa timu ya Bandari Mohammed Nassor Moyo, akiokoa mpira golini kwake wakati wa mchezo wa ligi Kuu ya Zanzibar mchezo uliofanyika katika uwanja wa Amaan timu hizo zimetoka sare ya 1-1.



Mchezaji wa timu ya Mafunzo Ali Juma kushoto akimpita mchezaji wa timu ya Bandari Rashid Omar kulia akijaribu kumzuiya wakati wa mchezo wa ligi kuu ya Zanzibar, timu hizo zimetoka sare ya 1--1
Mshambuliaji wa timu ya Bandari Mussa Omar akimpita beki wa timu ya Mafunzo Haji Abdi.
Imekula kwakohiyo ndivyo inavyoonekana kwa mchezaji wa timu ya bandari Samora Masanja( kushoto) huku mchezaji wa timu ya mafunzo Haji Abdi akikata mbuga.


1 comment:

  1. Du! Kweli Soccer la Zenji! linaporomoka kila miaka ikienda. yaani majukwaa meupeee!!! watu hawana hamu hata kwenda mpirani!!! si mchezoo!!!

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.