Na
Masanja Mabula,Pemba
WATU
watatu wamefariki dunia kwenye matukio mawili tofauti yaliyotokea katika Wilaya
ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba likiwemo na watoto wawili kuzama baharini
wakati wakitoka kuchukua kuni katika bahari ya Pondeani Kinowe.
Akithibitisha
kutokea kwa tukio hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Juma
Sadi alisema katika tukio hilo
lililotokea siku ya Jumapili watoto hao wakiwa na wenzao sita waliondoka
nyumbani kwao kwa ajili ya kwenda kuokota kuni wakiwa na chombo aina ya dau.
Aliwataja
waliokufa maji kwenye tukio hilo
kuwa ni Hamad Mwinyi Hamad (10) ambaye tayari amezikwa pamoja na Ali Mwinyi
Hamad (6) ambaye bado hajaonekana na juhudi za kumtafuta zinaendelea.
Aidha
kamanda Sadi amewataja walionusurika kufa kuwa ni Mohammed Hamad Mohammed (10)
, Rashid Juma Rashid (10) Ali Juma Rashid (8)
Rashid Mansour Rajab (10) Suleiman Mwalim Mkongwe (8) pamoja na nahodha wa chombo hicho
Rajab Mansour Rajab (26).
Aidha
aliwataka wazazi kuwa na uangalifu na udhibiti wa watoto wakati wanapotaka
kwenda baharini ikiwa ni kufuatana na watu wazima zaidi ya watatu ili kuweza
kukinga na maafa yanayoweza kuzuilika.
Kwa
upande wake sheha wa Shehia ya Tumbe Mashariki, Seif Omar alisema tayari
kijana Hamad Mwinyi Hamad ameshazikwa na kwa sasa wanendelea kuutafuta
mwili wa Ali Mwinyi Hamad kwa kushirikiana na jeshi la polisi.
"Boti
za wavuvi wa Tumbe , wananchi wa Tumbe
kwa kushirikiana na jeshi la polisi wanaendelea kuutafuta mwili wa Ali
Mwinyi Hamad katika bahari za Tumbe," alieleza .
Na
katika tukio jengine mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 55 mkaazi wa kijiji
cha Chamboni shehia ya Micheweni
anayefahamika kwa jina la Bihaba Omar Juma amefariki dunia baada ya kuangukiwa
na jiwe wakati akiokota mawe kwa ajili ya kutengeza kokoto.
Tukio
hilo limetokea Jumapili majira ya saa tano za asubuhi wakati mwanamke huyo akiwa katika harakati
zake za kujitafutia riziki, na akichukua mawe kwenye machimbo ya mawe huko
Micheweni jiwe kubwa lilimwangukia na kusababisha kifo chake.
Matukio
ya watu kuangukiwa na mawe na kisha kufariki dunia yamekuwa yakitokea mara kwa
mara katika machimbo ya mawe Micheweni na kusababisha vifo vya watu mbali
mbali.
No comments:
Post a Comment