Na Elizabeth John
KIUNGO wa Azam FC, Abdulhalim Humud ‘Gaucho’ amefuzu kucheza soka la kulipwa
katika timu ya Jomo Cosmos FC ya Daraja la Kwanza nchini Afrika Kusini.
Nyota huyo wa zamani wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’, Mtibwa Sugar ya Morogoro
na Simba, amekuwa akikosa namba ya kudumu katika kikosi cha Azam kwa zaidi ya
misimu miwili, kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kuwa majeruhi.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Meneja Msaidizi wa Azam FC, Jemedari
Said, alisema Humud amefanikiwa kufuzu majaribio katika timu hiyo na kilichobaki
ni pande hizo kujadiliana ada ya uhamisho.
“Kwa ufupi Humud amefuzu kila kitu huko Afrika Kusini na muda wowote atarudi
nchini kuja kumalizia taratibu zingine za uhamisho, na tuna imani ataiwakilisha
timu yetu vizuri, pamoja na taifa lote kwa ujumla,” alisema Jemedari.
Akimzungumzia Humud, alisema ni mchezaji mzuri na mwenye kiwango cha juu,
lakini amekuwa akipata wakati mgumu kupata namba mara kwa mara, kutokana na
ushindani mkali uliopo hivi sasa katika timu yao.
Alisema kwa mujibu wa kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Afrika Kusini
‘Bafana Bafana’, Jomo Sono, ambaye pia ndiye mmiliki wa Cosmos walitoa nafasi
hiyo kwa Humud kutokana na kuwa na uhusiano mzuri na Azam na pia kuridhishwa na
kiwango cha kiungo huyo.
Chanzo - Tanzania Daima
No comments:
Post a Comment