Habari za Punde

Risala ya Zanema maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani


Risala ya Jumuiya Ya Waajiri  (ZANEMA) Katika Kuadhimisha

Siku Ya Wafanyakazi Duniani (May Day) Zanzibar

Uwanja wa Amaan Zanzibar

1/05/2013

 

Mh. Mgeni Rasmi, kwa niaba ya Jumuiya Ya Waajiri Zanzibar,(ZANEMA) naomba nitowe shukrani zangu za dhati, kwa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakzi Zanzibar (ZATUC) kwa kutualika katika kuadhimisha siku ya wafanyakazi duniani. Kwetu sisi waajiri, hii ni heshima kubwa na dalili tosha kuwa kuna ushirikiano mkubwa baina ya waajiri na vyama vya wafanyakazi Zanzibar.

Mh. Mgeni Rasmi, Wafanyakazi wa Zanzibar leo wana ujumbe wao unaosema

“Katiba mpya izingantie usawa wa haki na maslah ya wafanyakazi”

 Ni haki yao kudai. Ni haki yao kupata maslah bora. Lakini ni wajibu wao vilevile kufanyakazi kwa ufanisi na tija. Ujumbe wa ZATUC kwa kuitaka katiba izingatie haki na maslah maana yake wanataka majadiliano na mapatano sio nguvu wala mapambano. Hili niwapongeze kwa kuchaguwa njia muafaka wa kutaka madai yao yafikiriwe.

Suala hili la wafanyakazikudai haki zao halikuanza leo, Miaka 124 (1889) iliyopita, kule Marekani , Chicago wafanyakazi walidai haki na maslah lakini njia iliyotumika ilisababisha watu kadhaa kupoteza maisha yao .

Hiyo ni historia, haisahauliki na hatutaki tuirejee. Waajiri wa leo wanaamini kuwa majadiliano sehemu ya kazi ( social diologue) ndio  suluhisho la matatizo sehemu ya kazi.

Shirika la Kazi Duniani limejitahidi sana kuweka misingi na haki sehemu za kazi kwa kupitisha mikataba na maazimio yake. Mikataba miwili muhimu ambayo nchi nyingi duniani zimeridhia ni Mikataba namba 87 na 98 juu ya Haki Ya Kujiunga na Majadiliano“freedom of Association and Collective Bargaining”

Waajiri wanakubaliana na wazo hilo. Hata hivyo katika katiba ya Jamhurri ya Muungano ya Tanzania ibara ya  20 na ile ya Zanzibar ibara ya 20 zote zimetowa fursa kubwa juu ya wafanyakazi kujiunga na kudai maslah mazuri kutokana na kazi zao.

Lakini Mheshimiwa mgeni Rasmi wafanyakazi wasisahau kuwa siku zote haki na maslah bora sehemu ya kazi ni pamoja na wajibu wao wakiwa kazini . Kama tungeruhusiwa waajiri kuongeza neno katika ujumbe wa Vyama vya Wafanyakazi, waaliongeza kitu  Katiba mpya izingantie usawa wa haki , maslah na wajibu wa wafanyakazi.

Kumtaka muajiri aweke maslah bora pahala ambapo hapana uzalishaji wenye tija ni mtihani.

Mh, hayo ni ya wafanyakazi ambao sasa hivi wamo kwenye ajira. Lakini katika kuwasikiliza vilio vya wafanyakazi wenye ajira lazima tuende samamba na kuliangalia kundi jengine. Kuna kundi la   vijana  ambao hawana ajira ambalo linajumuisha

1.  Vijana wanawake kwa wanaume waliomaliza masomo yao, lakini hawana ajira

2.  Vijana wenye ujuzi lakini bado hawajaajiriwa na bahati mbaya  hawajajiajiri kwa matatizo mbali mbali ikiwemo mitaji

3.  Kuna watu tayari wanazo ajira lakini uwezo wao wa kufanyakazi ni mdogo kitaaluma. Uwezekano wa kukusa ajira zao ni mkubwa.

Tatizo hili ni la dunia, tusilidharau hata kidogo. Migogoro mingi inayotokea duniani leo chanzo kikubwa ni vijana kukosa ajira.

Katika mkutano wa 101 uliofanywa kule Geneva mwaka 2012 Shirika la Kazi duniani lilitilia mkazo suala zima la ajira kwa vijana na waajiriri walitakiwa kushirikiana kiamilifu katika kupambana na tatizo  hili. Mambo yafuatayo yalitiliwa mkazo zaidi    

·        Uajiri na sera za uchumi 

·        Uajiri,Elimu, Mafunzo na Ujuzi

·        Ujasiriamali na kuajiajiri wenyewe

·        Sera juu za Soko la ajira

Waajiri tunalitilia mkazo suala hili kwasababu kama suala hili litapata ufumbuzi , waajiri wataweza kuwaajiri wazalendo wengi zaidi jambo ambalo litaondoa gharama za kuchukuwa wafanyakazi, wa baadhi ya fani, nje ya nchi jambo ambalo kwetu ni gharama.

Mheshimiwa tusikatae ukweli , tuna ajira hazina watu na (ujuzi na uwezo wa watu wetu) na wakati huohuo tunawatu hawana ajira (kwa maana ya watu wetu hawana ujuzi) . Hili ni tatizo lazima litafutiwe ufumbuzi.

Mheshimiwa Mgeni rasmi sisi Waajiri tungefurahi sana kuona ajira zote zinachukuliwa na wazalendo lakini tujiulize ni kweli kila ajira inaweza kuchukuliwa na kila mtu bila kuzingatia ujuzi­­ na uwezo?

Waajiri tunajuwa, kuwa sasa muelekeo wa Serikali ni kuanzisha viwanda kama njia moja ya kuongeza pato la nchi na ajira . Tarehe 19 January 2013. Mh Raisi wa Zanzibar ambaye pia ni  mwenyekiti wa Baraza la Biashara Zanzibar ilisisitiza kuwa sasa tunaelekea kwenye viwanda na hatuna mzaha kwa hili.

Ni kweli sasa Zanzibar inataka kuikuza sekta ya Viwanda . lakini pakuanzia ni wapi? Mara nyingi tunahesabu

1.  Kwanini viwanda vilikufa Zanzibar?.

2.  Uongozi, Ujuzi, uzowefu , fedha na vianzio vyake

3.  Mitaji, Zana na vifaa

4.  Hali ya uwekezaji

5.  Umeme, maji,miundo mbinu

6.  Masoko na viwango

7.  leseni na makodi makubwa, nk

Haya ni muhimu sana lakini suala moja bado halijapewa uzito nalo ni muhimu, ni suala zima la Raslimali watu na Ujuzi (Human Capital).

Hatuwezi kuiedeleza sekta yoyote ile kama hatujaamua kwa makusudi kukuza raslimali watu. Serikali na sekta binafsi tushirikiane kuwaendeleza vijana ili waajirike katika sekta hii vyenginenevyo,  tutaendelea kuunda ajira zisizokuwa na watu, wakati tukiwa na watu wasiokuwa na ajira.

Mheshimiwa, Tunaishi katika dunia ambapo kuna mashindano makubwa ya

·        uzalishaji,

·        mitaji,

·        uwekezaji,

·        teknologia na

·        soko la ajira .

Haya yote kwa pamoja yanachangia ajira iweje na maslah ya muajiri pamoja na wafanyakazi. Tunataka watu watakaoweza kupambana na hali hii.

Tumo ndani ya Soko la pamoja la Afrika ya mashariki ambapo 2010 tumeridhia uingiaji wa watu na bidhaa katika nchi zetu.Katika hali hiyo waajiri bado  tunakabiliwa  na  mtihani mkubwa katika ngazi zote,  juu ya nani wamuajiri.

Mheshimiwa kwa kutaka mambo yaende vizuri Waajiri wote wanachangia 5% ya mishahara ya wafanyakazi wote ili kusaidia vijana wetu kupata mafunzo ya amali ili waajirike na kuweza kuingia katika soko la ajira. Lakini sisi waajiri bado tuna maswali mengi.

a.   Kiasi cha fedha zinazokusanywa ni kikubwa mno,kwa kuendeleza vyuo vya amali, lakini waajiri bado hawajaekewa wazi  hadi hii  leo wamechangia kiasi gani.

b.  Hatuja ekewa wazi matumizi ya fedha hizi na mipango ya baadaye.

Kwa kuzingatia hayo na mengineyo Waajiri Tunashauri:

 

1.   Kuangalia upya Uajiri na sera za uchumi.

 

2.  Iko haja ya Uajiri, Elimu, Mafunzo na Ujuzi yawekewe mikakati ya hali juu.

 

3.  Serikali ishirikiane na Waajiri na wadau wengine waipitie mitaala yetu ili iweze kuzalisha vijana kulingana na soko la ajira

 

4.  Serikali kuweka mazingira rafiki kwa waajiri kupunguza msururu na ukubwa usumbufu  wa kodi, bei za umeme, maji, leseni, ushuru nk na kuwa na kituo kimoja cha mambo ya leseni na kodi   (one stop centre) ili Waajiri wapunguziwe usumbufu wa kumjuwa nani ana dhamana gani.

 

5.  Taaluma za ujasiriamali na ujuzi zifanane na mahitaji ya masoko.

 

6.   Serikali ianzishe Viwanda au iwakaribishe wawekazaji  sambamba na  kupanua Kilimo cha kisasa na cha kibiashara ambavyo vitaweza kutowa nafasi za ajira na kukuza uchumi.

 

7.  Iko haja Kwa Wizara zote na taasisi zote za Serikali na Watu Binafsi kwa pamoja kuifanya zanzibar kuwa nikituo kikubwa cha uwekazaji na biashara.  

Kwa mujibu wa takwimu za utafiti juu ya uchumi wa Zanzibar mwaka 2011, waajiri binafsi wameajiri wafanyakazi 15,620 kati ya hao wanaume ni 10,778 na wanawake 4,08423. Huu ni mchango mkubwa wa waajiri kwa nchi yetu.

Mwisho kabisa, naomba nitowe wito kwa wale ambao hawataki kufahamu au pengine hawajui, kuwa waajiri, kushiriki katika mambo yanayohusu, mipango, majadiliano, sera, sheria, maazimio, mikataba na mengineyo yanayohusiana nayo, ya kitaifa na kimataifa kuhusu kazi na ajira ni haki yao si fursa au upendeleo.

 

Ahsanteni kwa kunisikiliza.

 Salahi Salim Salahi

Mkurugenzi Mtendaji

Jumuiya Ya Waajiri Zanzibar

(Zanzibar Employers Association) ZANEMA

Tel. +255 0242236921

Mobile: 0777424797


 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.