Habari za Punde

Hadithi ya leo (13)

 

Mtume Muhammad Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam amesema:

{ أتاني جبريل فقال: يا محمد، عش ما شئت فإنك ميت، وأحبب من شئت فإنك مفارقه، واعمل ما شئت فإنك مجزي به، واعلم أن شرف المؤمن قيامه بالليل، وعزه استغناؤه عن الناس } [رواه الحاكم والبيهقي وحسنه المنذري والألباني].

Alinijia Jibril ‘alayhis Salaam na akasema:

Ewe Muhammad; ‘ishi utakavyo lakini (ujue) utakufa  (na kuwa maiti), mpende umpendae lakini (ujue) utatengana nae, fanya ufanyalo lakini (ujue) utalipwa (kwa matendo yako) na utambue kwamba hadhi ya Muumin ( wa kweli hutambulika) ni kusimama na kuuhuisha usiku na kusali na utukufu wake (hujulikana) pale anapokuwa mbali na watu(akijiepusha na shari zao)

Imepokewa Haakim na Bayhaqiy na Sheikh Albaani amesema ni hasan.

Hadithi nyengine ya Ruwaza wetu na kipenzi chetu inayotuhimiza na kutusisitizia suala zima la kusimama usiku na kusali na kutuonesha hadhi halisi ya aliyemuamini Allaah Subhaanahu Wata’ala kikweli ni kwa kuacha kile anachokipenda ( kustarehe na usingizi au na ahli yake) na kujipinda na kujibidiisha na ibada wakati ambao hakuna mwengine anaemuona zaidi ya Allaah Subhaanahu Wata’ala (Ikhlaasi iliyokamilika)

Mambo ya kuzingatia na kukusaidia kukuwezesha kuuhuisha usiku na kusali Tahajjud

1     Kutokula sana wakati wa kufutari ili mwili uweze kupata nguvu ya kutosha na kutochoka usiku.

2     Kutojishughulisha sana mchana wa Ramadhaan na mambo yasiyokuwa muhimu kuuandaa mwili na Tahajjud ili usichoke.

3     Kupata muda mchana na kujipumzisha kwa kulala (Qayluulah) ili mwili usiwe mchovu wakati wa usiku

4     Kujieepusha na kufanya maasi mchana wa Ramadhaan kwani maasi humzuia mja na kuzifanya ibada nzito

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.