Na
Mwantanga Ame, DODOMA
BAADHI
ya Mawaziri wa Serikali ya Zanzibar, wamefunguka na kuwajia juu baadhi ya wajumbe
wa bunge maalum la katiba, kwa kudai hoja zao hazitikisi kibiriti kwa kuwa
hazina mashiko.
Mawaziri
hao walikuja juu baada ya baadhi ya wajumbe wa bunge hilo, akiwemo Mwakilishi
wa Mji Mkongwe, Ismail Jussa Ladhu,
kudai baadhi ya mawaziri wa serikali ya Zanzibar wamekuwa vigeu geu na wamekuwa
wasaka tonge, kwa kushindwa kuelezea hoja zao kama walivyokuwa wakifanya Zanzibar .
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti mawaziri hao, walisema wanawashangaa wajumbe hao kwa
kuwashushia lawama kwa kudai wako kimnya, huku wao wakisimama na kutoa hoja
zilizojaa matusi.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora, Dk. Mwinyihaji Makame, akitoa
mchango wake, alisema ipo haja kwa wajumbe wa bunge kujiuliza ni kwanini tume
zilizoundwa kabla ya mapendekezo ya rasimu ya sasa, maoni yao yaliokataliwa.
Alisema
wanaotaja mawaziri wa Zanzibar, kwenye mjadala huo hawana hoja na inaonesha
jinsi walivyofilisika kisiasa katika
kutetea hoja zao.
“Mawaziri
walikuwa wakitetea hoja hakuna anaekataa hoja kwani mambo yote waliyazungumza
baada ya kukubalika katika serikali na sio kama wamekaa kimya,” alisema
Mwinyihaji.
Alisema
serikali katika kutetea hilo tayari imefanikiwa kuruhusiwa kukopa, kujiunga na
Umoja wa Mataifa kwa mambo yasiokuwa ya Muungano, kupunguza orodha ya mambo ya muungano kutoka 32 hadi
saba jambo ambalo linajionesha kama kazi waliyoifanya imetoa matunda.
Alisema
inasikitisha kwa baadhi ya wajumbe kuanza kudai kuwa ndani ya miaka 50 hakuna
maendeleo Zanzibar jambo ambalo sio kweli kwani Zanzibar hivi sasa ni
tofauti na miaka 300 ya utawa wa
kikoloni.
Alisema
madhumuni ya wajumbe hao kudai mfumo wa serikali tatu wanataka kupewa kiti Umoja wa Mataifa, kiti cha EAC, Benki Kuu na sarafu yao, mamlaka ya
kuamua sera na uchumi, uraia na kuukataa uraia wa Zanzibar .
Nae
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Vikosi Maalum, Haji Omar
Kheir, alisema anashangaa kuona mawaziri wa Zanzibar wanasakamwa kwa kudaiwa
kuwa wao ni wasaka tonge, na wako mstari wa mbele kuvuruga Muungano huku
wengine wakiwataka wasirudi Zanzibar .
Alisema
vitisho hivyo ni sawa na kutikisa kibiriti ambacho kwao kimejaa na haoni haja
kwa wajumbe wa bunge hilo
kuanza kutishana.
Mohammed
Aboud Mohammed, ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais,
akitoa maelezo yake, alisema katiba ya Zanzibar
haikani utanzania na sio jambo jema kwa wajumbe hao kutoa maeneo ambayo hayana
ukweli.
Alisema
kuna watu waliokuwa wakitoa maoni ambayo yalionekana kukinzana tangu awali na
haitashangaza wajumbe hao kuona wanawashutumu mawaziri.
Nae
mjumbe, Pereira Ame Silima, alisema wazo la kuleta mfumo wa serikali tatu yeye
binafsi hakubaliani nalo kwa vile vigezo vinavyotumika havionekani kama vina mantiki ya kufanyika kwa mabadiliko ya mfumo wa
sasa wa muungano.
Mjumbe
Waride Bakari Jabu, alimuumbua mjumbe mwenzake Chiku Abwao ambae alidai hashangai kumuona apendekeza muungano wa
serikali mbili uvunjike kwa vile yeye ni raia wa Congo .
Aidha
mjumbe Hija Hassan Hija, akitoa mchango wake alisema mfumo wa serikali tatu
ndio utakaosaidia Zanzibar
kupata haki zake.
Felister
Bura, alisema bila ya kuwepo mfumo wa serikali mbili basi watambue Watanzania
watagawana mbao na ni lazima wajumbe wa bunge hilo kujenga mshikamano.
Makame
Mshimba Mbarouk, alisema anashangazwa na Katibu Mkuu wa CUF kutaka serikali
tatu wakati hapo awali alitaka serikali
mbili.
Nae
Faharia Khamis Shomari, alisema dhamira ya serikali ya kumruhusu Jemshid, alikuwa
na dhamira ya kumfanya aje aone maendeleo ya Zanzibar na sio kutawala Wazanzibari kwa
mlango wa nyuma.
Said
Arif alisema sehemu kubwa ya maoni ya katiba yamechafuliwa na wasomi kwani
baadhi yao
wamekuwa wakitoa maoni yanayotofautiana.
Nae
Januari Makamba akitoa maelezo yake, alisema kama
Watanzania wanataka kuvunja Muungano ndani ya mwaka mmoja ama miwili na kuunga
mkono mfumo wa serikali tatu basi watambue hayo ni majanga.
Dk.
Ave Maria Semakafu, alisema fursa iliyopo ya kurudi kwenye katiba itasaidia
wananchi kwani hivi sasa kuna mahitaji makubwa ya kielimu ambayo yamekuwa
yakichangiwa na bajeti ndogo inayotengwa na serikali.
mimi watu wa bara kutetea muungano wa serekali mbili sishangai nashangaa hao wazanzibar wanaotaka serekali mbili
ReplyDeleteMawaziri wa CCM Zanzibar ni vigeugeu, hawawezi kuitetea Zanzibar wanatetea matumbo yao na wakiambiwa kweli hugeuka kuwa wabaguzi
ReplyDeleteMwinyihaji Makame. Unazungumzia mambo ya Mungano kutoka 32 hadi 7. Iwapo hao wapinzani munaowalaumu hawakupiga kelele nyie kwa akili zenu za kuchangiwa dodoma si mungeliona ni sawa tu kama munavyoona ni sawa hili suala la Serikali mbili ambalo ndio jinamizi kuu la mafanikio na maendeleo ya Zanzibar. Musidanganye wazanzibari. Hamuna mpango wowote ni wizi tu.
ReplyDelete