Habari za Punde

Rais Kikwete ahudhuria mkutano wa (EU Africa Summit)

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com press@ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
       P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
                                         
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewasili Brussels,  Ubelgiji leo asubuhi 2 Aprili,2014 kuhudhuria kikao cha siku mbili cha Wakuu wa Nchi wa nchi za Afrika na za Umoja wa Ulaya (EU-Africa Summit).

Kikao  hiki cha siku 2 kitatoa nafasi kwa viongozi hawa kutathmini mafanikio ya uhusiano wao  na  kutafuta njia zingine mpya za kuboresha mahusiano hayo .

Kauli mbiu ya mkutano wa Mwaka huu inasisitiza katika kuwekeza kwa watu,Mafanikio na Amani (Investing in people, prosperity and peace) na baadaye kufanya mazungumzo na  Rais wa Kamisheni wa Nchi  za Ulaya (EU) Bw. Jose Manuel Barosso.

Akiwa Brussels Rais Kikwete anatarajia kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki  Moon na Waziri Mkuu wa Uholanzi Mheshimiwa Mark Rutte.

Rais Kikwete anatarajia kuondoka Brussels mara baada ya Mkutano kumalizika na kurejea Dar es Salaam.

Imetolewa na;

Premi Kibanga
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Brussels, Ubeligiji.
2 Aprili, 2014

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.