Na Hafsa Golo
MBUNGE wa
jimbo la Kwahani, Dk. Hussein Mwinyi, amesema Zanzibar
inakusudia kupeleka mswada bungeni kudai maslai yake kama
mjadala kuhusu katiba mpya utashindikana kuendelea.
Awamu ya pili
ya mjadala kuhusu katiba mpya unatarajiwa kuanza Agosti 5.
Dk. Mwinyi
ambae ni Waziri wa Ulinzi, alisema hayo
katika mahojiano maalum na mwandishi wa habari hizi baada ya kukabidhi vifaa
kwa ajili ya jimbo la Kwahani.
Alisema
mswada huo utazingatia suala la uchumi na maslahi ya Zanzibar ambapo mambo
mbali mbali ya msingi yatawasilishwa,
ikiwemo suala la mafuta na gesi.
Alisema mswada
huo huenda ukapelekwa katika bunge la kawaida mwezi Novemba, lakini iwapo
katika mpya itashindikana.
Juzi Katibu
wa Bunge la Katiba, Yahya Khamis Hamad, alisema mjadala wa katiba hautawezekana
kuendelea bila ya kuwepo wa jumbe kutoka Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA)
ambao wanasusia mjadala huo.
Alisema
hakuna sababu ya msingi ya kukosekana maslahi ya Zanzibar
hasa hata kama katiba ya sasa itaendelea
ikizingatiwa bunge ndio chombo kikuu cha maamuzi ya sheria za nchi.
"Naamini
Zanzibar itakuwa na maslahi mazuri sina wasiwasi hata kama bunge la katiba halikukaa,"alisema.
Akizungumzia
suala la kugombea uongozi alisema hajawa na maamuzi hasa akizingati bado ni
mapema.
No comments:
Post a Comment