Na Himid Choko, BLW
Mkurugenzi
wa Mashtaka Zanzibar Ndugu Ibrahim Mzee Ibrahim
amesema ni kosa la jinai kwa Afisa yeyote wa Umma kutoa majibu ya uongo
kwa kamati za Baraza la Wawakilishi.
Amesema
Kifungu cha 22 cha sheria ya Baraza la
wawakilishi Nambari 4 ya mwaka 2007 inayohusu Kinga, uwezo na Fursa kinakataza mtu kuidanganya kamati ya Baraza la
Wawakilishi na atakaethibitika kwa
makusudi kutenda kosa hilo ataadhibiwa kwa mujibu wa sheria ya Makosa ya
Jinai.
Ndugu
Ibrahim amesema hayo leo wakati akitoa mada inayohusu Wajibu na utekelezaji wa
Kazi za makatibu Kamati huko hoteli ya Coconut
Tree Village, Marumbi Mkoa wa Kusini Unguja.
Amesema
Kamati za Baraza la Wawakilishi
zinauhalali wa Kikatiba na sheria hivyo
si vyema kwa maafisa wa umma kutoa majibu au ushahidi wa uwongo kwa
kamati hizo.
“
Ni haki ya Wajumbe wa kamati kupata taarifa wazitakazo kutoka kwa maaafisa wa
umma (kifungu cha 9 Cha Sheria ) . Maafisa wa Umma hawatakiwi kukataa kutoa
ushahidi , hawatakiwi kukataa kuwasilisha nyaraka kwenye kamati , hawatakiwi
kukataa kuwasilisha taarifa kwenye Sekretarieti
ya Baraza isipokuwa kama Rais ataelekeza vinginevyo kwa maslahi ya
Umma”. Alifafanua Mkurugenzi huyo wa Mashtaka.
Mkurugenzi
huyo wa Mashtaka pia ametanabahishwa kwamba ni kosa la jinai kumtisha, na
kumuadhibu mtu aliyetoa ushahidi kwenye kamati .
Amesema,
pia ni kosa kuidharau kamati kwa kukataa wito wa kutoa ushahidi au kutokuwa na nidhamu na kuzuwia shughuli za
kamati hizo.
Amesema
Kamati za Baraza la wawakilishi zinauwezo
wa kumuita mtu yeyote kuhudhuria kwenye kamati
na kutoa ushahidi ama nyaraka aliyonayo ikihitajika katika kazi zake na kwamba mtu huyo atakuwa na fursa na kinga kama
zile anazokuwanazo shahidi anapotoa ushahidi mahakamani.
Hata
hivyo amesema mtu anaweza kukataa kujibu
maswali anayoulizwa au kuwasilisha nyaraka
zinazohusu mambo binafsi ya mtu huyo ambayo hayataathiri uchunguzi
unaofanywa na Kamati.
Wakati huo huo Mkurugenzi huyo wa mashtaka
amesema ni kosa kwa mjumbe au Afisa wa Baraza kutoa au kupokea rushwa au kufanya vitendi visivyofaa kulingana na
hadhi na itifaki zao.
Wakitoa
uzowefu wao katika kazi za kamati za baraza ,
Wenyeviti wa kamati za Baraza la Wawakilishi wamesema hadhi
ya Baraza inashuka kutokana na tatizo kubwa la utoro na Ucherewaji pamoja
na kukosa uwajibikaji mzuri kwa baadhi
ya wajumbe
suala ambalo mara nyengine huathiri akidi katika vikao vya Baraza na kamati zake.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Fedha , Biashara na Kilimo Mheshimiwa Salmin Awadh
Salmin na Mwenyekiti wa Kamati ya Kusimamamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa
Kitaifa Mheshimiwa Hamza Hassan
Juma wameuomba uongozi wa Ofisi ya Baraza la Wawakilishi kufikiria utaratibu wa malipo ya Wajumbe ili
kudhibiti mahudhurio na utoro katika vikao vya Baraza na kamati zake.
Mapema
akifungua mafunzo hayo Spika wa Baraza la Wawakilishi Mheshimiwa Pandu Kificho
amewataka Makatibu wa Kamati kutoa
huduma kwa usawa na kuwa wastahamilivu
wakielewa kwamba wanawahudumia
wajumbe wenye uzowefu, elimu na misimamo tofauti .
Amewataka
Makatibu hao kuweka kumbu kumbu za Mikutano yao vizuri na kuwashauri vyema wenyeviti wao ili kuhakikisha kwamba kanuni za baraza la
wawakilishi zinafuatwa ili shughuli za
kamati hizo kufanyika kama zilivyokusudiwa.
Kamati
za kudumu za Baraza la wawakilishi hivi sasa zinaendelea na kazi zake za
kawaida tokea tarehe 10/07/2014 hadi tarehe 23/07/ 2014 hapa Unguja na Mkutano ujao wa Baraza
unategemewa kufanyika Oktoba 22
mwaka huu.
No comments:
Post a Comment