Habari za Punde

Serikali kuwalipa wamiliki wa Shamba lililotumika kuwazika wahanga wa Mv Skagit

BAADA ya wamiliki wa shamba lililotumika kuzika watu waliofariki katika ajali ya meli ya Mv.Skagit kulalamika kuporwa shamba lao liliopo Kama, hatimae serikali imesema itawalipa shamba jengine katika eneo la Selemu.
 
Shamba hilo kabla ya kuchukuliwa na serikali lilikuwa limetolewa wakfu na marehemu,Sultan Ahmed Mohamed El –Mugheriy.
 
Maiti za ajali hiyo zililazimika kuzikwa katika shamba hilo baada ya makaburi ya Mwanakwerekwe kujaa huku serikali ikipanga maiti za ajali hiyo kuzikwa eneo moja.
 
Ahadi ya kulipa fidia ilitolewa na Mkurugenzi wa Ardhi katika Wizara ya Ardhi Maji na Nishati January Fusi, alipokuwa akizungumza na gazeti hili ofisini kwakwe Forodhani.
 
Alisema suala la kukubali au kukataa eneo ambalo serikali itafidia litabaki kuwa la wamiliki.
 
Hata hivyo, wamiliki wa shamba hilo walisema bado hawajapewa taarifa ya kufidiwa shamba hilo.
 
Alisema serikali inafahamu na  inaheshimu sheria za Wakfu lakini kutokana na dharura iliyojitokeza isingekuwa na eneo jengine kwa ajili ya kuwazika watu hao.

Aidha alisema kwa kuwa sehemu ya  shamba hilo pia limeshachukuliwa na JKU, isingekuwa busara kwa wamiliki kuendelea kulitumia badala yake ni vyema wakakubali kupokea shamba watakalopewa na serikali.
 
Mmoja wa warithi wa marehemu,Qussay Juma Mugheir, alisema kitendo cha JKU kuvamia shamba lao hakikuwaridhisha kwa sababu hawakujulishwa.
 
Alisema JKU walivamia shamba hilo tokea serikali ya awamu ya tano na uvamizi huo unaendezwa na serikali za wamu awamu zote.
 
“Hali hii imekuwa ikiendelea katika awamu zote ambapo pamoja na kupeleka barua Kamisheni ya Wakfu na mali ya Amana,Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu,i mpaka hivi sasa hakuna majibu yoyote tuliyojibiwa,” alisema.
 
 
Alisema wanakusudia kuifungulia mashtaka serikali kwa kitendo cha kuvamia ardhi yao bila ya ridhaa ya 

1 comment:

  1. Hii habari kaka Othman Mapara mbona haijakamilika? imekatika hapo mwisho, tafadhali kama ipo habari kamili tuwekee

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.