Kutoka kwa Mdau
Katika mechi za mpira wa miguu ambazo bado
nina kumbukumbu yake vizuri tu ni mchezo mkali uliofanyika mwaka 1982 kati ya
KMKM ya Zanzibar na Pan African ya Dar.
Gemu hii ilipigwa katika Uwanja Amaan
mjini Zanzibar katika kugombania ubingwa wa Tanzania wakati
ulee ambapo kulikuwa na ligi ndogo inayojumuisha mshindi wa kwanza na wa pili
wa ligi ya Tanzania Bara na Zanzibar ambao hukutana na kucheza mechi za mzunguko na hatimaye kupata wawakilishi wawili waliotuwakilisha katika kombe la klabu bingwa na kombe la washindi kwa wakati huo.
Ilikuwa ni kipindi pekee ambacho huwa tunabahatika
kuziona timu za bara na Zanzibar zikibadilishana viwanja katika kuwania ubingwa
halisi wa Tanzania. pia kuwaona wachezaji wengi kutoka bara ambao kwa wakati huo tulikuwa tukiwasikia tu kwenye redio na kuwasoma kwenye magazeti. Pia ilikuwa ni changamopto kwa timu za Zanzibar kuwerza kupata upinzani wa aina nyengine wa soka.
Mechi imebaki katika kumbukumbu yangu
kutokana na aina ya kandanda iliyochezwa siku hii na jinsi ya mwenendo wa
mchezo wenyewe.
Timu ya KMKM iliyokuwa chini ya Kocha
Marehemu Mzee Kheri aliamua kuipanga kama hivi ifuatavyo kama kumbukumbu yangu bado ipo sahihi:
Golini Ramadhan Korosheni, Beki wa kulia
ni Abdullah Maulid, Beki wa kushoto alikuwa ni Hassan Mrisho(Zitto) Mabeki wa
kati walikuwa ni Ibrahim Kapenta na Mohammed Rajab Kiungo mkabaji aliekuwa
akijua kukaba hasa alikuwa na Mohammed Kombo ( Msomali) na kiungo mshambuliaji
alikuwa Marehemu Ali Issa (Kapteni) Pembeni alikuwepo Mcha Khamis ( baba yake Khamis
Mcha wa Azam) na upande wa pili alikuwepo Said Hamad, Katikati safu ya
ushambuliaji kulikuwa na Mohammed Kidevu ( Sheha wa Tomondo kwa sasa) na Shaaban
Ramadhan ( Kocha kwa sasa).
Timu ya Pan African ilipangwa hivi, Golini
Juma Pondamali (Mensah), beki wa kulia Mohammed Mkweche, kushoto Jaffar
Abdulrahman, mabeki wa katikati walikuwa Jella Mtagwa na Leonard Tenga kiungo
alikuwa Mohammed Adolf Rishard na Kassim
Manara ila safu ya ushambuliaji ilikuwa
ni Godian Mapango winga wa kulia Mohammed Yahya ( Tostao) Ali Katolila na Peter
Tino Winga ya kushoto.
Mchezo ilianza taratibu huku kila timu
ilikuwa ikiusoma mchezo wa timu pinzani . Lakini uwezo mkubwa uliooneshwa na
timu zote mbili katika kumiliki mpira na kutoeleana mapande ya uhakika ndio
jambo lililonifanya nisiusahau mchezo huu.
Pan African walikuwa wa kwanza kuandika bao
la kwanza liliwekwa kimiani na Ali Katolila wakati mvua ikinyesha kitu ambacho kilikuwa cha ajabu siku hiyo kwani kila ikinyesha mvua Pan walikuwa wakiandika bao. KMKM wakapapatua na
kuwasazisha bao lilifungwa na Mcha Khamis.
Mvua ikasimama na iliponyesha tena Pan African wakaweka bao la pili
mfungaqji Mohammed Yahya “Tostao”. Mvua ikasimama na gemu kuendelea hadi Shaaban
Ramadhan aliposawazisha na kufanya matokeo 2-2 nadhani hadi mapumziko.
Kipnidi cha pili ambapo KMKM walikuwa
wakicheza mpira wa uhakika waliofundishwa darasani na Mzee Kheri walijitahidi
kutandaza kandanda safi lakini walishtukizwa na mabao mawili ya haraka haraka
yaliyowekwa wavuni na Peter Tino na Mohammed Yahya Tostao baada ya kupokea krosi
maridhawa kutoka kwa Ali Katolila na kupiga Bullet header iliyomshinda kipa
Korosheni. Na hadi kumalizika kwa mchezo Pan African 4 KMKM 2
Ingawa KMKM walikubali kipigo lakini kwa waliobahatika kuwepo uwanjani siku hii mimi nikiwa mmojawapo niliridhishwa kabisa na viwango vya timu zote mbili vya uwezo wa kuumiliki , kutoa pasi zenye macho, kujihami kwa pamoja, na magoli yaliyofungwa bado vipo fresh licha ya kupita zaidi ya miaka 30!
Ingawa KMKM walikubali kipigo lakini kwa waliobahatika kuwepo uwanjani siku hii mimi nikiwa mmojawapo niliridhishwa kabisa na viwango vya timu zote mbili vya uwezo wa kuumiliki , kutoa pasi zenye macho, kujihami kwa pamoja, na magoli yaliyofungwa bado vipo fresh licha ya kupita zaidi ya miaka 30!
Je una gemu yoyote ya zamani unayoikumbuka? Turushie
mdau kidogo kwenye kumbukumbu zangu huyu (msomali)alikuwa omar kombo na sio mohammed kombo otherwise uko sawa nimeipenda hii
ReplyDeleteNa hapa kidogo nakuweka sawa peter tino alicheza number 10 na winger ya kushoto ni Ibrahim kiswabi!
ReplyDeletehiyo game sio kmkm no small simba n.a. oan
ReplyDeleteKikosi Cha Pan African hakikuwa hicho
ReplyDeleteAdolf
Pondamali
Jafar AbdulRahman
Tenga
hawakuwepo
Kikosi kilikuwa kama ifuatavyo
1) Ali Yusuf
2) Mkweche
3 ) John Faya
4) Rashid Idd Chama
5) Jellah Mtagwa
6) Salum Mwinyimkuu Carlos
7) Tostao
8) Hussein Ngulungu
9) Abdallah Burhan
10) Ali Katolila
11) Peter Tino