Na
Mwantanga Ame, Dodoma
MWENYEKITI
wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta, amesema mapendekezo yanayotolewa
na makundi tofauti, hayatabadili rasimu ya Katiba iliyopo, bali yanalenga
kuweka msisitizo wa kutambulika mahitaji ya makundi hayo kwani Bunge la Katiba
halipokei maoni mapya.
Mhe.
Sitta, aliyasema hayo jana wakati akipokea mapendekezo ya kundi la Wasanii wa
Tanzania, wakiwemo wa Zanzibar, huko Mjini Dodoma, ambapo vikao vya Bunge
Maalum la Katiba vinaendelea kufanyika katika kamati 12 za Bunge hilo.
Maoni
hayo yaliwasilishwa na kundi la Wasanii wa kazi za Muziki wa kizazi kipya,
Wasanii wa Filamu, Wasanii wa kazi za Sanaa Ufundi na Maonyesho.
Wiki
iliyopita Bunge hilo lilipokea maoni yaliyotoka katika makundi ya wakulima,
wafugaji na wavuvi, baada ya makundi hayo kukabidhi waraka rasmi uliokuwa una
mambo mbalimbali yaliyokuwa yakiyahusu makundi hayo.
Mhe.
Sitta alisema amelazimika kuweka wazi hilo kwa vile Ofisi yake inachokifanya ni
kupokea mitazamo ya makundi hayo kwa dhamira ya kuona ni vipi yataweza
kuzingatiwa na Wajumbe wa Bunge hilo, wakati wakiendelea na kazi zao ndani ya
Kamati.
Alisema
mchakato wa kupatikana kwa Katiba mpya imeweza kuzingatia mambo mengi ikiwemo
sura ya nne inayoyahusu makundi ya kijamii ambapo baadhi yake yameonekana
kusahaulika kwa baadhi ya mambo.
Alisema
kwa vile rasimu hiyo bado sio msahafu ndio maana Wajumbe wa Bunge hilo
wamelazimika kuwapo hapo ili kuifanyia kazi kwa kuona ni vipi wataweza
kuzingatia mambo ya msingi kuwamo ndani ya Katiba mpya.
Alisema
Tanzania hivi sasa, vijana wake wengi wamekuwa wakifanya kazi za usanii jambo
ambalo ni la msingi kuzingatiwa ndani ya mchakato huo ili kuona ni vipi
wataweza kufanikisha mambo yao.Alisema
ni kweli Katiba iliyopo tayari imeshapitwa na wakati, na maamuzi ya kutunga
Katiba mpya yachukuliwe kuwa ni rafiki kwa Wananchi wa kawaida, kwa vile kuna
maeneo ambayo ni muhimu kuangaliwa na kuzingatiwa kwa faida ya jamii.
Akiyataja
maeneo hayo alisema ni yale ambayo yamekuwa yakihusu suala la haki hasa kwa
vile Katiba ya sasa imekuwa ikiizingatia zaidi mali isiyohamishika huku mali
isiyoshikika ikiwa haitambuliki.
Alisema
hilo ni tatizo na ni lazima Bunge hilo, lione umuhimu wa kuzingatia m aoni ya
makundi tofauti kwa vile ni sehemu itayoweza kupatikana kwa Katiba bora.
Nea
Makamu Mwenyekiti wa Bunge hilo, Mhe. Samia Suluhu Hassan, alisema kitendo cha
makundi tofauti kuamua kutoa maoni yao, imekuwa ikilipa moyo Bunge hilo ili
liweze kuendelea vizuri kufanya kazi zake.
Alisema
mchakato wa Katiba umekuwa unachukua mambo muhimu na ya msingi na maoni ya
makundi yasioshikika yanauwezo wa kuifanya kazi hiyo vizuri.
No comments:
Post a Comment