Na Amina Omari, Tanga
KATIBU Mkuu Kiongozi, Balozi
Ombeni Sefue, amewataka watendaji wa utumishi wa umma, kutojihusisha na
ushabiki wa kisiasa ili kutekeleza majukumu yáo kwa ufanisi.
Kauli hiyo ameitoa jana wakati
akizungumza na watumishi wa sekretarieti ya mkoa na taasisi za serikali
zilizopo mkoani Tanga.
Alisema nia ni kuhakikisha
watendaji hao wanasimamia chaguzi zinazokuja kwa huru na haki.
Alisema taratibu za utumishi wa
umma hazimruhusu mtumishi kujihusisha na ushabiki wa kisiasa wa aina yoyote.
Aliwata watumishi hao
kufanyakazi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma ili
kuimarisha utendaji kazi serikalini.
Alisema ni lazima maadili ya
utumishi wa umma yazingatiwe katika kutoa huduma kwa wananchi ili kuepusha
migongano.
"Kuna malalamiko yanatokea
kwenye huduma tunazotoa, wakati mwingine hadi majibu tunayotoa sio mazuri kwa
wananchi hali hii inasababisha serikali tuonekane hatufanyi kazi,”alisema.
Alisemakwa sasa watakuwa
wakichukua hatua kali kwa watendaji waoghushi madai ili kuitia hasara serikali.
Katibu tawala wa mkoa wa Tanga,
Salum Chima, aliiomba serikali kuhakikisha wanawasilisha kwa muda fedha za
miradi ya maendeleo ili kutekeleza kwa ufanisi.
No comments:
Post a Comment