Na
Mahmoud Ahmad, Arusha
Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu, imemteua Jaji Mkuu (mstaafu) wa Tanzania,
Agustino Ramadhan, kuwa Rais wa mahakama hiyo, kwa kipindi cha miaka miwili.
Anachukua
nafasi ya Sophia Akuffo wa Ghana, aliemaliza muda wake.
Jaji
Ramadhan anakuwa Mtanzania wa kwanza kushikilia kiti hicho tokea kuanzishwa
mahakama hiyo baada ya kupata kura saba dhidi ya kura nne alizopata mpinzani
wake.
Makamu
wake anakuwa Jaji Eisie Thompson, kutoka Nigeria.
Akizungumza
na vyombo vya habari baada ya uteuzi huo, Jaji Ramadhan, alisema ni heshima kwa
Tanzania kwani ndio mara yake ya kwanza kupata nafasi hiyo.
“Kesi
yeyote inayohusu nchi yangu mimi sitakuwepo kutokana na sheria zetu za mahakama
hii. Tayari Watanzania watano wamefungua kesi katika mahakama hii na mbili
zimetolewa hukumu ikiwemo ya Mchungaji Mtikila na Zongo,”alisema.
Aidha
mahakama hiyo iliwaapisha Majaji watatu kabla ya kuanza mchakato wa upigaji
kura kumteuwa Rais wa mahakama hiyo.
"Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu, imemteua Jaji Mkuu (mstaafu) wa Tanzania, Agustino Ramadhan, kuwa Rais wa mahakama hiyo" hiki cheo hakimfai Mtanzania yeyeto kwa sababu TZ tunaendeshwa kidiktete, angalia mfano wa mashekhe wetu, viongozi wetu madikteta na huyo alikuwa jaji kwahivyo ile system itakuwemo kwenye damu yake tu
ReplyDelete