Habari za Punde

Mkutano wa Majeshi ya Anga ya Nchi za SADC - SAC, Wafanyika Zanzibar Hoteli ya Zanzibar Beach Resort.

Meja Generali wa JWTZ ,Joseph Furaha Kapwani akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Majeshi ya Anga yalioko chini ya Kusini mwa Afrika, Akitowa maelezo ya mkutano huo na kumkaribisha mgeni Rais Waziri wa Nchi Ofisi Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum Zanzibar, Mhe Haji Omar Kheri, kuufungua mkutano huo unaofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mazizini Zanzibar.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum Zanzibar Mhe Haji Omar Kheri, akihutubia  Maofisa wa Majeshi wa Anga wa SADC – SAC ,wakati wa ufunguzi wa mkutano huo wa  Majeshi ya Anga Yalioko Chini ya Kusini mwa Afrika (SADC-SAC)unaofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Zanzibar Beach Resort mazizini Zanzibar na kushiriki Nchi washiriki wa Jumuiya hiyo. 
Maofisa wa Jeshi la Anga wa JWTZ wakifuatilia mkutano huo 
Maofisa wa Majeshi wa Nchi cha SADAC -SAC wakimsikiliza mgeni rasmin wakati wa ufunguzi wa mkutano huo unaofanyika Zanzibar. katika hoteli ya Zanzibar Beach Resort


       Wajumbe kutoka Nchini Malawi wakiwa ukumbi wa Mkutano wakifuatilia Mada zinazowakilishwa.
                               Wajumbe wa South Africa wakifuatilia mkutano.




No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.