HOTUBA
YA BAJETI YA OFISI YA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS
KWA
MWAKA WA FEDHA 2015/2016
HOTUBA
YA WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS MHESHIMIWA
FATMA
ABDULHABIB FEREJ
KUHUSU
MAKADIRIO
YA MAPATO NA MATUMIZI YA OFISI YA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS KWA MWAKA WA FEDHA
2015/2016
UTANGULIZI
1. Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako naomba kutoa hoja
kwamba Baraza lako sasa likae kama Kamati ya matumizi ili liweze
kupokea, kuzingatia, kujadili, kuchangia na hatimae kuidhinisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya
Makamu wa Kwanza wa Rais kwa mwaka wa fedha 2015/2016.
2. Mheshimiwa Spika,
hatuna budi kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kutujaalia uzima na afya
njema na kuweza kukutana kwa lengo la kujadili hotuba hii ya OMKR. Namuomba
Mwenyenzi Mungu atuwezeshe kukamilisha vizuri miaka mitano ya awamu hii ya saba
tukimalizia uwasilishaji wa hotuba ya bajeti kwa mwaka 2015/2016 mbele ya
Baraza lako.
3. Mheshimiwa Spika,
napenda kuchukua nafasi hii kumshukuru sana Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dk. Ali Mohammed Shein kwa kuwa karibu nasi kwa
muda wote katika utendaji wa kazi zetu za OMKR.
Hakika ukaribu wake huo tunauthamini sana maana umetuwezesha kutekeleza
majukumu yetu ya kuwahudumia wananchi bila ya hofu na kwa mafanikio.
4. Mheshimiwa Spika, vile
vile sina budi kuwapongeza viongozi
wetu wa kitaifa Makamu wa Kwanza wa Rais Mheshimiwa Maalim Seif Sharif
Hamad na Makamu wa Pili wa Rais Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi kwa jitihada
zao za kumsaidia Mheshimiwa Rais katika kuwatumikia wananchi wa Zanzibar.
5. Mheshimiwa Spika,
natoa shukurani na pongezi maalumu kwa Makamu wa Kwanza wa Rais Mheshimiwa
Maalim Seif Sharif Hamad kwa uongozi wake imara. Miongozo na ushauri wake anaotupa katika
kukabiliana na changamoto za utekelezaji wa masuala mtambuka yanayosimamiwa na
Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais umekuwa ni chachu kwa mafanikio
tuliyopata. Kwa niaba ya wafanyakazi
wote wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, tunaahidi kuendelea kushirikiana
naye ili kuleta maendeleo kwa jamii na Taifa kwa ujumla.
6. Mheshimiwa Spika, kwa
namna ya pekee naomba nikupongeze wewe binafsi Mheshimiwa Spika pamoja na
wasaidizi wako wakiwemo Naibu Spika na Wenyeviti wa Baraza kwa kuliongoza
vyema.
7. Mheshimiwa Spika,
namshukuru Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Baraza la Wawakilishi ya Kusimamia
Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitafifa Mheshimiwa Hamza Hassan Juma, pamoja na
wajumbe wote wa Kamati yake kwa kushirikiana nasi bega kwa bega katika
kuhakikisha tunafanikisha utekelezaji wa malengo ya OMKR. Naishukuru pia Kamati ya Kudumu ya Baraza la
Wawakilishi ya Hesabu za Serikali chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa Omar Ali
Shehe, Mwakilishi wa wananchi wa Jimbo la Chake Chake kwa mashirikiano mema na
OMKR.
8. Mheshimiwa Spika,
napenda kuwashukuru wajumbe wenzangu wa Baraza hili la Wawakilishi, kwa
mashirikiano yao ya dhati kwangu mimi binafsi pamoja na watendaji wa Ofisi yetu
tukiwa ndani ya Baraza na hata katika majimbo yao. Tunamuomba Mwenyezi Mungu
atujaalie uchaguzi wa salama na atuwezeshe kukutana tena katika awamu
ijayo. Aidha, nachukua nafasi hii
kuwatakiwa wote mafanikio mema katika uchaguzi unaokuja.
9. Mheshimiwa Spika,
napenda kuwapongeza Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu kwa mashirikiano makubwa
wanayonipa katika utekelezaji wa majukumu ya Ofisi yetu. Vilevile, napenda
kuwashukuru kwa dhati Afisa Mdhamini wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais,
Wakurugenzi pamoja na wafanyakazi wote wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kwa
juhudi, bidii na ustahamilivu katika kutekeleza majukumu yao ya kazi na kuleta
ufanisi na tija kwa Taifa letu.
10.
Mheshimiwa
Spika, katika mvua zinazoendelea za masika za
mwaka huu ndani ya nchi yetu, mwanzoni mwa mwezi wa Mei tumeshuhudia mvua
katika kiwango kikubwa ambacho hakijawahi kutokea kwa miongo ya hivi karibuni.
11.
Mheshimiwa
Spika, mvua hizo zimesababisha maafa
mbalimbali yakiwemo kupoteza maisha kwa wananchi wetu na uharibifu wa makaazi
na miundo mbinu uliotokana na mafuriko katika maeneo mbalimbali.
12.
Mheshimiwa
Spika, nachukua fursa hii kuwashukuru viongozi
na wananchi wote kwa jumla kwa mashirikiano waliyoonesha katika kukabiliana na
maafa hayo. Aidha, naomba nitoe mkono wa pole kwa wafiwa na waathirika,
nawaomba wawe na moyo wa subira kwa mtihani huo nakufahamu kuwa hiyo ni kadari
ya Alla. Serikali itaendelea kuwa pamoja na wananchi katika kukabiliana na
changamoto hizo.
13.
Mheshimiwa Spika,
kwa niaba ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais napenda kutoa mkono wa pole
kwako Mheshimiwa Spika na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, familia pamoja na
wananchi wa Jimbo la Magomeni kwa kuondokewa na Mwakilishi wao mpendwa marehemu
Salmin Awadh Salmin. Tunamuomba Mwenyezi
Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi Amin.
MALENGO MAKUU YA OFISI
YA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS
14.
Mheshimiwa
Spika, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais ina
jukumu la kusimamia na kuratibu Ofisi ya Faragha ya Mheshimiwa Makamu wa Kwanza
wa Rais, mipango, sera na utafiti, uendeshaji na utumishi, masuala ya mazingira
na mabadiliko ya tabianchi, watu wenye ulemavu, udhibiti wa dawa za kulevya na
muitiko wa Taifa wa kupambana na UKIMWI. Katika kutimiza jukumu hili, Ofisi ya
Makamu wa Kwanza wa Rais imekuwa na malengo makuu yafuatayo:-
1.
Kuratibu na kusimamia
shughuli za Makamu wa Kwanza wa Rais.
2.
Kuratibu mipango, sera
na utafiti unaohusiana na maeneo ya majukumu ya OMKR.
3.
Kuimarisha usimamizi
endelevu wa mazingira na kuratibu masuala ya mabadiliko ya tabianchi.
4.
Kuimarisha na kutetea
uzingatiaji wa haki na fursa sawa kwa watu wenye Ulemavu ndani ya jamii.
5.
Kuratibu na kudhibiti
usafirishaji, uingizwaji, matumizi na biashara haramu ya dawa za Kulevya.
6.
Kuratibu Mwitiko wa
Taifa juu ya kinga dhidi ya UKIMWI na kupunguza athari kwa jamii.
15.
Mheshimiwa
Spika, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais
inatekeleza majukumu yake kupitia Taasisi zifuatazo:-
1.
Ofisi ya Faragha
2.
Idara ya Mipango, Sera
na Utafiti
3.
Idara ya Uendeshaji na
Utumishi
4.
Idara ya Mazingira
5.
Idara ya Watu wenye
Ulemavu
6.
Ofisi ya Makamu wa
Kwanza wa Rais Pemba
7.
Tume ya Kitaifa ya
Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya
8.
Tume ya UKIMWI
16.
Mheshimiwa
Spika, kufuatia kupitishwa na kusainiwa kwa
Sheria ya Mazingira ya mwaka 2015, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kwa mwaka
2015/2016 inategemea kuwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar
(Zanzibar Environmental Management Authority – ZEMA) ili kuongeza nguvu katika
utekelezaji wa majukumu ya usimamizi wa mazingira, Zanzibar.
MUHTASARI
WA MAFANIKO NA CHANGAMOTO ZA OMKR KWA MIAKA MITANO (5)
17.
Mheshimiwa
Spika, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais
imeanzishwa mwaka 2010 mara baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi Oktoba,
2010. Tokea kuanzishwa kwake, pamoja na
kuendelea na utekelezaji wa majukumu yake ya msingi, pia ilijikita katika
kutayarisha nyenzo ambazo zitasaidia kufanyakazi kitaalamu na kwa ufanisi zaidi
kwa miaka kadhaa ijayo.
18.
Mheshimiwa
Spika, kwa kuwa kipindi cha miaka mitano
kimepita tokea kuanzishwa kwa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, na hasa kwa
vile tunamaliza bajeti ya awamu hii, naomba nieleze kwa muhtasari baadhi ya
mafanikio ya msingi yaliyopatikana na OMKR.
19.
Mheshimiwa
Spika, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais imeweza
kuratibu kwa ufanisi mkubwa shughuli za Mheshimiwa Makamu wa Kwanza wa Rais
zikiwemo safari za ndani na nje ya nchi ambapo miongozo kwa taasisi mbali mbali
imetolewa ikiwa ni sehemu ya kuyatafutia ufumbuzi matatizo ya kijamii pamoja na
kufanikisha usimamizi wa masuala yanayosimamiwa na OMKR. Aidha, uratibu wa mikutano kati ya Mheshimiwa
Makamu wa Kwanza wa Rais na Mabalozi waliopo nchini, viongozi wa nchi na
mashirika mbali mbali ya kimataifa ulifanyika kwa ufanisi mkubwa ambapo pamoja
na mambo mengine mikutano hiyo imekuza mahusiano kati ya Zanzibar na nchi au
mashirika hayo.
20.
Mheshimiwa
Spika, pamoja na mafanikio hayo, Ofisi ya
Faragha imekuwa na changamoto ya msingi iliyodumu ndani ya kipindi cha miaka
mitano ambayo ni kukosekana kwa makaazi rasmi ya Mheshimiwa Makamu wa Kwanza wa
Rais huko Dar-es-Salaam. Hali hiyo
imemlazimisha kufikia hotelini, jambo ambalo limepelekea kuwa na gharama zaidi.
21.
Mheshimiwa
Spika, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais
imeandaa Mpango Mkakati kwa kipindi cha 2014 – 2020 na Mpango Mkuu wa Utafiti
kwa kipindi kama hicho kwa masuala yanayoratibiwa na OMKR. OMKR pia imeandaa muongozo wa uzingatiaji
pamoja na mfumo wa ufuatiliaji na tathmini kwa mambo mtambuka yanayosimamiwa na
OMKR.
22.
Mheshimiwa
Spika, ni jukumu la taasisi na wadau wengine
kuutumia muongozo huo na mingine ya kisekta iliyoandaliwa katika kuhakikisha
mambo mtambuka yakiwemo ya mazingira, masuala ya Watu wenye Ulemavu na UKIMWI
yanazingatiwa katika mipango yao mbalimbali.
23.
Mheshimiwa
Spika, katika sekta ya mazingira, Ofisi ya
Makamu wa Kwanza wa Rais imeandaa sera ya mazingira ya mwaka 2013, Mkakati wa
Zanzibar wa Kukabiliana na Athari za Mabadiliko ya Tabianchi wa mwaka 2014,
Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2015, Mkakati wa Mawasiliano ya
Mazingira, Mkakati wa Mawasiliano wa Mabadiliko ya Tabianchi, Muongozo wa
Uzingatiaji wa Mabadiliko ya Tabianchi kwa sekta mbalimbali pamoja na kanuni za
mifuko ya plastiki na maliasili zisizorejesheka. Jumla ya Tathmini 71 za Athari za Kimazingira
zimefanyika na kutolewa vyeti vya mazingira kwa miradi hiyo. Aidha, wananchi
8,000 wa kijiji cha Nungwi wamepatiwa maji safi na salama ambao kwa muda mrefu
maji yao yalikuwa na chumvi-chumvi kutokana na athari za mabadiliko ya
tabianchi.
24.
Mheshimiwa
Spika, mafanikio mengine katika sekta ya
mazingira ni kukua kwa uelewa wa masuala ya mazingira katika jamii ambapo
kamati, vikundi na asasi zisizokuwa za Kiserikali (NGOs) mbalimbali zimeundwa
ndani ya jamii kwa lengo la kusaidia usimamizi wa mazingira nchini. Aidha, kupungua kwa matumizi ya mifuko ya
plastiki ndani ya Zanzibar ni mafanikio ya kupigiwa mfano yaliyofikiwa na OMKR.
25.
Mheshimiwa
Spika, pamoja na mafanikio hayo, bado sekta ya
mazingira inakabiliwa na changamoto za kuwepo kwa athari za mabadiliko ya
tabianchi, uharibifu na uchafuzi wa mazingira kwa baadhi ya maeneo.
26.
Mheshimiwa
Spika, katika masuala ya Watu wenye Ulemavu,
Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais imeweza kufanya usajili wa Watu wenye Ulemavu
katika Mikoa yote mitano ambao utaiwezesha Serikali kuwatambua walipo pamoja na
kuzingatia mahitaji yao katika mipango ya maendeleo. Aidha, OMKR imeanzisha Mfuko wa Watu wenye
Ulemavu kwa lengo la kudumisha utoaji wa huduma kwa watu hao, kuandaa rasimu ya
sera ya Watu wenye Ulemavu ambayo inatarajiwa kuwasilishwa Serikalini hivi
karibuni. Aidha, watu 281 wenye ulemavu (Unguja 150 na Pemba 131) wamepatiwa
visaidizi na dawa ili pamoja na mambo mengine kurahisisha shughuli zao za
maisha.
27.
Mheshimiwa
Spika, pamoja na juhudi hizo, Serikali
inakabiliwa na changamoto za kuwepo kwa udhalilishaji kwa Watu wenye Ulemavu
hasa wenye ulemavu wa akili pamoja na baadhi ya wadau na jamii kutozingatia
mahitaji ya watu wenye ulemavu katika mipango yao.
28.
Mheshimiwa
Spika, katika sekta ya UKIMWI, Ofisi ya Makamu
wa Kwanza wa Rais imetayarisha Mkakati wa Pili wa Taifa wa UKIMWI Zanzibar kwa
kipindi cha 2011 – 2016 na Sheria ya Kukinga na Kusimamia Masuala ya UKIMWI ya
mwaka 2013. Sheria hii itaondoa
unyanyapaa pamoja na kuimarisha haki za binadamu kwa kuwalinda walioambukizwa
na wasioambukizwa na VVU. Aidha, Tume
imeandaa Mkakati wa Utafutaji wa Rasilimali kwa ajili ya kusaidia utekelezaji
wa shughuli za UKIMWI.
29.
Mheshimiwa
Spika, pamoja na juhudi hizo ambapo pia
kumekuwa na kupungua kwa unyanyapaa kwa watu wanaoishi na VVU, sekta hii ya
UKIMWI inakabiliwa na changamoto ya kupungua kwa upatikanaji wa fedha kutoka
kwa washirika wa maendeleo hali inayokwaza juhudi za mapambano dhidi ya UKIMWI.
30.
Mheshimiwa
Spika, katika kushughulikia tatizo la dawa za
kulevya, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais imefanya mapitio ya Sheria ya
Udhibiti wa Dawa za Kulevya ya mwaka 2009 ambayo yamepelekea kuundwa kwa Tume
ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya. Aidha, OMKR imeandaa muongozo kwa ajili ya
uanzishwaji wa nyumba za makaazi ya vijana walioacha matumizi ya dawa za
kulevya. Hivi sasa Serikali inaendelea
na ujenzi wa Kituo cha Tiba na Marekebisho ya Tabia kwa wanaotumia dawa za
kulevya ambacho kinahitajika sana katika kukabiliana na tatizo la dawa hizo
hapa nchini.
31.
Mheshimiwa
Spika, pamoja na kuimarika kwa mashirikiano
miongoni mwa taasisi wadau katika suala la udhibiti wa dawa za kulevya, bado
Serikali inakabiliwa na changamoto za kuwepo kwa uingizwaji na usambazwaji wa
dawa hizo unaopelekea kuendelea kwa matumizi yake hapa Zanzibar.
UTEKELEZAJI
WA MALENGO YA OMKR KWA MWAKA 2014/2015
OFISI
YA FARAGHA
32.
Mheshimiwa Spika,
Ofisi ya Faragha ina jukumu la kuratibu shughuli za Mheshimiwa Makamu wa Kwanza
wa Rais.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Ofisi ya Faragha
ilipanga kutekeleza malengo yafuatayo:-
1. Kusimamia
na kuratibu shughuli zote za Makamu wa Kwanza wa Rais.
2. Kuimarisha
mazingira ya kazi katika kuleta ufanisi.
33.
Mheshimiwa Spika, hadi
kufikia Machi 2015, Ofisi ya Faragha imeweza kutekeleza yafuatayo katika
malengo iliyopanga:-
34.
Mheshimiwa Spika,
katika kuimarisha mashirikiano ya kijamii na kiuchumi, Mheshimiwa Makamu wa
Kwanza wa Rais amefanya ziara 4 za nje. Aidha, ziara mbali mbali za ndani ya
nchi zilifanyika na ripoti za ziara hizo kuwasilishwa sehemu husika kwa ajili
ya kufanyiwa kazi. Kwa upande wa ziara za ndani miongozo mbali mbali imetolewa
kwa taasisi na jamii zilizo tembelewa.
35.
Mheshimiwa
Spika, wageni 25 kutoka nje ya nchi walipata
kuonana na Mheshimiwa Makamu wa Kwanza na kubadilishana mawazo juu ya mambo
mbali mbali yanayohusu uchumi, kijamii na mazingira. Vile vile, Mheshimiwa Makamu wa Kwanza wa
Rais ameonana na wageni wa ndani na kubadilishana mawazo juu ya mambo mbali
mbali ya kijamii na ushauri wa mambo hayo umetolewa. Sambamba na hayo, katika kusaidia shughuli za
kiuchumi na kimaendeleo Mheshimiwa Makamu wa Kwanza wa Rais amesaidia jumuiya
na vikundi vya jamii.
36.
Mheshimiwa Spika, katika
kukuza mawasiliano na upatikanaji wa
taarifa kuhusiana na utekelezaji wa shughuli za Mheshimiwa Makamu wa Kwanza wa
Rais, jumla ya kalenda 2,000 za mwaka 2015 zenye ujumbe mbali mbali
zimechapishwa na kusambazwa kwa wadau mbalimbali. Ununuzi wa vifaa mbalimbali vya habari
umefanyika na kuongeza utoaji wa habari za Mheshimiwa Makamu wa Kwanza wa Rais.
37.
Mheshimiwa
Spika, katika kuimarisha mazingira ya kazi na ya wafanyakazi wa Ofisi ya
Faragha, matengenezo madogo ya ofisi ya faragha na nyumbani kwa Mheshimiwa
Makamu wa Kwanza wa Rais yamefanyika. Vifaa mbali mbali kwa ajili ya matumizi
ya ofisini na nyumbani vimenunuliwa.
38.
Mheshimiwa Spika,
Ofisi ya Faragha kwa mwaka wa fedha 2014/15 ilikadiria kutumia TZS 411,150,000/- kwa kuendeshea kazi.
Hadi kufikia Machi, 2015 ilikwisha kuingiziwa TZS 143,902,500/- sawa na asilimia 35.
IDARA
YA MIPANGO, SERA NA UTAFITI
39.
Mheshimiwa Spika,
Idara hii ina jukumu la kuandaa na kusimamia utekelezaji wa sera na
mipango ya maendeleo; kuratibu shughuli
za utafiti pamoja na kufuatilia na
kutathmini utekelezaji kwa taasisi zote zilizo chini ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Idara ya Mipango, Sera
na Utafiti ilipanga kutekeleza malengo yafuatayo:-
1.
Kujenga uwezo wa
utafiti kwa watendaji 20 na kufanya tafiti tatu katika maeneo ya OMKR
(Mazingira, Watu wenye Ulemavu na Dawa za Kulevya).
2.
Kuratibu utekelezaji wa
masuala mtambuka ya OMKR.
3.
Kuratibu shughuli za
sera, mipango na miradi ya maendeleo.
40.
Mheshimiwa
Spika, hadi kufikia Machi 2015 Idara ya
Mipango, Sera na Utafiti imeweza
kutekeleza yafuatayo katika malengo iliyopanga:-
41.
Mheshimiwa
Spika, mafunzo ya utafiti ya siku tano kwa wafanyakazi
wa OMKR yametolewa. Mafunzo hayo yaliwashirikisha watendaji 30 kutoka OMKR na
yalilenga kuwawezesha watendaji kutumia matokeo ya utafiti katika kupanga na
kufuatilia mipango ya kila siku.
42.
Mheshimiwa Spika, utafiti
wa kimazingira unaohusu masuala ya athari na kiwango cha uingizaji wa vifaa
chakavu vya umeme na elektroniki (e-waste) umefanyika na ripoti yake
itawasilishwa kwa wadau hivi karibuni.
43.
Mheshimiwa
Spika, katika kuhakikisha sekta zinazingatia
masuala mtambuka yanayosimamiwa na OMKR ndani ya mipango yao ya kimaendeleo,
mafunzo ya siku tatu ya wakufunzi (Unguja na Pemba) yalitolewa. Mafunzo hayo
yalihusu utekelezaji wa muongozo wa mambo mtambuka ulioandaliwa na OMKR na
kuwashirikisha watendaji 25 kutoka katika sekta mbali mbali za serikali.
44.
Mheshimiwa
Spika, taarifa mbali mbali za utekelezaji za
robo mwaka na za mwaka zimeandaliwa na kuwasilishwa sehemu husika ikiwemo Tume
ya Mipango, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Wizara ya Fedha na taasisi
nyengine kila ilipohitajika.
45.
Mheshimiwa
Spika, Idara ya Mipango, Sera na Utafiti kwa
mwaka wa fedha 2014/15 iliidhinishiwa kutumia TZS 146,065,000/- kwa kuendeshea kazi. Hadi kufikia Machi, 2015
ilikwisha kuingiziwa TZS 51,819,000/-
sawa na asilimia 35.
UTEKELEZAJI
WA MIRADI YA MAENDELEO
46.
Mheshimiwa Spika, katika
mwaka wa fedha 2014/2015 Idara ya
Mipango, Sera na Utafiti iliratibu utekelezaji wa miradi (2) ya maendeleo
ifuatayo:-
a) Mradi
wa kujenga Kituo cha Tiba na Marekebisho ya Tabia kwa watumiaji wa dawa za
kulevya (Construction of Treatment and Rehabilitation center).
47.
Mheshimiwa Spika, mradi
huu unatekelezwa kwa fedha za SMZ, kwa mwaka wa fedha 2014/15 ulilenga kukamilisha
ujenzi wa sehemu ya chini, hadi kufikia Machi 2015 ujenzi wa msingi pamoja na
uwekaji wa jamvi umekamilika.
48.
Mheshimiwa
Spika, mradi huu kwa mwaka wa fedha 2014/15
uliidhinishiwa kutumia TZS 1,400,000,000/-.
Hadi kufikia Machi, 2015 ilikwisha kuingiziwa TZS 250,000,000/- sawa na asilimia 18.
b) Mradi wa kujenga uwezo wa utekelezaji wa
masuala ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi.
49.
Mheshimiwa Spika, mradi
huu unatekelezwa kwa fedha za Washirika
wa Maendeleo (UNDP) kupitia programu
ya UNDAP. Mradi huu unatekelezwa kupitia malengo saba ambapo malengo manne kati
ya hayo yanatekelezwa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais. Malengo hayo ni:-
i.
Kuhakikisha masuala ya
mazingira na mabadiliko ya tabianchi yanaingizwa katika mipango ya maendeleo
ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa MKUZA II.
ii. Kutayarisha
Mkakati wa Zanzibar wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi na kusaidia
utekelezaji wake.
iii. Kuimarisha
muundo wa kitaasisi kwa ajili ya kusimamia masuala ya mabadiliko ya tabianchi.
iv. Kukuza
kiwango cha upatikanaji wa taarifa na uelewa juu ya athari za mabadiliko na
mikakati ya kukabiliana nayo miongoni mwa jamii na taasisi za Serikali.
50.
Mheshimiwa
Spika, malengo mengine matatu ya mradi huu
yanatekelezwa kupitia Wizara ya Fedha, Wizara ya Kilimo na Maliasili na Wizara
ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati.
Aidha, jumuiya ya Maendeleo ya Jamii na Uhifadhi wa Mazingira Zanzibar (COmmunity
Deverlopment and Environmental COnservation in Zanzibar CODECOZ) nayo
inashiriki katika utekelezaji wa mradi huu kwenye lengo moja la kukuza kiwango
cha upatikanaji wa taarifa na uelewa juu ya athari za mabadiliko na mikakati ya
kukabiliana nayo miongoni mwa jamii na taasisi za Serikali.
51.
Mheshimiwa
Spika, hadi kufikia Machi 2015 OMKR kupitia
mradi huu imeweza kutekeleza yafuatayo:-
52.
Mheshimiwa
Spika, rasimu za mipango kazi ya kisekta ya
kuzingatia mabadiliko ya tabianchi zimetayarishwa. Sekta zilizohusika na utayarishaji huo ni
Uvuvi, Miundombinu, Utalii na Kilimo.
53.
Mheshimiwa
Spika, hekta 30 za mikandaa/mikoko zimepandwa
katika maeneo sita ya Unguja na Pemba. Maeneo hayo ni Kiongwe, Mafufuni na
Kisakasaka kwa Unguja na Ndagoni, Wambaa na Pujini kwa Pemba.
54.
Mheshimiwa
Spika, ripoti ya ukusanyaji wa taarifa za msingi za kutayarisha mpango wa jamii wa kuhimili athari za
mabadiliko ya tabianchi imetayarishwa na inategemewa kuwasilishwa kwenye vikao vya Ofisi ya Makamu
wa Kwanza wa Rais kwa mapitio na kuridhiwa.
55.
Mheshimiwa
Spika, hatua za utayarishaji wa Mpango kazi wa
Utekelezaji Mkakati wa Mabadiliko ya Tabianchi zimeshaaza na utayarishaji wa
mpango huo unategemewa kumalizika mwezi Januari, 2016 kwa hatua za uhamasishaji
wa nyenzo za utekelezaji.
56.
Mheshimiwa
Spika, watendaji wawili kutoka Ofisi ya Makamu
wa Kwanza wa Rais waliwezeshwa kuhudhuria mkutano wa 20 wa Dunia wa mabadiliko
ya tabianchi uliofanyika Lima, Peru na mashirikiano ya wadau mbalimbali wa
mabadiliko ya tabianchi wa nje ya nchi yameongezeka.
57.
Mheshimiwa
Spika, vipindi 6 vya elimu ya athari mabadiliko
ya tabianchi vilitayarishwa na kurushwa kupitia redio jamii za Micheweni,
Makunduchi na Tumbatu. Uelewa wa jamii juu ya masuala ya mabadiliko ya
tabianchi umeongezeka.
58.
Mheshimiwa
Spika, Wajumbe 5 kutoka Ofisi ya Makamu wa
Kwanza wa Rais, Idara ya Ushirika na Asasi ya kiraia ya Community Forest Pemba (CFP) wamepatiwa safari ya kimasomo huko
Arusha Tanzania bara kujifunza utayarishaji na utekelezaji wa mipango ya jamii
ya kuhimili athari za mabadiliko ya tabianchi (Local Adaptation Plans of Action
– LAPA).
59.
Mheshimiwa
Spika, kwa mwaka wa fedha 2014/2015 mradi huu
uliidhinishiwa kutumia TZS 577,500,000/-. Hadi kufikia Machi, 2015 mradi ulikwisha
kuingiziwa TZS 245,620,000/- sawa na
asilimia 43.
IDARA
YA UENDESHAJI NA UTUMISHI
60.
Mheshimiwa Spika,
Idara hii ina jukumu la kusimamia shughuli za kila siku za uendeshaji na
utumishi zikiwemo sheria na kanuni za utumishi, mafunzo, maslahi na maendeleo
ya wafanyakazi.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Idara ya Uendeshaji na
Utumishi ilipanga kutekeleza malengo yafuatayo:-
- Kusimamia, kukuza
na kuimarisha mazingira ya utendaji kazi wa OMKR na kuleta ufanisi.
- Kuwajengea uwezo
wafanyakazi na kuwapatia maslahi.
61.
Mheshimiwa Spika, hadi
kufikia Machi 2015, Idara imeweza kutekeleza yafuatayo katika malengo
iliyopanga:-
62.
Mheshimiwa Spika, katika
kuimarisha mazingira ya utendaji kazi vifaa mbali mbali vimenunuliwa pamoja na
huduma mbali mbali za ofisi zimetolewa.
63.
Mheshimiwa
Spika, katika kushiriki mikutano ya Kitaifa,
Kikanda na Kimataifa, wafanyakazi 23 wamewezeshwa kushiriki katika mikutano ya
ndani kwa ajili ya kufuatilia wa shughuli za Ofisi (Pemba, Dar-es-Salaam na
Dodoma) na 9 wamewezeshwa kushiriki katika mikutano ya kikanda na kimataifa nje
ya nchi (Kenya, Malaysia, Qatar, Lima na Singapore). Safari hizi zimeongeza
mahusiano na washirika wa maendeleo.
64.
Mheshimiwa Spika, taarifa
mbali mbali zinazohusiana na majukumu ya OMKR zimetolewa kupitia vyombo vya
habari na mitandao ya kijamii, makala
2 zenye maudhui yanayohusu mabadiliko ya tabianchi na sheria ya mazingira
zimetolewa katika gazeti la Zanzibar Leo. Aidha, filamu fundishi 2 kuhusiana na
mabadiliko ya tabianchi moja ikiwa kwa lugha ya Kiswahili na Kiengereza
zinazohusu mabadilko ya tabianchi zimetayarishwa.
65.
Mheshimiwa
Spika, wafanyakazi 33 wamesaidiwa gharama za
ada na vifaa na kupatiwa fursa za mafunzo katika ngazi za Cheti, Stashahada,
Shahada ya kwanza na ya pili, pamoja na shahada ya uzamili katika fani tofauti
(Angalia Kiambatanisho Nam. 1).
66.
Mheshimiwa
Spika, katika kusimamia ufanisi wa utendaji wa
OMKR, vikao viwili vya kamati ya uongozi vimekaa na kujadili rasimu ya sera ya
watu wenye ulemavu, mkakati wa mawasiliano ya mabadiliko ya tabianchi pamoja na
kupokea taarifa ya utekelezaji wa kazi za maabara ya utalii zinazotekelezwa na
OMKR. Aidha, kikao kimoja cha zabuni
kilichojadili kumpata mkandarasi wa ujenzi wa kituo cha marekebisho ya tabia
(Construction of treatment and rehabilitation center) kimefanyika. Vilevile,
ripoti ya fedha ya mwaka 2013/2014 imetayarishwa na kuwasilishwa kwa Mdhibiti
na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na Wizara ya Fedha.
67.
Mheshimiwa
Spika, kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Idara ya
Uendeshaji na Utumishi iliidhinishiwa kutumia TZS 1,610,084,000/-. Kati ya
fedha hizo, TZS 320,084,000/- kwa
ajili ya matumizi mengineyo, na TZS
1,290,100,000/- kwa ajili ya mishahara.
Hadi kufikia Machi, 2015 Idara ya Uendeshaji na Utumishi ilikwisha
kuingiziwa TZS 1,110,748,833/- zikiwemo
TZS 173,444,933/- kwa matumizi
mengineyo ambazo ni sawa na asilimia 54,
na TZS 937,303,900/- kwa mishahara
ambazo ni sawa na asilimia 73.
68.
Mheshimiwa
Spika, Idara ya Uendeshaji na Utumishi ndio
Idara pekee iliyoingiziwa fedha zaidi ya asilimia 50 kwa vile kazi zake nyingi
zinajumuisha kuzihudumia Idara zote ikiwemo mafunzo kwa wafanyakazi wote,
huduma za jingo na utekelezaji na usimamizi wa vikao vyote kwa misingi ya
utawala bora.
IDARA
YA MAZINGIRA
69.
Mheshimiwa Spika,
Idara hii ina jukumu la kukusanya na
kuhifadhi taarifa za kimazingira, kutoa taarifa za kimazingira ili ziweze
kusaidia katika kutayarisha na kutekeleza mipango na miradi ya kimaendeleo,
kufuatilia mwenendo wa hali ya kimazingira, kukabiliana na matatizo ya
kimazingira, kuhamasisha wadau kuchukua hatua za kuhifadhi mazingira pamoja na
kutoa elimu ya mazingira kwa jamii.
Aidha, Idara hii pia inajukumu la kuratibu masuala ya mabadiliko ya
tabianchi.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Idara ya Mazingira
ilipanga kutekeleza malengo yafuatayo:-
1. Kuimarisha na kusimamia utekelezaji wa Sera, Sheria
na Kanuni za Mazingira.
2. Kusimamia uingizwaji wa masuala ya mazingira katika miradi ya maendeleo.
3. Kukuza uelewa wa elimu ya mazingira kwa jamii na
wadau wengine.
70.
Mheshimiwa Spika, hadi
kufikia Machi 2015, Idara ya Mazingira
imeweza kutekeleza yafuatayo katika
malengo iliyopanga:-
71.
Mheshimiwa Spika, jumla ya operesheni 33 za uzuiaji matumizi ya mifuko
ya plastiki zimefanyika (Angalia Kiambatanisho Nam. 2). Katika
operesheni hizo, watu 23 wamekamatwa na kupelekwa mahakamani na kutozwa faini
ya jumla ya TZS 3,170,000/-. Aidha, wastani wa kilo 759 za mifuko ya
plastiki zimekamatwa na kuangamizwa.
Vile vile, jumla ya operesheni 27 zimefanyika Unguja na Pemba za
kuwakamata wanaovuna na kusafirisha maliasili kinyume na utaratibu.
72.
Mheshimiwa
Spika, sheria ya
Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2015 imepitishwa na Baraza la Wawakilishi
Zanzibar katika kipindi hiki cha 2014/2015.
Napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru kwa dhati kabisa Waheshimiwa
Wajumbe wote wa Baraza lako kwa kuipitisha Sheria hiyo. Ni imani ya OMKR kuwa
sheria hiyo itasaidia sana kupunguza uharibifu na uchafuzi wa mazingira uliopo
hivi sasa na kuongeza ufanisi wa kusimamia masuala ya mabadiliko ya
tabianchi. Aidha, naomba pia nichukue
nafasi hii kuliarifu Baraza lako kuwa Mheshimiwa Rais ameshatia saini Sheria
hiyo.
73.
Mheshimiwa Spika,
jumla ya miradi kumi na
tatu (13) imefanyiwa tathmini ya athari za mazingira na kijamii na tayari
ripoti za tathmini hizo zimeshafanyiwa mapitio na wadau kwa uratibu wa Idara ya
Mazingira. Kufuatia mapitio hayo, miradi
yote imepatiwa vyeti vya kimazingira na imetakiwa kuendelea na utekelezaji kwa
kufuata masharti yaliyotolewa (Angalia Kiambatanisho Nam. 3).
74.
Mheshimiwa
Spika, mafunzo ya
aina mbili ya tathmini ya athari za kimazingira yamefanyika. Mafunzo hayo
yaliwashirikisha watu 40 kutoka taasisi mbalimbali za kiserikali na zisizo za
kiserikali ambayo yameongeza ujuzi na ufahamu wa Tathmini za Athari za
Kimazingira na usimamizi na ufuatiliaji wa Tathmini hizo.
75.
Mheshimiwa
Spika, jumla ya
vipindi 13 (11 vya redio na 2 vya TV) vimetayarishwa na kurushwa kupitia ZBC
Redio na TV (Angalia
Kiambatanisho Nam. 4). Vipindi 10 vya radio vilihusu matumizi ya
majiko sanifu (2), umuhimu wa umeme wa jua (2),
marufuku ya mifuko ya plastiki (2), mmong’onyoko wa fukwe (2), kanuni ya
maliasili zisizorejesheka (2) na matumizi endelevu ya maliasili zisizorejesheka
(1). Aidha, vipindi viwili vya TV
vinavyohusu matumizi ya majiko sanifu na umeme wa jua vimerushwa hewani
76.
Mheshimiwa
Spika, kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Idara ya
Mazingira iliidhinishiwa kutumia TZS
113,284,000/- kwa ajili ya kuendeshea kazi.
Hadi kufikia Machi, 2015 Idara ya Mazingira ilikwisha ingiziwa TZS 44,2745,000/- sawa na asilimia 39.
77.
Mheshimiwa
spika, kwa kipindi cha mwaka 2014/2015 OMKR
iliidhinishiwa kukusanya TZS 10,
500,000 kupitia Idara
ya Mazingira. Fedha hizi zinatokana na ada ya hifadhi ya mazingira ikiwa ni
pamoja na vyeti vya Mazingira. Kazi ambayo inategemea idadi ya miradi
inayowasilishwa kutoka Mamlaka ya Uwekezaji Vitega Uchumi Zanzibar au miradi ya
maendeleo ambayo inastahili kufanyiwa tathmini. Hadi kufikia Machi 2015, jumla ya TZS
8,700,000/-
zimekusanywa ambazo ni
sawa na asilimia 83.
IDARA
YA WATU WENYE ULEMAVU
78.
Mheshimiwa Spika, Idara
ya Watu Wenye Ulemavu ina jukumu la kuratibu, kusimamia na kufuatilia masuala mbali
mbali yanayohusu Watu wenye Ulemavu ili kuhakikisha ujumuishwaji katika
shughuli zote za kimaendeleo zikiwemo za kiuchumi na kijamii.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Idara ya Watu wenye
Ulemavu ilipanga kutekeleza malengo yafuatayo:-
- Kuimarisha
na kusimamia utekelezaji wa Sheria, kanuni Miongozo kwa Watu wenye
Ulemavu.
- Kusimamia
haki, fursa sawa na ujumuishwaji wa Watu wenye Ulemavu.
- Kuanzisha
programu ya Makuzi ya Awali Maendeleo ya Mtoto (Early Childhood
Development).
79.
Mheshimiwa Spika, hadi
kufikia Machi 2015, Idara ya Watu wenye
Ulemavu imeweza kutekeleza yafuatayo katika malengo iliyopanga:-
80.
Mheshimiwa Spika, rasimu ya Sera ya Watu wenye Ulemavu imeandaliwa na
taratibu za kukamilisha rasimu ya mpango kazi kwa ajili ya utekelezaji wa sera
ya Watu wenye Ulemavu zinaendelea ili kwa pamoja ziweze kuwasilishwa
Serikalini.
81.
Mheshimiwa Spika, kikao kimoja cha Baraza la Taifa la Watu
wenye Ulemavu kimefanyika kujadili taarifa mbali mbali zinazohusiana na
maendeleo na changamoto zinazowakabili Watu wenye Ulemavu.
82.
Mheshimiwa Spika, kikao kimoja cha maafisa waratibu wa masuala ya
Watu wenye Ulemavu kimefanyika. Kupitia
kikao hiki utekelezaji wa masuala ya Watu wenye Ulemavu katika sekta mbalimbali
ulijadiliwa. Vilevile mafunzo juu ya uwezeshaji wa Watu wenye Ulemavu na
Mkataba wa Kimataifa wa Haki na fursa za Watu wenye Ulemavu yametolewa kwa
maafisa waratibu 14 wa wizara na waratibu 10 wa jumuiya zinazoshughulika na
masuala ya watu wenye ulemavu.
83.
Mheshimiwa Spika, ziara
kumi (10) zimefanywa katika taasisi za Serikali na binafsi kwa lengo la
kuhamasisha masuala ya Watu wenye Ulemavu na Kuzungumzia Ujumuishwaji wa Watu
wenye Ulemavu katika sekta hizo. Vile
vile safari moja imefanywa nchini Kenya na nne (4) za ndani ya nchi kwa lengo la kukuza mashirikino juu ya utekelezaji wa
programu zinazohusu masuala ya Watu wenye Ulemavu.
84.
Mheshimiwa Spika, waandishi
wa habari 20 wamepatiwa elimu na kujengewa uelewa juu ya masuala ya makuzi ya
awali ya maendeleo ya mtoto mwenye ulemavu.
85.
Mheshimiwa Spika, mafunzo
ya usimamizi wa fedha na uongozi kwa viongozi 35 (23 Unguja na 12 Pemba) wa Jumuiya za Watu wenye Ulemavu yametolewa
kwa lengo la kuzijengea uwezo na kuleta
ufanisi katika kazi.
86.
Mheshimiwa Spika, Watu
wenye Ulemavu 225 (Pemba 131 na Unguja 94) wamepatiwa visaidizi vya aina mbali
mbali ili pamoja na mambo mengine kurahisisha shughuli zao za maisha (Angalia Kiambatanisho Nam. 5).
87.
Mheshimiwa Spika, sambamba
na hayo, siku ya Kimataifa ya Watu
wenye Ulemavu imeadhimishwa ambapo maadhimisho ya mwaka huu yamefanyika
kisiwani Pemba kwa kufanyika shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuielimisha
jamii juu ya haja ya kuzingatia haki za Watu wenye Ulemavu.
88.
Mheshimiwa Spika, Idara
ya Watu wenye Ulemavu kwa mwaka wa fedha 2014/15 iliidhinishiwa kutumia TZS 278,442,000/- kwa kuendeshea
kazi. Hadi kufikia Machi, 2015 ilikwisha
ingiziwa TZS 100,724,500/- sawa na
asilimia 36.
OFISI
KUU PEMBA
89.
Mheshimiwa Spika, Ofisi
Kuu Pemba ina jukumu la kuratibu, kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa
shughuli zote za Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kwa upande wa Pemba.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Ofisi kuu Pemba
ilipanga kutekeleza malengo yafuatayo:-
- Kuwajengea uwezo wafanyakazi na kuwapatia
maslahi.
- Kuimarisha mazingira ya utendaji kazi.
- Kuratibu na kusimamia utekelezaji wa shughuli za
OMKR Pemba.
- Kukuza na kuimarisha mawasiliano ya habari.
90.
Mheshimiwa Spika, hadi
kufikia Machi 2015, Ofisi kuu Pemba
imeweza kutekeleza yafuatayo katika
malengo iliyopanga:-
91.
Mheshimiwa Spika, ziara
zote za Mheshimiwa Makamu wa Kwanza wa Rais huko Pemba na ziara mbili za Kamati
ya Kudumu ya Baraza la Wawakilishi ya kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa
Kitaifa zimeratibiwa. Ziara hizo
zimeweza kuishauri Ofisi juu ya utekelezaji wa majukumu yake pamoja na kukagua
shughuli mbalimba zinazofanywa na jamii.
92.
Mheshimiwa Spika, katika
jitihada za kupunguza athari za uharibifu wa mazingira, ziara nane za ukaguzi
zimefanywa kwenye maeneo yanayotumika kwa uchukuaji wa maliasili zisizorejesheka
kama vile mchanga, mawe na kifusi. Maeneo yaliyokaguliwa ni Ging’ingi, Mwambe,
Mkanyageni, Kiungoni, Ole, Pujini, Uwandani na Mvumoni Tundauwa.
93.
Mheshimiwa Spika, katika
kuwajengea uwezo wafanyakazi gharama za mafunzo ya usimamizi wa mazingira
zimelipiwa kwa mfanyakazi mmoja anayesoma katika chuo kikuu cha Dodoma ngazi ya
shahada ya pili (Angalia
Kiambatanisho Nam. 1). Hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za kukuza na kuimarisha ufanisi wa kiutendaji.
94.
Mheshimiwa
Spika, katika
kuimarisha mazingira ya utendaji kazi, jengo la Idara ya Mazingira Pemba
limeezekwa. Ofisi Kuu Pemba pia imeweza
kununua gari na vifaa mbali mbali kwa ajili ya matumizi ya Ofisi.
95.
Mheshimiwa Spika,
Ofisi Kuu Pemba kwa mwaka wa fedha 2014/15 iliidhinishiwa kutumia TZS 369,575,000/-. Kati ya fedha hizo, TZS 159,575,000/- kwa ajili ya matumizi mengineyo, na TZS 210,000,000/- kwa ajili ya
mishahara. Hadi kufikia Machi, 2015
Ofisi Kuu Pemba ilikwisha kuingiziwa TZS
251,169,450/- zikiwemo TZS
77,100,000/- sawa na asilimia 48 kwa
matumizi mengineyo, na TZS 174,069,450/-
kwa mishahara ambazo ni sawa na asilimia 83.
TUME
YA KITAIFA YA KURATIBU NA UDHIBITI WA DAWA ZA KULEVYA
96.
Mheshimiwa Spika, Tume
ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya ina jukumu la kuratibu mapambano dhidi ya
matumizi, biashara na usafirishaji wa
dawa za kulevya kwa kushirikiana na wadau mbali mbali, kutoa taaluma kwa
jamii juu ya athari ya dawa za kulevya na kutoa huduma za tiba na ushauri nasaha kwa watumiaji wa dawa za
kulevya.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Tume ya Kitaifa ya
Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za kulevya ilipanga kutekeleza malengo yafuatayo:-
- Kupunguza matumizi ya dawa za kulevya.
- Kupunguza usafirishaji na usambazaji wa Dawa za
Kulevya.
- Kuweka mazingira bora ya
kazi na kuleta ufanisi katika mapambano dhidi
ya
dawa za kulevya.
97.
Mheshimiwa Spika, hadi
kufikia Machi 2015, Tume ya Kitaifa ya
Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za kulevya imeweza kutekeleza yafuatayo katika malengo
iliyopanga:-
98.
Mheshimiwa Spika, jumla ya vipindi viwili vya redio vimerushwa kupitia
ZBC Redio kwa lengo la kuelimisha jamii juu ya athari ya Dawa za Kulevya. Ziara
za utoaji taaluma kuhusu athari ya Dawa za kulevya zimefanywa kwenye skuli 42 (Angalia Kiambatanisho Nam. 6) ambapo wanafunzi 2,806 (1,716 wanawake; 1,090 wanaume) walipatiwa
taaluma hiyo. Vile vile, ziara kama hizo zimefanyika kwa Shehia 39 Unguja na
Pemba. Aidha, nyumba kumi (10) za
makaazi ya vijana walioacha matumizi ya Dawa za Kulevya zimepatiwa ruzuku (Angalia Kiambatanisho Nam. 7) ambapo viongozi wa nyumba
hizo walifanyiwa mikutano ya kupewa
taaluma juu ya ugawaji wa vifaa vya
kutendea kazi vilivyotoka Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Kudhibiti Dawa za
Kulevya (UNODC).
99.
Mheshimiwa Spika, katika
kupunguza usafirishaji na usambazaji wa dawa za Kulevya, Tume imetoa mafunzo ya
sheria ya dawa za Kulevya kwa taasisi za Serikali za Unguja na Pemba zikiwemo Polisi, waendesha mashtaka, Mahakimu,
Watumishi wa Uwanja wa ndege, Bandari, TRA, Mkemia, ZRB na Taasisi ya Kupambana
na Kuzuwia Rushwa. Mafunzo hayo yalikuwa na lengo la kujadili mwenendo na
changamoto wa kesi za dawa za kulevya na kuimarisha mahusiano ya kisekta.
100. Mheshimiwa Spika, mkakati wa pamoja kati ya viongozi wa Tume, Wilaya,
Shehia na wadau wengine juu ya kudhibiti uingizaji, usambazaji na matumizi ya
Dawa za Kulevya katika Shehia umeandaliwa na utekelezaji wake umepelekea
kuvunjwa kwa vijiwe na kusambaratisha maeneo
yanayofanyiwa biashara ya dawa za kulevya yaliyomo kwenye shehia husika na kuunda kamati za
Udhibiti wa Dawa za Kulevya za Shehia.
Pia Kikao kimoja kimefanyika ili kutathmini na kujadili changamoto na mafanikio
mbalimbali yaliyojitokeza katika kufanikisha kazi ya uratibu na udhibiti wa
dawa za kulevya.
101. Mheshimiwa Spika, wafanyakazi
watano wamepatiwa mafunzo ya muda mfupi ya utunzaji wa kumbukumbu na mfanyakazi
mmoja amelipiwa sehemu ya gharama za mafunzo ya utawala shahada ya pili.
102. Mheshimiwa Spika, Tume
ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya kwa mwaka wa fedha
2014/15 iliidhinishiwa kutumia jumla ya TZS
364,000,000/-. Kati ya fedha hizo, TZS 220,000,000/- kwa ajili ya matumizi
mengineyo, na TZS 144,000,000/- kwa
ajili ya mishahara. Hadi kufikia Machi,
2015 Tume ilikwisha kuingiziwa TZS
269,920,950/- zikiwemo TZS
162,138,000/- kwa matumizi mengineyo ambazo ni sawa na asilimia 74, na TZS 107,782,950/- kwa mishahara ambazo ni sawa na asilimia 75.
TUME
YA UKIMWI
103. Mheshimiwa Spika, majukumu
makuu ya Tume ya UKIMWI ni kuhakikisha kwamba sera na mikakati ya taifa ya
kupiga vita UKIMWI zinatayarishwa na
kutekelezwa, kutafuta rasilimali zitakazotumika katika utekelezaji wa Muitiko
wa Kitaifa wa Kupambana na UKIMWI, kuimarisha uwezo wa wadau katika kufanyia
kazi programu za UKIMWI na kuratibu shughuli zao, kushajihisha utoaji wa huduma za tiba na matunzo kwa watu walioathirika na
kuathiriwa, kufuatilia na kutathmini umakini na ufanisi wa utekelezaji wa
mikakati, sera na muitiko wa kitaifa na kutoa taarifa zote zinazohusiana
na UKIMWI.
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Tume ya UKIMWI ilipanga
kutekeleza malengo yafuatayo:-
- Kuongoza, kuratibu na kusimamia utekelezaji wa Sera, Sheria na Mkakati
wa pili wa Kitaifa wa UKIMWI kwa
wadau wote.
- Kuimarisha ubora wa taarifa
zinazokusanywa pamoja na kufuatilia matumizi ya taarifa zinazotokana
na ufuatiliaji, tathmini na utafiti wa pgrogramu za UKIMWI.
- Kutoa miongozo na kuratibu
masuala ya habari, utetezi na mawasiliano kuhusu UKIMWI ili kuchochea mabadiliko ya tabia katika jamii na
makundi maalumu.
- Kuongoza pamoja
kuimarisha mazingira mazuri
ya kazi na wafanyakazi wa Tume
kwa ajili ya kuleta ufanisi
katika shughuli za uratibu wa masuala ya UKIMWI.
104.
Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Machi 2015 Tume ya UKIMWI imeweza kutekeleza yafuatayo katika malengo
iliyopanga:-
105.
Mheshimiwa Spika, katika kukuza mawasiliano na habari, nakala 5,000 za Toleo la 18 na 5,000 toleo la 19 la
Jarida la JIHADHARI lenye ujumbe tofauti wa mapambano dhidi ya UKIMWI
zimechapishwa na kusambazwa kwa wadau mbalimbali.
106.
Mheshimiwa
Spika, katika kutekeleza
Mkakati wa Pili wa Taifa wa UKIMWI (Zanzibar National Strategic Plan – ZNSP
II), Tume imeiwezesha kifedha Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana
Wanawake na Watoto kwa ajili ya
kutayarisha mpango wa utekelezaji (operational plan) wa miaka miwili (2015 –
2016) ambao utawezesha kutekeleza programu ya kuzuia udhalilishaji wa kijinsia (Gender Based Violence – GBV).
107.
Mheshimiwa Spika, jumla ya watu 756 walio katika makundi maalumu wameweza
kufikiwa na kupatiwa ushauri nasaha (342 wanaotumia dawa za kulevya, watu 6
wanaotumia dawa za kulevya kwa njia ya kujidunga, 389 dada-poa na 19
kaka-poa). Miongoni mwao 138 waliweza
kupima VVU ambapo watano (5) kati yao (3 w’me na 2 w’ke) waligundulika kuishi
na VVU. Aidha, watu 62 walipatiwa rufaa
na kupelekwa katika vituo vya tiba kwa uchunguzi zaidi.
108.
Mheshimiwa Spika, jumla ya vipeperushi 4,200 vimechapishwa na kusambazwa
kwa waliofikiwa kupitia mikutano 16 iliyofanyika (Unguja 8 na Pemba 8).
109.
Mheshimiwa
Spika, Zanzibar
tumeungana na nchi nyengine Duniani kuadhimisha
Siku ya UKIMWI ambayo ni tarehe 1 Disemba ya kila mwaka. Maadhimisho hayo yalifanyika kijiji cha Machomane, Wilaya ya Chake-Chake Pemba ambapo shughuli
mbalimbali za kilele zilifanyika ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha jamii juu ya
mapambano ya UKIMWI.
110.
Mheshimiwa Spika, wafanyakazi watano wamelipiwa gharama za masomo katika
ngazi ya shahada ya pili na stashahada
katika fani tofauti. Wafanyakazi
wawili wamepatiwa mafunzo ya muda
mfupi juu ya ufuatiliaji na tathmini (Angalia Kiambatanisho Nam. 1). Aidha, safari 6 za ndani za ufuatiliaji zimefanyika
ambazo zimeongeza uratibu na ufanisi wa kazi za Tume.
111. Mheshimiwa Spika,
kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Tume ya UKIMWI iliidhinishiwa kutumia jumla ya TZS 811,000,000/-.
Kati ya fedha hizo, TZS 533,208,700/-
kwa ajili ya matumizi mengineyo, na TZS
277,791,300/- kwa ajili ya mishahara.
Hadi kufikia Machi, 2015 Tume ya UKIMWI ilikwisha kuingiziwa TZS 503,194,400/-. Kati ya hizo TZS 258,789,946/- sawa asilimia 49 kwa ajili ya matumizi mengineyo, na TZS 244,404,454/- sawa asilimia
88 kwa ajili ya mishahara.
UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO
112.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015 Tume ya UKIMWI ilitekeleza kazi mbalimbali zilizopatiwa
fedha na Washirika wa Maendeleo. Fedha hizo ni kutoka UNFPA, UNDP na UNICEF. Shughuli zilizotekelezwa kupitia fedha
hizo ni kama zifuatazo:-
a) Utekelezaji
wa kazi zilizofadhiliwa na UNFPA
113.
Mheshimiwa Spika, mikutano miwili ya wadau wa sheria kutoka taasisi mbali
mbali imefanyika kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kutetea masuala ya mapambano
juu ya udhalilishaji wa kijinsia na kukinga maambukizi mapya ya UKIMWI na
kuangalia mapungufu yaliyopo kiutekelezaji, kutoa mapendekezo na kuwezesha
matumizi mazuri ya sheria zilizopo.
114.
Mheshimiwa Spika, katika kupunguza vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa
kijinsia, Tume imefanya mikutano 4 kwa viongozi wa dini yenye jumla ya
washiriki 80 (40 Unguja, 40 Pemba) ambao walihamasishwa juu ya mbinu bora za
kukinga na kudhibiti maambukizi ya
UKIMWI kwa vijana pamoja na kupunguza vitendo vya ubakaji na
udhalilishaji wa kijinsia.
115. Mheshimiwa Spika, katika
kufanya uhamasishaji katika jamii juu ya kupinga vitendo vya udhalilishaji kwa
wanawake na watoto na kuimarisha mapambano dhidi ya UKIMWI, maigizo19
yalifanyika katika shehia 19 Unguja na Pemba.
Kwa Unguja Shehia hizo ni 10 ambazo ni Bumbwini Kiongwe, Mafufuni,
Nyamanzi, Pwani Mchangani, Unguja Ukuu Kaebona, Kiwengwa, Mpapa, Chukwani
(buyu), Unguja Ukuu Tindini na Mbuzini.
Kwa Pemba Shehia hizo ni 9 ambazo ni Wambaa, Wesha, Chumbageni, Pujini
Dodo, Chachani, Bopwe, Mchangamdogo, Mzambarauni, Pujini Kibaridi. Jumla ya
wananchi 1,592 kutoka Shehia kumi za Unguja wamefikiwa, kati ya hao 650 ni
wanaume na 942 ni wanawake. Aidha, jumla ya wananchi 2,250 kutoka Shehia tisa
za Pemba wamefikiwa kati ya hao 900 ni wanaume na 1350 ni wanawake.
116. Mheshimiwa Spika, katika
kuwasaidia watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI, vikundi vitano (3 Unguja na 2 Pemba) vya ujasiriamali vya wanawake
wanaoishi na virusi vya UKIMWI vimepatiwa fedha na missada mbalimbali kwa ajili
ya kujiendeleza (Angalia Kiambatanisho
Nam. 8).
117. Mheshimiwa Spika, jumuiya
ya ZAYEDESA imepatiwa msaada wa kuimarisha kituo cha huduma rafiki cha vijana
kilichoko Mkoani Pemba. Baada ya kuimarishwa kituo hicho, jumuiya hiyo imeweza
kuwatumia waelimishaji rika wake katika kuwafikia walio katika makundi maalum
17 (dada poa 11, kaka poa 3 na watumiaji wa dawa za kulevya 3).
118. Mheshimiwa Spika, kupitia
mikusanyiko ya kidini yenye lengo la kuimarisha maadili mema na kurekebisha
tabia ili kuweza kujikinga na maambukizo mapya ya UKIMWI pamoja na kupunguza
vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia, Tume imeiwezesha Jumuiya ya Maimamu
Zanzibar (JUMAZA) kufanya ziara 9 (5 Unguja na 4 Pemba) za uhamasishaji ambapo
wanashehia 270 Unguja na 214 kwa Pemba waliweza kufikiwa.
119. Mheshimiwa Spika, Vilevile
vipindi 5 vya redio (3 ZBC na 2 redio Adhana) vilitayarishwa na kurushwa hewani
kwa ajili ya kutoa elimu ya mwitiko wa taifa wa mapambano dhidi ya UKIMWI.
120. Mheshimiwa Spika, mikutano
2 ya uratibu (1 Unguja na 1 Pemba) iliyowashirikisha viongozi wa dini (kiislamu
na kikiristo) iliyolenga kukemea vitendo vya udhalilishaji na unyanyasaji
ilifanyika. Jumla ya viongozi wa kidini 50 (25 Unguja na 25 Pemba) walishiriki.
121. Mheshimiwa Spika, shehia 20 (Unguja 9, Pemba 11) zinazotekeleza mpango
shirikishi wa kuziwezesha jamii (community capacity enhancement) zimefanyiwa
ufuatiliaji. Shehia hizo kwa Pemba ni
Kiwani, Makombeni, Michezani, Chonga, Vitongoji, Nawara, Kiuyu Kigongoni,
Msuka, Tumbe Mashariki, Tumbe Magharibi na Kizimbani. Kwa upande wa Unguja Shehia hizo ni Tumbatu
Jongowe, Tumbatu Uvivini, Tumbatu Gomani, Kiboje, Mkwajuni, Koani, Malindi,
Mlandege na Nungwi.
b) Utekelezaji
wa kazi zilizofadhiliwa na UNDP
122.
Mheshimiwa Spika, mkutano mmoja wenye washiriki 40 kutoka kamati za UKIMWI
za shehia, sekta kuu za Serikali, taasisi za kisheria, taasisi za kiraia,
makundi maalum na taasisi za watu wenye ulemavu ulifanyika Pemba kwa lengo la
kuhakikisha ufanisi katika kuongeza uwezo wa programu za habari utetezi na
mawasiliano kwa kuchochea mabadiliko ya tabia katika masuala ya UKIMWI.
123.
Mheshimiwa Spika, mikutano miwili ya uratibu imeandaliwa (1 Unguja na 1
Pemba). Jumla ya washiriki 40 (20 Unguja na 20 Pemba) walishiriki katika
mikutano hiyo ambao ni waratibu wa shughuli za UKIMWI katika ngazi za wilaya,
sekta kuu za Serikali, jumuiya na sekta binafsi katika mapambano dhidi ya
UKIMWI (ABCZ), Jumuiya ya Watu wanaoishi na VVU, taasisi za kiraia, mtandao wa
waelimishaji rika katika makundi maalum.
c) Utekelezaji
wa kazi zilizofadhiliwa na UNICEF
124. Mheshimiwa
Spika, Tume ya UKIMWI
ilifanya ziara za kuwapitia wadau wanaofanyakazi na makundi maalum kwa lengo la
kutambua shughuli wanazofanya na changamoto wanazokabiliana nazo na kusaidia
kupata ufumbuzi. Miongoni mwa taasisi
zilizotembelewa ni pamoja na kanisa la Anglikana, nyumba
ya wanawake ya makaazi ya vijana
walioacha matumizi ya dawa za kulevya, watu
waliokuwa wakitumia dawa za kulevya na wamepata nafuu (Zanzibar recovery
community), mtandao wa watu walio katika makundi maalumu (Key Population
Network), mkusanyiko wa vijana wa Zanzibar kwa ajili ya kupambana na UKIMWI
(Zanzibar Youth Forum), na jumuiya ya kidini ya mapambano dhidi ya UKIMWI
(ZEYADA). Aidha mkutano wa robo mwaka kwa wadau wanaofanyakazi na makundi
maalum ulifanywa kutathmini mafanikio na changamoto mbali mbali wanazokabiliana
nazo na namna wanavyozitatua.
125.
Mheshimiwa Spika, zoezi la kuzitambua na kuzifanyia uhakiki asasi za kiraia
zinazowalenga vijana katika maeneo ya UKIMWI na Afya ya uzazi limefanyika kwa
Unguja na Pemba. Jumla ya asasi za kiraia 68 (Unguja 51, Pemba 17)
zimetambuliwa na kati ya hizo asasi 36
tu ndio zimeonekana kuwa na uwezo wa kufanyakazi kitaalamu.
126. Mheshimiwa Spika,
kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Tume ya UKIMWI iliidhinishiwa kutumia jumla ya TZS 1,369,000,000/-
kutoka kwa Washirika wa Maendeleo. Hadi
kufikia Machi, 2015 Tume ya UKIMWI ilikwisha kuingiziwa TZS 633,427,500/-
sawa na asilimia 46.
127. Mheshimiwa Spika,
kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Tume ya UKIMWI iliidhinishiwa kutumia TZS 50,000,000/-
ikiwa ni mchango wa Serikali katika kazi za maendeleo. Hadi kufikia Machi, 2015 hakuna fedha
zilizopatikana.
MALENGO
YA OMKR KWA MWAKA 2015/2016
128. Mheshimiwa Spika,
kama ilivyokwishaelezwa kuwa kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Serikali inaendelea
kutekeleza mageuzi ya mfumo wa bajeti kutoka katika bajeti inayotumia vifungu
(line item) kwenda katika mfumo unaotumia programu (Program Based Budget –
PBB).
129. Mheshimiwa Spika,
Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kwa mwaka 2015/2016 inakusudia kufanikisha
utekelezaji wa majukumu yake kupitia Programu kuu saba (7) zifuatazo:-
A. Programu ya Usimamizi wa
Mazingira na Mabadiliko ya tabianchi;
B. Programu
ya Usimamizi wa masuala ya Watu wenye Ulemavu;
C. Programu
ya Mipango na Utawala;
D.
Programu ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya;
E.
Programu ya Mipango na Utawala wa Tume ya Kitaifa ya Kuratibu; Udhibiti
wa Dawa za Kulevya;
F.
Programu ya Kuratibu Muitiko wa Taifa wa UKIMWI; na
G.
Programu ya Mipango na Utawala wa Tume ya UKIMWI
(Angalia Kiambatanisho Nam. 9).
- PROGRAMU YA
USIMAMIZI WA MAZINGIRA NA MABADILIKO YA TABIANCHI
130.
Mheshimiwa
Spika, programu
hii itatekelezwa kupitia programu ndogo mbili (2) na matarajio yake ya muda
mrefu ni kuimarisha usimamizi wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi.
A.1. Programu ndogo ya
Usimamizi wa Mazingira
131.
Mheshimiwa
Spika, programu
hii ndogo ina lengo kuu la kufikia mazingira endelevu ambapo huduma
zinazotarajiwa kutolewa ni kuendeleza mazingira endelevu kwa jamii pamoja na
kukuza uelewa wa jamii juu ya usimamizi wa mazingira.
132. Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji wa programu hii ndogo
yatapimwa kutokana na idadi ya kanuni na
miongozo ya usimamizi wa mazingira itakayotayarishwa; idadi ya mikutano ya
kimataifa ya mazingira itakayohudhuriwa; idadi ya miradi ya wahisani
itakayoanzishwa; idadi ya misaada ya kitaalamu itakayopatikana; idadi ya
operesheni za kimazingira zitakazofanywa; idadi ya ziara za ufuatiliaji na
ukaguzi wa kimazingira zitakazofanywa; idadi ya miradi itakayokaguliwa; idadi
ya miradi itakayofanyiwa tathmini ya athari za kimazingira; idadi ya miradi itakayofanyiwa
ukaguzi wa kimazingira; idadi ya vipindi vya radio na vipindi vya TV
vitakavyorushwa; idadi ya vipeperushi na vijarida vilivyotayarishwa na
kusambazwa; pamoja na idadi ya mikutano ya uhamasishaji itakayofanyika
133. Mheshimiwa
Spika, utekelezaji
wa Programu hii ndogo ya Usimamizi wa Mazingira utafanywa kwa pamoja kati ya Idara ya Mazingira na
Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (Zanzibar Environmental Management
Auhtority – ZEMA).
134. Mheshimiwa
Spika, programu hii
ndogo inakadiriwa kutumia jumla ya TZS 174,076,000/- kutoka Serikalini.
A.2. Programu ndogo ya
Usimamizi wa Mabadiliko ya Tabianchi
135. Mheshimiwa Spika, programu hii ndogo ina lengo kuu la kuratibu na
kusimamia masuala ya
mabadiliko ya tabianchi ambapo huduma zinazotarajiwa kutolewa ni kutayarisha nyenzo na mipango ya
usimamizi, kuratibu mikutano ya usimamizi, kujenga uwezo wa wadau, kukuza
uelewa juu ya athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na kuzisaidia jamii
katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
136.
Mheshimiwa
Spika, matokeo
ya utekelezaji wa programu hii ndogo yatapimwa kutokana na kuwepo kwa mpango
kazi wa utekelezaji wa Mkakati wa Mabadiliko ya tabianchi utakaotayarishwa,
kuwepo kwa utaratibu maalumu wa kifedha kwa ajili ya kugharamia masuala ya
mabadiliko ya tabianchi utakaoandaliwa,
kuwepo kwa mfumo wa utayarishaji wa mipango wa kijamii ya kuhimili
athari za mabadiliko ya tabianchi utakaotayarishwa, idadi ya maeneo yaliyoathiriwa na mabadiliko ya
tabianchi yatakayoendelezwa, idadi ya taasisi zitakazosaidiwa kuingiza
mazingira na mabadiliko ya tabianchi kwenye programu za taasisi hizo, idadi ya
taasisi zitakazosaidiwa kuanzisha vitengo vya mazingira na mabadiliko ya
tabianchi kwenye taasisi hizo, idadi ya mikutano ya Kamati za mabadiliko ya
tabianchi itakayofanyika, idadi ya wafanyakazi watakaosaidiwa kushiriki mafunzo
mafupi na mikutano ya kimataifa ya mabadiliko ya tabianchi, idadi ya mikutano,
vipeperushi na programu za TV na redio za kuelimisha jamii na wadau juu ya
masuala ya mabadiliko ya tabianchi zitakazotayarishwa na idadi ya majiko sanifu
yatakayotengenezwa na kutumika.
137.
Mheshimiwa
Spika, utekelezaji
wa Programu hii ndogo ya Usimamizi wa Mabadiliko ya Tabianchi utafanywa na Idara ya Mazingira,
Wizara ya Kilimo na Maliasili kupitia Idara ya Misitu na Maliasili
zisizorejesheka, Wizara Fedha kupitia Idara ya Fedha za Nje, Wizara ya Ardhi,
Makaazi, Maji na Nishati kupitia Idara ya Nishati na Madini na Jumuiya ya Maendeleo
ya Jamii na Uhifadhi wa Mazingira Zanzibar (COmmunity Deverlopment and
Environmental COnservation in Zanzibar CODECOZ) na utaratibiwa na Idara ya Mipango, Sera na
Utafiti.
138. Mheshimiwa
Spika, programu hii
ndogo inakadiriwa kutumia jumla ya TZS 450,000,000/- kutoka kwa
Washirika wa Maendeleo.
139.
Mheshimiwa
Spika,
naliomba Baraza lako kuidhinisha jumla ya TZS 624,076,000/- kwa ajili ya utekelezaji wa Programu hii ya
Usimamizi wa Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi. Kati ya hizo TZS 174,076,000/- kutoka Serikalini na TZS 450,000,000/- kutoka
kwa Washirika wa Maendeleo.
- PROGRAMU
YA USIMAMIZI WA MASUALA YA WATU WENYE ULEMAVU
140.
Mheshimiwa
Spika, programu
hii itatekelezwa kupitia programu ndogo moja (1) na matarajio yake ya muda
mrefu ni kuimarisha ujumuishaji wa mahitaji ya Watu wenye Ulemavu katika Sera,
Sheria na Mipango mbalimbali.
B.1. Programu ndogo ya Usimamizi wa Masuala ya Watu
wenye Ulemavu
141. Mheshimiwa Spika, programu hii ndogo ina lengo kuu la kuhakikisha
upatikanaji wa haki na fursa sawa kwa Watu wenye Ulemavu. Huduma zinazotarajiwa
kutolewa ni kutetea ujumuishwaji wa Watu wenye Ulemavu; kukuza uelewa wa jamii
juu ya masuala ya watu wenye ulemavu pamoja na uwezeshaji wa Watu wenye
Ulemavu.
142. Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji wa programu hii ndogo
yatapimwa kutokana na sheria itakayofanyiwa
mapitio; idadi ya nakala za sheria zitakazo chapishwa na kusambazwa; idadi ya
miongozo na kanuni zitakazotayarishwa; idadi ya mikutano ya Baraza la Taifa la
Watu wenye Ulemavu; idadi ya mikutano ya waratibu wa masuala ya watu wenye
ulemavu; idadi ya vipindi vya radio na vipindi vya TV; idadi ya mikutano ya
uhamasishaji; idadi ya Watu wenye Ulemavu
waliopatiwa visaidizi na dawa; idadi ya jumuiya za Watu wenye Ulemavu
zitakazosaidiwa; pamoja na idadi ya vikundi vya ujasiriamali vya Watu wenye
Ulemavu vitakavyosaidiwa.
143.
Mheshimiwa
Spika, programu hii
ya Usimamizi wa Masuala ya Watu
wenye Ulemavu inakadiriwa
kutumia jumla ya TZS 155,460,000/- kutoka Serikalini, na utekelezaji
wake utafanywa na Idara ya Watu
wenye Ulemavu. Hivyo, naliomba Baraza
lako kuidhinisha jumla ya TZS
155,460,000/- kwa ajili ya utekelezaji wa Programu hii.
- PROGRAMU
YA MIPANGO NA UTAWALA
144.
Mheshimiwa
Spika, programu
hii itatekelezwa kupitia programu ndogo tatu (3) na matarajio yake ya muda
mrefu ni kuimarisha ufanisi na ubora katika utoaji wa huduma katika OMKR.
C.1. Programu ndogo ya Uongozi na Utawala
145. Mheshimiwa Spika, programu hii ina lengo kuu la
kuratibu shughuli za uongozi na rasilimali watu ambapo huduma zinazotarajiwa
kutolewa ni kuimarisha ufanisi wa utendaji kazi
na uongozi; kuisaidia jamii katika kazi za maendeleo pamoja kuongeza uelewa wa
jamii juu ya masuala yanayosimamiwa na OMKR.
146. Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji wa programu hii yatapimwa
kutokana na asilimia
ya utekelezaji wa mpango wa manunuzi; idadi ya wafanyakazi waliopatiwa mafunzo;
asilimia ya mahudhurio kazini; idadi ya wafanyakazi waliopatiwa stahiki; idadi
ya vikundi vilivyopatiwa msaada; idadi ya mikutano na waandishi wa habari
(press conference) na idadi ya vipindi vya redio na vipindi vya TV.
147. Mheshimiwa
Spika, utekelezaji
wa Programu hii ndogo ya Uongozi na Utawala utafanywa na Idara ya Uendeshaji na Utumishi pamoja na
Ofisi ya Faragha.
148. Mheshimiwa
Spika, programu hii
ndogo inakadiriwa kutumia jumla ya TZS 2,051,997,000/- kutoka
Serikalini.
C.2. Programu ndogo ya Mipango, Sera na Utafiti
149. Mheshimiwa Spika, programu hii lengo kuu ni kuongeza
ufanisi wa utekelezaji wa Sera, Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini kwa masuala
yanayosimamiwa na OMKR ambapo huduma zinazotarajiwa kutolewa ni kuimarisha
mfumo wa upatikanaji taarifa na kuzisambaza kwa wadau; kuratibu masuala
mtambuka yanayosimamiwa na OMKR; na kutayarisha sera, mipango na bajeti za
OMKR.
150. Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji wa programu hii ndogo
yatapimwa kutokana na idadi ya tafiti zitakazofanywa; idadi ya
nakala za ripoti za utafiti zitakazochapishwa; idadi ya mikutano ya kuwasilisha
taarifa za utafiti kwa wadau; idadi ya taasisi zenye mpango wa kujumuisha mambo
mtambuka; idadi ya mikutano ya uratibu wa masuala mtambuka; idadi ya mikutano
ya ufuatiliaji na tathmini; hotuba ya bajeti na Mfumo wa Matumizi wa Muda wa
Kati (MTEF) itakayotayarishwa; na idadi ya nakala za sera ya Watu wenye Ulemavu
zitakazochapishwa.
151. Mheshimiwa
Spika, utekelezaji
wa Programu ndogo ya Mipango, Sera na Utafiti utafanywa na Idara ya Mipango, Sera na
Utafiti.
152. Mheshimiwa
Spika, programu hii
ndogo inakadiriwa kutumia jumla ya TZS 93,719,000/- kutoka Serikalini.
C.3. Programu ndogo ya Uratibu wa masuala ya OMKR
Pemba
153. Mheshimiwa Spika, programu hii lengo lake kuu ni kuratibu
shughuli za uongozi, rasilimali watu na shughuli za Mheshimiwa Makamu wa Kwanza
wa Rais Pemba ambapo huduma zinazotarajiwa kutolewa ni uimarishaji
wa ufanisi wa utendaji kazi na uongozi pamoja na kuratibu, kufuatilia na kukuza
mashirikiano kwa masuala ya OMKR Pemba.
154. Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji wa programu hii ndogo
yatapimwa kutokana na asilimia ya utekelezaji
wa mpango wa manunuzi; idadi ya wafanyakazi watakaopatiwa mafunzo; asilimia ya
mahudhurio kazini; idadi ya wafanyakazi watakaopatiwa stahiki; na idadi ya
ziara za vijijini (field visits) zitakazofanywa kufuatilia shughuli za Ofisi ya
Makamu wa Kwanza wa Rais.
155. Mheshimiwa
Spika, utekelezaji
wa Programu hii ndogo utafanywa na Ofisi Kuu Pemba.
156. Mheshimiwa
Spika, programu hii
ndogo inakadiriwa kutumia jumla ya TZS 448,148,000/- kutoka Serikalini.
157. Mheshimiwa
Spika, naliomba
Baraza lako kuidhinisha jumla ya TZS 2,593,864,000/- kwa ajili ya
utekelezaji wa Programu hii ya Mipango na Utawala wa OMKR.
- PROGRAMU YA
UDHIBITI WA DAWA ZA KULEVYA
158.
Mheshimiwa
Spika, programu
hii itatekelezwa kupitia programu ndogo mbili (2) na matarajio yake ya muda
mrefu ni kuiwezesha jamii kuwa huru na athari ya dawa za kulevya.
D.1. Programu ndogo ya Uratibu wa Udhibiti wa
Usafirishaji na Usambazaji wa dawa za kulevya
159. Mheshimiwa Spika, programu hii ndogo ina lengo kuu la kuzuia
uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa dawa za kulevya ambapo huduma
zinazotarajiwa kutolewa ni kudhibiti uingizaji na usafirishaji wa dawa za
kulevya pamoja na kuzuia usambazaji wa dawa za kulevya.
160. Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji
wa programu hii ndogo yatapimwa kutokana na kuwepo muongozo wa utoaji taarifa;
idadi ya mikutano ya kuhamasisha jamii; na idadi ya operesheni zitakazofanyika
na maeneo yanayofanyiwa biashara ya dawa za kulevya yatakayosambaratishwa.
161. Mheshimiwa
Spika, programu hii
ndogo inakadiriwa kutumia jumla ya TZS 57,814,000/- kutoka Serikalini.
D.2. Programu ndogo ya Kinga ya msingi ya Mahitaji na
Matumizi ya Dawa za Kulevya
162. Mheshimiwa Spika, programu hii ndogo ina
lengo kuu la kupunguza tatizo la utegemezi wa dawa za kulevya katika jamii
ambapo huduma zinazotarajiwa
kutolewa ni uhamasishaji wa jamii juu ya athari
ya dawa za kulevya pamoja na kuzijengea uwezo nyumba za upataji nafuu.
163. Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji wa programu
hii ndogo yatapimwa kutokana na idadi ya skuli, taasisi za binafsi na za
Serikali zilizofikiwa; idadi ya nyumba zilizosaidiwa na idadi ya waliofaidika
na programu za ujasiriamali.
164. Mheshimiwa
Spika, programu hii
ndogo inakadiriwa kutumia jumla ya TZS 33,250,000/- kutoka Serikalini.
165. Mheshimiwa
Spika, utekelezaji
wa Programu ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya utaratibiwa na Tume
ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya, naliomba Baraza lako
kuidhinisha jumla ya TZS
TZS 91,064,000/- kwa ajili ya utekelezaji
wa Programu hii ya Udhibiti wa dawa za kulevya.
- PROGRAMU YA MIPANGO NA UTAWALA WA TUME YA KITAIFA YA KURATIBU NA
UDHIBITI WA DAWA ZA KULEVYA
166.
Mheshimiwa
Spika, programu
hii itatekelezwa kupitia programu ndogo mbili (2) na matarajio yake ya muda
mrefu ni kuwezesha mazingira bora ya kazi ndani Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na
Udhibiti wa Dawa za Kulevya.
E.1. Programu ndogo ya Utawala na Uendeshaji wa Tume
ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya
167. Mheshimiwa Spika, programu hii ndogo
ina lengo kuu la kuongeza uwezo wa kufanya kazi na kuweka mazingira mazuri ya
kazi ambapo huduma
zinazotarajiwa kutolewa ni kujenga uwezo wa
wafanyakazi katika uratibu wa mapambano ya dawa za kulevya.
168. Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji wa
programu hii ndogo yatapimwa kutokana na asilimia ya utekelezaji wa mpango
mkakati wa Tume; idadi ya wafanyakazi waliopatiwa mafunzo ndani ya kazi pamoja
na asilimia ya bajeti ya utekelezaji wa mipango ya Tume.
169. Mheshimiwa
Spika, utekelezaji
wa Programu hii ndogo utafanywa na Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na
Udhibiti wa Dawa za Kulevya.
170. Mheshimiwa
Spika, programu hii
ndogo inakadiriwa kutumia jumla ya TZS 304,690,000/- kutoka Serikalini.
E.2.
Programu ndogo ya Uratibu wa masuala ya Dawa za kulevya Pemba
171. Mheshimiwa Spika, programu hii ndogo
ina lengo kuu la kuongeza uwezo wa kufanya kazi na kuweka mazingira mazuri ya
kazi ambapo huduma
zinazotarajiwa kutolewa ni uratibu wa shughuli
za Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya kisiwani Pemba.
172. Mheshimiwa
Spika, utekelezaji
wa Programu hii ndogo utafanywa na Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na
Udhibiti wa Dawa za Kulevya ofisi ya Pemba na inakadiriwa kutumia jumla ya TZS 71,346,000/- kutoka Serikalini.
173. Mheshimiwa
Spika, naliomba Baraza lako
kuidhinisha jumla ya TZS
376,036,000/- kwa ajili utekelezaji wa Programu hii ya Mipango na Utawala
wa Tume Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya.
- PROGRAMU YA
KURATIBU MUITIKO WA TAIFA WA UKIMWI
174.
Mheshimiwa
Spika, programu
hii itatekelezwa kupitia programu ndogo mbili (2) na matarajio yake ya muda
mrefu ni kuwezesha kupungua
kwa maambukizi mapya ya VVU katika jamii.
F.1. Programu ndogo ya Mawasiliano na Utetezi.
175. Mheshimiwa Spika, programu hii ndogo
ina lengo kuu la kuimarisha utekelezaji wa mipango ya utetezi na uhamasishaji ili kupunguza
maambukizi mapya ambapo huduma zinazotarajiwa kutolewa ni uhamasishaji
na utetezi ili kupunguza mazingira ya hatari ya kuambukizwa VVU na kuchochea
mabadiliko ya tabia kwa makundi maalum na jamii.
176. Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji wa
programu hii ndogo yatapimwa kutokana na idadi ya shehia zitakazofikiwa kwa
njia ya sanaa za maonyesho; idadi ya programu za jamii zitakazofanyika kwa
makundi maalum; idadi ya watu wa makundi maalum watakaofikiwa; idadi ya
vipeperushi na majarida yatakayochapishwa na kusambazwa kwa walengwa; idadi ya
vipindi vya redio na TV vitakavyorushwa; idadi ya mikoa itakayohamasishwa na
kuchukua hatua za kupunguza mazingira hatarishi; idadi ya mikutano ya
kuziratibu taasisi zinazotekeleza
shughuli za utetezi na uhamasishaji; idadi ya taasisi zitakazojengewa uwezo; na
asilimia ya fedha zitakazotolewa kwa utekelezaji wa programu ya stadi za
maisha na afya ya uzazi kwa vijana nje
ya skuli.
177. Mheshimiwa
Spika, utekelezaji wa
Programu hii ndogo utafanywa na Tume ya
UKIMWI, na unakadiriwa kutumia jumla ya TZS 1,034,381,000/-
zikiwemo TZS 51,981,000/-kutoka Serikalini, TZS 932,400,000/- kutoka
kwa washirika wa maendeleo na TZS 50,000,000/- ikiwa ni mchango wa
Serikali katika kazi za maendeleo.
F.2. Programu ndogo ya Uratibu wa muitiko wa
Taifa wa UKIMWI.
178. Mheshimiwa Spika, programu hii ndogo
ina lengo kuu la kuongoza, kuratibu, kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa
miongozo ya kitaifa, sera na sheria ya kukinga na kusimamia masuala ya UKIMWI
ambapo huduma zinazotarajiwa kutolewa
ni utafutaji wa rasilimali kwa ajili ya muitiko wa UKIMWI; kuelimisha jamii juu
ya Sheria ya Kusimamia na Kudhibiti
UKIMWI ya mwaka 2014; kuandaa Mkakati wa Tatu wa Taifa wa UKIMWI; kuongeza
uwezo wa Tume, jamii, wizara na sekta binafsi kupambana na UKIMWI; na kufanya
ufuatiliaji na mikutano ya kuratibu shughuli za UKIMWI kwa sekta za serikali,
wilaya, sekta binafsi, asasi za kiraia na shehia.
179. Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji
wa programu hii ndogo yatapimwa kutokana na kuwepo kwa Mfuko wa Taifa wa
UKIMWI; idadi ya mapendekezo ya miradi; idadi ya vipindi vya redio na TV
vitakavyorushwa; kuwepo Mkakati wa tatu wa Taifa wa UKIMWI; idadi ya shehia
zitakazowezeshwa na zitakazopatiwa mafunzo; idadi ya mikutano ya uhamasishaji
kwa ABCZ; idadi ya wizara zitakazopatiwa muongozo wa kufanya mapitio ya mipango
ya UKIMWI; kuwepo ripoti ya Tathmini ya hali halisi na mahitaji ya huduma za
UKIMWI kwa maeneo ya masoko na usafiri wa daladala; idadi ya mikutano ya
uratibu; kuwepo kwa ripoti ya mwaka ya ufuatiliaji; idadi ya mikutano ya Kamati
ya Kitaalamu ya Ufuatiliaji; kuwepo kwa mpango wa utafiti wa Tume; na idadi ya
wadau wanaotekeleza shughuli za UKIMWI watakaofuatiliwa.
180. Mheshimiwa
Spika, utekelezaji wa
Programu hii ndogo utafanywa na Tume ya
UKIMWI, na unakadiriwa kutumia jumla ya TZS
100,833,000/- kutoka Serikalini.
181. Mheshimiwa
Spika, naliomba Baraza lako
kuidhinisha jumla ya TZS
1,135,214,000/- kwa ajili ya utekelezaji wa Programu hii ya Kuratibu
Muitiko wa Taifa wa UKIMWI, zikiwemo TZS 152,914,000/- kutoka
Serikalini, TZS 932,400,000/- kutoka kwa washirika wa maendeleo na TZS
50,000,000/- ikiwa ni mchango wa Serikali katika kazi za maendeleo.
- PROGRAMU YA
MIPANGO NA UTAWALA WA TUME YA UKIMWI
182.
Mheshimiwa Spika, programu hii itatekelezwa kupitia programu ndogo
mbili (2) na matarajio yake ya muda mrefu ni kuwezesha mazingira bora ya kazi
ndani ya Tume ya UKIMWI Unguja na Pemba.
G.1. Programu ndogo ya Utumishi na
Uendeshaji wa Tume ya UKIMWI
183. Mheshimiwa Spika, programu hii ndogo
ina lengo kuu la kuwa na mazingira wezeshi kwa Tume ya UKIMWI kutimiza majukumu
yake ambapo huduma
zinazotarajiwa kutolewa ni kuweka mazingira
mazuri ya kazi; kujenga uwezo wa wafanyakazi; na kusimamia matumizi mazuri ya
fedha, uwazi na uwajibikaji.
184. Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji wa programu hii ndogo yatapimwa kutokana na asilimia
za utekelezaji wa mpango wa manunuzi na matengenezo ya ofisi yaliyofanyika;
idadi ya wafanyakazi watakaopatiwa mafunzo pamoja na idadi ya wafanyakazi na
familia zao watakaoshiriki Siku ya Afya (wellness program).
185. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Programu hii ndogo utafanywa na Tume
ya UKIMWI na unakadiriwa kutumia jumla ya TZS
383,386,000/-.
G.2.Programu ndogo ya Uratibu wa masuala ya UKIMWI
Pemba.
186. Mheshimiwa Spika, programu hii ndogo lengo lake kuu ni kuratibu shughuli za UKIMWI Pemba kwa wadau wote,
187. Mheshimiwa Spika, matokeo ya utekelezaji wa programu hii ndogo yatapimwa kutokana na idadi ya
mikutano ya uratibu kwa Taasisi za Serikali, taasisi binafsi na Shehia
itakayofanyika, na idadi ya wafanyakazi watakaopatiwa mafunzo.
188. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa
Programu hii ndogo utafanywa na Tume ya UKIMWI ofisi ya Pemba na
unakadiriwa kutumia jumla ya TZS
184,900,000/-.
189. Mheshimiwa
Spika, naliomba Baraza lako
kuidhinisha jumla ya TZS
568,286,000/- kwa ajili ya utekelezaji wa Programu hii ya Mipango na
Utawala wa Tume ya UKIMWI.
SHUKURANI
190. Mheshimiwa Spika, naomba
kukushukuru tena, pamoja na Wajumbe wote wa Baraza lako kwa kunisikiliza kwa
utulivu na umakini wa hali ya juu. Ni dhahiri kwamba mashirikiano yenu, umoja,
upendo na nidhamu ndio siri kubwa ya mafanikio tuliyoyapata.
191. Mheshimiwa Spika, naomba
kuchukuwa nafasi hii kuwashukuru na kuwapongeza Makatibu wote wa Baraza
wakiongozwa na Katibu wa Baraza la Wawakilishi kwa umakini wao katika kulisaidia
Baraza, Kamati za Baraza na Wajumbe wa Baraza katika kutekeleza majukumu
yao. Aidha, naomba niwashukuru Waandishi
wote wa habari waliopata nafasi ya kushuhudia yale yaliyofanyika hapa Barazani
kwa vipindi tofauti vya mwaka lakini na wale tuliokuwa pamoja nje ya Baraza kwa
safari na mikutano mbalimbali katika jamii.
Wote wamekuwa na mchango adhimu wa kuwafikishia wananchi taarifa na
miongozo mbalimbali ya masuala yanayohusu nchi yao.
192. Mheshimiwa Spika, naomba pia kwa
namna ya pekee kuchukuwa nafasi hii kuwashukuru na kuwapongeza kwa dhati kabisa
Wafanyakazi wote wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kuanzia Katibu Mkuu,
Naibu Katibu Mkuu, Wakurugezi, Afisa Mdhamini pamoja na Maafisa wa ngazi zote
kwa kufanya kazi bila kuchoka zilizotuwezesha kutekeleza malengo na majukumu
yetu kwa ufanisi katika kipindi cha mwaka 2014/2015.
193. Mheshimiwa Spika,
natoa shukrani za dhati kwa nchi marafiki, mashirika ya Kimataifa na
watu binafsi kwa kuendelea kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu ya Ofisi
ya Makamu wa Kwanza wa Rais. Nchi hizo ni pamoja na Marekani, Finland, Norway,
Uingereza, Uholanzi, Australia, China, Brazil, India na Falme za nchi za
Kiarabu na Oman. Pia mashirika ya kimataifa yakiwemo UNDP, UNICEF, UNFPA,UNAIDS, UNEP, UNODC,
UNFCCC, WHO, World Bank, CDC, THPS, IOC, UNESCO, DFID, IIED, Save the Children
international pamoja na nchi na mashirika
mengine ambayo sikuyataja, lakini kwa njia moja au nyengine yanatuunga
mkono katika shughuli zetu za maendeleo. Juhudi na michango yao tunaithamini
sana.
194. Mheshimiwa
Spika, shukurani za pekee ziwaendee wote
walioshiriki kwa njia moja au nyengine katika kufanikisha utekelezaji wa kazi
za Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais. Mwisho napenda kuwashukuru wananchi wote
kwa ujumla kwa kufanikisha kazi za maendeleo ya nchi yetu.
195. Mheshimiwa Spika,
kwa namna ya
pekee napenda kuishukuru familia yangu kwa ustahamilivu wao na msaada
mkubwa wanaonipa katika kunijengea utulivu ili niweze kutekeleza majukumu yangu, nawaombea heri na
baraka katika maisha yao.
196. Mheshimiwa Spika,
mwisho napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru wananchi wote kwa ujumla kwa
kudumisha amani katika kipindi hichi chote cha miaka mitano chini ya Serikali
ya Umoja wa Kitaifa, sote tunaelewa amani ni nyenzo muhimu ya kutufikisha
katika maendeleo endelevu na ustawi wa jamii yetu, nawaomba wanasiasa na
wananchi wote kwa ujumla kuhakikisha tunadumisha amani katika kipindi hichi cha
kuelekea kwenye uchaguzi mkuu hadi kufikia kukamilisha uchaguzi kwa salama na
amani namuomba Mwenyezimungu atuwezeshe kuitunza amani ndani ya nchi yetu.
HITIMISHO
197. Mheshimiwa Spika, kwa
heshima kubwa sasa nachukuwa nafasi hii kuwaomba Wajumbe wa Baraza lako
waipokee, waijadili, washauri, waelekeze na hatimae kuidhinisha matumizi ya
Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais ya jumla ya shilingi Bilioni tatu, milioni
mia tatu na sabini na tatu na laki nne (T.Shs.
3,373,400,000/-)
kwa mwaka wa fedha 2015/2016, zikiwemo
shilingi Bilioni mbili, milioni mia tisa na ishirini na tatu na laki nne
(TZS 2,923,400,000/-)
kutoka Serikalini na shilingi Milioni mia nne na hamsini (T.Shs.
450,000,000/-) kutoka kwa Washirika wa Maendeleo. Kati ya fedha hizo, shilingi Milioni mia moja
na sabini na nne, na elfu sabini na sita (T. Shs. 174,076,000/-) kutoka Serikalini pamoja na shilingi Milioni mia nne na hamsini (T.Shs.
450,000,000/-) kutoka kwa Washirika wa Maendeleo zitakuwa kwa
ajili ya utekelezaji wa Programu ya Usimamizi wa Mazingira na Mabadiliko ya
tabianchi; shilingi Milioni mia moja na hamsini na
tano, laki nne na elfu sitini (T. Shs. 155,460,000/-) kutoka Serikalini kwa ajili
ya utekelezaji wa Programu ya Usimamizi wa masuala ya
Watu wenye Ulemavu; na shilingi Bilioni
mbili, milioni mia tano na tisini na tatu, laki nane na elfu sitini na nne (T.
Shs. 2,593,864,000/-) kutoka
Serikalini kwa ajili ya utekelezaji wa Programu
ya Mipango na Utawala (Angalia
Kiambatanisho Nam. 10).
198. Mheshimiwa Spika, aidha,
naliomba Baraza lako liidhinishie Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa
Dawa za Kulevya matumizi ya jumla ya
shilingi Milioni mia nne na sitini na saba na laki moja (T.Shs 467,100,000/-) kutoka Serikalini
kwa mwaka wa fedha 2015/2016. Kati ya fedha hizo, shilingi Milioni tisini na
moja na elfu sitini na nne (T.Shs
91,064,000/-) kwa ajili ya utekelezaji wa Programu ya Udhibiti wa Dawa
za Kulevya; na shilingi Milioni mia tatu na sabini
na sita na elfu thelathini na sita (TShs.
376,036,000/-) kwa ajili ya utekelezaji wa Programu ya Mipango na
Utawala wa Tume ya Kitaifa ya Kuratibu; Udhibiti wa Dawa za Kulevya (Angalia
Kiambatanisho Nam. 10).
199. Mheshimiwa Spika, aidha,
naliomba Baraza lako liidhinishie Tume ya UKIMWI matumizi ya jumla ya shilingi
Milioni mia saba na ishirini na moja na laki moja (T.Shs. 721,100,000/-)
kutoka Serikalini, shilingi
Milioni mia tisa na thelathini na mbili na laki nne (T.Shs. 932,400,000/-
kutoka kwa
Washirika wa Maendeleo, na shilingi Milioni hamsini (T. Shs. 50,000,000/-)
ikiwa ni mchango wa Serikali katika kazi za maendeleo kwa
mwaka wa fedha 2015/2016. Kati ya fedha
hizo, shilingi Milioni mia moja na hamsini na mbili, laki tisa na elfu kumi na
nne (T.Shs. 152,914,000/-)
kutoka Serikalini, shilingi
Milioni mia tisa na thelathini na mbili na laki nne (T.Shs. 932,400,000/-
kutoka kwa
Washirika wa Maendeleo, na shilingi Milioni hamsini (T. Shs. 50,000,000/-)
ikiwa ni mchango wa Serikali katika kazi za maendeleo, zitakuwa kwa
ajili ya utekelezaji wa Programu ya Kuratibu Muitiko wa Taifa wa UKIMWI;
na shilingi Milioni mia tano na sitini na nane, laki mbili na elfu themanini na
sita (TShs 568,286,000/-) kwa ajili
ya utekelezaji wa Programu ya Mipango na Utawala wa Tume ya UKIMWI (Angalia Kiambatanisho Nam. 10).
200.
Mheshimiwa
Spika, aidha,
naliomba Baraza lako likubali mchango wa jumla ya T. Shs. 34,712,000/- ikiwa ni mapato yaliyokadiriwa kukusanywa na
OMKR kwa mwaka 2015/2016.
201.
Mheshimiwa
Spika, kwa heshima na taadhima, naomba kutoa
hoja.
Kiambatanisho Nam. 1:
WAFANYAKAZI
WALIOPATIWA FURSA ZA MAFUNZO KWA MWAKA 2014/2015
NA
|
JINA
|
CHUO
|
FANI
|
DARAJA
|
MWAKA ALIONZA
|
MWAKA ANAOMALIZA
|
MFADHILI
|
||
Idara ya
Uendeshaji na Utumishi
|
|||||||||
1
|
Nd. Waziri
Abbas Sheha
|
Chuo cha
Utawala wa Umma
|
Utawala wa
Umma
|
Stashahada
|
2013
|
2015
|
OMKR
|
||
2
|
Nd. Ali
Msellem Khamis
|
Chuo kikuu
huria Tanzania
|
Uhusiano wa
Kimataifa
|
Shahada ya
pili
|
2014
|
2016
|
OMKR
|
||
3
|
Nd. Asya Mmanga Said
|
Institute Counting Professional Studies
|
Uwekaji kumbu kumbu
|
Cheti
|
2014
|
2015
|
OMKR
|
||
4
|
Nd. Jokha Nossor Mvinja
|
Chuo cha
Ununuzi Ugavi
|
Ununuzi na
Ugavi
|
Shahada ya
kwanza
|
2012
|
2015
|
OMKR
|
||
5
|
Nd. Khamis
Makame Ali
|
Chuo cha
Ununuzi Ugavi
|
Ununuzi na
Ugavi
|
Shahada ya
kwanza
|
2013
|
2016
|
OMKR
|
||
6
|
Nd. Bakari
Shaban Bakar
|
Chuo Kikuu cha
Zanzibar - Tunguu
|
Uchumi na
Fedha
|
Shahada ya
pili
|
2014
|
2016
|
OMKR
|
||
7
|
Nd. Abdillah
Mussa Mshandete
|
Chuo Kikuu
Mzumbe
|
Uongozi wa
Biashara
|
Shahada ya
pili
|
2014
|
2016
|
OMKR
|
||
8
|
Nd. Asha Rashid Juma
|
India
|
Kiingereza na Teknoloj
|
Kozi Fupi
|
2014
|
2014
|
INDIA
|
||
9
|
Nd. Saada Mussa Said
|
China
|
Mabadiliko ya Tabianchi
|
Kozi Fupi
|
2014
|
2014
|
CHINA
|
||
10
|
Nd. Zena Mussa
Mwinyi
|
Chuo cha
kumbu. Mwalim Nyerere
|
Uwekaji kumbu
kumbu
|
Kozi Fupi
|
2014
|
2014
|
OMKR
|
||
Idara ya Mipango, Sera na Utafiti
|
|
||||||||
11
|
Nd. Suleiman
Kheir Suleiman
|
Chuo cha
Mipango Dodoma
|
Usimamizi wa
miradi
|
Stashahada ya
Uzamili
|
2014
|
2015
|
OMKR
|
||
12
|
Nd. Jabu
Sharif Haji
|
Chuo kikuu
huria Tanzania
|
Uchumi
|
Shahada ya
pili
|
2014
|
2016
|
OMKR
|
||
Idara ya Watu wenye Ulemavu
|
|||||||||
13
|
Nd. Kombo
Muhidin Ame
|
Chuo kikuu
huria Tanzania
|
Rasilimali
watu
|
Shahada ya
pili
|
2013
|
2015
|
OMKR
|
||
14
|
Nd. Asma Adam
Ali
|
KIU
|
Uhasibu na
Fedha
|
Shahada ya
kwanza
|
2012
|
2015
|
OMKR
|
||
15
|
Nd.Abushir Said Khatib
|
Chuo kikuu
huria Tanzania
|
Uchumi
|
Shahada ya
pili
|
2014
|
2016
|
OMKR
|
||
Ofisi ya Faragha
|
|||||||||
16
|
Nd. Moh`d
Ibrahim Mikuto
|
Chuo cha
Utalii
|
Upishi
|
Stashahada
|
2013
|
2015
|
OMKR
|
||
17
|
Nd. Hassan
Hamad Kombo
|
India
|
Uandishi wa
habari
|
Kozi Fupi
|
2014
|
2014
|
INDIA
|
||
Idara ya Mazingira
|
|||||||||
18
|
Nd. Makame
Haji Khamis
|
Chuo cha
Mipango Dodoma
|
Mipango ya
Mazingira
|
Shahada ya
pili
|
2014
|
2016
|
UDHAMINI
BINAFSI
|
||
19
|
Nd.Mtoro
Abdalla Salim
|
Institute
Counting Professional Studies
|
Uhasibu
|
Stashahada
|
2014
|
2016
|
OMKR
|
||
20
|
Nd. Khadija
Othman Juma
|
Chuo Kikuu cha
Zanzibar - Tunguu
|
Uchumi
|
Shahada ya
kwanza
|
2013
|
2016
|
OMKR
|
||
21
|
Nd. Chiku
Ali Moh`d
|
Dar. Institute
of Arts Media Communiction
|
Vedio, Film
and TV production
|
Stashahada
|
2014
|
2016
|
HIMA
|
||
22
|
Nd. Ali Vuai
Pandu
|
Chuo cha
Mipango Dodoma
|
Mipango ya
Mazingira
|
Shahada ya
pili
|
2014
|
2016
|
UDHAMINI
BINAFSI
|
||
23
|
Hassan Hamad
Hassan
|
Chuo Kikuu cha
Dodoma
|
Bioanuai
|
Shahada ya
pili
|
2012
|
2014
|
UDHAMINI
BINAFSI
|
||
24
|
Nassor Jamal
Nassor
|
Chuo Kikuu cha
SUZA
|
Sayansi ya
Mazingira
|
Shahada ya
pili
|
2012
|
2014
|
COSTECH
|
||
25
|
Salma Moh’d
Aboud
|
Chuo Kikuu cha
Zanzibar - Tunguu
|
Sheria
|
Shahada ya
pili
|
2012
|
2014
|
UDHAMINI
BINAFSI
|
||
26
|
Mgeni Mwalim
Khamis
|
Chuo Kikuu cha
Bagamoyo
|
Mfumo wa
Habari
|
Shahada ya
pili
|
2014
|
2015
|
BODI YA MIKOPO
|
||
27
|
Alawi H. Hija
|
Chuo kikuu cha
SUZA
|
Sayansi ya
Mazingira
|
Shahada ya
pili
|
2014
|
2016
|
UDHAMINI
BINAFSI
|
||
28
|
Mwalim Khamis
Mwalim
|
Chuo Kikuu
Huria- Tanzania
|
Usimamizi wa
Miradi
|
Shahada ya
pili
|
2013
|
2015
|
HIMA
|
||
29
|
Juma Shaame
Salim
|
Chuo Kikuu
Huria- Tanzania
|
Elimu ya
Mazingira
|
Shahada ya
pili
|
2013
|
2015
|
UDHAMINI
BINAFSI
|
||
30
|
Nassor Majid
Nassor
|
Chuo Kikuu cha
Dar es salaam
|
Tathmini na
Usimamizi wa Mazingira
|
Shahada ya
pili
|
2013
|
2015
|
BODI YA MIKOPO
|
||
31
|
Mussa Khamis
Khamis
|
Chuo Kikuu
Huria- Tanzania
|
Kazi za
kijamii
|
Shahada ya
pili
|
2015
|
2017
|
UDHAMINI
BINAFSI
|
||
32
|
Zuwena Juma Bilal
|
Chuo cha Hotel na Uongozi - Dar es salaam (Tawi la
Pemba)
|
Ununuzi
|
Stashahada
|
2015
|
2017
|
UDHAMINI BINAFSI
|
||
33
|
Zuhura Msabaha
Khamis
|
Chuo cha
Uandishi wa Habari (Time) - Pemba
|
Uandishi wa
Habari
|
Stashahada
|
2015
|
2017
|
UDHAMINI
BINAFSI
|
||
Ofisi Kuu Pemba
|
|||||||||
34
|
Ali Othman
Mussa
|
Chuo cha
Mipango- Dodoma
|
Mipango na
Usimamizi wa Mazingira
|
Shahada ya
pili
|
2013
|
2015
|
HIMA
|
||
Tume ya UKIMWI
|
|||||||||
35
|
Nd. Yahya Abeid Ali
|
Chuo cha Utawala wa Umma
|
Teknolojia ya habari
|
Stashahada
|
2013
|
2014
|
TUME
|
||
36
|
Nd. Juma Mohammed Ahmed
|
Chuo cha Utawala wa Umma
|
Uhasibu
|
Stashahada
|
2013
|
2014
|
TUME
|
||
37
|
Nd. Fatma Khamis Ali
|
Chuo Kikuu cha Zanzibar - Tunguu
|
Uongozi wa Biashara
|
Shahada ya pili
|
2013
|
2014
|
TUME
|
||
38
|
Nd. Nassor Ali Abdalla
|
Chuo Kikuu Morogoro
|
Utekelezaji wa sera
kuzishirikisha taasisi za kiraia
|
Shahada ya pili
|
2013
|
2014
|
TUME
|
||
39
|
Nd. Mohammed Said Mohammed
|
INDIA
|
Ufuatiliaji na Tathmini
|
Kozi fupi
|
2014
|
2014
|
TUME
|
||
Kiambatanisho Nam. 2:
OPERESHENI
ZA KUDHIBITI MATUMIZI YA MIFUKO YA PLASTIKI ZILIZOFANYWA KWA MWAKA 2014/2015
Namb.
|
Mwezi
|
Idadi
ya Operesheni
|
Idadi
ya Watu waliokamatwa
|
Kiwango
cha Mifuko kilichokamatwa (Kgs)
|
1.
|
Julai,
2014
|
5
|
0
|
0
|
2.
|
Agosti,2014
|
3
|
3
|
2
|
3.
|
Septemba,
2014
|
3
|
0
|
0
|
4.
|
Oktoba,2014
|
12
|
14
|
694
|
5.
|
Novemba,
2014
|
-
|
-
|
-
|
6.
|
Disemba,
2014
|
-
|
-
|
-
|
7.
|
Jnuari,
2015
|
-
|
-
|
-
|
8.
|
Februari,
2015
|
10
|
6
|
63
|
9.
|
Machi,
2015
|
-
|
-
|
-
|
|
JUMLA
|
33
|
23
|
759
|
Kiambatanisho Nam. 3:
MIRADI
ILIYOFANYIWA TATHMINI YA ATHARI ZA KIMAZINGIRA (EIA) NA KUPEWA VYETI VYA
KIMAZINGIRA KWA MWAKA 2014/2015
Namb.
|
Jina la Mradi
|
Mahali Ulipo
|
Nambari ya Cheti
|
1.
|
Amber
Golf and Beach Resort
|
Mbuyu Tende-Matemwe
|
IM/EIA/51
|
2.
|
Construction
of New Port Project Phase 1 Zanzibar
|
Maruhubi
|
IM/EIA/52
|
3.
|
Zanzi
Gas Co Limited, Zanzibar
|
Welezo - Makufuli
|
IM/EIA/50
|
4.
|
Construction
of Terminal II of Abeid Amani Karume International Airport
|
Kisauni
|
IM/EIA/53
|
5.
|
Island
Paradise Inn Hotel
|
Mlandege - Zanzibar
|
IM/EIA/03
|
6.
|
Upgrading
of 62.6 km of Road in Unguja Island to Bitumen standards Zanzibar
|
North, South and west district of
Zanzibar
|
IM/EIA/54
|
7.
|
Zas
Villa Luxury and Resort
|
Kiwengwa Kumba Urembo North B district
|
IM/EIA/55
|
8.
|
Tulia
resort (nature safari lodge)
|
Pongwe Pwani
|
IM/EIA/56
|
9.
|
Beach
resort Project at Makunduchi (Fard company)
|
Shungi Makunduchi
|
IM/EIA/57
|
10.
|
Uzuri
Zanzibar Resort Project
|
Kendwa
|
IM/EIA/58
|
11.
|
Ujamaa
Beach Resort
|
Makunduchi
|
IM/ER/05
|
12.
|
Internet
Data Center
|
Fumba
|
IM/ER/03
|
13.
|
Trade
Wind Hotel
|
Matemwe
|
IM/ER/04
|
Kiambatanisho Nam. 4:
VIPINDI
VYA REDIO NA TV VILIVYORUSHWA HEWANI KWA MWAKA 2014/2015
NAMBA
|
MADA
YA KIPINDI
|
IDADI
|
KITUO
|
IDARA
HUSIKA
|
1
|
Marufuku
ya mifuko ya plastiki
|
1
|
ZBC
Redio
|
Idara
ya Mazingira
|
2
|
Matumizi
ya majiko sanifu
|
2
|
ZBC
Redio
|
Idara
ya Mazingira
|
3
|
Umuhimu
wa umeme wa jua
|
2
|
ZBC
Redio
|
Idara
ya Mazingira
|
4
|
Tangazo
la marufuku ya mifuko ya plastiki
|
1
|
ZBC
Redio
|
Idara
ya Mazingira
|
5
|
Kanuni
za Mali Asili zisizorejesheka
|
2
|
ZBC
Redio
|
Idara
ya Mazingira
|
6
|
Matumizi
endelevu ya Mali Asili zisizorejeseka
|
1
|
ZBC
Redio
|
Idara
ya Mazingira
|
7
|
Mmong’onyoko
wa fukwe
|
2
|
ZBC
Redio
|
Idara
ya Mazingira
|
|
Matumizi
ya majiko sanifu
|
1
|
ZBC
TV
|
Idara
ya Mazingira
|
|
Matumizi
ya umeme wa jua
|
1
|
ZBC
TV
|
Idara
ya Mazingira
|
|
JUMLA
|
13
|
|
|
Kiambatanisho Nam. 5:
AINA
NA IDADI YA VISAIDIZI VILIVYOTOLEWA KWA WATU WENY ULEMAVU WA AINA MBALIMBALI
KWA MWAKA 2014/2015
PEMBA
|
|||
Wilaya
|
Aina
ya kisaidizi
|
Wanawake
|
Wanaume
|
CHAKE CHAKE
|
Kiti cha magurudumu mawili
|
3
|
1
|
Fimbo nyeupe
|
4
|
5
|
|
Miwani + Kofia
|
6
|
3
|
|
Magongo ya kutembelea
|
2
|
3
|
|
MKOANI
|
Kiti cha magurudumu mawili
|
1
|
3
|
Fimbo nyeupe
|
4
|
5
|
|
Miwani + Kofia
|
6
|
3
|
|
Magongo ya kutembelea
|
1
|
2
|
|
WETE
|
Kiti cha magurudumu mawili
|
4
|
0
|
Fimbo nyeupe
|
4
|
8
|
|
Miwani + Kofia
|
5
|
3
|
|
Magongo ya kutembelea
|
6
|
10
|
|
MICHEWENI
|
Kiti cha magurudumu mawili
|
3
|
3
|
Fimbo nyeupe
|
6
|
9
|
|
Miwani + Kofia
|
3
|
6
|
|
Magongo ya kutembelea
|
0
|
9
|
|
JUMLA
|
58
|
73
|
|
UNGUJA
|
|||
KASKAZINI A
|
Kiti cha magurudumu mawili
|
1
|
6
|
Fimbo nyeupe + miwani
|
0
|
0
|
|
Miwani +Kofia
|
4
|
2
|
|
Magongo ya kutembelea
|
0
|
0
|
|
Fimbo nyeupe
|
0
|
0
|
|
KASKAZINI B
|
Kiti cha magurudumu mawili
|
1
|
1
|
Fimbo nyeupe + miwani
|
0
|
0
|
|
Miwani +Kofia
|
0
|
1
|
|
Magongo ya kutembelea
|
0
|
0
|
|
Fimbo nyeupe
|
0
|
2
|
|
MJINI
|
Kiti cha magurudumu mawili
|
3
|
6
|
Fimbo nyeupe + miwani
|
0
|
0
|
|
Miwani +Kofia
|
3
|
1
|
|
Magongo ya kutembelea
|
0
|
4
|
|
Fimbo nyeupe
|
1
|
3
|
|
MAGHARIBI
|
Kiti cha magurudumu mawili
|
1
|
1
|
Fimbo nyeupe + miwani
|
0
|
1
|
|
Miwani +Kofia
|
3
|
2
|
|
Magongo ya kutembelea
|
0
|
3
|
|
Fimbo nyeupe
|
4
|
1
|
|
KATI
|
Kiti cha magurudumu mawili
|
3
|
2
|
Fimbo nyeupe + miwani
|
4
|
6
|
|
Miwani +Kofia
|
1
|
1
|
|
Magongo ya kutembelea
|
1
|
5
|
|
Fimbo nyeupe
|
1
|
1
|
|
KUSINI
|
Kiti cha magurudumu mawili
|
2
|
3
|
Fimbo nyeupe + miwani
|
1
|
0
|
|
Miwani +Kofia
|
0
|
0
|
|
Magongo ya kutembelea
|
2
|
0
|
|
Fimbo nyeupe
|
2
|
4
|
|
JUMLA
|
38
|
56
|
Kiambatanisho Nam. 6:
IDADI
YA SKULI ZILIZOPATA ELIMU YA ATHARI YA DAWA ZA KULEVYA UNGUJA NA PEMBA KWA
MWAKA 2014/2015
UNGUJA
|
|||
1
|
JINA
LA SKULI
|
IDADI
YA WANAWAKE
|
IDADI
YA WANAUME
|
2
|
K/SAMAKI
|
34
|
27
|
3
|
DARAJANI
|
40
|
21
|
4
|
RAHALEO
|
30
|
22
|
5
|
AL-HARAMAYN
|
43
|
27
|
6
|
JANG’OMBE B MSINGI
|
56
|
30
|
7
|
NYERERE SEK
|
33
|
29
|
8
|
KIDONGO CHEKUNDU B MSING
|
40
|
31
|
9
|
JANG’OMBE SEK.
|
39
|
24
|
10
|
JANG’OMBE A MSINGI
|
36
|
20
|
11
|
K/CHEKUNDU A MSINGI
|
50
|
30
|
12
|
CHUKWANI
|
49
|
28
|
13
|
MFENESINI
|
49
|
20
|
14
|
MIKUNGUNI
|
56
|
26
|
15
|
M’KWEREKWE. A
|
40
|
32
|
16
|
M’KWEREKWE G
|
32
|
20
|
17
|
KITOPE
|
48
|
29
|
18
|
CHWAKA
|
50
|
24
|
19
|
KIANGA
|
40
|
28
|
20
|
NUNGWI
|
49
|
30
|
21
|
MTONI
|
50
|
27
|
22
|
E/MBADALA
|
50
|
18
|
23
|
MPENDAE
|
49
|
30
|
24
|
M’KWEREKWE. E
|
40
|
28
|
25
|
BUBUBU SEK.
|
55
|
38
|
26
|
MWERA
|
30
|
20
|
27
|
MACHUI
|
40
|
23
|
28
|
MUYUNI
|
39
|
30
|
29
|
VIKOKOTONI
|
38
|
20
|
|
JUMLA
|
1245
|
758
|
PEMBA
|
|||
1
|
CHANJAMJAWIRI SEK
|
40
|
27
|
2
|
CHANJAANI SEK
|
47
|
20
|
3
|
UWONDWE SEK
|
49
|
37
|
4
|
MICHEWENI MS
|
38
|
30
|
5
|
JADIDA MSINGI
|
37
|
20
|
6
|
OLE SEK
|
38
|
28
|
7
|
SHUNGI SEK
|
29
|
20
|
8
|
CHWAKA TUMBE SEK
|
37
|
34
|
9
|
TIRONI MSINGI
|
19
|
17
|
10
|
WINGWI SEK
|
18
|
19
|
11
|
MZAMBARAUNI SEK
|
37
|
30
|
12
|
CHAMBANI SEK
|
45
|
30
|
13
|
CHAMBANI MSINGI
|
37
|
20
|
|
JUMLA
|
471
|
332
|
Jumla
ya Unguja na Pemba
|
1,716
|
1,090
|
Kiambatanisho Nam. 7:
NYUMBA ZA
MAKAAZI (SOBER HOUSES) ZILIZOPEWA RUZUKU KWA MWAKA 2014/2015
MAELEZO
|
KIASI (TSH)
|
SEPTEMBA 2014
|
|
|
1,500,000
|
|
1,500,000
|
|
1,500,000
|
OKTOBA 2014
|
|
|
1,500,000
|
|
1,500,000
|
NOVEMBA 2014
|
|
|
1,500,000
|
|
1,500,000
|
|
1,500,000
|
DISEMBA 2014
|
|
|
1,500,000
|
1,500,000
|
|
JUMLA
|
15,000,000
|
Kiambatanisho
Nam. 8:
VIKUNDI VYA WAJASIRIAMALI KUTOKA ZAPHA+ VILIVYOPATIWA
FEDHA NA MISAADA MBALI MBALI KWA MWAKA 2014/2015
Jina la kikundi
|
Kazi za kikundi
|
Msaada waliopata
|
Pahala kilipo
|
Umoja ni nguvu
|
Kuweka na kukopa
|
Mafunzo na shs . 890,000/- za kuendeleza mradi
|
Welezo, Unguja
|
Female Individual Entrepreneurship
group
|
Kushona, kutengeneza sabuni na biashara ndogo
ndogo
|
Mafunzo na shs . 890,000/- za kuendeleza mradi
|
Bububu, Unguja
|
Umoja ni nguvu Micheweni
|
Kilimo cha mazao ya chakula na mboga mboga
|
Mafunzo na shs . 890,000/- za kuendeleza mradi
|
Micheweni - Pemba
|
Lengo letu moja
|
Ufugaji wa kuku
|
Mafunzo na shs . 890,000/- za kuendeleza mradi
|
Chake chake - Pemba
|
Jipe moyo
|
Utengenezaji wa sabuni
|
Mafunzo na shs . 890,000/- za kuendeleza mradi
|
Welezo, Unguja
|
Kiambatanisho Nam. 10:
MCHANGANUO
WA FEDHA ZINAZOOMBWA KWA PROGRAMU ZA OMKR, TUME YA UKIMWI NA TUME YA KITAIFA YA
KURATIBU NA UDHIBITI ZA DAWA ZA KULEVYA KWA MWAKA 2014/2015
PROGRAM KUU
|
PROGRAMU NDOGO
|
Fedha
Zinazoombwa kwa mwaka 2015/2016
|
|||
Matumizi ya Kawaida
|
Mchango wa SMZ katika kazi za
maendeleo
|
Washirika wa Maendeleo
|
Jumla TZS
|
||
Usimamizi wa
Mazingira na Mabadiliko ya tabianchi
|
Usimamizi wa Mazingira
|
174,076,000
|
0
|
0
|
174,076,000
|
Usimamizi wa Mabadiliko ya Tabianchi
|
0
|
0
|
450,000,000
|
450,000,000
|
|
Jumla kwa
Programu 1
|
174,076,000
|
0
|
450,000,000
|
624,076,000
|
|
Usimamizi
wa masuala ya Watu wenye Ulemavu
|
Usimamizi wa
masuala ya Watu wenye Ulemavu
|
155,460,000
|
0
|
0
|
155,460,000
|
Jumla kwa Programu
2
|
155,460,000
|
0
|
0
|
155,460,000
|
|
Mipango
na Utawala
|
Uongozi na Utawala
|
2,051,997,000
|
0
|
0
|
2,051,997,000
|
Mipango, Sera na Utafiti
|
93,719,000
|
0
|
0
|
93,719,000
|
|
Uratibu wa masuala ya OMKR Pemba
|
448,148,000
|
0
|
0
|
448,148,000
|
|
Jumla kwa
Programu 3
|
2,593,864,000
|
0
|
0
|
2,593,864,000
|
|
JUMLA YA OMKR - TZS
|
2,923,400,000
|
0
|
450,000,000
|
3,373,400,000
|
|
Udhibiti wa
Dawa za Kulevya
|
Uratibu wa Udhibiti wa Usafirishaji na Usambazaji wa dawa za
kulevya
|
57,814,000
|
0
|
0
|
57,814,000
|
Kinga ya msingi ya Mahitaji na Matumizi ya Dawa za Kulevya
|
33,250,000
|
0
|
0
|
33,250,000
|
|
Jumla kwa Programu 4
|
91,064,000
|
0
|
0
|
91,064,000
|
|
Mipango na
Utawala wa Tume ya Kitaifa ya Kuratibu; Udhibiti wa Dawa za Kulevya
|
Utawala na Uendeshaji wa Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti
wa Dawa za Kulevya
|
304,690,000
|
0
|
0
|
304,690,000
|
Uratibu wa masuala ya Dawa za kulevya Pemba
|
71,346,000
|
0
|
0
|
71,346,000
|
|
Jumla kwa Programu 5
|
376,036,000
|
0
|
0
|
376,036,000
|
|
JUMLA YA TUME YA KITAIFA YA KURATIBU NA UDHIBITI WA DAWA ZA KULEVYA -
TZS
|
467,100,000
|
0
|
0
|
467,100,000
|
|
Kuratibu Muitiko wa Taifa wa UKIMWI
|
Mawasiliano
na Utetezi.
|
51,981,000
|
50,000,000
|
932,400,000
|
1,034,381,000
|
Uratibu
wa muitiko wa Taifa wa UKIMWI.
|
100,833,000
|
0
|
0
|
100,833,000
|
|
Jumla kwa Programu 6
|
152,914,000
|
50,000,000
|
932,400,000
|
1,135,214,000
|
|
Mipango na Utawala
wa Tume ya UKIMWI
|
Utumishi
na Uendeshaji wa Tume ya UKIMWI
|
383,386,000
|
0
|
0
|
383,386,000
|
Uratibu wa masuala ya UKIMWI Pemba.
|
184,900,000
|
0
|
0
|
184,900,000
|
|
Jumla kwa Programu 7
|
568,286,000
|
0
|
0
|
568,286,000
|
|
JUMLA YA TUME
YA UKIMWI - TZS
|
721,100,000
|
50,000,000
|
932,400,000
|
1,703,500,000
|
No comments:
Post a Comment