WANAFUNZI wa kituo cha kulea watoto Mayatima cha
African Muslims Agency Mabaoni Chake Chake Pemba, wakishusha baadhi ya misada
iliyotolewa na kituo cha Huduma za Sheria Tawi la Pemba, kwa watoto hao katika
maadhimisho ya miaka 23 tokea kuanzishwa kwa ZLSC Zanzibar.(Picha na AbdI Suleiman, PEMBA.)
AFISA Mipango wa kituo cha huduma za sheria Zanzibar
Tawi la Pemba (ZLSC) Halfan Amour, akibeba kipolo cha mchele ikiwa ni miongoni
mwa misaada waliotoa kwa watoto mayatima wanaolelewa katika kituo cha Africa
Muslims Agency huko Mabaoni Chake Chake Pemba, baada ya ZLSC kutimiza miaka 23.(Picha na AbdI Suleiman, PEMBA.)
MRATIB wa kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Ofisi
ya Pemba, Fatma Khamis Hemed, akimkabidhi msimamizi wa Africa Muslims Agency
mabaaoni Chake Chake Pemba, ikiwa ni maadhimisho ya ZLSC kutimiza miaka 23
tokea kuanzishwa kwake.(Picha na AbdI
Suleiman, PEMBA.)
WAFANYAKAZI wa kituo cha Huduma za sheria Zanzibar
(zlsc) Ofisi ya Pemba, wakiwa elekea wodi ya watoto kutoa zawadi katika
hospitali ya Chake Chake kuwapatia zawadi, ikiwa ni maadhimisho ya kutimiza
miaka 23 kuanzishwa kwa kituo hicho.(Picha
na AbdI Suleiman, PEMBA.)
DAKTARI Dhamana wa Hospitali ya Chake Chake Dk
Yussuf Hamad Iddi, akiwawakaribisha watendaji wa kituo cha Huduma za sheria
Zanzibar (ZLSC) Ofisi ya Pemba, katika wodi ya watoto kwa lengo la kuwapatia
msada wao, ikiwa ni maadhimisho ya kutimiza miaka 23 kwa kituo hicho.(Picha na AbdI Suleiman, PEMBA.)
MRATIB wa Kituo cha Huduma za sheria Zanzibar ofisi
ya Pemba, Fatma Khamis Hemed akimpatia zawadi ya biskuti, mtoto aliyelazwa
katika wodi ya watoto ndani ya Hospitali ya Chake Chake ikiwa ni Maadhimisho ya
kutimiza miaka 23 kuanzishwa kwa kituo hicho.(Picha na AbdI Suleiman, PEMBA.)
MRATIB wa KItuo Cha Huduma za sheria Zanzibar Ofisi
ya Pemba, Fatma Khamis Hemed akimkabidhi Daktari dhamana wa Hospitali ya Chake
Chake Dk Yussuf Hamad Iddi, vifaa mbali mbali ikiwa ni maadhimisho ya kutimiza miaka
23 kwa kituo hicho.(Picha na AbdI
Suleiman, PEMBA.)
WAFANYAKAZI wa kituo cha huduma za sheria Zanzibar
ofisi ya Pemba, wakijumuika katika chakula cha mchana na mjumbe wao wa bodi wa
ZLSC Daudi Othamna Kondo wa pili kutoka kushoto, ikiwa ni maadhimisho ya
kutimiza miaka 23 kwa kituo hicho.(Picha
na Abdi Suleiman, PEMBA.)
No comments:
Post a Comment