Habari za Punde

Tanzania na Malta kuanzisha kuhusiano wa kidiplomasia

Wawakilishi wa Kudumu wa Tanzania,  Balozi Tuvako  Manongi na  Christopher  Grima Malta wakitia sahihi hati za kuanzisha uhusiano wa  kidiplomasia katika ngazi ya Mabalozi. Wanaoangalia utiaji sahihi  ni   Tully Mwaipopo Afisa Mwandamizi  wa Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania na Bw. Alan Cordina, Afisa wa Uwakilishi wa  Kudumu wa Malta

Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako  Manongi na  Mwakilishi wa Kudumu wa Malta katika Umoja wa Mataifa,  Balozi Christopher  Grima wakipongezana  mara  baada ya  kutia sahihi  hati  walizoshika za kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia katika ngazi ya Mabalozi. Hati hizo baadaye ya zitawasilishwa  rasmi  kwa  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Na Mwandishi Maalum, New York

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya  Malta zimekubaliana kuanzisha uhusiano  wa kidiplomasia baina  yao.

Wawakilishi wa Kudumu wa  mataifa hayo mawili katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi wa Tanzania na Christopher Grima  wa  Malta ndio waliotia sahihi hati za kuridhia kuanzishwa kwa  uhusiano huo na ambao utakuwa katika ngazi ya  Mabalozi.

Wakizungumza mara baada ya  utiaji sahihi hati hizo, wawakilishi  hao wameelezea kuwa kuanzishwa kwa uhusiano  huo ni hatua muhimu  sana katika kukuza na kuendeleza ushirikiano na uhusiano  kati ya mataifa hayo mawili na  watu wake.

Tanzania  imekuwa ikinufaika kwa ufadhili wa nafasi za masomo  kutoka  Malta kwa watumishi mbalimbali  wakiwamo wa Wizara ya Mambo ya Nje na  Ushirikiano wa Kimataifa na    Wizara nyingine.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.