Habari za Punde

Mafunzo ya namna ya kuandikwa Katiba na Sheria

 SHEHA wa shehia ya Utaani wilaya ya wete Pemba, nd: Massoud Msellem Shinei, akifungua mkutano wa kuelimishwa namna ya kuandikwa sheria na mafunzo ya katiba, ulioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, ZLSC tawi la Pemba, uliofanyika skuli ya Chasasa sekondari wilayani humo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 KAIMU Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, ZLSC tawi la Pemba, Khalfan Amour Mohamed akielezea kazi na majukumu ya kituo hicho, kabla ya kuanza kwa mkutano wa kuelezwa wananchi namna ya kuandika sheria na mafunzo ya katiba,uliofanyika skuli ya Chasasa wilaya ya Wete, kulia ni mwanasheria wa serikali Ali Amour na kushoto ni sheha wa shehia ya Utaani, Massoud Msellem, akifuatiwa na Afisa Mipango wa ZLSC Siti Habib Mohamed, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 MCHANGIA mada, akiuliza suali lake la kutaka tofauti kati ya katiba na sheria, kwenye mkutano ulioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC, tawi la Pemba juu ya kuwaeleza wananchi taratibu za kuandika sheria na mafunzo ya katiba, mkutano huo ulifanyika skuli ya Chasasa wete Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

 SHEHA wa shehia ya Majenzi wilaya ya Micheweni Pemba Faki Kombo Hamad, akifungua mkutano wa elimu ya katiba na utaratibu wa kuandikwa kwa sheria, mkutano ulioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC, tawi la Pemba, kulia ni Mratibu wa kituo hicho Fatma Khamis Hemed na kushoto ni mwanasheria Omar Ahmed Abdalla, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 BAADHI ya wananchi wa wilaya ya Micheweni wakifuatilia kwa makini mada ya utaratibu wa uandishi wa sheria, kwenye mkutano maalumu uliofanyika skuli ya Micheweni, ulioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, ZLSC tawi la Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MMOJA wa wananchi wa wilaya ya Micheweni Pemba, akichangia mada kwenye mkutano wa kuelimishwa namna ya kuandikwa kwa sheria, na mafunzo ya katiba ulioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC, tawi la Pemba na kufanyika skuli ya Micheweni sekondari, (Picha na Haji Nassor, Pemba). 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.