Wajumbe wa Bodi ya Ukaguzi kutoka kushoto, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali ya India, Bw. Shashi Kant Sharma, Sir Amyas Morse, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu kutoka Serikali ya India na Bw. Mussa Juma Assad, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu kutoka Serikali ya Tanzania wakitia saini zao katika ripoti 28 za ukaguzi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa zilizorejewa na kupitishwa na Bodi hiyo wakati wa mkutano wake wa siku mbili. ripoti hizo ni matokeo ya kazi kubwa ya Bodi hiyo
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ukaguzi ya Umoja wa Mataifa, Bw.Mussa Juma Assad akizungumza wakati wa hitimisho la mkutano wa siku mbili wa Bodi hiyo uliofanyika hapa Umoja wa Mataifa kuanzia Julai 22-23. Kushoto kwake ni Bw. Fransis Kitauli, Mkurugenzi wa Ukauzi wa Nje na Mwenyekiti wa Kamati ya Operesheni za Ukaguzi ( AOC) Akiwa Mwenyekiti wa AOC Bw. Kitauli ambaye alishika nafasi hiyo tangu mwaka 2012 amefanikisha utoaji wa ripoti za ukaguzi za Umoja wa Mataifa kwa miaka mitatu mfululizo
Ujumbe wa Bodi ya Tanzania ambao ni kutoka kushoto Jerome Francis, Naibu Mkurugenzi ukaguzi wa Nje, Bw. Salhina Mkumba, Naibu Mkurugenzi, Ukaguzi wa Nje na ambaye amefanya kazi kwa karibu sana na Bw. Fransis Kitauli tangu Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ilipoteuliwa kuingia kwenye Bodi ya Ukaguzi ya Umoja wa Mataifa wa mwisho ni Bw. Athuman S. Mbuttuka, Naibu Mkaguzi Mkuu.
Na
Mwandishi Maalum, New York
Bodi
ya Ukaguzi wa Hesabu za Mashirika ya Umoja wa Mataifa , imemaliza mkutano wake wa siku mbili kwa kurejea na kupitisha taarifa 28 za ukaguzi.
Taarifa 22 kati ya hizo zitawasilishwa mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na sita zitawasilishwa kwa
Mamlaka na vyombo vingine.
Mkutano
huo umefanyika hapa
Umoja wa Mataifa chini ya Uenyekiti wa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa
Hesabu za Serikali kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw. Mussa
Juma Assad
Wajumbe
wengine wa Bodi ni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu kutoka Serikali ya
Uingereza Sir Amyas Morse na Bw. Shashi Kant Sharma, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu kutoka Serikali ya
India.
Akizungumza mara baada ya kutia saini taarifa hizo,
jukumu lililofanywa kwa
pamoja na wadhibiti na
Wakaguzi hao watatu, Bw. Mussa
Juma Assad amewashukuru wajumbe wenzie
kwa kazi kubwa na nzuri ambayo
wameifanya katika siku hizo mbili pamoja
na ushirikiano mzuri waliompatia.
“
Nichukue fursa hii kuwashukuru sana kwa kazi hii nzuri na ushirikiano mkubwa
mlionipatia, ushirikiano ambao
umetuwezesha kukamilisha kazi hii kwa wakati na muda muafaka”, akasema Mdhibiti
na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali Bw. Assad
Wakijibu
shukrani hizo, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu kutoka Serikali
ya Uingereza, Sir Amyas Morse
alimshukuru Mwenyekiti kwa
uongozi wake na upeo mkubwa ikiwa ni pamoja na
ushirikiano wake kwa wajumbe wenzie.
Akatumia pia fursa hiyo kumpongeza na
kumshukuru kwa moyo wa dhati, Bw. Fransis Kitauli ambaye kwa
miaka mitatu akiwa Mwenyekiti wa
Kamati ya Operesheni amefanikiwa kutolewa kwa ripoti za ukaguzi bila kukosa.
Sir
Morse amemuelezea Bw. Kitauli kama Mkurungezi na Mwenyekiti ambaye ameonyesha weledi mkubwa na
kujituma kwa hali ya juu katika
utekelezaji wa majukumu yake amekuwa
Mkurugenzi anayemwakilisha Mkaguzi
Mkuu hapa Umoja wa Mataifa kwa
uadilifu wake, na weledi mkubwa katika
utekelezaji na usimamizi wa majukumu yake
na akamtakia kila la kheri arejeapo
Tanzania.
Kwa upande wake Mkaguzi
na Mdhibiti Mkuu wa Serikali
ya India, Bw. Shashi Sharma, pamoja na
kumshukuru Mwenyekiti kwa uongozi wake
mahili naye alimpongeza na kumshukuru Bw. Fransis Kitauli kwa uhodari wake, kujituma
na kazi kubwa aliyoifanyia katika utekelezaji na usimamizi wa majukumu
ya Bodi hiyo.
No comments:
Post a Comment