Mkurugenzi wa Zantel, Pratap Ghose akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma mpya kati ya kampuni yake na benki ya PBZ, Benki Yako Kiganjani.
Mkurugenzi wa Huduma ya Kifedha za simu za mtandao, Hashim Mkudi akielezea namna ya kutumia huduma ya Benki Kiganjani Mwako iliyozinduliwa kwa ushirikiano wa kampuni yake na benki ya PBZ.
Mkurugenzi wa benki ya PBZ,
Juma Mohammed akizungumza wakati wa kuzindua huduma ya Benki Kiganjani Mwako,
inayoendeshwa na kwa ushirikiano wa benki yake na kampuni ya Zantel.
Zanzibar, 31/8/2015: Kampuni ya simu ya Zantel leo imeingia ubia
na Benki ya Watu wa Zanzibar, kwa ajili ya kutoa huduma za kibenki kwa wateja
wao kupitia huduma ya simu ya Ezypesa.
Makubaliano haya yatawawezesha wateja
wa Ezypesa wenye akaunti za PBZ kufanya miamala kupitia simu zao za mkononi, kujua salio katika akaunti zao pamoja
na kupata taarifa fupi za akaunti zao.
Akizungumza wakati wa kuzindua
ushirikiano huo, Waziri wa Fedha wa Serikali ya Zanzibar, Mheshimiwa Omari
Yusuf Mzee, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo amesema ushirikiano
kati ya Zantel na Benki ya Watu wa Zanzibar ni faraja kubwa kwa wananchi kwani
itaongeza wigo na kurahisisha huduma za kibenki.
‘Ushirikiano kati ya benki ya PBZ na
Zantel ni wa muda mrefu, na kwa uzinduzi wa huduma hii leo ambao umekuwa
ukisubiriwa na Wazanzibari kwa muda mrefu wameweka historia’ alisema Mheshimiwa
Mzee.
Mheshimiwa Mzee pia alisema huduma hii
imekuja kwa wakati muafaka, kwani asilimia kubwa ya Wazanzibar wana simu za
Zantel na akaunti katika benki ya PBZ huku akiwachagiza makampuni kuoungeza
huduma zaidi za kijamii kwa watu wa Zanzibar.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Pratap
Ghose alisema ushirikiano baina ya PBZ na Zantel utawezesha ukuaji wa huduma ya
EzyPesa ambayo imekuwa ni sehemu ya maisha ya watu wa Zanzibar
“Ubia huu baina ya Zantel na PBZ utawarahishia wateja wetu
katika kutumia huduma za benki katika kufanya miamala ya kifedha kutoka katika
akaunti zao za PBZ kwenda kwenye akaunti zao za EzyPesa kwa njia rahisi na
salama” alisema Ghose.
Ghose aliongeza kwa
kusema kuwa wateja wa Zantel sasa wataweza kutumia simu zao kufanya shughuli za
kibenki na hivyo kuondoa usumbufu wa upatikanaji wa huduma za PBZ kwa mwananchi
wa kawaida.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mkuu wa PBZ, Juma
Mohammed, alisema kwamba ubia huo utawawezesha wateja kutoa na kuweka fedha
kwenye akaunti zao, kulipia huduma, kujua salio, kufanya miamala kutoka akaunti
moja kwenda nyingine pamoja na kununua muda wa maongezi.
‘Huduma hii itafanya huduma za kifedha zipatikane kwa urahisi
zaidi kwa wateja wetu kuliko ilivyokuwa awali, na pia itaboresha ubora wa
huduma pamoja na kupunguza msongamano wa wateja hasa kipindi cha mwisho wa
mwezi’ alisema Mohammed.
Uzinduzi
wa huduma hii kwa kushirikiana na PBZ inakuja kama
ongezeko baada ya huduma ya awali ya TUKUZA inayotolewa na Ezypesa kwa wateja
wote wa Zanzibar, wateja wanaweza kuanza kufurahia huduma hii moja kwa moja kwa
kubonyeza namba *150*02#.
‘Zantel ina miundombinu ya kisasa na
imara kuwezesha kufanya kazi sawasawa na kwa viwango vya dunia, hivyo wizara ya
miundombinu inawahakikishia wazanzibar waipokee huduma hii kwa mikono miwili’
alisema Mkurugenzi wa Mawasiliano Zanzibar, Dkt Mzee Suleiman Mndewa.
No comments:
Post a Comment