Habari za Punde

Balozi Seif Aweka Jiwe la Msingi Nyumba yas Askari Polisi Micheweni Pemba.

Nyumba ya Makaazi ya Askari wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Micheweni Pemba ambalo lina uwezo wea kuchukua familia kumi kwa wakati mmoja.
Makamu wa Pili wa rais Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akiondosha kitambaa, kuashiria kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba ya kulala askari Polisi wilaya ya Micheweni Pemba, ambayo inajengwa kwa ushirikiano kati ya wananchi na Jeshi la Polisi,
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akiwahutubia Wananchi na Askari wa Jeshi la Polisi Pemba wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi  la nyumba ya makaazi ya Polisi Wilaya ya Micheweni Pemba.
 Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mhe: Omar Khamis Othman akimkaribisha Makamu wa pili wa rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kwenye hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la nyumba Polisi wilaya ya Micheweni, yenye vyumba kumi

Kamanda wa Polisi Wilaya ya Micheweni Pemba, Fakih Mohamed Yussuf akisoma risala ya ujenzi wa nyumba ya kulala aksari Polisi inayojengwa kwa pamoja na Jeshi hilo na wananchi, katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi uliofanywa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd. 
 Viongozi wa Jeshi la Polisi wakimsikiliza Makamu wa Pili wa rais Mhe: Balozi Seif Iddi, mara baada ya kuweka jiwe la msingi la nyumba za kulala askari Polisi wilaya ya Micheweni Pemba. 
 Baadhi ya Wananachi na Viongozi wa Chama na Serikali wakimsikiliza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi mara baada ya kuweka jiwe la msingi la nyumba za kulala askari Polisi wilaya ya Micheweni Pemba

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.