Habari za Punde

Maendeleo makubwa kisiwani Pemba ni matunda ya Sera za Ilani ya CCM


  
STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Pemba                               2.10.2015
---

WANANCHI kisiwani Pemba wametakiwa kuwachagua viongozi wa CCM ambao watakaa pamoja na wao na sio wale viongozi wanaowachagua kutoka vyama vya upinzani ambao wakishapata nafasi za uongozi huwakimbia na kutojali matatizo yao.

Hayo yalielezwa leo na baadhi ya Viongozi wa CCM Zanzibar, katika Mkutano wa  Kampeni ya uchaguzi wa CCM uliofanyika katika Jimbo la  Gando, Mkoa wa Kaskazini Pemba uliohudhuria na maelfu ya wanaCCM na wananchi ambapo mgeni rasmi alikuwa mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM, Dk. Ali Mohamed Shein.

Viongozi hao walieleza kuwa viongozi wa vyama vya upinzani wanaochaguliwa na wananchi kisiwani Pemba mara baada ya kupata nafasi za uongozi huhamisha makaazi yao kisiwani humo na kuwasahau waliowachagua.

Katika mkutano huo Balozi Seif alisema kuwa amekuwa akipata amaelezo kutoka kwa wanachama wa CUF kuwa hivi sasa wamechoka kudanganywa na kuwaambia kuwa umefika wakati wa wao kujiunga na CCM.

"CUF imekuwa sawa na timu ya mpira kila siku ikiingia uwanjani inapigwa mabao hiyo si timu kwa nini wewe ubaki huko njooni CCM Sera zake zinatekelezeka tizameni ndani ya miaka mitano ilivyofanya... na karibu tunatengeneza barabara ya Wete- Chake"alisema Balozi.


Alisema kuwa Dk. Ali Mohamed Shein amefanya mambo mengi ikiwa ni pamoja na kutekeleza ahadi ya kununua meli mpaa ambayo itaingia nchi wakati wowote na Dk. Shein ndie atakae izindua.

Aidha, alisema kuwa CCM haitaki fujo wala shari huku akishangwaza na mgombea urais wa CUF ambaye ameanza kugombea nafasi hiyo tokea ujana wake.

Aliwataka wananchi kujiunga na CCM kwani ni chama ambacho hakijawahi kushindwa.

Nae Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho alitumia fursa hiyo kueleza kuwa miundombinu ya barabara Pemba imeimarika na kutoa shukurani kwa Dk. Shein kwa maendeleo yaliopatikana kisiwa humo.

Kificho alisema kuwa Zanzibar imeimarika kutokana na amani iliyopo hatua ambayo imepelekea kukua kwa sekta za maendeleo ikiwemo sekta ya utalii.

Aidha, alisema kuwa chama vyama vya upinzani vimekuwa havina hoja kutokana na maendeleo makubwa yaliofikiwa kisiwani humo na ndio maana vimekuwa  havizungumzii kuhusu maji, barabara, umeme, afya, elimu na sekta nyenginezo hiyo ni kutokana na kuwa vyote hivyo vimetekelezwa na Serikali ya CCM.

Alieleza kuwa kinachofanywa na vyama hivyo hivi sasa ni kudandia hoja ambazo tayari zimekuwa zikifanyiwa kazi na Serikali kupitia Ilani ya Uchaguzi ya CCM chini ya uongozi wa Dk. Shein huku akieleza haja ya Dk. Shein kupewa kura za ndio ili maendeleo zaidi yaweze kupatikana Unguja na Pemba.

Aliwataka wananchi hao wa Pemba kutowachagua viongozi ambao mchezo wao ni kukimbia katika vyombo vya kutunga sheria kama walivyofanya katika Baraza la Wawakilishi, Bunge la Katiba na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nae Waziri Kiongozi Mstaafu Shamsi Vuai Nahodha aliwaomba wananchi wa Pemba kujua kuwa viongozi waa CUF wameshindwa kufanya kazi za siasa na kuwaauliza viongozi wa chama hicho hata kujenga madarasa wanasubiri mamlaka kamili.

Aliwataka wananchi wa kisiwa cha Pemba kufanya mabadiliko na kuwachagua viongozi wa CCM kwani viongozi wote waliowachagua katika uchaguzi uliopita wakiwemo Wawakilikishi, Wabunge na Madiwani wa CUF wameshindwa kuwatumikia wananchi.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa na Waziri wa Maji, Ardhi na Nishati Ramadhani Abdalla Shaaban  alisema kuwa iwapo wananchi watamchagua Dk. Shein suala la mafuta na gesi litafanyiwa kazi vizuri kutokana na juhudi zake alizokwisha kuzianza.

Alisema kuwa suala la mafuta na gesi halikuanza leo kwa sababu watu ya kupiga kuwa kwani suala hilo limeanza tokea mwaka 1951 na Serikali iliyoopo amdarakanai inaendelea.

Alisema kuwa tokea alipoingia madarakani kuwa Waziri wa Wizara hiyo tayari Dk. Shein ameshaweka nguvu kubwa katika kuiendeleza sekta hiyo kwa ziara mbali mbali duniani na hadi leo amekuwa akiihangaikia kazi hiyo na anaiweza.

Aliwataka wananchi kutodanganyika kwani mafuta na gesi hayachimbwi kwa siku mia moja kama wanavyoelezwa na viongozi wa chama cha CUF.

Nae Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai aliwapongeza wananchi wa Pemba kwa kuhudhuria kwa wingi katika mikutano ya Kampeni za CCM na kuomba kwamba kutokana na kiu ya wananchi kutaka kuirimbua meli mpya inayotarajiwa kuwasili hivi karibuni iwachukue bure wananchi wa Pemba na akuwapeleka Unguja kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Dk. Shein.

Alisema kuwa CCM mara hii itahakikisha inapata Majimbo yote ya Zanzibar na kuwaomba wazee, vijana pamoja na makundi yote kumchagua Dk. Shein kutokana na uwezo wake mkubwa wa kuleta maendeleo na kuweza kuwaunganisha wananchi.

Sambamba na hayo, Vuai alisema kuwa Dk. Shein ni kiongozi wa watu kwani hana ubaguzi, hana choyo wala hana makuu pia, ni kiongozi ambaye anasimamia Katiba ya nchi bi la kumuogopa mtu yoyote.

Bi Zainab alisema kuwa katika uchaguzi wa mwaka huu wanaCCM wa Pemba wanatakiwa kushinda kwa kishindo na kupata viti kupitia wagombea wake.

Nae Bi Modlin Kastiko alisema kuwa kuna kila sababu ya kumchagua Dk. Shein kutokana na juhudi zake kubwa za kuimaarisha sekta za maendeleo ambazo  zimeimarika kwa upande wa Unguja na Pemba zikiwemo miundombinu ya barabara, elimu, afya, maji, umeme na nyenginezo.

Alisema kuwa hivi sasa kumekuwa kukitokezea vitisho vya kila aina na tayari wapo wanaCCM waliochomewa moto nyumba zao kwa sababu ya kukataa kutoa kadi zao za kupigia kura kisiwani humo.

Kastiko aliwataka akina mama, vijana pamoja na wananchi wote wa Pemba wasikubali kutishwa licha ya  vitimbi vinavyoendelea kufanywa na wafuasi wa vyama vya upinzani huku akiwataka kuwapigia kura viongozi wa CCM ili kuimarisha amani na utulivu.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.