Na Skolastika Tweneshe-Maelezo
Fedha zitakazopatikana katika Tamasha la mkesha wa kuombea
amani nchini zitatumika kuwasaidia watu wenye
mahitaji hasa
afya ya mama na mtoto.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti
wa Jumuiya wa Makanisa ya
Pentekoste , ambaye pia ni Askofu wa huduma ya Tanzania Fellowship Churches
(TFC), Askofu Godfrey Malassy
alipokuwa
akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
Malassy alisema kwamba, fedha zitakazopatikana katika tamasha
hilo zitanunua vifaa vinavyotumia nishati ya jua (solar Panels) ili
kuwasaidi
wamama wajawazito na watoto wanaozaliwa.
“Kina mama wajawazito na watoto wanakufa mahospitalini
kutokana na kukosa umeme hasa vijijini, hivyo tumeamua fedha
zitakazopatikana mkesha
huu tutanunua solar” alisema Malassy
Aidha Askofu Malassy amewaomba wananchi kuzidi
kumuombea Rais John Magufuli katika
kuliongoza Taifa la
Tanzania ili aendelee kufanya kazi yake kwa ufanisi ambayo
tayari
imekubalika ndani na nje ya nchi.
Mwenyekiti huyo alitambulisha kitabu kiitwacho IJUE SIRI YA
AMANI
KWA TAIFA ambacho kinauzwa Sh.5000 amesema
kuwa kitabu hicho kina lengo la kuelimisha thamani
na jukumu la
watanzania kuilinda Amani
bila kujali itikadi za dini,
siasa wala
ukabila
Pia ameomba kwa atakaeguswa na matatizo yanayowakumba
wamama wajawazito
anaweza kutuma mchango wake kwa namba
zifuatazo
0755202204,0719202204,0684202204.
Mkesha huo ni wa 18
tangu uanze kufanyika na mwaka huu
utafanyika katika Uwanja wa Uhuru usiku
wa tarehe 31 ambapo
mgeni rasmi atakuwa Rais wa Awamu ya Tano Mhe. John Pombe
Magufuli.
No comments:
Post a Comment