Habari za Punde

Tasaf yafanya mafunzo ya wakufunzi wa maeneo ya mradi wa kaya masikini


AFISA Mdhamini wizara ya nchi afisi ya Makamu wa pili wa rais Pemba (katikati), Issa Juma Ali akisalimiana na Mkurugenzi wa Uratibu kutoka TASAF makao makuu, Alphonce Kyriga, wakati mdhamini huyo akiwasili kwenye ukumbi wa TASAF Pemba, kwenye mafunzo ya wakufunzi wa maeneo ya mradi juu ya uundaji na utoaji mafunzo kwa kaya masikini, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

MRATIBU wa mafunzo ya wakufunzi wa maeneo ya mradi, juu ya uudaji na utoaji mafunzo kwa kaya masikini, Catherine Kisanga, akielezea jinsi TASAF ilivyojipanga katika kukuza pato la walengwa, kwenye shehia na vijiji kadhaa Tanzania, mafunzo hayo yalifanyika ukumbi wa TASAF Chakechake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

 WAKUFUNZI wa maeneo ya mradi, juu ya uundaji wa utoaji wa mafunzo ya vikundi vya kuweka akiba kisiwani Pemba, wakisikiliza mada zinavyowasilishwa, kwenye mafunzo ya siku tano yaliofanyika ukumbi wa TASAF Chakechake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 AFISA Mdhamini wizara ya nchi afisi ya makamu wa pili wa rais Pemba, Issa Juma Ali akielezea jinsi TASAF inavyoweza kuwakomboa watu wanaoishi kwenye wingu la umaskini, kwenye mafunzo ya wakufunzi ya uundaji na utoaji wa mafunzo ya kuweka akiba, kulia ni Mkurugenzi wa Uratibu  TASAF Alphonce Kyriga, na kushoto ni Msaidizi wa Makamu wa pili Pemba Amran Massoud Amran, (Picha na Haji Nassor, Pemba).  
 MKURUGENZI wa Uratibu TASAF Tanzania, Alphonce Kyriga, akifungua mafunzo ya uundaji wa utoaji wa mafunzo ya vikundi vya kuweka akiba, kwa wakufunzi wa Kisiwani Pemba, kulia ni Mratibu wa TASAF Pemba Mussa Issa Kisenge na kushoto ni Afisa Mdhamini wizara ya nchi afisi ya Makamu wa pili Pemba Issa Juma Ali, (Picha na Haji Nassor, Pemba). 


 MSAIDIZI wa Makamu wa pili wa rais Pemba Amran Massoud Amran akitoa neno la shukuran, kwenye mafunzo ya uundaji wa utoaji wa mafunzo ya vikundi vya kuweka akiba, kwa wakufunzi wa Kisiwani Pemba, mafunzo yaliofanyika afisi ya TASAF Chakechake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 PICHA ya pamoja ya watendaji wa TASAF makao makuu Tanzania bara na kisiwani Pemba, pamoja na wakufunzi wa mafunzo ya vikundi vya kuweka akiba kwa wale waliokwenye mpango wa kunusuru kaya maskini kisiwani Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MRATIBU wa TASAF Pemba Mussa Said Kisenge akichangia jambo kwenye mafunzo ya wakufunzi ya vikundi vya kuweka akiba kwa wale waliokwenye mapango wa kunusuru kaya masikini, mafunzo yaliofanyika TASAF Chakechake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).    

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.