HOTUBA YA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA
OFISI YA MAKAMU
WA PILI WA RAIS KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017
KATIKA BARAZA
LA WAWAKILISHI LA ZANZIBAR
-------------------------------------------
1.0
Mheshimiwa
Spika,
naomba kutoa hoja kwamba Baraza lako Tukufu lipokee na lijadili na hatimae
likae kama Kamati ya Mapato na Matumizi ili liidhinishe Makadirio ya Mapato na
Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa
Rais kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
2.0
Mheshimiwa
Spika, awali
ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kutujaalia afya njema na kuweza
kutukutanisha hapa leo kwa ajili ya kuipokea hotuba hii, kuijadili na hatimae kuidhinisha
Makadirio ya Mapato na matumizi ili tupate nyenzo za kutuwezesha kuwatumikia
wananchi wetu.
3.0
Mheshimiwa
Spika, namshukuru
na kumpongeza kwa dhati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein kwa juhudi zake anazozichukua katika kuiongoza
nchi yetu. Mheshimiwa Rais amekuwa akitoa maelekezo na miongozo inayotekelezeka
na yenye muelekeo wa kutuletea maendeleo na tija katika nchi yetu. Hotuba
aliyoitoa wakati akilizindua Baraza la Tisa (9) la Wawakilishi imeonesha wazi
azma yake ya kuwahudumia wananchi na kuwaletea maendeleo katika nyanja zote. Ni
imani yangu kwamba wananchi wote tutaendelea kumuunga mkono Mheshimiwa Rais
katika juhudi zake hizi.
4.0
Mheshimiwa
Spika, aidha,
nachukua fursa hii kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kazi kubwa aliyoifanya katika
kipindi kifupi cha uongozi wake chini ya kauli mbiu ya “Hapa Kazi Tu”. Pia
nawapongeza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia
Suluhu Hassan na Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa kwa kumsaidia
vyema Mheshimiwa Rais Magufuli katika kufanikisha majukumu yake.
5.0
Mheshimiwa
Spika,
naomba nitumie fursa hii kukupongeza wewe Mheshimiwa Spika pamoja na wasaidizi
wako kwa kuliongoza vyema Baraza hili Tukufu. Aidha, nawapongeza Wenyeviti na
Wajumbe wa Kamati za Kudumu za Baraza kwa kuteuliwa na kuanza vyema kazi za
kusimamia utendaji wa Taasisi za Serikali.
Vile vile, natoa shukrani maalum kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya
Kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa Mheshimiwa Omar Seif Abeid,
Mwakilishi wa Wananchi wa Jimbo la Konde, Makamu Mwenyekiti, Mheshimiwa Panya
Ali Abdalla, Mwakilishi wa Viti Maalum na Wajumbe wote wa Kamati hiyo kwa
kuyapitia Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais ya
mwaka 2016/2017 na kutupatia ushauri na miongozo juu ya Makadirio hayo na kuikubali
iwasilishwe katika kikao chako hichi kitukufu.
HALI
YA SIASA:
6.0
Mheshimiwa
Spika, Tume
ya Uchaguzi ya Zanzibar iliendesha Uchaguzi Mkuu wa marudio tarehe 20 Machi
2016. Jumla ya Vyama 14 vilishiriki
kugombea nafasi ya Urais ambapo Chama Cha Mapinduzi kiliibuka na ushindi wa
kishindo.
7.0
Mheshimiwa
Spika,
katika kipindi cha uchaguzi kulijitokeza hali ya uvunjifu wa amani kwa baadhi
ya wananchi kuchoma moto mali za Serikali na za wananchi wenzao vikiwemo vituo
vya afya, mashamba ya mikarafuu na nyumba za makaazi. Aidha, kumejitokeza tabia
kwa baadhi ya wananchi kususiana na kubaguana kutokana na tofauti za itikadi za
kisiasa katika shughuli mbali mbali za kijamii na kiuchumi. Hata hivyo, Serikali
inaendelea kuchukua hatua madhubuti za kuhakikisha hali ya umoja, amani na
utulivu inaendelea nchini. Nachukua fursa hii kutambua mchango mkubwa wa vyombo
vya Ulinzi na Usalama katika kusimamia amani ya nchi yetu. Nawaomba wananchi waendelee kushirikiana
katika shughuli zao za kijamii pamoja na kutoa ushirikiano kwa viongozi wa
ngazi zote za Serikali katika kudumisha hali ya umoja, amani na utulivu.
HALI YA UCHUMI WA ZANZIBAR:
8.0
Mheshimiwa
Spika, kama alivyoeleza Waziri wa Fedha na Mipango
wakati akiwasilisha Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 katika
Baraza lako Tukufu, uchumi wa Zanzibar umekua kwa asilimia 6.6 mwaka 2015
ikilinganishwa na ukuaji wa wastani wa asilimia 4.0 kwa nchi zinazoendelea na
asilimia 3.4 kwa nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara. Hata hivyo, kasi hiyo
inaashiria kupungua kidogo ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 7.0 mwaka 2014.
9.0
Mheshimiwa
Spika, pato
halisi la Taifa kwa mwaka 2015 limeongezeka na kufikia thamani ya Shilingi 2,308.0
Bilioni ikilinganishwa na thamani ya Shilingi 2,133.5 Bilioni mwaka 2014. Vile
vile, wastani wa pato la mtu binafsi limeongezeka kufikia Shilingi 1,632,000
sawa na Dola za Kimarekani 817
mwaka 2015 kutoka Shilingi 1,552,000 sawa na Dola za Kimarekani 939 mwaka 2014 kwa bei za miaka
husika. Kushuka kwa thamani ya sarafu ya Tanzania dhidi ya Dola ya Kimarekani
kwa wastani wa asilimia 20.8
mwaka 2015 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 3.4 mwaka 2014 imepelekea thamani ya pato la Mtu binafsi kwa
Dola kupungua. Hata hivyo, kwa kutumia bei za kudumu za mwaka 2007 bado wastani
wa pato la mtu binafsi limeongezeka kutoka Dola za Marekani 651 mwaka 2014 hadi
Dola 674 mwaka 2015.
10.0
Mheshimiwa
Spika, kasi
ya mfumko wa bei imefikia wastani wa asilimia 5.7 mwaka 2015 kutoka asilimia
5.6 mwaka 2014. Kasi ya mfumko wa bei kwa bidhaa za chakula umeongezeka kufikia
asilimia 7.4 mwaka 2015 kutoka asilimia 4.4 mwaka 2014. Aidha, mfumko wa bei
kwa bidhaa, zisizo za chakula ulishuka hadi kufikia asilimia 4.0 mwaka 2015
kutoka asilimia 6.8 mwaka 2014. Hali hii inatokana na kushuka kwa bei za bidhaa
za mafuta ikiwemo dizeli, petroli na mafuta ya taa.
11.0
Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2016/2017 maeneo muhimu yatakayoendelea kupewa kipaumbele na
Serikali ni pamoja na kuhakikisha mapato ya Serikali yanakusanywa kikamilifu,
kusimamia utunzaji na uendelezaji wa miundombinu na mawasiliano, kuendeleza
utalii, kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ya kilimo, kuimarisha huduma
za elimu, afya, pamoja na maslahi ya wazee nchini.
12.0
Mheshimiwa
Spika, kuhusu
suala la Mafuta na Gesi, Serikali imekamilisha utayarishaji wa Rasimu ya
Sera na Rasimu ya Sheria ya Mafuta na Gesi Asilia ambazo zinatarajiwa
kukamilika katika mwaka wa fedha 2016/2017. Kukamilika kwa sera na sheria hizo kutaiwezesha
Serikali kuwa na miongozo mizuri katika kusimamia masuala ya Mafuta na Gesi
Asilia hapa nchini.
13.0
Mheshimiwa
Spika,
katika kuhakikisha wananchi wa
vijijini wanapata huduma za umeme, Serikali imejenga njia za kupitishia umeme
mkubwa zipatazo kilomita 33.1 na
kilomita 83.9 za laini ndogo. Aidha,
Serikali imeweka transfoma 35 za kusambaza umeme katika vijiji
36 (Unguja vijiji 16 na Pemba 20).
14.0
Mheshimiwa
Spika, Sekta
ya Viwanda inaendelea kuimarika na tunategemea itachangia kwa kiasi kikubwa
katika kukuza uchumi na kutoa ajira kwa wananchi. Kuanza kazi kwa Kiwanda cha Sukari
cha Mahonda kunatoa matumaini ya kujitegemea kwa sukari hapo baadae. Pia Kiwanda
cha Upigaji Chapa, Kiwanda cha Maziwa Fumba, viwanda vya maji na viwanda
vyengine mbali mbali vikiwemo vya uchongaji na usindikaji vinatoa mchango
mkubwa katika ukuzaji wa uchumi wetu.
HUDUMA
ZA JAMII:
15.0
Mheshimiwa
Spika, huduma
za jamii zitaendelea kupewa msukumo mkubwa katika kipindi hiki cha pili cha Awamu
ya Saba. Serikali itaendelea kuchukua
hatua mbali mbali za kuimarisha huduma za elimu, afya, maji safi na salama
pamoja na makaazi ili kuleta ustawi mzuri kwa jamii.
16.0
Mheshimiwa
Spika, sekta
ya elimu ni muhimu sana katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Sekta hii ina jukumu la kutoa elimu
kwa wananchi wa Zanzibar kwa mujibu wa malengo yaliyoainishwa katika Mipango na
Sera ya Elimu, Dira ya Maendeleo 2020 na MKUZA. Katika kufikia malengo hayo,
Serikali itaendelea kuimarisha Skuli za Maandalizi, Msingi na Sekondari, Elimu
Mbadala pamoja na Elimu ya Juu.
17.0
Mheshimiwa
Spika, Serikali
inaendelea kutekeleza programu mbali mbali za elimu ikiwemo programu za vituo
vya Tucheze Tujifunze (TuTu) na kufanya tathmini ya vituo hivyo pamoja na kusaidia
watoto wenye mahitaji maalum kwa kuwapatia vifaa. Aidha, Serikali inaendelea na
ujenzi wa vituo viwili (2) vya mafunzo ya Amali Makunduchi kwa Unguja na Daya
kwa Pemba; Upanuzi wa Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia; Upanuzi wa
Chuo cha Maendeleo ya Utalii pamoja na Kukamilisha Kituo cha Elimu Mbadala – Wingwi
Mtemani ili kuwajenga vijana kitaaluma
na kiujuzi ili waweze kuingia katika soko la ajira kwa uhakika.
18.0
Mheshimiwa
Spika, kwa
upande wa Sekta ya Afya, Serikali imeendelea kuimarisha huduma za afya kwa
wananchi kwa kuifanya Hospitali ya Mnazimmoja kuwa ya Rufaa kwa kuiongezea
huduma za matibabu ya saratani, kuimarisha huduma za uchunguzi (Magnetic Resonance
Imaging - MRI). Hospitali za Abdalla Mzee na Wete Pemba pia zimeendelea
kuimarishwa ili zifikie hadhi ya kuwa Hospitali za Mkoa.
19.0
Mheshimiwa
Spika, Serikali
itaendelea kushirikiana na Washirika mbali mbali wa Maendeleo katika
utekelezaji wa Miradi/Programu za Afya
ikiwemo; Programu ya Kuimarisha Miundombinu ya Afya, Programu ya Kudhibiti
Maradhi ya Malaria, Mradi Shirikishi wa UKIMWI na Kifua Kikuu, Programu
Shirikishi ya Huduma za Afya ya Uzazi wa Mama na Mtoto na Mradi wa Taaluma za
Afya. Ni matumaini yangu kuwa shughuli zote hizi zilizopangwa zitatekelezwa kwa
ufanisi na kwa maslahi ya wananchi wote.
20.0
Mheshimiwa
Spika, kwa
upande wa Sekta ya Uwezeshaji, Serikali inaendelea kukabiliana na changamoto za
ajira kwa kuwajengea uwezo vijana ili waweze kujiajiri na kuajirika. Aidha,
kupitia Mfuko wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Serikali inaendelea kusimamia
jukumu la kutoa mitaji kwa wananchi wenye kipato kidogo ili watumie katika
shughuli za uzalishaji mali kwa kujiajiri na kupunguza umasikini. Mfuko huo
umefanikiwa kutoa jumla ya mikopo 307 yenye thamani ya Shilingi Milioni
467,278,000. Mikopo hiyo imeelekezwa katika shughuli za kilimo, ufugaji, uvuvi,
kazi za mikono, usindikaji matunda, viwanda vidogo vidogo vya mafuta ya nazi na
mafuta ya mgando pamoja na viwanda vya sabuni za kufulia na kukogea.
21.0
Mheshimiwa Spika,
kwa upande wa Sekta ya Ujenzi, Serikali inaendelea na ujenzi na matengenezo ya barabara
mbali mbali za Unguja na Pemba ili kuimarisha huduma za usafiri kutoka sehemu
moja kwenda nyengine. Katika kipindi cha 2015/2016 miongoni mwa Barabara zinazoendelea
na ujenzi ni pamoja na Ole - Kengeja yenye urefu wa kilomita 35, Jendele – Cheju
- Kaebona yenye urefu wa kilomita 11.6 na Koani - Jumbi yenye urefu wa kilomita
6.4. Aidha, matengenezo makubwa ya barabara yamefanyika kwa barabara kuu na za
ndani.
22.0
Mheshimiwa Spika,
kwa upande wa uimarishaji wa usafiri wa anga, Serikali inaendelea na kazi ya
ujenzi wa jengo jipya la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha
Abeid Amani Karume na kazi hiyo inategemewa kukamilika katika mwaka wa fedha
2017/2018.
MASUALA
MTAMBUKA:
Mazingira:
23.0
Mheshimiwa
Spika, utunzaji
wa mazingira ni suala la lazima na ni muhimu kulitekeleza ili kuleta maendeleo endelevu
na kupunguza umasikini nchini kwetu. Nchi zote duniani na mashirika mbali mbali
ya kimataifa yanatoa kipaumbele katika suala la kukabiliana na Mabadiliko ya
Tabianchi ili kupunguza athari zinazotokana na hali hiyo. Kwa kutambua umuhimu
huo, Serikali imekuwa ikihimiza wananchi kutunza maeneo ya misitu na kupanda
miti kwa wingi maeneo ya wazi ikiwemo fukwe za bahari pamoja na kuachana na
tabia ya kukata miti ovyo na uchimbaji wa rasilimali zisizorejesheka.
Athari za mvua za
Masika:
24.0
Mheshimiwa
Spika, siku
ya tarehe 17 Aprili, 2016 ilinyesha mvua kubwa iliyofikia milimita 212.4 na
kusababisha mafuriko katika maeneo mengi hasa ya Mkoa wa Mjini Magharibi.
Kufuatia mvua hiyo, jumla ya nyumba 3,330 zenye kaya 4,712 ziliathirika na
kuilazimu Serikali kufungua kambi maalum katika Skuli ya Mwanakwerekwe C ili
kuwahudumia wananchi hao. Jumla ya watu
420 walihifadhiwa na kupatiwa huduma mbali mbali za kibinaadamu katika kambi
hiyo. Athari nyengine zilizotokana na mvua hizo ni upotevu wa maisha ya mtu
mmoja pamoja na kupotea kwa mali za wananchi. Nachukua fursa hii kuwapa pole
wale wote waliopata athari ya mvua hizi. Naomba kuwanasihi wananchi wenzangu
tuache kujenga katika maeneo ya mabondeni na katika njia za maji. Aidha,
naziagiza Mamlaka zinazohusika na utoaji wa viwanja na vibali vya ujenzi
wafuate taratibu zilizowekwa ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza.
25.0
Mheshimiwa Spika, mwanzoni
mwa mwezi wa Septemba 2015, visiwa vyetu vya Zanzibar vilikabiliwa na ongezeko
kubwa la wagonjwa wa maradhi ya kuharisha na kutapika yaliyoripotiwa katika Vituo
vya Afya vilivyopo Unguja na Pemba. Baada ya kupata matokeo ya uchunguzi wa
kimaabara, ilithibitika kuwepo kwa mripuko wa maradhi ya kipindupindu. Kufuatia
mripuko huo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushirikiana na Washirika wa
Maendeleo, imeendelea kuchukua jitihada za dhati katika kukabiliana na maradhi
haya.
26.0 Mheshimiwa Spika, Serikali ilifungua kambi
maalum za matibabu ya kipindupindu Unguja na Pemba, ambapo hadi kufikia tarehe 11 Mei, 2016 jumla ya wagonjwa 3,897 walilazwa na kutibiwa. Kati ya hao,
wagonjwa 2,450 walilazwa katika kambi za Unguja na wagonjwa 1,447 walilazwa katika
kambi za Pemba. Jumla ya wagonjwa 59 wameripotiwa kufariki (46 Unguja na 13
Pemba).
27.0
Mheshimiwa
Spika,
mripuko wa maradhi haya katika kipindi hiki, umechukua muda mrefu zaidi kuliko
miaka ya nyuma. Sababu kubwa zilizopelekea hali hiyo ni wananchi kutofuata
kanuni za afya na usafi wa mazingira.
Hata hivyo, ni jambo linalotia matumaini kuona kwamba maradhi haya
tumeanza kuyadhibiti baada ya kuchua hatua mbali mbali. Nawaomba wananchi tuongeze
juhudi za kusafisha mazingira yetu pamoja na kufuata miongozo na kanuni za afya.
Aidha, nachukua fursa hii, kuwashukuru na kuwapongeza kwa dhati watendaji wote
ambao kwa namna moja ama nyengine wanashiriki katika hatua za kulitokomeza janga
hili.
Masuala ya Watu Wenye Ulemavu:
28.0
Mheshimiwa Spika, suala la udhalilishaji kwa
Watu wenye Ulemavu ikiwemo ubakaji,
kupigwa, kutelekezwa, kuitwa majina mabaya na kunajisiwa ni kubwa katika jamii
yetu. Serikali inaendelea na juhudi za kudhibiti vitendo hivi vya udhalilishaji
na itaendelea kuchukua hatua kwa wale wote watakaojihusisha na vitendo hivyo. Kwa
mantiki hiyo, naviagiza vyombo vya kusimamia haki na sheria kutimiza wajibu wao
ikiwa ni pamoja na kuzishughulikia kesi za namna hii kwa haraka na kuwapatia
haki watu wenye ulemavu ili kulinda utu wao. Pia, naiasa jamii kuacha vitendo
vya udhalilishaji kwa Watu Wenye Ulemavu kwani wao pia ni binaadamu na
wanastahiki kuheshimiwa na kutendewa haki na kupatiwa fursa sawa katika jamii.
Uwajibikaji,
Utawala Bora na Mapambano dhidi ya Rushwa:
29.0
Mheshimiwa
Spika,
wakati wa kulizindua Baraza lako hili Tukufu tarehe 05 Aprili, 2016 Mheshimiwa
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, alilikemea kwa nguvu zake
zote suala la rushwa na kusisitiza masuala ya uwajibikaji na utawala bora.
Katika kufikia azma hiyo Serikali inaendelea kutekeleza Sheria ya Kuanzisha
Mamlaka ya Kupambana na Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar Namba 1 ya mwaka 2012
pamoja na Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Namba 4 ya mwaka 2015. Hatua za
utekelezaji wa Sheria hizi unaendelea ambapo hivi karibuni Mheshimiwa Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi amemteuwa Mwenyekiti wa Tume ya
Kusimamia Maadili ya Viongozi ili Tume hiyo iweze kuanza kazi rasmi.
Hali ya Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI:
30.0
Mheshimiwa
Spika, kiwango
cha maambukizi ya Virusi vya UKIMWI hapa Zanzibar ni asilimia 1 na kuwa ni
miongoni mwa nchi chache kusini mwa Jangwa la Sahara yenye kiwango cha chini
cha maambukizi ya UKIMWI. Maambukizi haya yanawaathiri zaidi wanawake kuliko
wanaume kwa uwiano wa 3 kwa 1. Hata hivyo, kuna makundi maalum ambayo kiwango
cha maambukizi ni kikubwa ukilinganisha na kile kilichomo katika jamii. Makundi
hayo ni wanawake wanaojiuza (19.3), wanaojidunga dawa za kulevya (11.3) na
wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume wenzao (2.9). Serikali itaendelea na
jitihada za kupambana na ongezeko la maambukizi kwa makundi yote haya na jamii
kwa jumla. Natoa wito kwa wananchi kuendelea kubadili tabia na kudhibiti
mazingira hatarishi kwa maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na kuacha kuwanyanyapaa
watu wenye maambukizo ya Virusi vya UKIMWI.
Mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya:
31.0
Mheshimiwa Spika,
Dawa za Kulevya bado ni tatizo sugu duniani
kote na hapa Zanzibar linaendelea kutuathiri siku hadi siku. Hali halisi
inaonesha kwamba vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa ndio wanaoathirika zaidi
na matumizi ya dawa hizo. Katika kupambana
na changamoto hii Serikali kwa kushirikiana na wadau inaendelea kuchukua hatua
za kuondoa kabisa usafirishaji na usambazaji, matumizi na athari zinazotokana
na matumizi ya dawa hizo. Hivyo, nachukua fursa hii, kuvitaka vyombo vyote
vinavyosimamia udhibiti wa dawa za kulevya kufanya kazi hiyo kwa uadilifu
mkubwa ili kurahisisha utekelezaji wa mipango ya udhibiti wa dawa hizo.
MALENGO
NA UTEKELEZAJI WA KAZI ZA KAWAIDA NA MIRADI YA MAENDELEO KWA
KIPINDI CHA MIEZI TISA (JULAI-MACHI) 2015/2016:
32.0
Mheshimiwa
Spika, katika kipindi cha miezi tisa (Julai - Machi) cha
mwaka wa fedha 2015/2016, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais na Taasisi zake
imechukua juhudi kubwa katika kutekeleza malengo iliyojipangia katika Programu zake
kama ifuatavyo:-
1. Programu
ya Uratibu wa Shughuli za Makamu wa Pili wa Rais (C011):
|
33.0
Mheshimiwa
Spika, Katika mwaka wa fedha 2015/2016
Programu hii imetekeleza kazi zifuatazo:-
i)
Ofisi
imeratibu ziara 16 za ndani ya nchi pamoja na kutekeleza ahadi 10 za masuala
mbali mbali zilizoahidiwa na Mheshimiwa Makamu wa Pili wa Rais;
ii)
Ili
kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa nchi na Taasisi mbali mbali za ndani na
nje ya nchi, Kikanda na Kimataifa, Mheshimiwa Makamu wa Pili wa Rais alikutana
na Wageni Mashuhuri na Mabalozi wa nchi 14.
iii)
Ofisi
imefanya matengenezo makubwa katika nyumba ya makaazi ya Mheshimiwa Makamu wa
Pili wa Rais Mazizini na Dar es Salaam;
iv)
Ofisi
imempatia mafunzo ya muda mrefu mfanyakazi mmoja nje ya nchi. Aidha imewalipa stahiki za likizo wafanyakazi
watano (5).
2. Programu ya Uratibu wa Shughuli za
Serikali (CO12):
|
34.0
Mheshimiwa
Spika, Kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Programu hii imetekeleza
kazi zifuatazo: -
i.
Ofisi
imetayarisha Taarifa ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuhusu Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya
2010 - 2015 kwa kipindi cha miaka mitano (Novemba, 2010 hadi Julai, 2015).
ii.
Ofisi
imeendelea kuratibu utekelezaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo, ikiwa ni pamoja
na kufuatilia marejesho ya matumizi ya fedha za mwaka 2014/2015 pamoja na
kufuatilia miradi iliyotekelezwa kwa ufadhili wa Mfuko huo. Pia, Ofisi imeandaa
Rasimu ya Kanuni ya Sheria ya Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo ambayo inatarajiwa kuanza
kutumika katika mwaka wa fedha wa 2016/2017.
iii.
Ofisi
imeratibu na kusimamia utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (TASAF
III) unaotekelezwa katika Shehia 204 (Unguja 126 na Pemba 78). Katika kipindi cha miezi tisa, Ofisi imefanya
malipo kwa Kaya Masikini 33,632 (Unguja 18,944 na Pemba 14,688) ambapo jumla ya
Shilingi 6,188,276,000 zimelipwa. Aidha, mafunzo ya wataalamu 20 wa kisekta
kuhusu uibuaji na usanifu wa miradi 94 ya kutoa ajira za muda (Unguja 43 na
Pemba 51) yamefanyika. Mafunzo juu ya kujaza fomu za masharti ya elimu na afya
yametolewa kwa watumishi wa vituo vya afya na walimu 338 (Unguja 135 na Pemba
203) wa skuli zinazohusika na Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini kwa Unguja na
Pemba.
iv.
Ofisi
imeandaa muundo mpya na kutayarisha mapendekezo ya uendeshaji wa Ofisi ya
Uratibu wa Shughuli za SMZ Dar es Salaam.
v.
Ofisi imetoa mafunzo ya kujiandaa na kukabiliana na
maafa kwa wanafunzi wa skuli za Msingi na Sekondari kwa Wilaya za Kusini, Kati
na Kaskazini ‘B’ kwa Unguja, Mkoani na Chake Chake kwa Pemba ambapo jumla ya
wanafunzi 500 wa Skuli za Msingi na 490 wa Sekondari wamepatiwa mafunzo hayo.
vi.
Ofisi
imeratibu na kutoa huduma katika majanga na maafa yaliyotokea ndani ya visiwa
vya Unguja na Pemba yakiwemo maafa ya mafuriko, ajali za moto na maradhi ya
kipindupindu.
vii.
Ofisi
imeendesha mafunzo kwa wafanyakazi 22 wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais,
watano (5) kutoka Wilaya tano za Unguja na Pemba na mmoja kutoka ZBC radio
walishiriki katika ziara ya kimafunzo ya wiki moja juu ya kujiandaa na kukabiliana
na maafa katika Wilaya za Kinondoni, Kilosa na Chamwino Tanzania Bara. Aidha,
makongamano matatu ya kujiandaa na kukabiliana na maafa yameendeshwa kwa
wanafunzi kutoka Chuo cha Utawala wa Umma (IPA) na Chuo cha Usimamizi wa Fedha
(ZIFA) kwa upande wa Unguja pamoja na Chuo cha Ualimu Benjamin Mkapa kwa upande
wa Pemba.
viii.
Ofisi
imeratibu Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
ikiwa ni pamoja na kusimamia kilele cha Sherehe hizo zilizofanyika tarehe 12
Januari, 2016 Uwanja wa Amaan.
ix.
Ofisi
imeratibu Hitima na Dua ya Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume iliyofanyika
Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui tarehe 7 Aprili, 2016.
x.
Ofisi
imejenga kaburi la Rais Mstaafu wa Zanzibar wa Awamu ya Nne, Marehemu Sheikh
Idris Abdulwakil huko Makunduchi na kuendelea kusimamia mazingira ya eneo
lilipo kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume,
Kisiwandui.
3. Programu ya Usimamizi wa
Shughuli za Upigaji Chapa (C013):
|
35.0
Mheshimiwa
Spika, Kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Programu hii imetekeleza
yafuatayo: -
i.
Ofisi
imetayarisha Rasimu ya Sheria inayoipa mamlaka Kiwanda cha Upigaji chapa iwe
Taasisi inayojitegemea.
ii.
Ofisi
imechapisha nyaraka na machapisho mbali mbali ya Serikali kama vile Gazeti
Rasmi la Serikali, Miswaada ya Sheria, Sheria na machapisho mengine
yaliyowasilishwa kiwandani kwa mujibu wa mahitaji ya Taasisi husika.
iii.
Ofisi
imenunua mitambo mipya kwa awamu ya pili ambayo tayari imeshaanza kufungwa
kiwandani.
4. Programu ya Mipango na Utawala (C014):
|
36.0
Mheshimiwa
Spika, kwa mwaka wa
fedha 2015/2016 Programu hii imetekeleza kazi zifuatazo:-
i.
Ofisi
imefanikiwa kununua vifaa mbali mbali vya kuendeshea kazi ikiwa ni pamoja na kompyuta tatu (3); Aidha, Ofisi imelipia huduma za maji,
umeme, mawasiliano pamoja na kufanya matengenezo madogo madogo ya Ofisi.
ii.
Ofisi
imewapatia mafunzo ya muda mrefu wafanyakazi 28, wafanyakazi 27 wapya
wamepatiwa mafunzo ya awali (Induction
Course) pamoja na kulipia stahiki za likizo kwa wafanyakazi 72.
iii.
Ofisi
imefanya kikao kimoja cha Kamati ya Uongozi,
vikao vitatu vya Kamati ya Ukaguzi na kikao kimoja cha kujadili makisio ya
mishahara na maposho ya wafanyakazi. Aidha, Ofisi imeratibu na kusimamia vikao vitatu vya Bodi
ya Zabuni na kuendelea kulifanyia mapitio daftari la mali za Serikali.
iv.
Ofisi
inaendelea na utayarishaji wa ripoti ya tathmini ya mahitaji ya mafunzo ili
kuandaa mpango mkuu wa mafunzo.
v.
Ofisi
imeandaa Taarifa za Utekelezaji kwa kipindi cha mwaka mzima 2015/2016, miezi
sita (6) Julai - Disemba na taarifa ya Utekelezaji miezi mitatu (Oktoba –
Disemba) 2015/216. Aidha, Ofisi imetayarisha Mpango wa Matumizi wa Muda wa Kati
(MTEF) wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais.
vi.
Ofisi
kwa kupitia kitengo cha Kusimamia miradi ya Malaria, UKIMWI na Kifua Kikuu
inayofadhiliwa na Mfuko wa Dunia wa Kupambana na maradhi hayo (ZGFCCM)
imeendesha vikao viwili vya robo mwaka vya kawaida na Kikao kimoja cha dharura
pamoja na vikao vyengine vya Kamati vikiwemo Kamati ya “Oversight ommittee”,
Kamati Tendaji na Kamati ya Fedha. Aidha, Kitengo kimefanya uchaguzi wa kuwapata
wajumbe wake katika majimbo saba ya ZGFCCM ambayo yanaundwa na Sekta tofauti.
BARAZA LA WAWAKILISHI:
Programu ya 1: Kutunga Sheria, kupitisha Bajeti na
kusimamia Taasisi za Serikali (CO21):
|
|
Programu
ya 2: Uongozi na Utawala wa Baraza la
Wawakilishi (CO22):
|
37.0
Mheshimiwa
Spika, kwa mwaka wa
fedha 2015/2016 Baraza la Wawakilishi limetekeleza yafuatayo:-
i.
Ofisi
kupitia Baraza la Wawakilishi limekamilisha mkutano wa ishirini ambao ulikuwa
ni wa mwisho kwa Baraza la Nane (2010 – 2015).
ii.
Ofisi
kupitia Baraza la Wawakilishi ilisimamia uzinduzi wa Baraza jipya la Tisa.
iii.
Mafunzo
elekezi juu ya majukumu ya Mjumbe wa Baraza la tisa (9) yalitolewa.
iv.
Ofisi
imewapatia mafunzo watumishi 17 katika ngazi na fani mbali mbali, kama vile
Sheria, Utawala. Utawala wa Fedha, Utawala
wa rasilimali Watu. Ukatibu Muktasi,
Ukutubi, na Ukarani masjala kwenye ngazi ya Digrii ya Kwanza. Digirii ya Juu na Digrii ya Uzamivu.
TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR:
Programu ya 1: Uendeshaji wa Shughuli za Uchaguzi:
|
|
Programu
ya 2: Usimamizi wa Kazi za Utawala na
Uendeshaji wa Shughuli za Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar:
|
38.0
Mheshimiwa
Spika, Kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Tume ya Uchaguzi imetekeleza
yafuatayo:-
i.
Ofisi kupitia Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar imeendesha na kusimamia
Uchaguzi wa Rais wa Zanzibar, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi pamoja na
Madiwani.
ii.
Ofisi imesomesha wafanyakazi wawili kwa kiwango cha Shahada ya Pili na
Shahada ya Kwanza kwa lengo la kuongeza taaluma na kuleta ufanisi zaidi katika
utendaji wa kazi. Aidha, wafanyakazi
watatu walipatiwa mafunzo ya muda mfupi nchini Afrika ya Kusini yanayohusiana
na mambo ya Uchaguzi.
iii.
Ofisi
iliandaa Semina kwa Majaji na Mahakimu kwa lengo la kutatua migogoro na kesi za uchaguzi.
iv.
Ofisi
imeendesha makongamano
kwa vijana
ili wapate uelewa zaidi kuhusiana na Uchaguzi, kwa lengo la kuwaepusha
kujiingiza katika vurugu.
v.
Ofisi
kupitia Tume ya Uchaguzi kwa kushirikikiana na UNDP iliandaa Semina kwa Vyama
vya Siasa, vilivyoshiriki katika Uchaguzi.
vi.
Ofisi
kupitia Tume ya Uchaguzi kwa kushirikiana na UNDP imetoa elimu ya Mpiga Kura
katika maeneo mbali mbali
ya Unguja na Pemba kwa lengo la kuwawezesha wapiga kura kupata uelewa mzuri wa
Uchaguzi.
vii.
Ofisi
imenunua vifaa vya kuweka kumbukumbu za wapiga kura zikiwemo sava,
kompyuta na printa za kuchapisha kadi pamoja na kulipia huduma za mitandao.
UTEKELEZAJI
KIFEDHA KWA PROGRAMU:
39.0
Mheshimiwa Spika,
kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Baraza lako Tukufu liliidhinisha jumla ya Shilingi
625,568,698 kwa ajili ya Programu ya Uratibu wa Shughuli za Makamu wa Pili wa Rais. Hadi kufikia mwezi Machi, 2016 jumla ya Shilingi
357,646,714 zilipatikana na kutumika kwa kazi za kawaida ambazo ni sawa na
asilimia 57.2 Kiambatisho Nam. 1
40.0
Mheshimiwa Spika, katika
mwaka 2015/2016 Programu ya Uratibu wa Shughuli za Serikali ilipangiwa kutumia
jumla ya Shilingi 2,239,727,000 kwa
kazi za kawaida. Hadi kufikia mwezi wa Machi 2016, Programu hii imeingiziwa
jumla ya Shilingi 1,397,031,987
ikiwa ni sawa na asilimia 62. Kiambatisho Nam. 1.
41.0
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Baraza lako Tukufu
liliidhinisha jumla ya Shilingi 714,050,000
kwa Programu ya Usimamizi wa Shughuli za Upigaji Chapa. Hadi kufikia Machi 2016 jumla ya Shilingi 479,710,617 zimetumika kwa kazi za
kawaida ambazo ni sawa na asilimia 67.
Kiambatisho Nam. 1.
42.0
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Baraza lako Tukufu
liliidhinisha jumla ya Shilingi 1,587,354,000 kwa
Programu ya Mipango na Utawala. Hadi kufikia Machi 2016 jumla ya Shilingi
949,727,773 zimetumika kwa kazi za
kawaida ambazo ni sawa na asilimia 60. Kiambatisho Nam. 1.
43.0
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Baraza lako Tukufu
liliidhinisha jumla ya Shilingi 16,762,600,000 kwa programu za Baraza la Wawakilishi. Hadi kufikia Machi 2015
jumla ya shilingi jumla ya Shilingi. 4,546,691,512
zimetumika kwa kazi za kawaida ambazo ni sawa na asilimia 27. Kiambatisho
Nam. 1.
44.0
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Baraza lako Tukufu
liliidhinisha jumla ya Shilingi 1,404,000,000 kwa programu za Tume ya Uchaguzi. Hadi kufikia Machi, 2015 jumla
ya Shilingi 885,251,255 zimetumika kwa kazi za kawaida ambazo ni sawa na
asilimia 63. Kiambatisho Nam. 1.
UKUSANYAJI
WA MAPATO:
45.0
Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Makamu wa Pili wa
Rais inakusanya mapato kutoka Idara ya
Upigaji Chapa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali na Idara ya Sherehe na
Maadhimisho ya Kitaifa. Katika kipindi cha Miezi Tisa (Julai - Machi
2015/2016), Idara ya Upigaji Chapa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali ilipangiwa
kukusanya jumla ya Shilingi 600,000,000.
Hadi kufikia Mwezi Machi, 2016 Ofisi imekusanya jumla ya Shilingi 279,145,120 sawa na asilimia 47
ya lengo. Aidha, Idara ya Sherehe na Maadhimisho ya Kitaifa ilipangiwa
kukusanya jumla ya Shilingi
12,360,000. Hadi
kufikia mwezi wa Machi 2016, Ofisi imekusanya Shilingi 10,180,000
sawa na asilimia 82 Kiambatisho Nam. 2.
UTEKELEZAJI KWA TAASISI ZILIZOHAMISHIWA OFISI YA
MAKAMU WA PILI WA RAIS:
46.0
Mheshimiwa
Spika, kufuatia
mabadiliko ya Muundo wa Serikali yaliyofanyika katika Serikali ya Awamu ya Saba
kipindi cha Pili, Idara moja (1) na taasisi mbili (2) zilizokuwa chini ya
iliyokuwa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais zimehamishiwa katika Ofisi ya
Makamu wa Pili wa Rais. Taasisi hizo ni:-
i.
Idara ya Watu Wenye Ulemavu
ii.
Tume ya Kitaifa ya Kudhibiti na
Uratibu wa Dawa za Kulevya
iii.
Tume ya UKIMWI
IDARA YA WATU WENYE ULEMAVU:
Programu ya Usimamizi wa Masuala ya Watu
Wenye Ulemavu:
|
47.0
Mheshimiwa
Spika, kazi
za Programu hii zimetekelezwa na Idara ya Watu Wenye Ulemavu kama ifuatavyo:-
i.
Ofisi
imehudhuria Mikutano ya kupitia na kuandaa mpango kazi na Sera ya Watu Wenye
Ulemavu ya Afrika Mashariki iliofanyika Dar es Salaam na Kampala, Uganda.
ii.
Ofisi
imetoa elimu na kuhamasisha jamii juu ya upatikanaji wa haki na fursa kwa Watu
Wenye Ulemavu kupitia vipindi vya redio na televisheni, midahalo ya wanafunzi
pamoja na mikutano iliyofanywa kwa taasisi za umma na binafsi, vikundi vya watu
wenye ulemavu pamoja na kuzitembelea familia zenye watu wenye ulemavu Unguja na
Pemba.
iii.
Ofisi
kwa kushirikiana na watu binafsi imewapatia visaidizi Watu Wenye Ulemavu 48 (21
wanawake na 27 wanaume) Unguja na Pemba. Visaidizi hivyo ni pamoja na Viti vya
magurudumu mawili, viti vya chooni, magongo ya kutembelea na kusimamia.
TUME YA KITAIFA YA KURATIBU NA UDHIBITI WA DAWA ZA KULEVYA:
Programu ya Udhibiti wa
Dawa za Kulevya:
|
Programu ya Mipango na Utawala wa
Tume ya Kitaifa ya Kuratibu
na
Udhibiti wa Dawa za Kulevya:
|
48.0
Mheshimiwa Spika, kazi za Programu hizi zimetekelezwa na Tume ya
Kitaifa ya Kudhibiti na Uratibu wa Dawa za Kulevya kama ifuatavyo:-
i.
Ofisi imerusha hewani vipindi vinne (4) vya redio kwa lengo la kuelimisha jamii juu ya athari za Dawa za Kulevya, kufanya
ziara za utoaji taaluma kwenye Skuli 38 ambapo jumla ya wanafunzi 1620 (Wanawake
913, Wanaume 707) walipatiwa taaluma
hiyo. Pia ziara kama hizo zimefanyika kwenye Shehia 16 za Unguja na Pemba.
ii.
Ofisi imezipatia ruzuku nyumba 13 za Makaazi ya Vijana walioacha matumizi
ya Dawa za Kulevya (Sober Houses).
iii.
Ofisi kupitia Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za
Kulevya pamoja na wadau wengine imeandaa
muongozo wa kuwazawadia watoa taarifa kuhusu uingizaji na usambazaji wa dawa za
kulevya ambapo muongozo huo unasubiri vikao vya Tume kwa ajili ya kupatiwa
mapendekezo.
TUME YA UKIMWI:
Programu ya Kuratibu
Muitiko wa Taifa wa Ukimwi:
Programu
ya Utawala na Uendeshaji wa Tume ya Ukimwi:
49.0
Mheshimiwa Spika, kazi za Programu hizi zimetekelezwa na Tume ya UKIMWI
kama ifuatavyo:-
i.
Ofisi kupitia Tume ya UKIMWI imetoa mafunzo ya Sheria ya Kukinga na
Kusimamia Masuala ya UKIMWI Zanzibar (Nam.18 ya mwaka 2013) kwa wadau mbali mbali.
Aidha, Ofisi imetoa mafunzo kwa Viongozi 50 wa Taasisi za Kidini za Kiislamu na
Kikiristo Unguja na Pemba juu ya muongozo wa Taasisi za Kidini wa masuala ya
UKIMWI na afya ya uzazi kwa lengo la kuutambua muongozo huo na kuufanyia kazi.
ii.
Ofisi imeandaa Mkakati wa Tatu wa Taifa wa UKIMWI kwa mwaka 2016/2020 kwa
kuwashirikisha wadau mbali mbali ambao walitoa maoni ya vipaumbele,
shabaha na dira ya mkakati huo.
iii.
Ofisi imeandaa Jarida la JIHADHARI kwa kuchapisha nakala 5000 na
kusambazwa.
iv.
Ofisi imefanya ufuatiliaji na tathmini wa shughuli za UKIMWI ambapo
ilifanya ziara kwa wadau 16 na Shehia 49 Unguja na Pemba zinazotekeleza
shughuli mbali mbali za UKIMWI.
v.
Ofisi imetoa elimu kwa jamii juu ya masuala ya UKIMWI kupitia vipindi vya
redio, filamu, maonyesho ya sanaa pamoja na kuwapatia mafunzo ya stadi za
maisha vijana wenye ulemavu wa uziwi 60 na mafunzo ya ujasiriamali kwa
vijana 28 kutoka makundi maalum juu ya mbinu
za kujiongezea kipato ili kuepukana na tabia hatarishi.
UTEKELEZAJI KIFEDHA:
Mheshimiwa
Spika, Utekelezaji kifedha kwa Idara na Taasisi
hizi mbili ulikuwa kama ifuatavyo:-
50.0
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Baraza lako Tukufu liliidhinisha
jumla ya Shilingi 289,782,000
kwa Idara ya Watu Wenye Ulemavu. Hadi
kufikia Machi, 2016 jumla ya Shilingi 25,680,000
zimetumika kwa kazi za kawaida ambazo ni sawa na asilimia 8.8.
51.0
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Baraza lako Tukufu liliidhinisha
jumla ya shilingi 544,383,451 kwa Tume ya
UKIMWI. Hadi
kufikia Machi, 2016 jumla ya Shilingi 343,711,200 zimetumika
ambazo ni sawa na asilimia 60.
52.0
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Baraza lako Tukufu
liliidhinisha jumla ya Shilingi 351,218,753 kwa Tume ya Kitaifa
ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya. Hadi kufikia Machi, 2016 jumla ya Shilingi
237,449,000 zimetumika ambazo ni sawa na asilimia 70.
BAJETI
KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017:
53.0
Mheshimiwa
Spika, kutokana
na mabadiliko ya Muundo wa Serikali yaliyofanyika, Programu zilizo chini ya
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais pamoja na Taasisi zake zimeongezeka kutoka
programu kuu nane (8) na programu ndogo 14 hadi kufikia programu kuu kumi na
mbili (12) na programu ndogo ishirini na nne (24). Zifuatazo ni Programu Kuu:
i.
Uratibu
wa Shughuli za Makamu wa Pili wa Rais
ii.
Uratibu
wa shughuli za Serikali
iii.
Usimamizi
wa Shughuli za Upigaji Chapa
iv.
Mipango na Utawala
v.
Kutunga Sheria, kupitisha
Bajeti na kusimamia Taasisi za Serikali
vi.
Uongozi na Utawala wa Baraza
la Wawakilishi
vii.
Uendeshaji
wa Shughuli za Uchaguzi
viii.
Usimamizi
wa Kazi za Utawala na Uendeshaji wa Shughuli za Tume ya Uchaguzi ya
Zanzibar.
ix.
Udhibiti wa Dawa za Kulevya
x.
Utawala na Uendeshaji wa
Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya
xi.
Kuratibu Muitiko wa Taifa wa
UKIMWI
xii.
Utawala na Uendeshaji wa
Tume ya UKIMWI
54.0
Mheshimiwa
Spika, Ofisi
ya Makamu wa Pili wa Rais na Taasisi zake inatarajia kutumia jumla ya Shilingi 35,992,076,000 kwa ajili ya kutekeleza
program hizo kumi na mbili (12).
Programu ya kwanza: Uratibu wa
Shughuli za Makamu wa Pili wa Rais (C011):
|
55.0
Mheshimiwa
Spika, lengo
la Program hii ni kuimarisha utendaji wa kazi kwa Ofisi ya Faragha ya Makamu wa
Pili wa Rais. Matarajio ya muda mrefu ni
kuimarika kwa Ofisi hii na kutoa huduma bora kwa Mheshimiwa Makamu wa Pili wa
Rais. Huduma zinazotarajiwa kutolewa ni
kuratibu kazi za Mheshimiwa Makamu wa Pili wa Rais ikiwemo ziara za ndani na
nje ya nchi, mikutano na Mabalozi wa nchi mbali mbali, Wawakilishi wa Mashirika
ya Kitaifa na Kimataifa na mikutano na wananchi ya kusikiliza kero na
malalamiko yao.
56.0 Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha
2016/2017, Idara ya Faragha kupitia Programu ya (C011) ya Uratibu wa Shughuli
za Makamu wa Pili wa Rais imepanga kufanya
yafuatayo:-
a) Kuimarisha Ofisi ya Faragha kwa kuendelea
kuratibu ziara mbali mbali za ndani na nje ya nchi.
b) Kuimarisha uhusiano mwema na nchi rafiki kwa
kuongeza mashirikiano kwa kukaribisha wageni na Mabalozi wa nchi mbali mbali wa
Kitaifa na Kimataifa.
c) Kuratibu na kutekeleza ahadi zinazolenga
kuleta maendeleo katika jamii.
d) Kuyafanyia matengenezo makubwa Makaazi ya
Mheshimiwa Makamu wa Pili wa Rais yaliyoko Dar es Salaam na Dodoma pamoja na
kuimarisha huduma za usafiri.
e) Kuendelea kuwapatia mafunzo wafanyakazi
watatu (3) wa Ofisi ya Faragha katika kiwango cha Diploma pamoja na kuwapatia
stahiki za likizo wafanyakazi tisa (9).
Programu ya Pili: Uratibu wa
shughuli za Serikali (C012):
|
57.0
Mheshimiwa
Spika,
programu hii lengo lake kubwa ni kuweka mfumo imara na endelevu kwa Uratibu wa
Shughuli za Serikali, ambapo matarajio ya muda mrefu ni kutoa huduma bora za
Serikali kwa jamii.
Programu
hii ina programu ndogo tano ambazo ni: -
i. Kukabiliana na Maafa
ii. Sherehe na Maadhimisho ya Kitaifa pamoja na
Kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa.
iii. Shughuli za SMZ, SMT,
Utafiti na Masuala ya Muungano.
iv. Shughuli za Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar, Dar es Salaam
v. Usimamizi wa masuala ya watu
wenye mahitaji maalum.
Programu
ndogo C0121 Kukabiliana na Maafa:
58.0
Mheshimiwa Spika, Programu ndogo ya Kukabiliana na
Maafa ina lengo la kujenga uhimili wa
jamii katika kukabiliana na maafa kabla na baada ya kutokea. Huduma ambazo zinazotarajiwa
kutolewa ni Uratibu wa shughuli za Kukabiliana na Maafa ikiwemo kutoa mafunzo
kwa jamii, kuwahudumia waathirika wa majanga na maafa pamoja na kuandaa na
kutoa miongozo inayosimamia utekelezaji wa kazi za maafa.
59.0
Mheshimiwa
Spika,
katika mwaka wa fedha 2016/2017, Kamisheni ya Kukabiliana na Maafa kupitia
Programu ndogo (C0121) imepanga kufanya yafuatayo:-
a)
Kufanya tathmini na kutoa mafunzo ya
Kujiandaa na Kukabiliana na Maafa kwa Shehia 50 za Unguja na Pemba.
b) Kuijengea uwezo Kamisheni katika kujikinga,
kujiandaa, kukabiliana na kurejesha hali baada ya maafa.
c)
Kuandaa
Kanuni ya Sheria ya Kukabiliana na Maafa Namba 1 ya mwaka 2015.
d)
Kuendelea
kuandaa na kutoa miongozo inayosimamia utekelezaji wa kazi za maafa.
Programu
ndogo C0122: Uratibu wa Shughuli za Sherehe na Maadhimisho ya Kitaifa pamoja na
Kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa:
60.0
Mheshimiwa
Spika,
Programu ndogo ya Sherehe na Maadhimisho ya Kitaifa pamoja na Kuwaenzi Viongozi
wa Kitaifa ina lengo la kuwa na Sherehe zenye hadhi na kudumisha
historia na kumbukumbu za Viongozi Wakuu wa Kitaifa. Huduma ambazo zinatarajiwa kutolewa ni Uratibu wa shughuli za Sherehe na Maadhimisho ya Kitaifa pamoja na
Kuwaenzi
Viongozi wa Kitaifa.
61.0
Mheshimiwa
Spika,
katika mwaka wa fedha 2016/2017, Idara ya Sherehe na Maadhimisho ya Kitaifa
kupitia Programu ndogo (C0122) ya Uratibu wa Shughuli za Sherehe na Maadhimisho
ya Kitaifa pamoja na kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa imepanga kufanya yafuatayo:-
a)
Kuandaa mazingira mazuri ya Ofisi na
utendaji kazi kwa kununua vitendea kazi na kuendelea kulipia gharama za masomo
kwa wafanyakazi wawili (2).
b)
Kuratibu Maadhimisho ya Sherehe za
Miaka 53 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
c)
Kuratibu Hitma na Dua ya Marehemu
Sheikh Abeid Amani Karume na Viongozi wengine waliotangulia mbele ya haki.
d)
Kuratibu ushiriki wa Viongozi na
wananchi wa Zanzibar katika maadhimisho na sherehe za Kitaifa zitakazofanyika
nje ya Zanzibar.
e)
Kukamilisha mapitio ya Sheria Namba
10 ya mwaka 2002 ya kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa.
Programu
ndogo (C0123): Shughuli za SMZ, SMT, Utafiti na Masuala ya Muungano:
62.0
Mheshimiwa
Spika, katika
mwaka wa fedha 2016/2017 Programu ndogo ya
Uratibu wa Shughuli za SMZ, SMT, Utafiti na Masuala ya Muungano (C0123) imepanga kufanya yafuatayo:-
a)
Kuimarisha mfumo wa uratibu wa shughuli za
Serikali
b)
Kuratibu utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya
Chama Tawala (CCM) ya 2015 hadi 2020.
c)
Kuratibu shughuli za Muungano na Miradi ya
Muungano ndani ya Zanzibar, ikiwa ni pamoja na Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini
(TASAF III).
d)
Kuratibu shughuli za utafiti nchini.
Programu
Ndogo C0124: Shughuli za Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar Dar es Salaam:
63.0
Mheshimiwa
Spika, Programu ndogo ya Shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,
Dar es Salaam ina lengo la kuimarisha utoaji wa huduma kwa Taasisi za SMZ kwa
upande wa Tanzania Bara. Huduma inayotolewa ni Uratibu wa shughuli za Serikali
(SMZ) Dar es Salaam.
64.0
Mheshimiwa
Spika,
katika mwaka wa fedha 2016/2017, Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali Dar
es Salaam kupitia Programu ndogo (C0122) imepanga kufanya yafuatayo:-
a)
Kuimarisha mashirikiano baina ya
Ofisi ya uratibu shughuli za Serikali Dar es Salaam na Taasisi za SMZ na SMT,
Ofisi za Kibalozi na Taasisi za Kimataifa.
b)
Kukamilisha muundo mpya wa kitaasisi
na kiutumishi wa Ofisi.
c)
Kuweka mazingira mazuri ya kazi za
Ofisi kwa ununuzi wa vifaa vya Ofisi na samani.
d)
Kuwapatia mafunzo wafanyakazi wawili
(2) ili kuwaongezea utaalamu.
e)
Kufanya maandalizi ya awali ya ujenzi
wa jengo la ofisi ya Dar es Salaam.
Programu
Ndogo C0125: Usimamizi wa Masuala ya Watu
Wenye Ulemavu:
65.0
Mheshimiwa
Spika, Programu ndogo ya Usimamizi wa Masuala ya Watu wenye Ulemavu
ambapo lengo lake ni kupatikana kwa haki na fursa sawa kwa Watu wenye Ulemavu.
Huduma zinazotarajiwa kutolewa ni kuimarishwa ujumuishwaji wa watu wenye
ulemavu, uwezeshwaji wa watu wenye ulemavu na kukuza uelewa wa jamii juu ya
watu wenye ulemavu.
66.0
Mheshimiwa
Spika,
katika mwaka wa fedha 2016/2017, Idara ya Watu Wenye Ulemavu kupitia Programu ndogo (C0125)
ya Usimamizi wa Masuala ya Watu Wenye Ulemavu
imepanga kutekeleza yafuatayo:
a)
Kupitia
upya Sheria Nam.
9 2006 (HAKI NA FURSA) ya Watu wenye Ulemavu.
b)
Kusimamia
utekelezaji wa Sera, Sheria na Kanuni za Watu wenye Ulemavu.
c)
Kusimamia
upatikaji wa Haki na Fursa sawa za Watu wenye Ulemavu.
d)
Kufanya
ukondoeshwaji,
kuwajengea uwezo Watu wenye Ulemavu na taasisi zao na kufanya uhamasishaji wa
jamii juu ya masuala ya Watu wenye Ulemavu.
e)
Kuimarisha
mazingira ya kazi na kuwajengea uwezo wafanyakazi.
Programu ya Tatu: Usimamizi wa
Shughuli za Upigaji Chapa (C013):
|
67.0
Mheshimiwa
Spika, Programu hii lengo lake ni kukiimarisha Kiwanda cha Upigaji Chapa
ili kutoa huduma bora za machapisho na kwa ufanisi. Katika mwaka wa fedha
2016/2017 programu hii imepanga kutekeleza yafuatayo:
a)
Kutoa huduma bora za uchapishaji wa
nyaraka na Sheria za Serikali.
b)
Kutangaza na kushajiisha uelewa wa
utoaji huduma za Uwakala na Kiwanda kwa lengo la kuongeza idadi ya wateja na
mapato.
c)
Kufanya maandalizi ya uanzishaji wa
Bohari Kuu ya vifaa vya Ofisi.
d)
Kuweka mazingira mazuri ya kazi kwa
lengo la kutoa machapisho bora yanayoendana na teknolojia ya kisasa ya
uchapishaji.
Programu ya Nne: Mipango na
Utawala (C014):
|
68.0
Mheshimiwa
Spika, lengo
la Programu hii ni kuimarisha mazingira bora ya wafanyakazi, usimamizi
wa mipango na shughuli za Ofisi. Matokeo yanayotarajiwa ni kuimarika mipango na
utendaji kazi na kutoa huduma bora kwa wafanyakazi na wadau mbali mbali wa
Ofisi hii. Programu hii ina programu ndogo tatu (3) ambazo
ni:-
i.
Uongozi na Utawala
ii.
Mipango, Sera na Utafiti
iii.
Ofisi Kuu Pemba
Programu
ndogo (C0141): Uongozi na Utawala:
69.0
Mheshimiwa
Spika, Programu hii ndogo ina lengo la kuimarisha mazingira bora
ya kufanyia kazi na usimamizi wa shughuli za Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais.
Matokeo yanayotarajiwa ni matumizi bora ya rasilimali, wafanyakazi wenye ujuzi na
uzoefu na ufanisi katika utendaji kazi.
Huduma zinazotolewa ni kusimamia maslahi ya wafanyakazi na matumizi bora
ya rasilimali za Ofisi.
70.0
Mheshimiwa Spika, kwa
mwaka wa fedha 2016/2017 Ofisi kupitia
programu ndogo ya Uendeshaji na Utumishi imepanga kutekeleza kazi zifuatazo:-
a)
Kusimamia shughuli za
uendeshaji wa Ofisi za kila siku ikiwemo malipo ya umeme, maji, mawasiliano,
mafuta, vifaa vya usafi pamoja na vifaa vya kufanyia kazi.
b)
Kufanya ukarabati mdogo katika
jengo kongwe la Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Vuga.
c)
Kuimarisha huduma za usafiri.
d)
Kuimarisha Kitengo cha kumbukumbu
kwa kukifanyia ukarabati pamoja na kuwekwa samani za kisasa na vifaa vya kufanyia
kazi.
e)
Idara inaendelea kufanya
mapitio ya mahitaji ya mafunzo (Training Need Assessment -TNA).
f)
Kuendelea kuwapatia mafunzo ya
muda mrefu na mfupi wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais ili
kuimarisha utendaji kazi na kuongeza ufanisi.
g)
Kufanya semina moja juu ya
Sheria Nam. 2 ya mwaka 2011 na Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2014 na
Semina moja ya kujikinga na maambukizi na madhara ya UKIMWI pamoja na maradhi
yasioambukiza kwa wafanyakazi 100.
h)
Kuandaa vikao vinne (4) vya
Kamati ya Uongozi, Vikao vinne (4) vya Kamati ya Ukaguzi, Vikao vinne vya Bodi
ya Zabuni pamoja na kuendelea kufanyia mapitio daftari la mali za Serikali kwa
mujibu wa Sheria za Udhibiti wa mali za Serikali
Programu
ndogo (C0142): Mipango, Sera na Utafiti:
71.0
Mheshimiwa
Spika, Programu hii ndogo ina lengo la kuandaa na kusimamia Mipango na
Bajeti na kufuatilia utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ya Ofisi ya Makamu wa
Pili wa Rais. Matokeo yanayotarajiwa ni kuwa na mipango endelevu na yenye
kuleta maendeleo. Huduma inayotolewa ni kuandaa na kusimamia utekelezaji wa
Sera, Mipango na Bajeti.
72.0
Mheshimiwa
Spika,
katika mwaka wa fedha 2016/2017, Ofisi kupitia Programu ndogo (C0142) imepanga
kufanya yafuatayo:-
- Kuandaa Bajeti na
kutayarisha Miradi ya Maendeleo kwa mwaka wa fedha 2016/2017 na kufanya
ziara nne (4) za ufuatiliaji wa utekelezaji wa Programu/ Miradi ya
Maendeleo inayotekeleza chini ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais.
- Kusimamia tafiti zinazotekelezwa
chini ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais.
- Kuratibu Sera na
Sheria zinazotayarishwa kwa ajili ya shughuli zinazotekelezwa chini ya
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais.
- Kuwajengea uwezo
wafanyakazi wa Idara kwa kuwapatia mafunzo ya muda mfupi yanayohusu
ufuatiliaji na tathmini kwa kazi za kawaida na maendeleo na wafanyakazi
watatu (3) mafunzo ya muda mrefu.
- Kuratibu
utekelezaji wa Miradi ya Kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria
kupitia Mfuko wa Dunia (Global Fund).
Programu ndogo (C0143): Ofisi Kuu
Pemba:
73.0
Mheshimiwa Spika, lengo kuu la Program hii ndogo ni Kuimarisha mazingira bora ya
kufanyia kazi na usimamizi wa shughuli za Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais,
Pemba. Matokeo yanayotarajiwa ni utendaji na utekelezaji wa kazi za Ofisi ya
Makamu wa Pili wa Rais Pemba kwa ufanisi. Huduma inayotolewa ni Uratibu wa kazi
za Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Pemba.
74.0
Mheshimiwa
Spika,
katika mwaka wa fedha 2016/2017 Ofisi
Kuu Pemba itatekeleza Lengo la Kuratibu shughuli za Idara na Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Pemba kama
ifuatavyo:-
a)
Kuimarisha
mazingira bora ya kufanyia kazi na kusimamia shughuli za Ofisi ya Makamu wa
Pili wa Rais.
b)
Kuwapatia
mafunzo ya muda mrefu wafanyakazi wanne (4).
c)
Kuandaa
mipango ya Ofisi na Bajeti kwa mwaka wa Fedha 2017/2018.
d)
Kuimarisha
kazi za usimamizi na ufuatiliaji wa utekelezaji wa Programu na Miradi ya
Maendeleo iliyo chini ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais.
e)
Kuratibu
na kufuatilia utekelezaji wa shughuli za Serikali Pemba.
f)
Kutangaza
huduma za Kiwanda kwa ajili ya kuongeza idadi ya wateja na mapato.
75.0
Mheshimiwa
Spika, Ofisi
ya Makamu wa Pili wa Rais pia inaratibu shughuli za Baraza la Wawakilishi, Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Tume ya Kitaifa
ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya na Tume ya UKIMWI, ambazo nazo zina
Programu Kuu na Programu Ndogo kama ifuatavyo:-
BARAZA
LA WAWAKILISHI:
76.0
Mheshimiwa
Spika, Baraza
la Wawakilishi linatekeleza Program kuu mbili (2) ambazo ni:-
Programu ya tano: Kutunga
Sheria, kupitisha Bajeti na kusimamia Taasisi za Serikali:
|
77.0
Mheshimiwa
Spika, Programu
hii ina jukumu la kuhakikisha haki na utawala wa sheria
unatekelezwa Zanzibar, ambapo
matarajio yake ya muda mrefu ni kukua kwa demokrasia na
uwakilishi wa wananchi.
Huduma zinazotolewa ni kujadili, kurekebisha na kupitisha miswada ya
Sheria, kusimamia utendaji wa Taasisi za Serikali na kupitisha bajeti ya
Serikali.
Programu ya sita: Uongozi na
Utawala wa Baraza la Wawakilishi:
|
78.0
Mheshimiwa
Spika, Programu
hii ina jukumu la kuweka mazingira mazuri ya kazi, kuwajengea
uwezo Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na wafanya kazi wa Ofisi ya Baraza, ambapo matarajio yake ya
muda mrefu ni kuongezeka kwa ufanisi katika kutekeleza
majukumu ya Ofisi.
Huduma zinazotolewa ni kuwapatia Wajumbe na wafanyakazi wa Baraza
huduma na stahiki zao, kuimarisha uwezo wa Wajumbe na watendaji na kuimarisha
mazingira ya kazi ya Ofisi ya Baraza.
79.0
Mheshimiwa
Spika,
kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017 Baraza la Wawakilishi limepanga kutekeleza
mambo yafuatayo:-
a)
Kufanya
mikutano minne ya Baraza.
b)
Kuziwezesha
Kamati zake za kudumu kufanya kazi
c)
Kuendelea
kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa watumishi wake.
d)
Kuendeleza
mahusiano na vyombo vyengine vya Mabunge, Kanda ya Afrika na ngazi ya
Kimataifa.
e)
Kuendelea
kutoa mafunzo kwa Wajumbe ili waweze kutekeleza majukumu yao.
f)
Kuendelea
kutoa elimu kwa Umma inayohusu majukumu
ya Baraza kupitia Redio na Televisheni
g)
Kuendelea
kuweka mazingira mazuri ya majengo na kumbi za mikutano.
TUME
YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR:
80.0
Mheshimiwa
Spika,
Tume ya Uchaguzi inasimamia Programu kuu mbili kama zifuatazo:-
Programu ya saba: Uendeshaji wa
Shughuli za Uchaguzi:
|
81.0
Mheshimiwa
Spika,
Programu hii ina jukumu la kukuza Demokrasia na Umoja wa Kitaifa
ambayo
matarajio yake ya muda mrefu ni kuwa na
Uchaguzi Huru na wa haki na wenye kufuata misingi ya kisheria. Huduma zinazotolewa ni kufanya Uchaguzi Mkuu,
Chaguzi ndogo na Kura ya maoni, Kufanya Uchambuzi wa Idadi, Majina na Mipaka ya
Majimbo ya Uchaguzi, Kuratibu na kutoa elimu ya Wapiga Kura pamoja na
Uandikishaji wa Wapiga Kura na Uendelezaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
82.0
Mheshimiwa
Spika, katika
mwaka wa fedha 2016/2017 Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kupitia programu hii imepanga
kuendesha Chaguzi Ndogo.
Programu ya nane: Usimamizi wa
Kazi za Utawala na Uendeshaji wa Shughuli za Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar:
|
83.0
Mheshimiwa
Spika,
Programu hii ya pili ina jukumu la kuimarisha usimamizi
wa mwenendo wa Shughuli za Uchaguzi, ambayo matarajio yake ya muda mrefu ni uendeshaji bora wa kazi za Ofisi ya Tume ya Uchaguzi ya
Zanzibar.
Programu hii inasimamia programu ndogo mbili nazo ni:-
i. Usimamizi wa kazi za Utawala na Uendeshaji
wa Ofisi ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar
ii. Usimamizi wa kazi za Utawala na Uendeshaji
wa Ofisi Ndogo ya Tume ya Uchaguzi Pemba.
84.0
Mheshimiwa Spika, Programu ndogo ya
Usimamizi wa kazi za Utawala na Uendeshaji wa Ofisi ya Tume ya Uchaguzi ya
Zanzibar ina lengo la kuimarisha Usimamizi wa mwenendo wa
Shughuli za Uchaguzi.
Matokeo yanayotarajiwa ni uendeshaji bora wa kazi za Ofisi
ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar. Huduma zinazotolewa na program hii
ndogo ni kuimarisha mazingira bora ya kufanyia kazi, kuimarisha maslahi ya
wafanya kazi na kuwajengea uwezo wafanya kazi wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar.
85.0
Mheshimiwa
Spika,
Programu ndogo ya Usimamizi wa kazi za Utawala na Uendeshaji wa Ofisi Ndogo ya
Tume ya Uchaguzi Pemba ina lengo la kuimarisha Usimamizi wa mwenendo wa Shughuli za Uchaguzi Pemba.
Matokeo yanayotarajiwa ni uendeshaji bora wa Ofisi ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar. Huduma
zinazotolewa na program hii ndogo ni kuimarisha mazingira mazuri ya kufanyia
kazi ya Tume ya Uchaguzi Pemba.
86.0
Mheshimiwa
Spika,
kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017 Tume ya Uchaguzi kupitia programu hii imepanga
kutekeleza mambo yafuatayo:-
a)
Kuweka
na kusimamia mazingira mazuri ya utendaji kazi.
b)
Kuwapatia
mafunzo wafanya kazi
wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar.
TUME
YA KITAIFA YA KURATIBU NA UDHIBITI WA DAWA ZA KULEVYA:
87.0
Mheshimiwa
Spika, Tume
ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya ina jukumu kuu la
kuratibu mapambano dhidi ya matumizi, biashara na usafirishaji wa dawa za
kulevya, kutoa taaluma kwa jamii juu ya athari za dawa za kulevya pamoja na
tiba na ushauri nasaha kwa waathirika wa dawa hizo. Taasisi hii imepangiwa
kusimamia Program Kuu mbili kama ifuatavyo:-
Program ya tisa: Udhibiti wa
Dawa za Kulevya:
|
88.0
Mheshimiwa
Spika, shughuli
zilizopangwa kutekelezwa katika programu hii ni:-
a)
Kuzijengea uwezo nyumba za upataji nafuu (sober
houses).
b)
Kudhibiti uingizaji na usafirishaji wa dawa za kulevya
katika bandari zilizo na zisizo rasmi.
c)
Kuratibu
na kuendeleza mapambano juu ya uingizaji,
usambazaji
na usafirishaji
wa dawa
za kulevya
d)
Kupunguza
matatizo ya athari za utegemezi
wa dawa
za kulevya.
Programu ya kumi: Utawala na
Uendeshaji wa Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya:
|
89.0
Mheshimiwa
Spika,
lengo kuu la programu hii ni kuweka mazingira mazuri ya kazi za ofisi. Huduma
zinazotarajiwa ni upatikanaji wa huduma na vitendea kazi, kujenga uwezo wa
wafanya kazi na usimamizi wa matumizi ya fedha pamoja na kukuza uwajibikaji.
90.0
Mheshimiwa
Spika,
Kazi za programu hii zinatekelezwa na Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti
wa Dawa za Kulevya na ina program ndogo mbili ambazo ni:
i.
Utawala
wa Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya,
ii.
Uratibu
wa Masuala ya Dawa za Kulevya
Pemba.
Mheshimiwa Spika, shughuli zilizopangwa kutekelezwa
katika programu hii ni:-
a) Kuweka mazingira mazuri ya kazi na kusimamia
utekelezaji wake.
b) Kujenga uwezo wa
wafanyakazi katika mapambano ya dawa za kulevya.
c) Kuwapatia mafunzo ya
muda mrefu na mfupi wafanya kazi.
TUME
YA UKIMWI:
91.0
Mheshimiwa
Spika, Tume
ya Ukimwi ina jukumu la kuratibu masuala ya UKIMWI hapa Zanzibar, ambapo imepangiwa kusimamia Programu Kuu
mbili kama ifuatavyo:-
Programu ya kumi na moja: Uratibu wa Muitiko wa Taifa wa UKIMWI:
|
92.0
Mheshimiwa Spika, Programu
hii ina programu ndogo mbili ambazo ni:
i)
Uratibu wa muitiko wa Taifa wa UKIMWI.
ii)
Mawasiliano na Utetezi wa Masuala ya UKIMWI
93.0
Mheshimiwa
Spika, shughuli
zilizopangwa kutekelezwa na programu hii ni:
a)
Kuongeza
uelewa wa masuala ya UKIMWI na afya ya uzazi na matumizi ya huduma kwa makundi
ya vijana na rika baleghe (10 – 24).
b)
Kujenga
uwezo wa wadau na jamii kutekeleza
Mkakati wa Tatu utakaochangia kudhibiti kuenea UKIMWI, udhalilishaji wa
kijinsia na kuimarisha masuala ya afya ya uzazi.
c)
Kutekeleza
programu za ushawishi na mawasiliano kwa ubunifu zaidi na kukabiliana na changamoto
mpya.
d)
Kusimamia
mfumo wa ufuatiliaji na tathmini uendelee kufanya kazi.
e)
Kujenga
uelewa wa jamii wa Sheria ya Kukinga na Kusimamia Masuala ya UKIMWI Nam. 18 ya
mwaka 2013.
f)
Kuendeleza maandalizi ya uanzishwaji wa Mfuko wa Taifa
wa UKIMWI.
Program ya kumi na mbili: Utawala
na Uendeshaji wa Tume ya UKIMWI:
|
94.0
Mheshimiwa
Spika, lengo
kuu la programu hii ni kuweka mazingira mazuri ya kazi za ofisi. Huduma
zinazotarajiwa ni upatikanaji wa huduma na vitendea kazi, kujenga uwezo wa
wafanyakazi na usimamizi wa matumizi ya fedha, uwazi na uwajibikaji. Programu hii
imepangiwa kusimamia programu ndogo mbili ambazo ni: -
i. Uratibu wa masuala ya UKIMWI Pemba
ii. Utawala na uendeshaji Unguja.
95.0
Mheshimiwa
Spika, shughuli
zilizopangwa kutekelezwa katika programu hii ni:-
a)
Kununua vifaa,
huduma na kufanya matengenezo ya majengo, vifaa na gari.
b)
Kutoa mafunzo ya muda mrefu na mfupi ili kuongeza
ufanisi wa kazi.
c)
Kufanya mapitio ya Muongozo wa Fedha na Uhasibu wa
Tume na kutoa mafunzo ya mfumo wa kiuhasibu kwa wahusika.
d)
Kutekeleza programu ya afya kwa wafanya kazi na
familia zao.
96.0
Mheshimiwa
Spika, kwa muhtasari wa Programu na
Programu ndogo za Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais na Taasisi zake Angalia Kiambatisho Nam 3.
MGAO
WA FEDHA KWA PROGRAMU:
97.0
Mheshimiwa Spika, mgao wa fedha kwa Programu kumi na mbili (12) za Ofisi ya Makamu wa Pili
wa Rais na Taasisi zake ni kama ifuatavyo: -
Programu
ya kwanza: Uratibu wa Shughuli za Makamu wa Pili
wa Rais. Programu hii imepangiwa kutumia jumla ya Shilingi 756,466,000 kwa
kazi za kawaida.
Programu
ya pili: Uratibu
wa shughuli za Serikali. Programu hii imepangiwa kutumia jumla ya Shilingi 3,028,975,000 kwa kazi za kawaida na Shilingi
8,330,450,000 kwa kazi za maendeleo
(Shilingi 210,000,000 za SMZ na Shilingi 8,120,450,000 ni mchango wa Wahisani).
Programu ya tatu:
Usimamizi
wa Shughuli za Upigaji Chapa. Programu hii imepangiwa kutumia jumla ya Shilingi 873,940, 000 kwa
matumizi ya kawaida.
Programu ya nne: Mipango na Utawala. Programu hii
imepangiwa kutumia Shilingi 1,857,468,000
kwa kazi za kawaida na Shilingi 1,000,000,000
kwa kazi za maendeleo.
Programu ya tano: Kutunga Sheria, Kupitisha Bajeti na
Kusimamia Taasisi za Serikali. Programu hii imepangiwa kutumia Shilingi 6,542,950,000 kwa kazi za kawaida.
Programu ya sita: Uongozi na Utawala wa Baraza la
Wawakilishi. Programu hii imepangiwa kutumia Shilingi 10,595,550,000 kwa kazi za kawaida.
Programu ya saba: Uendeshaji na Usimamizi wa Shughuli
za Uchaguzi. Programu hii imepangiwa kutumia Shilingi 1,174,812,000 kwa kazi za kawaida.
Programu ya nane: Usimamizi wa Kazi za Utawala na
Uendeshaji wa Shughuli za Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar. Programu hii imepangiwa
kutumia Shilingi 185,388,000 kwa
kazi za kawaida.
Programu ya tisa: Udhibiti wa Dawa za Kulevya.
Programu hii imepangiwa kutumia Shilingi 88,813,000
kwa kazi za kawaida.
Programu ya kumi: Utawala wa Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na
Udhibiti wa Dawa za Kulevya. Programu hii imepangiwa kutumia Shilingi 351,087,000 kwa kazi za kawaida.
Programu ya kumi na moja: Kuratibu Muitiko wa Taifa wa UKIMWI. Programu hii
imepangiwa kutumia Shilingi 222,589,000
kwa kazi za kawaida na Shilingi 519,076,000
kwa kazi na maendeleo (Shilingi 20,000,000 fedha za SMZ na 499,076,000 mchango
wa Wahisani).
Programu ya kumi na mbili: Utawala na Uendeshaji wa Tume ya
UKIMWI. Programu hii imepangiwa kutumia Shilingi 464,511,000 kwa kazi za kawaida.
98.0
Mheshimiwa Spika, jumla ya makisio kwa Programu zote 12 za Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais
na Taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ni Shilingi 35,992,076,000.
Kiambatisho Nam. 3.
UKUSANYAJI
WA MAPATO:
99.0
Mheshimiwa Spika,
kwa mwaka wa
fedha 2016/2017, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais imepanga kukusanya mapato ya
jumla ya Shilingi 806,126,000 kwa mchanganuo ufuatao:-
Wakala
wa Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali: TShs.
793,766,000
Idara
ya Sherehe na Maadhimisho ya Kitaifa: TShs. 12,360,000
HITIMISHO:
100.0 Mheshimiwa Spika, baada ya kueleza hayo,
sasa naomba kuchukua fursa hii kumshukuru kwa dhati Waziri wa Nchi Ofisi ya
Makamu wa Pili wa Rais, Mheshimiwa Mohamed Aboud Mohamed, kwa kunisaidia
kutekeleza majukumu yangu kwa ufanisi mkubwa. Aidha, nawashukuru pia watendaji
na wafanyakazi wote wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais na Taasisi zilizo chini
ya Ofisi hii wakiongozwa na Katibu Mkuu, Ndugu Joseph Abdallah Meza na Naibu
Katibu Mkuu, Ndugu Ahmad Kassim Haji kwa juhudi zao katika kutekeleza majukumu
yaliyo mbele yetu.
101.0 Mheshimiwa
Spika, natoa shukurani zangu za dhati kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi,
na shukurani maalumu kwa Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Kusimamia
Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa kwa mashirikiano, ushauri na maelekezo waliyotupa katika kukamilisha bajeti. Aidha, napenda
kuwashukuru sana Washirika wa Maendeleo, (Development Patners) na nchi marafiki
ambazo zinaendelea kuchangia katika kufanikisha utekelezaji wa malengo ya Ofisi
yangu na ya nchi kwa jumla katika mwaka wa fedha 2015/2016. Miongoni mwao ni:
Benki ya Dunia, Clinton Foundation, China, FAO, Finland, Norway, India, Japan,
Marekani, Mfuko wa Dunia wa Kupambana na Kifua Kikuu Malaria na UKIMWI (Global
Fund), Oman, UNAIDS, USAID, UNDP, UNICEF, UNFPA, WHO, WFP na WIPO. Vile vile
naishukuru sana Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
Ofisi ya Waziri MKuu kwa ushirikiano wao mkubwa na Ofisi yangu. Pia nazishukuru Taasisi zisizo za Kiserikali,
Jumuiya ya Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Wakulima kwa kuendelea kuisaidia
Serikali katika kutoa huduma za jamii na kuleta maendeleo katika nchi yetu. Pia
nawashukuru sana wananchi wote ambao wamefuatilia na kusikiliza hotuba yangu
hii.
102.0 Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo, sasa naliomba Baraza lako Tukufu liidhinishe
jumla ya Shilingi 35,992,076,000 kwa
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais na Taasisi zake kwa ajili ya kutekeleza
Programu nilizozielezea hapo juu. Mchanganuo halisi wa fedha hizo ni kama
ifuatavyo:
i. Ofisi
ya Makamu wa Pili wa Rais TShs: 15,847,300,000
ii. Ofisi
ya Baraza la Wawakilishi TShs: 17,138,500,000
iii. Tume
ya Uchaguzi ya Zanzibar TShs: 1,360,200,000
iv. Tume
ya Kitaifa ya Kuratibu na
Udhibiti wa
Dawa za Kulevya TShs: 439,900,000
v. Tume
ya UKIMWI Zanzibar TShs: 1,206,176,000
Jumla: TShs: 35,992,076,000
Mheshimiwa
Spika, naomba
kutoa hoja.
No comments:
Post a Comment