Habari za Punde

Madaktari kutoka China watoa mafunzo kwa Madaktari Hospitali ya Mnazimmoja, wafanya operesheni za macho

 Baadhi ya Madaktari   wa vitengo hivyo walioshiriki mafunzo  hayo  wakimsikiliza Dkt. Liu  Qing Huai katika Hospitali ya Kuu ya Mnazimmoja Mjini Zanzibar.
 Mkuu wa Idara ya macho kutoka Hospitali ya Jimbo la Jiangsu Nchini China  Dkt. Liu Qing Huai akitoa mafunzo  kwa madaktari wa vitengo vya macho, matumbo ya akinamama na saratani  wa  Hospitali Kuu ya Mnazimmoja  katika kuwajengea uwezo wafanyakazi hao.


Waandishi wa Habari wakipata maelezo kutoka kwa Dkt. Liu Qing Huai kuhusu mafunzo wanayotolewa kwa wafanyakazi wa Hospitali Kuu ya Mnazimmoja.

                   Picha na Miza Othman  -Maelezo Zanzibar.

Na Maryam Kidiko -Maelezo Zanzibar.                                                       
Mkuu wa Kitengo cha macho Dkt Slim Moh’d Mgeni amesema jumla ya wagojwa 70 wanaosumbuliwa na matatizo ya macho kutoka Zanzibar  wanatarajiwa kupatiwa matibabu katika hospitali kuu ya Mnazi mmoja.

Akizumgumza na waandishi wa habari huko hospitali ya Mnazi mmoja, DKT. Slim  amesema wagojwa watakaofanyiwa matibabu hayo ni watu wazima  pamoja na wenye magojwa ya kinamama yakiwemo kensa ya kizazi.

Amesema matibabu hayo yatafanywa kwa ushirikiano na madaktari bingwa kutoka China ambao wamekuja  maalum kwa kazi hiyo wakiwa na vifaa vya kisasa vya  upasuaji.


Ameongeza  kuwa matibabu hayo yatatolewa bure kwa wananchi wote na kuwataka wale wenye matatizo hayo waende Hospitali ya Mnazimmoja ili  kupatiwa matibabu.

Nae Msaidizi Mganga Mkuu wa  Hospitali ya Mnazi Mmoja Dkt.  Munir Abdalla Moh’d amesema madaktari hao wamekuja kwa lengo la kutoa mafunzo  kwa madakatari wa  vitengo vya  magonjwa ya macho na magonjwa ya wanawake.

Aidha amesema madaktari  hao ambao watakuwepo nchini kwa muda wa wiki moja watashuhulikia zaidi  kesi ngumu zinazo hitaji upasuaji . 

 Nae Daktari bingwa   wa macho kutoka Hospitali ya Jimbo la Jiangsu Dkt. Liu Qing Huai amesema lengo la kutoa mafunzo kwa wataalamu wa kitengo cha macho Zanzibar  ni kuwajengea uwezo ili waweze kukabiliana na matatizo hayo ambayo yamekuwa yakiwasumbua wananchi  wengi hasa wanapoingi hatua ya uzee.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.