CEO wa Dubai Cares Tariq Al Gurg, akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali viliko Zanzibar na kutoka UAE, wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Furswa kwa Watoto uliozinduliwa katika ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Shangani Zanzibar.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Ndg Abdalla Mzee Abdalla akizindua Mradi wa Mpango kwa Furswa kwa Watoto kupitia ufadhili wa Dubai Cares, uzinduzi huo umefanyika katika ukumbi wa hoteli ya Hyatt Shangani Zanzibar.
Mkurugenzi Mkaazi wa Aga Khan Foundation Tanzania Abdi Mallick, akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo wa kuwaendeleza Watoto kupitia Mpango wa Fursa kwa Watoto.
Waandishi wa habari kutoka UAE, wakifuatilia uzinduzi huo wa Mradi wa mpango wa Fursa kwa Watoto Znzibar (Improving Access to and Quality of Early Childhood Development Program in Zanzibar.) uzinduzi huo umefanyika katika ukumbi wa hoteli ya Hyatt Zanzibar.
Maofisa wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar wakifuatilia uzinduzi huo wa Mpango wa kuwaendeleza Watoto kupitia kupitia Fursa kwa Watoto, unaodhaminiwa na Dubai Cares
Maofisa wa Madrasa Center Zanzibar, wakifuatilia uzinduzi wa mradi huo wa kuwaendeleza Watoto Zanzibar chini ya Ufadhili wa Dubai Cares
Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vya Zanzibar wakifuatilia uzinduzi wa mpango wa Mradi wa Fursa kwa Watoto wakati wa uzinduzi wa mradi huo iliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Hyatt Shangani Zanzibar.
No comments:
Post a Comment