HOTUBA
YA WAZIRI WA ARDHI, MAJI, NISHATI NA MAZINGIRA MHESHIMIWA SALAMA ABOUD TALIB
(MBM) KUHUSU
MAKADIRIO
YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017 KATIKA BARAZA LA WAWAKILISHI
UTANGULIZI
- Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako, naomba kutoa
hoja kwamba Baraza lako Tukufu sasa likae kama Kamati, ili liweze kupokea,
kujadili na hatimae kuidhinisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara
ya Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
- Mheshimiwa Spika, aidha, naomba nichukuwe fursa
hii kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kutujaalia uzima na afya njema
na kwa kuniwezesha kwa niaba ya wafanyakazi wenzangu kuwasilisha
muhutasari wa hotuba ya Wizara Ardhi, maji, Nishati na Mazingira mbele ya
Baraza lako.
- Mheshimiwa Spika, kwa furaha kubwa naomba
nichukue fursa hii kumpongeza kwa dhati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dk. Ali Mohammed Shein kwa kuchaguliwa tena
na Wananchi kuendelea Kuiongoza Zanzibar kwa ushindi mkubwa katika
uchaguzi wa marudio uliofanyika Machi 20, 2016. Kuchaguliwa kwake
kumedhihirisha kukubalika kwake kwa Wananchi kutokana na uongozi wake
imara wenye busara na hekima nyingi katika kuwaletea maendeleo Wananchi wa
nchi hii.
- Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako naomba pia
nichukue nafasi hii kumpongeza Balozi Seif Ali Iddi kwa kuteuliwa
tena na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar.
Kuteuliwa kwako ni ushahidi wa uwajibikaji katika kutekeleza majukumu ya
Serikali na kutoa mchango wako katika kuwaletea wananchi maendeleo yao
katika shughuli zao za kila siku.
- Mheshimiwa Spika, kwa namna ya kipekee napenda
kukupongeza kwa dhati wewe binafsi kwa kuchaguliwa kuwa Spika wa Baraza la
tisa la Wawakilishi, tunamuomba Mwenyezi Mungu akujaalie uwezo, hekima,
busara na uwadilifu katika kuliongoza vyema Baraza letu hili. Vilevile,
naomba kuwapongeza Wajumbe wa Baraza lako Tukufu waliochaguliwa na
wananchi na walioteuliwa na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar kupitia viti
maalum ili kuweza kushirikiana na Serikali katika kutatua changamoto mbali
mbali zinazowakabili wananchi.
- Mheshimiwa Spika, Naomba pia niungane na
Wafanyakazi wenzangu kutoa mkono wa pole kwa Wananchi wote walioathirika
kutokana na maafa yaliotokana na mvua kubwa zilizonyesha katika visiwa
vyetu. Sote tunaamini kwamba mvua ni neema lakini haya yote yametokea
kutokana na kudra ya Mwenyezi Mungu Muumba Mbingu na Ardhi. Hivyo
tunamuomba Mwenyezi Mungu awape subira wale wote ambao kwa namna moja au
nyengine wamefikwa na maafa haya.
- Mheshimiwa Spika, naomba uniruhusu kuelezea
utekelezaji wa shughuli za Wizara kwa mwaka wa fedha 2015/2016 na muelekeo
kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kama ifuatavyo:-
Mapato
na Matumizi:
- Mheshimiwa
Spika, suala la
ukusanyaji wa mapato ni kiashiria muhimu sana katika kupima mafanikio ya utekelezaji.
Wizara yangu katika Mwaka wa Fedha 2015/2016 ilipangiwa kukusanya jumla ya
Tsh 4,799,625,000/= kutokana na vyanzo mbali mbali vya Taasisi
zake. Hadi kufikia tarehe 31 Machi 2016 jumla ya Tsh 3,596,948,678/=
zimekusanywa. Kiwango hichi ni sawa na asilimia 75% ya makadirio.
Kwa ufafanuzi zaidi naomba angalia kiambatanisho “A”.
- Mheshimiwa
Spika, kwa
upande wa matumizi ya Mwaka wa Fedha 2015/16, Wizara yangu imepangiwa
kutumia jumla ya Tsh 35,949,460,587 /=. Kati ya Fedha hizo, kazi za
kawaida ni Tsh 7,198,900,000 /= na kazi za maendeleo ni Tsh
28,750,560,587 /=. Hadi kufikia tarehe 31 Machi 2016 Wizara yangu
ilikwishapatiwa Tsh 3,838,441,267/=
kwa kazi za Maendeleo sawa na asilimia 13.4% na Tsh 5,319,579,160/= kwa kazi za
kawaida sawa na asilimia 74 %ya makadirio, hivyo kufanya jumla ya
fedha zote tulizozipata kuwa ni Tsh 9,152,556,878/=
sawa na asilimia 25.5% ya
makisio yote.
Kwa ufafanuzi zaidi angalia kiambatanisho “B1 na B2 ”
- Mheshimiwa
Spika, kwa upande
wa utekelezaji wa shughuli za Wizara, kwa mwaka wa fedha 2015/2016
Wizara yangu ilifanikiwa kutekeleza majukumu yake kupitia programu kuu
tano zifuatazo:
Programu
1: Mipango, Sera na Utawala wa Ardhi,
Makaazi, Maji na Nishati.
Programu
2: Usimamizi na Upangaji wa Matumizi ya
Ardhi
Programu
3: Uhifadhi wa Mji Mkongwe, Uratibu na
Usimamizi wa Shughuli za Ujenzi na Nyumba za Serikali
Programu
5: Usimamizi wa Huduma za Uzalishaji
na Usambazaji wa Nishati na Maji.
Programu
6: Usimamizi wa Mazingira na
Mabadiliko ya Tabia nchi.
PROGRAMU
KUU: MIPANGO, SERA NA UTAWALA WA ARDHI, MAKAAZI, MAJI NA NISHATI
- Mheshimiwa Spika, Programu hii ilikuwa na
jukumu la uratibu katika utekelezaji wa kazi za Wizara. Programu hii
inatekelezwa na Idara Mipango, Sera na Utafiti, Idara ya Utumishi na
Uendeshaji, na Afisi Kuu Pemba kupitia programu ndogo tatu ambazo ni
Mipango na Sera za Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati, Utawala na Maendeleo
ya Rasilimali watu pamoja na programu ndogo ya Uratibu wa Shughuli za
Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati Pemba.
PROGRAMU
NDOGO YA MIPANGO NA SERA ZA ARDHI, MAKAAZI, MAJI NA NISHATI.
- Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016
utekelezaji wa Programu hii ndogo ulilenga kutekeleza shughuli za
Kuratibu/ kuandaa Mipango na Miongozo ya Kisera ya utekelezaji wa kazi za
Wizara, Kuratibu, kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa programu na
miradi na shughuli za Wizara pamoja na kuendeleza tafiti kwa ajili ya
kuleta ufanisi katika utoaji wa huduma katika sekta za Wizara.
- Mheshimiwa Spika, hadi kufikia mwezi wa Machi
2016 Idara ya Mipango, Sera na Utafiti imefanikiwa kutekeleza mambo
yafuatayo kwenye programu hii ndogo.
Kuratibu
shughuli zote za Wizara ikiwemo Programu na Miradi ya Maendeleo.
- Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Miradi ya
Maendeleo, Idara imesimamia Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwa kufanya
kazi za Uratibu, Ufuatiliaji na Tathmini ya Utekelezaji ( monitoring and
Evaluation) kwa lengo la kuhakikisha kwamba miradi hiyo inatekelezwa kwa
ufanisi kama ilivyopangwa. Miradi iliyosimamiwa na Idara hii ni hii
ifuatayo :-
- Usambazaji Umeme Vijijini.
- Uimarishaji wa miundombinu ya
Umeme na Kulijengea Uwezo Shirika.
- Usambazaji Maji Vijijini.
- Uimarishaji wa Shughuli za Maji
Mijini.
- Kuijengea Uwezo Mamlaka ya Maji
Awamu ya Pili.
- Usambazaji Maji na Usafi wa
Mazingira.
- Utekelezaji wa Sera ya Nishati
- Utafiti wa Nishati Mbadala.
- Mheshimiwa Spika, katika uandaaji wa miongozo
ya Kisera na Kisheria, Wizara imekamilisha utayarishaji wa Rasimu ya Sera
na Sheria ya Mafuta na Gesi Asilia na hivi sasa ipo katika hatua za mwisho
za ukamilishwaji wake. Hatua hii itaihakikishia Zanzibar kupata fursa ya
uendelezaji wa shughuli za mafuta na Gesi Asilia.
- Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016,
Katika kutekeleza programu ndogo ya Mipango na Sera za Ardhi, Makaazi,
Maji na Nishati, jumla ya Tsh 161,884,000/= ziliidhinishwa
kutumika. Hadi kufikia Machi, 2016, fedha zilizoingizwa ni Tsh
101,654,949/= sawa na asilimia 63% ya Makadirio.
PROGRAMU
NDOGO YA UTAWALA NA MAENDELEO YA RASILIMALI WATU
- Mheshimiwa Spika, Program hii ndogo
inatekelezwa na Idara ya Utumishi na Uendeshaji na inajukumu la usimamizi
na utawala wa rasilimali za Wizara ambapo kwa mwaka wa Fedha 2015/2016
iliweza kutekeleza yafuatayo:-
- Kuajiri wafanyakazi 12 katika
fani mbalimbali ambazo zilihitajiwa kujazwa kwa sababu tofauti ili
kuongeza ufanisi wa kazi kwa kutoa huduma zenye tija kwa wananchi.
- Jumla ya wafanyakazi 546
wamepatiwa fursa ya kushiriki mafunzo mafupi, wafanyakazi 162 wanaendelea
na mafunzo ya muda mrefu, na jumla ya wafanyakazi 41 wamemaliza mafunzo ya
muda mrefu.
- Iliratibu shughuli za
kustaafisha Wafanyakazi na kuwatayarishia mafao yao ambapo jumla ya
wafanyakazi 45 walistaafu na kuratibiwa mafao yao.
Kwa
ufafanuzi zaidi wa uendelezaji wa mafunzo Viambatanisho C na D
vinahusika.
- Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016,
Katika kutekeleza programu ndogo ya Utawala na Maendeleo ya Rasilimali
watu jumla ya Tsh 804,252,000/= ziliidhinishwa kutumika. Hadi
kufikia Machi, 2016, fedha zilizoingizwa ni Tsh 570,016,314/= sawa
na asilimia 71% ya makadirio
PROGRAMU
NDOGO YA URATIBU WA SHUGHULI ZA ARDHI, MAKAAZI, MAJI NA NISHATI PEMBA.
- Mheshimiwa Spika, Program hii ndogo
inatekelezwa na Afisi Kuu Pemba na ina jukumu la uratibu na usimamizi
thabiti wa kazi za Wizara ikiwemo Programu na Miradi ya Maendeleo kwa
Pemba ambapo kwa mwaka wa Fedha 2015/2016 iliweza kutekeleza yafuatayo:-
- Kufanya utambuzi wa maeneo
(parcels) 4,939 katika maeneyo ya Kiungoni, Limbani, Selemu na
Kipangani kwa Wilaya ya Wete. Wara, Msingini na Mkoroshoni kwa Wilaya ya
Chake Chake. Chokocho, Uweleni na Ng’ombeni kwa Wilaya ya Mkoani pamoja na
Kusajili jumla ya maeneo (parsels) 544 yaliyofanyiwa utambuzi. Vile
vile taratibu za kuwapatia kadi za usajili wa ardhi wananchi 236
ambao wameomba kupatiwa kadi hizo tayari zimeanza.
- Jumla ya Hati Miliki za
matumizi ya ardhi 58 zimetayarishwa kati ya hizo hati za muda
(provisional) ni 34 na hati za kudumu ni 24.
- Kukamilishwa kwa kazi ya
uthamini wa Nyumba zilizoathirika katika ujenzi wa barabara ya Ole/
Kengeja na uthamini wa mimea katika barabara ya Bahanasa /Mtambwe. Vile
vile kazi za uthamini wa maombi 138 ya uhaulishaji wa ardhi
zimefanywa.
- Jumla ya viwanja 324 vimepimwa
kwa ajili ya shughuli mbali mbali kama vile makaazi, biashara,
taasisi, vitega uchumi mashamba na mengineo.
- Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016,
Katika kutekeleza programu ndogo ya uratibu wa Shughuli za Ardhi, Makaazi,
Maji na Nishati Pemba jumla ya Tsh 1,018,229,000/= ziliidhinishwa
kutumika. Hadi kufikia Machi, 2016, fedha zilizoingizwa ni Tsh
624,347,150/= sawa na asilimia 61% ya makadirio.
PROGRAMU KUU: USIMAMIZI NA UPANGAJI WA MATUMIZI YA ARDHI
- Mheshimiwa
Spika, Kufuatia
kuundwa kwa Kamisheni
ya Ardhi, jukumu la programu hii limeanza kutekelezwa chini ya chombo hili
kipya chini ya usimamizi wa Katibu Mtendaji. Chombo hiki ndio chenye
dhamana ya Utawala na Usimamizi wa Ardhi hapa nchini. Jukumu la
program hii ni kuhakikisha kunakuwepo na usalama wa matumizi ya Ardhi kwa
maendeleo ya nchi (Security of tenure) pamoja na kujenga matarajio ya kuwa
na matumizi ya Ardhi yaliobora na fanisi lilipangiwa kutekelezwa na Idara
ya Ardhi, Afisi ya Usajili wa Ardhi, Idara ya Upimaji na Ramani na Idara
ya Mipango Miji na Vijiji, ambazo zote hizo zimo ndani ya Sheria ya Muundo
wa Kamisheni.
Mbali na taasisi hizo Mahakama ya Ardhi nayo inahusika katika
utekelezaji wa programu hii. Utekelezaji wa programu hii umegawanyika katika
programu ndogo mbili ambazo ni Utawala wa Ardhi na Upangaji Miji na Matumizi ya
Ardhi.
PROGRAMU NDOGO YA UTAWALA WA ARDHI
- Mheshimiwa Spika, Program hii ndogo inatekelezwa
na Idara ya Ardhi na Usajili, Idara ya Upimaji na Ramani pamoja na Afisi
ya Msajili wa Ardhi ambapo kwa mwaka wa Fedha 2015/2016 programu hii ndogo
iliweza kutekeleza Huduma za Ugawaji na Usimamiaji wa Ardhi, Uthamini wa
Ardhi, Usajili wa Ardhi pamoja na utatuzi wa migogoro ya Ardhi kwa
kutekeleza shughuli za msingi zinazohusiana nazo.
- Mheshimiwa Spika, Kuhusu utayarishaji wa Hati
Miliki jumla ya
Hati 362 zilitayarishwa kati ya Hati 650 zilizolengwa kutayarishwa. Hii ni
sawa na asilimia 55.69 ya lengo lilowekwa. Kati ya hizo Hati 131 ni za
Muda na Hati 231 ni za kudumu. Kuhusu Utayarishaji wa Mikataba ya
Ukodishaji Ardhi, jumla ya Mikataba 58 ya Ukodishwaji Ardhi
ilitatayarishwa kati ya mikataba 60 iliyopangwa. Hii ni sawa na asilimia
96 ya lengo lilowekwa.
- Mheshimiwa
Spika, kwa
upande wa shughuli za Uthamini wa Ardhi jumla ya kazi za utiaji thamani
200 kwa mali zisizohamishika zilipangwa kutekelezwa ambapo hadi kufikia
Machi Mwaka 2016 kazi 121 zilitekelezwa ikiwa ni asilimia 60.5% ya lengo
la mwaka. Kazi hizo ni pamoja na kazi 116 za uthamini kwa ajili ya
mirathi, 1 kwa ajili ya uthamini wa fidia, na 4 kwa ajili ya uthamini wa
kujua soko la sasa (yaani market determination).
- Mheshimiwa
Spika, Shughuli
ya Utambuzi wa Kumjua Mwenye Haki ya Matumizi Ardhi ni utangulizi wa zoezi la usajili
wa ardhi na haikuainishwa katika malengo ya Wizara ya mwaka 2015/16 lakini
ilitekelezwa kwa mashirikiano ya bajeti ya washirika wa maendeleo Finland
chini ya mradi wa SMOLE na pia Mradi wa Urasimishaji Mali na Biashara (MKURABITA)
unaotekelezwa kwa pamoja baina ya SMZ na SMT. Jumla ya maeneo 1,207
vilifanyiwa utambuzi kati ya hayo maeneo 300 ni katika Shehia ya Chwaka na
maeneo 907 yalifanyiwa katika Shehia ya Jang’ombe.
- Mheshimiwa
Spika, Idara ya
Upimaji na Ramani kwa mwaka wa fedha 2015/2016 hadi Machi, 2016, katika
kutekeleza programu ndogo ya Utawala wa Ardhi imetekeleza yafuatayo:
Usimamiaji wa Shughuli za Upimaji.
- Mheshimiwa
Spika, Idara ya
Upimaji na Ramani, Katika mwaka wa fedha 2015/16 imeweza kupima jumla ya
viwanja 506, kwa matumizi mbalimbali, kama inavyoonekana katika jaduweli
iliyopo chini.
Jaduweli Namba 1 : Maeneo Yaliyopimwa
Nam
|
Matumizi
|
Idadi ya Viwanja
|
1
|
Makaazi
|
202
|
2
|
Hudma mbalimbali
|
41
|
3
|
Vitega Uchumi
|
46
|
4
|
Taasisi
|
15
|
5
|
Mashamaba ya Kilimo (Watu binafsi)
|
202
|
JUMLA
|
506
|
Chanzo: Idara ya Upimaji na Ramani
Idara pia imeweza kuweka Mipaka ya Wilaya ya Unguja na
Pemba, kwa kusirikiana Uongozi wa Mikoa na Wilaya husika. Kazi iliyofanywa
inakadiriwa kufikia Asilimia 32% ya mipaka yote.
Aidha Idara imeanza zoezi la kuzingiza kumbukumbu za
Alama za Upimaji (Control Points) katika database maalumu ili ziweze kupatikana
na kutumika kwa urahisi katika kazi mbalimbali za Upimaji na Ukushanyaji
taarifa za Kijografia. Kazi hii nayo imeweza kufanikishwa kwa asilimia 20%.
Utayarishaji na utowaji wa Ramani Msingi.
- Mheshimiwa
Spika, Idara
Katika utayarishaji na utowaji wa Ramani Msingi. Idara imeweza kuchapisha
ramani msingi (Topographical Base Map)100 za Zanzibar za kipimo cha
(1:10,000) na ramani picha (Othorphotographs) 31. Aidha katika kufuatilia
taarifa za kupwa na kujaa kwa maji ya bahari, kutoka chombo kilichopo
Malindi (Tide Gaudge) Idara imeweza kukushanya taarifa za utabiri wa mwaka
mzima.
Ukushanyaji na uwekaji wa taarifa za Ardhi
- Mheshimiwa
Spika, Idara ya
Upimaji na Ramani kwa kushirikiana na Idara za sekta ya Ardhi
zilizopo, ambazo sasa ziko chini ya Kamisheni ya Ardhi, imeimarisha Mfumo
wa ukusanyaji wa taarifa za ardhi (Zanzibar Land Information System
(ZALIS) kwa kiwango cha asilimia 25%. Kwa ushirikishaji wa wadau wengine.
Aidha jitihada za awali zimeanza kuchukuliwa kwa kuwaeleimsha wadau husika
wa matumizi ya mfumo huo wa ZALIS.
AFISI YA MRAJIS WA ARDHI
- Mheshimiwa Spika, Afisi ya Mrajis wa Ardhi ni
Taasisi yenye jukumu la kusajili ardhi yote ya Zanzibar kwa kuweka taarifa
za wamiliki wa haki ya matumizi ya ardhi. Kwa mwaka wa fedha 2015/2016
Afisi ya Mrajis imeweza kutekeleza program ndogo ya Utawala wa Ardhi kwa
kutoa huduma ya kusajili ardhi na utowaji wa kadi za usajili, kama
ifuatvyo:
Usajili
wa Ardhi
- Mheshimiwa Spika, katika kazi za usajili jumla
ya maeneo 300 yalisajiliwa kwa upande wa Unguja, baadhi ya Shehia za
Wilaya za Mjini na Magharibi ndizo zilizokwisha sajiliwa, na jumla ya
maeneo 109 yamesajiliwa kwa shehia ya Mkoroshoni na Limbani za huko Pemba.
- .Mheshimiwa Spika, kwa
upande wa huduma ya Utolewaji wa kadi za usajili wa ardhi, hadi
Machi Jumla ya Kadi za usajili wa ardhi 410 zimetolewa kwa
wananchi ambao ardhi zao zimeshasajiliwa kwa Unguja. Kwa Pemba wananchi
236 wanategemewa kutengenezewa kadi zao kwa kipindi cha miezi mitatu
kijacho.
- Mheshimiwa Spika, Afisi ya Mrajisi katika
kufanikisha huduma ya usajili pia imefanikiwa kuanzisha mfumo wa
elektroniki katika usajili wa ardhi ambao utafanyakazi kwa karibu na sekta
nzima ya Ardhi. Hatua za matayarisho ya kutumia mfumo wa elektroniki
katika uhifadhi wa data za usajili wa ardhi zinaendelea. Kwa sasa viwanja
3000 taarifa zake tayari zimeshaingizwa katika mfumo wa electroniki.
- Mheshimiwa Spika, Katika utowaji wa huduma ya
Usajili wa Ardhi Afisi ya Mrajisi inawajibu wa kufanyakazi kwa karibu na
Afisi ya Usajili Wa Ardhi Za Mirathi. Katika mwaka 2015/16 hadi
Machi,2016, Jumla ya nyumba za mirathi 934 kati ya 1415 kwa Wilaya za
Mjini na Magharibi, 266 Nungwi, 62 kati ya 114 Chwaka tayari
zimeshafunguliwa majalada ya mirathi Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana.
- Mheshimiwa Spika, Katika kufanikisha suala zima
la Usajili wa Ardhi, Afisi inafahamu umuhimu wa kutoa eleimu kwa ngazi
tofauti, katika mwaka tunaomaliza Afisi iliweza Kutoa elimu ya usajili kwa
Wananchi kwa kufanya mikutano mitatu (3) ya kuelimisha wananchi kuhusiana
na usajili wa ardhi. Mikutano hiyo imefanyika katika Shehia ya Jang’ombe,
Mji Mkongwe na Shehia ya Chwaka. Aidha, mikutano hiyo pia ilitumika kutoa
elimu ya mirathi kwa wananchi kwa kushirikiana na Kamisheni ya Wakfu na
Mali ya Amana.
MAHAKAMA
YA ARDHI
- Mheshimiwa Spika, Mahakama ya Ardhi inaendelea na
kazi zake za kupokea, kusikiliza na kuamua kesi za migogoro ya ardhi
zinazowasilishwa na wananchi pamoja na taasisi mbali mbali. Kwa mwaka
wa fedha 2015/2016 Mahakama ya Ardhi imepokea kesi mpya 168 ambazo
zimefunguliwa Unguja na Pemba pamoja na kesi za awali. Mahakama imeendesha
vikao 12,283 vya kusikiliza kesi ambapo kesi 138 zimetolewa hukumu kwa
mchanganuo ufuatao:-
Unguja: Kesi mpya 118 zimepokelewa na kesi 96 zimetolewa maamuzi.
Pemba: Kesi mpya 50 zimepokelewa na kesi 40 zimetolewa maamuzi.
- Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016,
Katika kutekeleza programu ndogo ya Utawala wa Ardhi jumla ya Tsh
1,011,941,000/= ziliidhinishwa kutumika. Hadi kufikia Machi, 2016,
fedha zilizoingizwa ni Tsh 728,607,314/= sawa na asilimia 72% ya
makadirio
PROGRAMU NDOGO YA UPANGAJI WA MIJI NA MATUMIZI YA ARDHI
- Mheshimiwa Spika, Program hii ndogo
inatekelezwa na Idara ya Mipango Miji na Vijiji, ambapo katika kutekeleza programu hii ndogo kwa mwaka
wa Fedha 2015/2016 Idara hii ililenga kutowa huduma zifuatazo:
Kupanga Matumizi bora ya ardhi kwa miji yote ya Zanzibar
Kusimamia maendeleo ya ardhi mijini, mikoani na maeneo ya fukwe
Kuimarisha miji ili kukuza uchumi na kuleta maisha bora
- Mheshimiwa
Spika, Katika
kipindi cha mwaka 2015/2016, Idara kupitia programu hii ndogo imeweza
kutekeleza malengo yake kama ifuatavyo:
Kupanga matumizi bora ya Ardhi kwa Miji yote ya Zanzibar
- Mheshimiwa
Spika, Katika kutekelza
lengo hili Idara imeweza kutekeleza yafuatayo:
- Kuelimisha
jamii kuhusu malengo ya Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Ardhi
Zanzibar (National Spatial Development Strategy - NSDS). Jumla ya
semina tatu (3), zilizowashirikisha wadau mbali mbali zilifanywa. Serikali
ilipitisha rasmi Mkakati wa Maendeleo ya Ardhi Zanzibar (NSDS), mnamo
tarehe 4 Machi 2015.
- Kupanga
matumizi ya ardhi ya miji midogo miwili, mmoja Pemba na mmoja Unguja ili
kuongeza huduma katika mikoa yote ya Zanzibar na kuhakikisha kuwa wananchi
wote wa Zanzibar wanakuwa karibu na miji midogo na wanapata huduma zao
zote katika miji hiyo. Idara ya Mipango Miji na Vijiji tayari imeshapanga
mipango midogo (Local Area Plan) ya miji mitatu hadi sasa. Miji hiyo ni Chwaka,
Mkokotoni na Nungwi.
- .Idara ya
Mipango Miji na vijiji tayari imeshayapanga maeneo matatu ya wazi. Eneo la
Kibanda maiti, eneo la Daraja bovu na eneo la Kiembe samaki. Hivi sasa
Idara inafanya jitihada kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Mji (Urban
Development Fund) kuyajenga maeneo hayo. Lengo la Serikali ni
kuhakiksha kuwa katika maeneo yote ya makaazi kuna maeneo ya wazi yenye
hadhi kama ile ya bustani ya Forodhani.
Kusimamia Maendeleo ya Ardhi Mijini, Mikoani na maeneo ya
Fukwe
- Mheshimiwa
Spika, Katika kutekelza
lengo hili Idara imeweza kutekeleza yafuatayo:
- Sambamba
na utayarishaji wa Master Plan, Idara ilitayarisha rasimu ya sheria mpya
ya mipango miji, (Planning and Developement Act), ili kuchukua nafasi ya
sheria kongwe ya Mipango Miji na Vijiji (Town and Country Act, Cap 85) ya
mwaka 1955.
- Kuelimisha
jamii juu ya Sera, Sheria na kanuni mpya za Mipango Miji kwa kufanya
mikutano mitatu juu ya Sera na kuweka kanuni mpya. Mnamo Agosti 2015 ,
kanuni mpya ya usimamizi na udhibiti ujenzi Zanzibar ilipitishwa rasmi (GN
38, 2015). Kanuni hii imeweka mfumo mpya wa utoaji vibali ambao
unasimamiwa na taasisi saba, ikiwemo Manispaa, Halmashauri, Wilaya ya
Magharibi B, Mamalaka ya Mji Mkongwe, Bodi ya wataalam wa ujenzi, na
Jumuiya ya Wafanya Biashara Zanzibar.
Kuimarisha Miji ili kukuza uchumi na kuleta maisha bora
- Mheshimiwa
Spika, Katika kutekelza
lengo hili Idara imeweza kutekeleza yafuatayo:
- Mnamo
tarehe 4 Machi 2015, Serikali ilipitisha Mpango Mkuu wa Matumizi ya Ardhi
ya Jiji la Zanzibar (Zanzibar City Master Plan). Kwa mujibu wa mpango huu,
kitovu cha Mji wa Zanzibar kinahama kutoka eneo la Mji Mkogwe na kuja eneo
la Ng’ambo. Kwa maana nyengine maeneo mapya ya shughuli mbali mbali za
kijamii, kibiashara na kiuchumia kama vile maofisi, maduka, sehemu za
huduma na sehemu za mapumziko zitaongezwa na kuimarishwa katika eneo la
Ng’ambo.
Idara kwa msaada wa Serikali ya Holand, kupitia Manispaa ya Mji wa
Amsterdam, ilifanya mpango mdogo (Local Area Plan) wa eneo la Ngambo: ”Ng’ambo
Tuitakayo”. Mpango huu umefanywa kwa mashirikiano na taasisi za Serikali, za
kiraia na wananchi kwa ujuma. Aidha, idara imefanya mikutano na wakaazi na
masheha wa Shehia zote 15 ambazo zimo katika eneo la kitovu cha mji, ambazo ni
shehia ya Mchangani, Vikokotoni, Mwembetanga, Kikwajuni juu, Kikwajuni Bondeni,
Rahaleo, Gulioni.
- Kuimarisha
kitengo cha utafiti na maendeleo. Katika kipindi cha mwaka 2015/2016,
Idara ilipokea jumla ya wanafunzi 40 kutoka nchi mbali mbali kama vile
Sweden, Holand, Ufaransa, Finland na Uengereza. Wanafunzi hao walikuja
Zanzibar kufanya tafiti mbali mbali zinazohusiana na Mipango Miji na
Vijiji kwa kushirikiana na wafanyakazi wetu na hivyo kutoa fursa ya
kubadilishana uzoefu na upeo. Aidha, Idara yenyewe imefanya tafiti tano
(5) muhimu zinazohusu maendeleo ya Mji wa Zanzibar, ikiwemo utafiti juu ya
maendeleo ya Kitovu kipya cha biashara na huduma Ng’ambo, utafiti juu ya
Mipango ya miji midogo ya Chwaka, utafiti juu ya Utumiaji wa mitandao
(GIS) na utafiti juu ya uanzishwaji wa kituo kipya cha mabasi Ng’ambo.
- Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2015/2016, Katika kutekeleza programu ndogo ya Upangaji wa
Miji na Matumizi ya Ardhi jumla ya Tsh 270,055,000/= ziliidhinishwa
kutumika. Hadi
kufikia Machi, 2016, fedha zilizoingizwa ni Tsh 226,514,649/= sawa
na asilimia 84 % ya makadirio.
PROGRAMU
KUU: UHIFADHI WA MJI MKONGWE, URATIBU NA USIMAMIZI WA UJENZI NA NYUMBA ZA
SERIKALI
- Mheshimiwa Spika, Programu hii ilikuwa na
jukumu la kusimamia shughuli za ujenzi wa Nyumba na Uhifadhi wa Mji
Mkongwe. Programu hii inatekelezwa na Idara ya Ujenzi, Shirika la Nyumba
na Mamlaka ya Uhifadhi na Uendelezaji Mji Mkongwe kupitia programu ndogo
mbili, ambazo ni Uratibu na Usimamizi wa Shughuli za Ujenzi na Nyumba za
Serikali na Uhifadhi na Uendelezaji wa Mji Mkongwe.
PROGRAMU
NDOGO YA URATIBU NA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA UJENZI NA NYUMBA ZA SERIKALI.
- Mheshimiwa Spika, Program hii ndogo
inatekelezwa na Idara ya Ujenzi na Shirika la Nyumba, ambapo kiutekelezaji
programu hii ndogo kwa mwaka wa Fedha 2015/2016 kupitia taasisi hizi mbili
zilizotajwa imeweza kutekeleza shughuli zake kama ifuatavyo :
Kuzifanyia
matengenezo nyumba za maendeleo Unguja na Pemba.
- Mheshimiwa Spika, Shirika la Nyumba Zanzibar
limeweza kutapisha/kutoa maji machafu ikiwa ni pamoja na kujenga sock-pit
Mombasa na kutapisha Septic tank Michenzani na pia kubadilisha mabomba
yaliyoharibika. Aidha Shirika limefanikiwa kuondoa matope yaliokuwa
yakisababisha kujaa kwa makaro na kusambaa kwa maji machafu katika Nyumba
za Mchina Mombasa na baadhi ya Nyumba za Michenzani.
Uimarishaji
wa Mapato
- Mheshimiwa Spika, Shirika la Nyumba la Zanzibar
kwa mwaka wa fedha 2015/2016 ilipangiwa kukusanya jumla ya Tsh.
624,000,000/=. Hadi kufikia tarehe 31 Machi 2016 Shirika limefanikiwa
kukusanya jumla ya Tsh. 471,650,550/= sawa na asilimia 76% ya
makadirio.
- Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa Idara ya
Ujenzi, kwa mwaka wa fedha 2015/2016 imeweza kutekeleza yafuatayo:-
- Kuandaa michoro
na makadirio ya ujenzi kwa jengo la ZRB Pemba pamoja na jengo la ZECO-
Unguja
- Kuandaa michoro
na kusimamia matengenezo ya jengo la Tume ya Sayansi liliopo Maruhubi.
- Kusajili wakandarasi 29 na
kufikisha jumla ya 181.
- Kusajili miradi 97 ambao
imesimamiwa na wataalamu waliosajiwa
- Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016,
Katika kutekeleza programu ndogo ya Uratibu na Usimamizi wa Shughuli za
Ujenzi na Nyumba za Serikali jumla ya Tsh 757,854,000/=
ziliidhinishwa kutumika. Hadi kufikia Machi, 2016, fedha zilizoingizwa ni Tsh
564,614,059/= sawa na asilimia 75 % ya makadirio.
PROGRAMU
NDOGO YA UHIFADHI NA UENDELEZAJI WA MJI MKONGWE
- Mheshimiwa Spika, Program hii ndogo
inatekelezwa na Mamlaka ya Uhifandhi na Uendelezaji Mji Mkongwe ambapo
kiutekelezaji programu hii ndogo kwa mwaka wa Fedha 2015/2016 kupitia
taasisi hii imeweza kutekeleza malengo yaliyokusudiwa kama ifuatavyo :
Utekelezaji wa mpango wa matumizi ya barabara
- Mheshimiwa
Spika, Mamlaka
imetayarisha na kuwasilisha Serikalini mpango wa matumizi ya barabara
zilizomo katika eneo la Mji Mkongwe (eneo la Urithi wa Kimataifa), kwa
madhumuni ya kupunguza msongamano mkubwa ulioukabili mji huu unaoletea
athari kubwa kwa majengo ya kihistoria pamoja na viliyomo, unaoushushia
hadhi Mji huu kama ni Urithi wa Kimataifa.
Ujenzi
wa Ukuta wa Ukingo wa Bahari ya Mizingani
- Mheshimiwa
Spika, Kazi ya
ujenzi wa ukuta mpya inaendelea vizuri, ambapo kutokea upande wa bustani
ya Forodhani mita 30 za ujenzi wa ukuta umekamilika, na kwa kutokea upande
wa mkahawa wa Mercury kazi ya ujenzi wa msingi (foundation) wa ukuta huo imekamilika. Kinachoendelea hivi sasa ni ujenzi
wa ukuta ambapo wastani wa asilimia 22 ya kazi ya ujenzi wa ukuta mpya kwa
pande zote imekamilika.
Ukarabati
wa Jengo la Chawl liliopo Darajani
- Mheshimiwa Spika, Jengo la Chawl ni miongoni
mwa majengo mashuhuri (Monuments) yenye daraja la kwanza ndani ya Mji
Mkongwe. Mamlaka ilikamilisha utayarishaji wa ramani za awali (Existing
drawings) na za mapendekezo (Proposed drawings) pamoja na makisio ya
gharama kwa ajili ya ukarabati wa jengo hilo na baadae kuwasilishwa (
ZSSF) ambao ndio waliokabidhiwa rasmi jengo hili na Serikali kwa ukarabati
na kulirejesha tena kwenye matumizi ambayo yatakuwa na tija zaidi tofauti
na hali ya sasa. ZSSF wameanza kuchukua hatua za awali kwa kuwatumia
washauri elekezi ambao wanahitajika kufuata maelekezo ya kiutalaamu wa
kiuhifadhi kutoka Mamlaka ya Mji Mkongwe.
Ukarabati
wa Jengo la Beit-el-Ajaib
- Mheshimiwa Spika, Jengo la Beit el Ajab ni
miongoni mwa majengo mashuhuri yanayotambulikana kimataifa na lenye daraja
la kwanza kiuhifadhi. Mamlaka ya Mji Mkongwe imekamilisha utayarishaji
wa ramani za awali (existing drawings) na za mapendekezo (proposed
drawings) pamoja na makisio ya gharama kwa ukarabati na ujenzi mpya wa
eneo lililoanguka wa jengo la Beit el Ajaib na kuwasilisha nchini
Oman. Kilichofata ni kuletwa kwa mtaalamu kutoka Oman kwa ajili ya uhakiki
wa makisio hayo, utayarishaji wa nyaraka nchini Oman na zabuni (tender
documents). Kwa kushirikiana na wataalamu wa Mamlaka ya Mji Mkongwe kazi
hiyo imemalizika na kuwasilishwa nchini Oman. Mamlaka tayari imepokea
barua kutoka Wizara ya Urithi na Utamaduni ya Oman ambayo ndiyo iliyokuwa
ikishughulikia suala hili tangu hapo awali na kwamba shughuli za ujenzi wa
Beit el Ajab zinatarajiwa kuanza rasmi mapema mwezi wa Juni 2016.
Kuweka kumbukumbu za matumizi ya maeneo ya wazi.
- Mheshimiwa
Spika, Mamlaka
inaendelea na kazi ya kuhakiki na kuweka kumbukumbu za matumizi ya maeneo
yote ya wazi yaliyomo ndani ya Mji Mkongwe ambayo baadhi yake hayakuwa na
mpangilio mzuri wa matumizi ambayo yanatambulika na Mamlaka. Mamlaka
imeandaa mpango wa matumizi ya maeneo hayo ambao unahusisha utoaji wa
mikataba kwa watu binafsi kwa matumizi yao mbali mbali ya kijamiii na
kibiashara, bila kuathiri uhifadhi na kwamba bado maeneo hayo yatakuwa
milki ya Serikali. Jumla ya mikataba 10 imefungwa baina ya Mamlaka na
watumiaji binafsi wa maeneo ya wazi kwa kuchangia mapato na uimirashaji wa
uhifadhi ndani ya Mji Mkongwe.
Mpango wa Uwekaji wa Posta na Mabango ya Matangazo
- Mheshimiwa
Spika, Mamlaka
imetayarisha mpango wa uwekaji wa mabango ya matangazo na ubandikaji
“advertisements and publications” (postas) kama inavyokubalika kwa miji
yenye hadhi Ulimwenguni. Madhumuni ni kuondoa tatizo la kuzagaa kwa
mabango ya matangazo ya aina mbali mbali katika kuta za majengo, miti na
mapambo ya ndani ya Mji Mkongwe ili kusaidia kuuweka mji wetu katika hali
ya usafi ambao hivi sasa kuta nyingi zimechafuliwa kwa ubandikaji ovyo wa
mabango ya matangazo hayo.
Takwimu za Idadi ya Mahoteli na Maduka ya Vinyago
- Mheshimiwa Spika, ukaguzi
uliofanywa na Mamlaka umegundua kuwepo kwa mahoteli 68 ndani ya Mji
Mkongwe na maduka 94 ya biashara za vinyago hususani katika eneo la
Shangani. Lengo la takwimu hizi ni kuweka mpango utakaosaidia Mamlaka
kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yake.
- Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016,
Katika kutekeleza programu ndogo ya Uhifadhi na Uendelezaji Mji Mkongwe
jumla ya Tsh 360,047,000/= ziliidhinishwa kutumika. Hadi kufikia
Machi, 2016, fedha zilizoingizwa ni Tsh 306,343,500/= sawa na
asilimia 85% ya makadirio.
PROGRAMU
KUU: USIMAMIZI WA HUDUMA ZA MAJI NA NISHATI
- Mheshimiwa Spika, Program hii inajumuisha
Programu Ndogo moja tu ambayo ni Usimamizi, Uendelezaji na Usambazaji wa
Huduma za Maji na Nishati na inatekelezwa na Taasisi nne ambazo ni Mamlaka
ya Maji (ZAWA), Shirika la Umeme (ZECO), Mamlaka ya Kudhibiti na Kusimamia
Ubora wa Viwango vya Huduma za Maji na Nishati Nchini (ZURA) na Idara ya
Nishati na Madini na ina jukumu la kusimamia Uzalishaji na Usambazaji
Endelevu wa Huduma za Maji na Nishati.
MAMLAKA YA MAJI
- Mheshimiwa Spika, Sekta ya maji
inaendelea kutoa mchango mkubwa katika ustawi wa jamii zetu Mijini na
Vijijini katika kuimarisha afya za wananchi kwa matumizi ya majumbani,
maendeleo ya kiuchumi katika kuendeleza Kilimo, utalii, biashara, na kubwa
zaidi ni umuhimu wa maji katika utunzaji wa mazingira kwa ajili ya ustawi
wa maendeleo ya Taifa letu.
Ukusanyaji wa Mapato
- Mheshimiwa
Spika, Mamlaka
ya Maji Zanzibar kwa bajeti ya mwaka a fedha 2015/2016 ilipangiwa
kukusanya jumla ya TShs bilioni 5.1 kutokana na mauzo ya maji na
shughuli nyenginezo. Hadi kufikia Machi 2016, jumla ya TShs bilioni 1.9
zimekusanywa sawa na asilimia 42% ya makadirio ya makusanyo yote.
- Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016
Sekta ya Maji kupitia Mamlaka ya Maji ilifanikiwa kutekeleza Shughuli za
Programu na Miradi ya Maji sita ambayo ni Programu ya Usambazaji wa Maji
Vijijini, Programu ya Uhuishaji na Upanuzi wa Shughuli za Maji Mijini,
Mradi wa Kuijengea Uwezo Mamlaka ya Maji Awamu ya Pili (JICA PHASE 2), Mradi wa
Kuimarisha Miundombinu ya Maji na Kuijengea Uwezo Mamlaka kifedha (ADF
12), Mradi wa uchimbaji visima wa Ras al- khaimah pamoja na Kazi za
Kawaida zikiwemo Kulinda na kuhifadhi vianzio vya Maji na Kufanyia
Matengenezo Miundombinu ya Maji.
- Mheshimiwa
Spika, kwa
kipindi hichi cha mwaka wa fedha 2015/2016 Wizara yangu iliendelea kuwapatia
Maji safi na salama wananchi waishio vijijini kupitia Programu ya
Usambazaji Maji Vijijini kwa kujikita zaidi na ukarabati wa miundombinu ya
maji kwa ulazaji wa mabomba, ujenzi wa vibanda vya kuendeshea mitambo,
ununuzi na ufungaji mita za watumiaji maji, ujenzi wa vituo vya malipo ya
maji na huduma kwa wateja pamoja na ujenzi wa matangi katika maeneo mbali
mbali ya Vijijini Unguja na Pemba kama inavyoonesha katika jadweli
lifuatalo:
Jaduweli namba 2. Utekelezaji wa Programu ya
Usambazaji Maji Vijijini
SN
|
KAZI ZILIZO TEKELEZWA
|
MAELEZO YA UTEKELEZAJI
|
MAENEO HUSIKA
|
1
|
Ulazaji wa
mabomba
|
Jumla ya kilomita 17.634 zimefanyiwa kazi ambapo kilomita 10.134 kwa
Unguja na 7.5 kwa Pemba kazi hii
ni endelevu
|
Mwanguo, Mvuleni, Makunduchi, Tumbatu na Kinduni kwa
Unguja. Kidundo, Mtambwe, Mtuhaliwa, Wambaa, Rui na kilindi kwa Pemba.
|
2
|
Uwekaji wa
Pampu na Mota mpya
|
Maeneo
husika yamefanyiwa kazi kutokana na na pampu na mota za awali kuungua au
kuzidiwa na mahitaji ya watumiaji. Aidha kazi hii ni endelevu
|
Kizimkazi, Kitogani, Ukongoroni, Kisongoni, Matemwe,
Jambiani Kivulini, Bwejuu na Kibele kwa Unguja.
Na kwa Pemba ni Mgagadu,
Mchanga Mdogo, Shengejuu Ng’ambwa, Konde ,Kironjo A, na Michenzani.
|
3
|
Ujenzi wa Vibanda vya kuendeshea pampu
|
Kazi
hii inatarajiwa kuendelezwa katika mwaka wa fedha ujao.
|
Kinduni,
Makunduchi Uwandani, Kibuteni kwa Unguja. Na kwa Pemba ni Shumbavyamboni na
Mahuduthi.
|
4
|
Ujenzi wa
matangi ya kuhifadhia Maji
|
Kazi imekamilika kiasi kwa hatua za awali kwa upande wa makunduchi na
imekamilika kwa maeneo yaliyobakia.
|
Makunduchi,
Mtende, Michamvi, Upenja na Tunguu Mjonga
|
5
|
Ujenzi wa ofisi ya afisa
wa maji wilaya ya kusini na huduma kwa wateja
|
Kazi hii inaendelea na inatarajiwa kukamilishwa ndani ya mwaka wa
fedha ujao ili kurahisisha upatikanaji wa Huduma kwa Wateja hususan huduma za
malipo kwa wananchi wa ukanda wa Kusini ya Unguja
|
Paje.
|
6.
|
Ufungaji
wa Mita za
watumiaji maji.
|
jumla ya mita 48 zimefungwa kwa upande wa unguja na mita 118 zimefungwa
kwa upande wa pemba kazi hii
ni endelevu
|
Marumbi, Matemwe na Pwani Mchangani kwa Unguja.
Mgagadu,Jadida, Kizimbani, Limbani, Kipangani na Kifumbikai kwa Pemba.
|
Chanzo:
Mamlaka ya Maji, Zanzibar
Uhuishaji na Upanuzi wa Shughuli za Maji Mijini
- Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha 2015/2016
Wizara yangu kupitia Mamlaka ya Maji ilifanikisha kazi za Programu ya
Uhuishaji na Upanuzi wa Shughuli za Maji Mijini kwa kuhusisha shughuli
tofauti katika maeneo mbali mbali ya Mjini Unguja na Pemba kama inavyojionesha
katika jaduweli ifuatayo:
Jaduweli
nambari 3 : Uhuishaji na Upanuzi wa Shughuli za Maji Mijini
S/N
|
KAZI ZILIZOFANYIKA
|
UTEKELEZAJI HALISI
|
MAENEO HUSIKA
|
1.
|
Ufungaji
wa Mita za watumiaji maji
|
jumla ya mita 211 zimefungwa kwa upande wa unguja na mita 477
zimefungwa kwa upande wa pemba
Kazi ya
ufungaji mita ni endelevu
|
Melinne
kwa Unguja. Wawi, Tibirizi, Madungu, Uwanja wa Ndege, Limbani, Jadida, Bopwe,
Uweleni, Mkoroshoni Bahanasa na kwa Pemba.
|
2.
|
Uwekaji wa
Pampu na Mota Mpya
|
Maeneo
husika yamefanyiwa kazi kutokana na na pampu na mota za awali kuungua au
kuzidiwa na mahitaji ya watumiaji. Aidha kazi hii ni endelevu
|
Kaburi
Kikombe, Kinumoshi N4, Mbweni matrekta, chumbuni,Selemu No 1, Mombosa kwa
Mchina kongwe, Masumbani, Magogoni, Welezo, K/Kikombe, Mombasa afisini, na
Kwa binti Amrani No 2 kwa Unguja. Na kwa Pemba ni kwa Sharif Ali namba-1,2 na 3, Darajani,
Jondeni, Jamvini na Kwa Bi Mtumwa.
|
3.
|
Ulazaji wa
Mabomba
|
Jumla ya kilomita 3.103 zimefanyiwa kazi Kazi hii ni Endelevu
|
Kwerekwe
C, Welezo na Masingini kwa Unguja.
|
4.
|
Ununuzi wa
vidhibiti umeme
|
Jumla ya vidhibiti umeme 15 vimenunuliwa
|
Chunga, M/Mchomeke,Kianga na Welezo kwa Unguja. Kwa
Pemba ni kironjo Kijuki na Sizini, Mtambwe kaskazini, Kwa sharifuali na
Darajani Mkoani.
|
5.
|
Upelekaji
wa Umeme Vituoni
|
Kazi
imekamilika
|
Kwerekwe C Unguja
|
6.
|
Ujenzi wa
Matangi ya Kuhifadhia Maji
|
Kazi
imekamilika
|
Chumbuni, Dole na Kianga
|
Chanzo:
Mamlaka ya Maji, Zanzibar.
- Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016
mbali na shughuli za Programu,Wizara yangu imefanikiwa kutekeleza Miradi
ya Maji kama ifuatavyo.
Mradi
wa Kuijengea Uwezo Mamlaka ya Maji (Awamu ya Pili)
- Mheshimiwa Spika, Mradi huu unaofadhiliwa kwa
pamoja kati ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Japan kupitia
Shirika lake la Maendeleo (JICA), umeendelea na kazi zinazohusu kuijengea
Uwezo Mamlaka ya Maji kwa kutekeleza shughuli za Mradi huu kama
inavyoonekana katika jaduweli ifuatayo.
Jaduweli
nambari 4: Utekelezaji wa Kazi za Kuijengea Uwezo Mamlaka ya Maji (Awamu ya
Pili)
SN
|
Shughuli Mahsusi Zilizotekelezwa
|
Utekelezaji Halisi
|
1.
|
Ununuzi na
Ufungaji wa mabomba na viungio vyake katika maeneo ya Gulion hadi Makadara
|
Jumla ya
mabomba yenye ukubwa wa inchi 2½ hadi inchi 16 yamenunuliwa na tayari
kilomita 2 zimeshalazwa.
|
2.
|
Ukusanyaji
na Utunzaji wa taarifa za Mamlaka ya Maji.
|
Kukusanya taarifa zilizoweza kutambua mivujo ya maji kuanzia mwaka
2013-2015 kupitia (Survace leakage survey) ambapo jumla ya shehia 45 za Mjini
na 23 za Magharibi zimeweza kuhifadhiwa katika mfumo wa GIS.
|
3.
|
Kupanga na Kutekeleza Shughuli za Kupunguza mivujo ya
Maji
|
kukutana kwa wiki mara moja na kujadili
jinsi ya kuandaa michoro (Technical Standards) juu ya uandaaji michoro,
ulazaji na matengenezo ya mabomba,
kuendelea na ulazaji wa mabomba katika
eneo la Gulioni-Makadara na kuanzisha mfumo wa manifold kwa nyumba ishirini
zilizofungwa mita ili ziatakazorahisisha ufungaji wa mita na matengenezo.
|
4.
|
Kuongeza
viwango vya elimu na taaluma kwa wafanyakazi wa Mamlaka ambapo
|
Jumla ya
wafanyakazi 4 wamepatiwa mafunzo nchini Japan
|
5.
|
Kuendesha
Utafiti na Ukaguzi kwa Wateja kwa baadhi ya maeneo ya Mjini Magharibi ambapo
|
zoezi hili
tayari limekamilika kwa zoni ya Saateni na lipo katika hatua za kumalizia
katika zoni ya Mpendae
|
Chanzo: Mamlaka ya Maji, Zanzibar
Mradi wa Kuimarisha Miundombinu ya Maji na Kuijengea
Uwezo Mamlaka Kifedha (ADF 12)
- Mheshimiwa
Spika, Mradi huu
umekamilisha kazi ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa Mradi kwa
wakandarasi kutoka kampuni ya NSPT ya Tanzania kwa kazi ya Ujenzi wa
vianzio vya maji na Kampuni ya SPENCON kwa kazi ya ujenzi wa miundo mbinu
ya Maji ambapo tayari wakandarasi wote hao wawili wameshakabidhiwa maeneo
ya mradi kwa ajili ya kuanza kazi. Kwa upande wa ujenzi wa vyoo maskulini
na usafi wa mazingira ambayo ni sehemu mojawapo ya Mradi huu tayari
Mshauri elekezi wa Kampuni ya Howard Humphreys Tanzania Ltd.
ameshakamilisha Ripoti ya Usanifu wa Mradi na kuiwasilisha kwa hatua
zinazofuata.
Aidha,
kwa upande wa Kazi ya Kuijengea Uwezo Mamlaka ya Maji, Mradi umeendesha warsha
ya uchambuzi wa zabuni (Tender Evaluation Workshop) kwa lengo la kuijenga uwezo
kamati ya uchambuzi wa zabuni na tayari taratibu za ununuzi wa mita 6,900 za watumiaji wa maji
zinaendelea.
Mradi wa Uchimbaji Visima wa Ras al- Khaimah
- Mheshimiwa
Spika, hadi kufikia
Machi 2016, jumla ya visima 136 vimechimbwa kati ya 150 sambamba na ujenzi wa
matangi 6 ya kuhifadhia maji, ulazaji wa mabomba, na ujenzi wa miundo
mbinu mengine ya maji. Kazi inayoendelea kwa sasa ni ukamilishaji wa
visima 14 vilivyobakia.
- Mheshimiwa
Spika, kama
zilivyo Mamlaka nyengine, Mamlaka ya Maji Zanzibar ina wajibu wa
kutekeleza Kazi zake za Kawaida kupitia vyanzo vyake vya mapato ili
kutimiza dhana ya kuwa Taasisi inayojitejemea na kujiendesha kibiashara,
kwa lengo la kuondokana na utegemezi wa rasilimali, hususan fedha kutoka
Serikali kuu.
- Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2015/2016, Mamlaka imefanikiwa kutekeleza shughuli mbali
mbali zinazohusiana na matengenezo ya miundombinu ya maji kama
inavyoonekana katika jaduweli ifuatayo:
Jaduweli
nambari 5: Matengenezo ya Miundombinu ya Maji
S/n
|
Kazi zilizotekelezwa
|
Maeneo yaliyohusika
|
1.
|
Matengenezo ya mabomba
|
Migombani, Kianga, Jang’ombe, Mchangani,
Bambi, Kihinani, M/Makumbi, Kijangwani, M/Mchomeke, Shaurimoyo, Lumumba,
Mpendae, Kijichi, M/Kwerekwe, Nungwi, Matemwe, Welezo, Kwamtipura, Magogoni,
Chunga, Mbweni, Meya, Mikunguni, Sogea, Baraza la Wawakilishi, Kilimani,
Michenzani, Kilimahewa, M/Ladu, Pangawe, Michungwa Miwili, Kinuni, Migombani
Ikulu, Mwanyanya, Kibweni, Kwamchina, Kombawapya, na Daraja bovu, Matemwe,
kilimani, Michenzani, Migombani, Meya, Welezo, Melitano, Mkunazini, Elimu
Mbadala, Kwarara, Tunguu na Kianga kwa Unguja. Na kwa upande wa Pemba ni Jamvini, Mjini
Chake, Mjini Mkoani, Mjini Wete, Kinyikani, Wesha,Vitongoji
Kilindi,Kisiwapanza, Mtambile, Shumba Mjini Changaweni, Makangale, Konde,
Makongwe, Gando, Junguni, Kojani, Pandani ,Ole.Wambaa na Ukunjwi.
|
3.
|
Marekebisho ya Umeme
|
Visima vya Kiashange, Kaburi Kikombe, Mwembe Mchomeke
No 51,Kibuteni, Bumbwini, Kidanzini, Kiboje, Bweleo, Manzese, Mgambo, Muyuni,
Chunga No 09, Chwaka, Chaani, Dunga S.S.Metha, Chumbuni,Kibele, Bweleo,
Msikiti Mzuri No 10, Msikiti Mzuri 12, Kisongoni Nungwi Kae, Matrekta,
Mfenesini, Kinumoshi No 3,4,5, Machui, Welezo No 2, Mombasa Ofisini, Umbuji,
Kitogani, Kianga No 7 na Salem 1 kwa Unguja. Na
Sizini,Kironjo,Kijichame,Makangale,Gawani,Bunguni, Kibomani,
Penjewani,Ziwani,Ngambwa,Kwapweza, Kwa Sharifuali, Chanjaani, Changaweni,
Mtambile, Ngombeni, Ngwachani, Mjimbini kwa upande wa Pemba.
|
4.
|
Matengenezo ya pampu na mota zilizoungua
|
Visima vya Bweleo, Machui, KaburiKikombe, Bumbwini
Kidanzini, Mombasa Afisini, Kieshange No 4 Kitogani, Mwanyanya, Jendele,
Maungani na usafishaji wa visima (Flushing) imefanyika katika maeneo ya
MigombaniPangeni, K/Kikombe,Welezo na Saateni workshop kwa Unguja. Na Pemba
ni Visima vya Mfikiwa, Ukutini, Makangale,Changaweni Chake Chake, Mjimbini,
Sharifuali no-3 na Wingwi Mlindo. FlUshing Kwa Pemba imefanyika Visima vya
Ng’ambwa, Mauleni, Ng’wachani, Bogoa, Kijichame,Mfikiwa, Ole skuli, Mazurui,
Kwamkoba, na kinowe.
|
Chanzo: Mamlaka ya Maji, Zanzibar
IDARA YA NISHATI NA MADINI
- Mheshimiwa
Spika, Idara
ya Nishati na Madini ni taasisi inayohusika na Usimamizi na Usambazaji wa
Huduma ya Nishati hapa nchini kwa lengo la Kuimarisha Upatikanaji na
Usambazaji wa Nishati yenye ufanisi, kwa bei nafuu na inayozingatia
Uendelevu wa Mazingira yaliyo salama na rafiki kwa maendeleo ya kiuchumi
na kijamii ambapo kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Idara hii ilisimamia
na kutekeleza mambo yafuatayo:-
Mradi wa Utekelezaji wa Sera ya Nishati
- Mheshimiwa
Spika, Mradi huu unatekelezwa kwa pamoja kati ya
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Washirika wa Maendeleo na unahusika
zaidi katika maeneo makubwa mawili ambayo ni Kuijenga uwezo Sekta ya
Nishati - Awamu ya Pili (Zanzibar Energy Sector Support
Consolidated Phase) kwa mashirikiano na Shirika la maendeleo la Sweden
(SIDA) na eneo kuu la pili ni Kuimarisha Mazingira pamoja na
Kupambana na Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi ambapo baada ya kukamilika
kwa maeneo haya mawili, bila shaka sekta ya Nishati kwa Zanzibar itakuwa
imeimarika na kuongeza ufanisi kiutekelezaji ambayo ni hatua muhimu sana
kwa mustakbali wa uchumi wetu na sekta zote kwa ujumla.
- Mheshimiwa
Spika, katika
utekelezaji wa mradi wa Kuijenga uwezo Sekta ya Nishati - Awamu ya
Pili, Idara kwa kushirikiana na Ubalozi wa Sweeden tayazi imetiliana saini
na Kampuni ya Multy Consultant ASA ya nchini Norway ambayo ilishinda
zabuni ya ushauri Elekezi kwa mradi huu unaotarajiwa kutekelezwa kwa kipindi
cha miaka mitatu kuanzia mwaka huu wa fedha.
Aidha, Idara kwa kushirikiana na iliyokuwa Afisi ya Makamo wa Kwanza wa
Rais chini ya mradi wa mabadiliko ya Tabia nchi kwa ufadhili wa UNDAP
imetekeleza yafuatayo:-
- Jumla ya mifumo (38) ya umeme wa jua (Solar Units) imewekwa
katika maeneo mbali mbali Unguja na Pemba.
- Ziara za ukaguzi katika maeneo yaliyofungwa mifumo hiyo kwa
kutathmini ufanisi zimefanyika.
- Hati ya muongozo (guidelines document) imeandaliwa sambamba
na kuendesha semina ya kushajihisha matumizi ya miongozo hiyo.
- Kuandaa Mpango Kazi wa utekelezaji wa Será ya Nishati
- Kuandaa Kanuni za kupiga marufuku matumizi ya taa zenye kutumia
umeme mwingi (incandescent bulbs).
- Kufunga taa sanifu (energy saving bulbs) katika maeneo
maalum ya majaribio (pilot areas) ambayo ni Fumba na Mwakaje.
Mradi wa Utafiti wa Nishati Mbadala
- Mheshimiwa
Spika, Serikali inaendelea na azma yake ya kukamilisha
Mradi huu wa Nishati MbadalaUnaofadhiliwa kwa pamoja kati ya Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar na Jumuiya ya Nchi za Ulaya (EU) wenye lengo
la kufanya utafiti ili kubaini uwezekano wa Zanzibar kupata umeme kwa njia
mbadala.
- Mheshimiwa
Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/206, Wizara
imesimamia zoezi la usafishaji maeneo pamoja na ujenzi wa minara mitano
yenye urefu wa mita sabiini na moja (71 m) pamoja na kufunga vifaa vya
kurikodia (sensors) kwa lengo la kukusanya taarifa za mwenendo wa upepo na
nguvu za jua. Ujenzi huo umetekelezwa chini ya Kampuni ya AGMIN kutoka
Italy. Vile vile Wizara imekamilisha kupatikana kwa mkandarasi (Kampuni ya
MWH ya Spain) ambae atashughulikia masuala ya kisheria pamoja na
kuzijengea uwezo taasisi zinazoshughulikia miradi ya Nishati Mbadala.
Aidha, Mshauri elekezi (Kampuni ya Intec Gopa ya Ujerumani) anaendelea na
kazi na ukusanyaji wa tarifa hizo (data collection) na tayari ameshatoa
ripoti yake awali ya miezi mitatu (Oktoba-Disemba 2015) inayoonesha
mwelekeo mzuri wa mwenendo wa upepo na nguvu za jua.
- Mheshimiwa Spika, mbali na shughuli za
Maendeleo kwa mwaka wa fedha 2015/2016 imefanikiwa kutekeleza Kazi za
Kawaida kama ifuatavyo:-
Kushiriki
katika Mikutano ya Masuala yote yanayohusu Nishati ya Kitaifa, Kikanda na
Kimataifa pamoja na Kuendelea kusimamia Upatikanaji wa Mafuta Zanzibar.
- Mheshimiwa Spika, Katika kutekeleza hili, Idara
imefanikiwa kusiriki mikutano kadhaa iliyofanyika ndani na nje ya nchi
ikiwemo vikao vya Jumuiya ya Afrika Masharikikatika masuala ya nishati ya
umeme ( Dar es Salaam- Tanzania na Kigali - Rwanda). Bilashaka
fursa hii inaongeza uzoefu na utaalamu kwa wafanyakazi wa Idara hii.
Aidha,
katika kuhakikisha nishati ya mafuta inapatikana kwa uhakika na, Idara
inaendelea kushirikiana na Mamlaka ya Kusimamia na Kudhibiti nishati nchini ili
kutambua mwenendo wa biashara ya mafuta pamoja na kufanya ufuatiliaji na ukaguzi
kwenye vituo vyote vya makampuni yanayoendesha biashara ya mafuta hapa nchini.
Kuendeleza Mashirikiano na Wadau wa Maendeleo katika
Kuendesha Mafunzo yanayohusiana na suala la Mafuta na Gesi Asilia pamoja na
Kujenga Uelewa kwa Wananchi juu ya Masuala ya Nishati.
- Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kuendeleza
Mashirikiano na wadau mbali mbali wa maendeleo wa ndani na nje, Idara
imefanikiwa kuendesha semina tatu zinazohusiana na masuala ya mafuta na
gesi asilia ambazo zimewashirikisha wafanyakazi wa Idara ya Nishati na
Madini ikiwa ni sehemu ya kuwajengea uwezo Kitaaluma. Jumla ya semina
mbili, vipindi vya redio na televisheni na mikuano kadhaa imefanyika kwa
lengo la kujenga uelewa kwa wananchi .
SHIRIKA
LA UMEME
- Mheshimia Spika, Shirika la Umeme ni taasisi
inayohusika na Usimamizi na Usambazaji wa Huduma ya Nishati ya Umeme hapa
nchini kwa lengo la Kuimarisha Upatikanaji na Usambazaji wa Nishati hiyo
kwa ufanisi, yenye uhakika na kwa bei nafuu kwa ajili ya maendeleo ya
kiuchumi na kijamii ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa programu ya
usimamizi wa huduma za Maji na Nishati. Kwa mwaka wa fedha 2015/2016
Taasisi hii ilisimamia na kutekeleza
kazi ya Usambazaji na Uimarishaji wa Miundo Mbinu ya Umeme Mjini na
Vijijini.
Mapato
na Matumizi
- Mheshimia Menyekiti,kimsingi Shirika hili kama
ilivyo kwa mashirika mengine ya umma hapa nchini sio tu yana wajibu wa
kuhakikisha upatikanaji wa huduma zenye ubora unaokubalika kitaifa na
kimataifa na kwa gharama nafuu kwa lengo la kuimarisha ustawi wa jamii
yetu kiuchumi, kijamii na kimazingira bali pia kuliwezesha Shirika
kujiendesha kibiashara na hatimaye kuweza kuchangia katika mfuko mkuu wa
Serikali.
- Mheshimia Menyekiti, kwa mwaka wa fedha 2015/2016,
Shirika lilikadiria kukusanya Tsh. 107,063,020,514/= kutokana na Biashara
ya kuuza umeme na huduma nyenginezo zinazotolewa kwa wananchi na
wafanyabiashara ikiwemo wawekezaji mbali mbali hapa nchini. Hadi kufikia
tarehe 31 Machi, 2016 Shirika limekusanya jumla ya Tsh. 63,277,985,396/=
sawa na asilimia 59.1% ya makadirio.
Kwa
upande wa Matumizi, Shirika lilikadiria kutumia jumla ya Tsh. 99,838,743,939/=.
Hadi kufikia tarehe 31 Machi 2016, Shirika lilikwishatumia Tsh. 67,980,810,349/=
sawa na asilimia 68.1% ya makadirio kama inavyoonekana katika jaduweli
lifuatalo.
Jaduweli
nambari 6: Matumizi
ya Shirika la Umeme kwa mwaka wa fedha 2015/2016
MAELEZO
|
MAKADIRIO YA MWAKA 2015-2016
|
MATUMIZI HALISI Julai,2015 hadi Machi, 2016.
|
Ununuzi wa
Umeme
TANESCO
|
58,456,165,441.00
|
46,281,896,474.96
|
Kazi ya
kawaida
|
26,378,880,650.00
|
11,699,728,964.07
|
Kazi ya
maendeleo
|
15,003,697,848.00
|
9,999,184,910.39
|
Jumla
|
99,838,743,939.00
|
67,980,810,349.42
|
Chanzo:
Shirika la Umeme, Zanzibar
- Mheshimiwa
Spika, Kwa
kipindi hichi cha mwaka wa fedha 2015/2016 Wizara yangu kupitia Shirika la
Umeme iliendelea kuwapatia huduma za umeme wananchi waishio mijini na
vijijini kupitia Programu na Miradi ya Umeme nchini kwa kushirikiana na
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar pamoja na Washirika mbali mbali wa
Maendeleo waliopo ndani na nje ya nchi kwa kujikita zaidi na ukarabati wa
miundombinu ya umeme na usambazaji wa umeme Vijijini Unguja na Pemba.
Usambazaji
wa Umeme Vijijini
- Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka wa
fedha 2015/2016 Shirika limejenga kilomita 33.1 ya umeme mkubwa na
kilomita 83.9 za laini ndogo ya Umeme pamoja na uwekaji wa Transfoma 35 za
kusambaza umeme katika Vijiji 36 kwa Unguja na Pemba kama inavyoonekana
katika jaduweli ifuatayo-:
Jadueli
nambari 7: Vijiji Vilivyopatiwa Umeme
UNGUJA
|
PEMBA
|
Binguni
Mtakuja
|
Chupwe
Micheweni
|
Bungi
Usalama
|
Gongomawe
|
Cheju
Kisomanga
|
Kisiwa cha
Makoongwe
|
Donge
Kiongwe Kidogo
|
Kisiwa cha
Shamiani Muambe
|
Hanyegwa
Mchana
|
Kisiwa
Panza
|
Kandwi
|
Kiziwani
Shungi
|
Kijini
|
Konde
Mipurani
|
Matetema
|
Mazoweya
Pujini
|
Maungani
Kichakapunda
|
Mgeni nje
Shumba vyamboni
|
Mbuyu
Tende
|
Michungwani
|
Mgambo
|
Mitungujani
|
Ndijani
Nyambiza
|
Mjananza
Wingwi
|
Tunguu
|
Mjimbini
Kangani
|
Ubago
Wilayani.
|
Mtimbu
Pujini
|
Upenja
Kaskazini
|
Muambe
kwasaanani
|
Uzi Pwani
|
Mwachawa
|
Pujini
Kibaridini
|
|
Sebudawa
Micheweni
|
|
Shengejuu
Mtambwe
|
|
Wawi Magome
|
Chanzo:
Shirika la Umeme, Zanzibar
Uimarishaji
wa Miundombinu ya Umeme.
- Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha miezi 9,
Shirika limebadilisha waya chakavu kilomita 37.9, nguzo mbovu 1,319 na
kupima transfoma 577 kwenye maeneo ya Mijini na Vijijini pamoja na
kuzifanyia marekebisho zile zilizokuwa na matatizo ili kuhakikisha kwamba
hali ya upatikanaji wa huduma bora ya Umeme inapatikana kwa uhakika na kwa
wakati wote.
Ufungaji
wa Mita za TUKUZA:
- Mheshimiwa Spika, lengo la mradi huu ni kuimarisha
ukusanyaji wa mapato ya Shirika na kupunguza malimbikizo ya madeni. Hadi
kufikia Machi, 2016, Shirika limenunua mita 13,000 za TUKUZA kwa gharama
ya Tsh.1,423,500,000/=. Kati ya hizo, Mita 6,645 zimefungwa kwa
Wateja wapya na Mita 6,355 zimebadilishwa kwa wateja wa zamani wenye mita
za kawaida na mbovu.
MAMLAKA
YA UDHIBITI YA HUDUMA ZA MAJI NA NISHATI
- Mheshimiwa
Spika, Mamlaka ya Udhibiti ya Huduma
za Maji na Nishati ni Taasisi yenye jukumu la kusimamia Huduma za Maji
safi na Maji taka, Nishati ya umeme pamoja na Mafuta na Gesi (down stream)
na kwa hiyo inalenga kutekeleza lengo kuu la Programu ya Usimamizi wa
Huduma za Maji na Nishati ambalo ni Kufikia Usimamizi Endelevu na
Usambazaji Toshelezi wa Huduma za Maji na Nishati kwa mujibu wa Mahitaji
ya Jamii.
- Mheshimiwa
Spika, Kwa
Mwaka wa Fedha wa 2015/2016 Mamlaka
ya Udhibiti ya Huduma za Maji na Nishati imefanikiwa kutekeleza mambo
yafuatayo:-
Kuandaa Kanuni za Usimamiaji wa Sekta ya Mafuta kuanzia Uagiziaji,
Upakuaji, Uhifadhi, Usambazaji, Uuzaji na Ujenzi wa Vituo vya Mafuta.
- Mheshimiwa Spika, Mamlaka katika kusimamia vyema
majukumu ya kusimamia biashara ya mafuta nchini, imeandaa Kanuni za
Kusimamia Biashara ya Mafuta (Petroleum Supply Regulations,2015) na Kanuni
za Kusimamia ujenzi wa vituo vya Mafuta ili kuweka mazingira ya vituo
hivyo kuwa katika viwango vinavyokubalika.
Kuanza
Shughuli za utoaji wa leseni.
- Mheshimiwa Spika, Katika kutekeleza hili,
Mamlaka imeanza kufanya ukaguzi wa vituo vyote vya mafuta kwa upande wa
Unguja ili kujiridhisha juu ya viwango na ubora wa vituo hivyo. Hadi
Machi, 2016 Mamlaka imekagua vituo 30 kati ya vituo vyote 50 vilivyopo
Zanzibar na kutoa maelekezo ya kufanya matengenezo na marekebisho kwa
vituo ambavyo havikidhi viwango kabla ya kuwapa leseni.
Kuanza kupanga bei za mafuta ya Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa.
- Mheshimiwa Spika, Mamlaka ilikabidhiwa rasmi
jukumu la kupanga bei elekezi na Bodi ya Mapato ya Zanzibar mapema mwezi
Disemba 2015. Kuanzia mwezi Februari, 2016 Mamlaka imeanza kazi ya kupanga
na kutoa bei elekezi kwa bidhaa zote za mafuta hapa nchini ambapo zoezi
hili linafanyika kila mwezi.
Kujenga uelewa juu ya majukumu na kazi za
Mamlaka kwa wadau na Jamii kwa jumla.
- Mheshimiwa Spika, Kwa vile Mamlaka hii ni mpya,
ni wazi kuwa wananchi wanahitaji kuijua na kuielewa Mamlaka vizuri, hivyo
Mamlaka imekuwa ikifanya mikutano na Makampuni yanayoleta mafuta Zanzibar
(Oil Marketing Companies), wamiliki wa vituo vya mafuta na wataalamu
kutoka katika taasisi mbali mbali za Serikali na zisizo za Serikali kwa
lengo la kuwaelimisha kuhusu Majukumu na Kanuni zinazosimamiwa na ZURA.
Jumla ya semina Nne (4) zimefanyika kwa Unguja na Pemba. Vile vile Mamlaka
imeanza kutoa vipindi vya kuelimisha jamii kwa njia ya televisheni.
Ushirikiano
na Taasisi za Kikanda zinazohusiana na udhibiti wa huduma za Maji na Nishati
- Mheshimiwa Spika, katika utekelezaji wa suala
hili, Mamlaka imekuwa ikishirikiana kwa karibu na Taasisi za Tanzania Bara
kama vile Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), Taasisi
inayosimamia uhifadhi wa Mafuta (TIPER), Wakala wa uagizaji wa Mafuta ya
jumla Tanzania (PBPA), Kampuni ianayoweka alama katika mafuta (GFI) nk.
Vile vile Mamlaka imejenga uhusiano mzuri na Taasisi inayohifadhi mafuta
ya Mombasa Kenya (Kipevu Oil Jet).
- Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016,
Katika kutekeleza program ya Usimamizi wa Huduma za Nishati na Maji jumla
ya Tsh 31,565,198,587/= ziliidhinishwa kutumika. Hadi kufikia
Machi, 2016, fedha zilizoingizwa ni Tsh 6,030,458,943 /= sawa na
asilimia 19% ya makadirio.
PROGRAMU
KUU: USIMAMIZI WA MAZINGIRA/MABADILIKO YA TABIANCHI
- Mheshimiwa
Spika; Itakumbukwa
kwamba kufuatia uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 20 Machi, 2016 Serikali
ya Mapinduzi Zanzibar imefanya mabadiliko ya miundo ya Mawizara zake
iliyopelekea kuundwa kwa Wizara ya Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira, hivyo programu hii ya
usimamizi wa Mazingira/mabadiliko ya tabianchi hapo awali ilikua chini ya
usimamizi wa Afisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais na hivi sasa inasimamiwa na
Wizara ya Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira.
- Mheshimiwa
Spika, Kama
tunavyofahamu kwamba suala la mazingira linachukua nafasi kubwa na ya
pekee wakati wa kujadili suala la Mabadiliko ya Tabianchi. Kwa mantiki
hiyo ni kweli kwamba suala la mazingira linapaswa kupewa kipaumbele wakati
wa kujadili dhana nzima ya Mabadiliko ya Tabianchi huku tukilenga
kuyafikia maendeleo endelevu ya kiuchumi.kiteknolojia na kijamii bila ya
kuathiri mazingira yaliyotuzunguka katika maisha yetu ya kila siku.
- Mheshimiwa
Spika, Idara ya
Mazingira na Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira (ZEMA) kwa mwaka wa fedha 2015/2016
kupitia programu ndogo mbili ambazo ni Usimamizi wa Mazingira na Usimamizi
wa Mabadiliko ya tabianchi kwa pamoja zilipanga na kutekeleza majukumu
kama ifuatavyo:
Programu ndogo ya Usimamizi wa Mazingira
- Mheshimiwa Spika, Programu hii ndogo
inatekelezwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira na Idara ya Mazingira
ambapo kwa mwaka wa fedha 2015/2016 imefanikiwa kutekeleza mambo
yafuatayo:-
Kutayarisha Kanuni za Usimamizi wa Mazingira.
- Mheshimiwa
Spika, rasimu
za awali za mapitio ya Kanuni ya Tathmini ya Athari za Kimazingira ya
mwaka 2002 na Kanuni ya Marufuku ya Mifuko ya Plastiki ya mwaka 2011
zimetayarishwa kwa kuondosha mapungufu yaliyokuwepo na kuingiza hoja
muhimu za wadau.
Kuendesha Operesheni 84 za mifuko ya plastiki na pia 84 kwa
maliasili zisizorejesheka.
- Mheshimiwa Spika, jumla ya operesheni 16 za
mifuko ya plastiki zimefanyika kwa Unguja na Pemba ambapo zaidi ya kesi 17
zimefikishwa mahakama husika na kutolewa hukumu.
Kufanya ufuatiliaji wa kimazingira kwenye maeneo 84 yaliyoharibiwa
kimazingira.
- Mheshimiwa Spika, jumla ya maeneo 35
yenye uharibifu na uchafuzi wa mazingira yametembelewa na kutolewa
muongozo wa kimazingira na kisheria. Kati ya maeneo hayo 23 yapo
Unguja na 12 yapo Pemba. Kwa ufafanuzi zaidi angalia Kiambatanisho
E.
Kufanya shughuli za Ufuatiliaji, Tathmini na Ukaguzi wa
kimazingira kwa miradi ya Uwekezaji iliopo hapa nchini.
- Mheshimiwa Spika, jumla ya miradi 45
imefanyiwa ufuatiliaji na kutolewa muongozo wa kimazingira na kisheria.
Kati ya miradi hiyo 30 Unguja na 15 Pemba Miongozo hiyo ilikuwa inahusisha
usimamizi wa taka na maji machafu hasa kutoka kwenye mabwawa ya kuogelea.
Vilevile jumla ya miradi 25 imefanyiwa Tathmini za Kimazingira na
kupewa vyeti vya kimazingira. Aidha jumla ya miradi 18 imefanyiwa
ukaguzi wa kimazingira na kupewa vyeti vya ukaguzi huo. Kwa ufafanuzi
zaidi angalia Viambatanisho F na G.
Kuelimisha jamii juu ya Sheria ya Mazingira kupitia vipindi vya
Radio, TV na mikutano ya uhamasishaji.
- Mheshimiwa Spika, jumla ya vipindi 25 (18 Radio
na 7 TV) vya kuelimisha jamii juu ya usimamizi wa mazingira vimetayarishwa
na kurushwa kupitia ZBC Radio, ZBC TV, Coconut, Hits FM Chuchu FM. Aidha,
ZEMA na Idara ya Mazingira zilitembelea Wizara zote pamoja na Ofisi za Mikoa
kuonana na watendaji wakuu wa taasisi hizo pamoja na taasisi zilizo chini
ya Wizara hizo kwa lengo la kuelimisha wadau juu ya Sheria ya Mazingira ya
mwaka 2015.
- Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016,
Katika kutekeleza programu zake, Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira na
Idara ya Mazingira ziliidhinishiwa kutumia Tsh 255,000,000/=. Hadi
kufikia Machi, 2016 taasisi hizi zilikwisha ingiziwa Tsh 38,375,000/= sawa
na asilimia 15%.
Programu
ndogo ya Mabadiliko ya Tabianchi
- Mheshimiwa Spika, Programu hii ndogo
inatekelezwa na Idara ya Mazingira, Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na
Uvuvi kupitia Idara ya Misitu na Maliasili zisizorejesheka, Wizara Fedha
na Mipango kupitia Idara ya Fedha za Nje, Wizara ya Ardhi, Maji, Nishati
na Mazingira kupitia Idara ya Nishati na Madini na Jumuiya ya Maendeleo ya
Jamii na Uhifadhi wa Mazingira Zanzibar (Community Development and
Environmental Conservation in Zanzibar - CODECOZ).
- Mheshimiwa Spika, Mpango kazi wa utekelezaji wa
Mkakati wa Mabadiliko ya Tabianchi umetayarishwa kutokana na vipaumbele
vilivyoainishwa kwenye Mkakati wa Mabadiliko ya Tabianchi wa Zanzibar wa
mwaka 2014. Mpango kazi huo unategemewa kuzinduliwa rasmi mwezi wa Juni,
2016 kwa ajili ya utekelezaji.
- Mheshimiwa Spika, Mpango wa Kijamii wa Kuhimili
Athari za Mabadiliko ya Tabianchi (Local Adaptation Plan of Action - LAPA)
kwa Wilaya 3 (Micheweni, Kaskazini “A” na Kusini Unguja) umetayarishwa.
Mpango huu unakusudiwa kutumika katika kuhamasisha nyezo za utekelezaji za
Mpango huo na hatimae kutayarisha mipango ya Wilaya nyengine zilizobakia
hatua kwa hatua kutegemea na upatikaaji wa fedha. Aidha, katika suala la
kuendelezwa baadhi ya maeneo yaliyoathiriwa na mabadiliko ya tabianchi,
jumla ya hekta 100 za mikoko/mikandaa imepandwa kwenye maeneo 17 ya Unguja
(10) na Pemba (7) kwa ajili ya kuendeleza maeneo yaliyoharibiwa.
- Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016,
Katika kutekeleza programu ndogo ya Mabadiliko ya Tabianchi, jumla ya Tsh
450,000,000/= ziliidhinishwa kutumika. Hadi kufikia Machi, 2016, fedha
zilizoingizwa ni Tsh 459,345,000/= sawa na asilimia 102%.
MUELEKEO
KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017
- Mheshimiwa Spika, kwa heshima naomba
kuwasilisha muelekeo wa Bajeti yenye kuzingatia programu ya Wizara ya
Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
Wizara
ya Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira ina jumla ya Programu Kuu nne ambazo ni;
- Programu 1: Mipango, Sera na Utawala wa
Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira
- Programu 2: Usimamizi na Upangaji wa
Matumizi ya Ardhi
- Programu 5: Usimamizi wa Huduma za Maji na
Nishati
- Programu 6: Usimamizi wa Mazingira na
Mabadiliko ya Tabianchi.
- Mheshimiwa Spika, jumla ya Tsh Bilioni
57,456,186,000 zinatarajiwa kutumika katika utekelezaji wa Programu hizi
nne.
- Mheshimiwa Spika, Naomba sasa uniruhusu kutoa
maelezo kwa ufupi kuhusu Programu na Programu ndogo zinazohusiana na
Wizara yangu kama ifuatavyo.
PROGRAMU YA MIPANGO, SERA NA UTAWALA WA ARDHI, MAJI, NISHATI NA
MAZINGIRA
- Mheshimiwa Spika, programu hii inajukumu la
kuimarisha uratibu katika utekelezaji wa Kazi za Wizara ambapo matokeo ya
muda mrefu yanayotarajiwa ni Kukuza ufanisi katika utawala wa rasilimali
ardhi pamoja na utoaji huduma za kijamii. Programu itasimamiwa na Idara ya
Utumishi na Uendeshaji, Idara ya Mipango, Sera na Utafiti na Afisi Kuu
Pemba ambapo jumla ya Tsh. 2,342,446,000/= zinatarajiwa
kutumika kwa utekelezaji wake. Programu hii imegawanyika katika Programu
ndogondogo kama ifuatavyo:-
Mipango
na Sera za Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira/Mabadiliko ya Tabianchi
- Mheshimiwa Spika, dhumuni la Programu ndogo hii
ni Uratibu wa Shughuli na Kazi za Wizara kwa Ufanisi, ambapo matokeo ya
muda mfupi (output) yanayotarajiwa katika utekelezaji wa Programu hii ni
Kuratibu/Kuandaa Mipango na Miongozo ya Kisera ya Utekelezaji wa Kazi za
Wizara, Kuratibu, Kufuatilia na Kutathmini Utekelezaji wa Programu, Miradi
na shughuli za Wizara na Kuandaa Tafiti kwa ajili ya Kuendeleza ufanisi
katika utoaji wa huduma katika sekta za Wizara. Jumla ya Tsh
173,067,000/= zinatarajiwa kutumika.
Utawala na Maendeleo ya Rasilimali watu
- Mheshimiwa Spika, dhumuni la programu ndogo hii
ni kuhakikisha usimamizi thabiti na utawala wa rasilimali za Wizara,
ambapo matokeo ya muda mfupi (output) yanayotarajiwa katika utekelezaji wa
programu hii ni Kukuza Viwango vya Wafanyakazi na kuhifadhi kumbukumbu na
Taarifa za Wafanyakazi wa Wizara. Jumla ya Tsh 808,112,000/=
zinatarajiwa kutumika.
Uratibu wa Shughuli za Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira Pemba
- Mheshimiwa Spika, dhumuni la programu ndogo hii
ni Uratibu na Usimamizi Thabiti wa Kazi za Wizara kwa pemba, ambapo
matokeo ya muda mfupi (output) yanayotarajiwa katika utekelezaji wa
programu hii ni Kuratibu Shughuli za Mipango na Utawala pamoja na Kuratibu
na Kusimamia masuala ya Ardhi, Makaazi maji na Nishati Pemba. Jumla ya Tsh
1,361,267,000/= zinatarajiwa kutumika.
PROGRAMU
YA USIMAMIZI NA UPANGAJI WA MATUMIZI YA ARDHI
- Mheshimiwa Spika, programu hii inajukumu la
kuhakikisha kunakuwepo na usalama wa matumizi ya ardhi kwa maendeleo ya
nchi (security of land tenure). Matokeo ya muda mrefu yanayotarijiwa ni
kuwa na matumizi ya ardhi yaliyobora na fanisi. Programu hii inasimamiwa
na Kamisheni ya Ardhi na Mahakama ya Ardhi ambapo jumla ya Tsh. 2,275,072,000/=
zinatarajiwa kutumika.
- Mheshimiwa Spika, programu hii imegawanyika
katika Programu ndogo ndogo kama ifuatavyo:
Utawala
wa Ardhi
- Mheshimiwa Spika, Dhumuni la Programu ndogo hii
ni kuhakikisha Usalama wa Umiliki wa Ardhi kwa Wananchi ambapo matokeo ya
muda mfupi (output) yanayotarajiwa katika utekelezaji wa Programu hii ni
ugawaji na usimamiaji wa ardhi kwa matumizi mbali mbali, Uthamini wa ardhi
na Usimamiaji wa shughuli za Upimaji na Ramani, Usajili wa ardhi. Jumla ya
Tsh 1,065,460,000/= zinatarajiwa kutumika.
Upangaji
wa Miji na Matumizi ya Ardhi
- Mheshimiwa Spika, dhumuni la programu ndogo hii
ni Kuhakiksha Kunakuwepo Uwiano wa matumizi ya Ardhi kati ya Matumizi ya
Uchumi na Kijamii, ambapo matokeo ya muda mfupi (output) yanayotarajiwa
katika utekelezaji wa programu hii ni kuwepo kwa Mipango ya Matumizi Bora
ya Ardhi kwa Miji yote ya Zanzibar, Kusimamia Maendeleo ya Ardhi Mijini,
Mikoani na maeneo ya Fukwe, Kuimarika kwa Miji ili Kukuza Uchumi na Kuleta
Maisha Bora. Jumla ya Tsh 1,021,398,000/= zinatarajiwa
kutumika.
Utatuzi
wa Migogoro ya Ardhi
- Mheshimiwa Spika, Dhumuni la Programu ndogo hii
ni kuhakikisha kwamba kunakuwepo na utatuzi wa migogoro ya ardhi kwa
haraka zaidi kadri ya inavyojitokeza, ambapo matokeo ya muda mfupi
(output) yanayotarajiwa katika utekelezaji programu hii ndogo ni pamoja na
kupungua kwa migogoro ya Ardhi. Jumla ya Tsh 188,214,000/=
zinatarajiwa kutumika.
PROGRAMU
YA USIMAMIZI WA HUDUMA ZA MAJI NA NISHATI
- Mheshimiwa Spika, jukumu la programu hii
ni kuhakikisha kunakuwepo upatikanaji wa Huduma za Nishati na Maji
inayotosheleza mahitaji ya Watu. Matokeo ya muda mrefu yanayotarajiwa ni
upatikanaji wa huduma bora za Nishati, Umeme na Maji kwa wananchi.
- Mheshimiwa Spika, Programu hii itasimamiwa
na Idara ya Nishati na Madini, Mamlaka ya Kudhibiti Huduma za Maji na
Nishati, Shirika la Umeme na Mamlaka ya Maji ambapo jumla ya Tsh. 48,978,195,000/=
zinatarajiwa kutumika katika utekelezaji wake.
- Mheshimiwa Spika, matokeo ya muda mfupi (output)
yanayotarajiwa katika utekelezaji wa programu hii ni usimamizi wa
usambazaji wa mafuta nchini, usambazaji wa huduma za Umeme, uhifadhi wa
maeneo ya vianzio vya maji, upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama
kwa watumiaji mijini na vijijini.
PROGRAMU YA USIMAMIZI WA MAZINGIRA NA MABADILIKO YA TABIANCHI
- Mheshimiwa Spika, proramu hii itatekelezwa kupitia
programu ndogo ya Usimamizi wa Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi na
utekelezaji wake utaimarisha usimamizi wa mazingira na mabadiliko ya
tabianchi. Programu hii inasimamiwa na Idara ya Mazingira na Mamlaka ya
Usimamizi wa Mazingira.
- Mheshimiwa Spika, dhumuni la programu hii ni
kuhakikisha usimamizi thabiti wa masuala ya kimazingira , ambapo matokeo
ya muda mfupi (output) yanayotarajiwa katika utekelezaji wa programu hii
ni Kudhibiti athari za kimazingira kwa kuyaendeleza maeneo yaliyoathirika
na mabadiliko ya tabianchi, kuendeleza tathmini za kimazingira pamoja na
miongozo ya uimarishaji wake. Jumla ya Tsh 3,860,473,000/=
zinatarajiwa kutumika katika utekelezaji wa programu hii.
- Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Programu hii
ndogo ya Usimamizi wa Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi unajumuisha
Mamlaka ya Mazingira na Idara ya Mazingira na utatekelezwa kwa
mashirikiano na wadau mbalimbalikwa upande wa Mabadiliko ya Tabianchi.
HITIMISHO
- Mheshimiwa Spika, kwa heshima kubwa sana naomba
kuchukua nafasi hii kwa mara nyingine tena kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa
kunipa fursa ya kuwatumikia Wananchi wenzangu kupitia Wizara hii.
- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Wizara na
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, naomba kuchukua nafasi hii kutoa
shukurani zangu za dhati kwa Nchi marafiki, Mashirika ya Kimataifa na
yasiyo ya Kimataifa, Sekta binafsi, NGOs, CBOs na wananchi kwa jumla kwa
mashirikiano makubwa waliyoyaonesha kwa Wizara yangu kwa misaada yao ya
hali na mali waliyoitoa na wanayoendelea kutoa kwa Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar kupitia Wizara hii. Washirika hao ni JAPAN, NORWAY, SWEDEN,
CHINA, OMAN, FINLAND, UNICEF, UNESCO, UNDP, JICA, Sida, UN HABITAT, AfDB,
TASAF, NORAD, BENKI YA DUNIA, RAK GAS TANZANIA, EU, pamoja na wale wote
ambao kwa bahati mbaya hatukuweza kuwataja. Tumepata faraja kubwa sana kwa
michango yao kwa maendeleo ya nchi yetu, tunaahidi kuienzi na kuiendeleza
na kuithamini michango hiyo.
- Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hii
kumshukuru Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohammed Shein; kwa kuniamini na kunipa dhamana ya
kuiongoza Wizara hii pamoja na miongozo yake mbali mbali anayoendelea
kupatia ambayo inalengo la utendaji wetu katika kuimarisha sekta zetu
muhimu zenye kugusa maisha ya kila siku kwa wananchi wetu.
- . Mheshimiwa Spika, Shukurani za pekee kwako
Mheshimiwa Spika, Naibu Spika, Mheshimiwa Mwenyekiti wa Baraza, Wenyeviti
wa Kamati za Kudumu za Baraza na Waheshimiwa Wajumbe wote wa Baraza lako
kwa kunisikiliza kwa utulivu na umakini wa hali ya juu.
- . Mheshimiwa Spika,
shukurani maalumu nazitoa kwanza kwa Mwenzangu na Ndugu yangu Mheshimiwa
Naibu Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira Ndugu Juma Makungu Juma
kwa mashirikiano yake makubwa anayoendelea kunipa katika kuongoza Wizara
hii. Vile Vile shukurani kwa Katibu Mkuu Ndugu Ali Khalil Mirza, Katibu
Mtendaji Kamisheni ya Ardhi, Wakurugenzi, Mameneja, Afisa Mdhamini,
Wenyeviti wa Bodi, Mahakimu na Maafisa wa ngazi zote ambao walinipa
mashirikiano yao ya hali juu kwa wakati wote na kutuwezesha kutekeleza
malengo na majukumu yetu kwa ufanisi katika kipindi cha mwaka 2015/2016.
- . Mheshimiwa Spika, napenda
kuishukuru sana familia yangu, mama, baba na mwanangu kwa msaada wao
mkubwa ulioniwezesha kufanya kazi zangu vizuri katika kipindi hiki kigumu
kwangu kilichonikabili.
- . Mheshimiwa Spika, naomba waheshimiwa wajumbe wa Baraza lako Tukufu
wayapokee, wayajadili kwa kina, watushauri na kutuelekeza na hatimae
wayapitishe makadirio haya. Tunaimani kubwa kuwa michango ya waheshimiwa
wajumbe wa Baraza lako hili itatusaidia sana katika kutekeleza majukumu
yetu ya kazi vizuri zaidi katika kipindi kijacho cha mwaka wa fedha
2016/2017.
- . Mheshimiwa Spika, ili Wizara yangu iweze kutekeleza programu kuu na
programu ndogo nilizozieleza, naliomba Baraza lako Tukufu iidhinishe
matumizi ya jumla ya Tsh Bilioni 57,456,186,000/= na pia naomba
idhini ya kukusanya mapato ya Tsh Bilioni 6,100,000,000/= kutokana
na vianzio mbali mbali vilivyomo ndani ya Wizara yangu kwa Mwaka wa Fedha
2016/2017.
Kwa
ufafanuzi zaidi ninaomba muangalie kiambatanisho “H1, H2 na H3”
- . Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja
No comments:
Post a Comment