Habari za Punde

Zantel yatoa milioni 10 kwa Jumuiya ya Wakulima wa Mwani Zanzibar

  • Kuendesha mafunzo ya ujasiriamali na usimamizi wa fedha kwa wanawake 2000.
Katika jitihada za kukuza ujasiriamali pamoja na kuongeza uwezo wa wanawake katika kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za kijamii na kiuchumi, kampuni inayoongoza visiwani Zanzibar, Zantel, leo imetoa kiasi cha shillingi millioni 10 kwa Jumuiya ya Wakulima wa mwani Zanzibar

Kampuni ya Zantel pia itaandaa mafunzo ya ujasiriamali, 

utawala na usimamizi kwenye maswala ya fedha kwa zaidi 

ya wanawake 2000 yatakayoendeshwa katika kipindi cha 

mwaka 2016 na 2017.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano hayo, Afsa 

Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Zantel, Bwana Benoit Janin 

alisema msaada wa Zantel kwa Jumuiya ya Wakulima wa 

mwani Zanzibar unaendelea kuonyesha jitihada za kampuni 

ya Zantel katika kutekeleza ahadi zake kwa ajili ya ustawi 
wa jamii ya wanawake.

‘Wanawake wanakabiliwa na changamoto mbalimbali 

ikiwemo tatizo la upatikanaji wa rasilimali,maarifa na 

huduma, hivyo basi ili kukabiliana na changamoto hizi 

tunaamini msaada utabadilisha maisha ya wanawake wengi 

wanaotegemea mradi huu katika  kuendesha maisha’ 

alisema Bw.Janin.

Kilimo cha mwani ni shughuli muhimu ya kiuchumi 

inayotegemewa na wakazi wanaoishi katika miamba ya 

matumbawe ya visiwa vya Unguja na Pemba. Aina hii ya 

kilimo inafanywa zaidi na wanawake kwani kati ya wakulima 

23,654 asilimia 80% ni wanawake.

'Imani yetu kama Zantel ni kuwa uwezeshaji wa wanawake 

ni jambo muhimu na sahihi la kufanya, kwa sababu mwanamke ndiye nguzo ya jamii na hivyo tukitoa fursa za kiuchumi kwa wanawake tutaigusa jamii pana zaidi’ alisema Bi Rachel Samren, Mwenyekiti wa Bodi wa Zantel na Makamu wa Rais wa Mambo ya nje wa Millicom.

Akitoa shukurani zake za kwa kampuni ya Zantel, 

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wakulima wa mwani Zanzibar, Bi Pavu Mcha Khamis alisema msaada waliopewa na kampuni ya Zantel utasaidia kuhakikisha upatikanaji wa vifaa vya kilimo kama kamba kwa ajili ya kilimo cha mwani.

'Kwa kipindi kirefu tumekuwa tunakabiliwa na changamoto 

mbalimbali, hivyo tunaishukuru kampuni ya Zantel kwa 

kutusaidia kuongeza upatikanaji wa vifaa vya kilimo pamoja 

na fursa za masoko hivyo kuwaongezea wanachama wetu 

kipato’ alisema Bi Pavu Mcha Khamis.

Jumuiya ya Wakulima wa mwani Zanzibar ilianzishwa 

mnamo mwaka 2010,kwa lengo la kuwaunganisha wakulima 

wote wa zao la mwani Zanzibar ili kuwawezesha kupata 

muongozo wa kukuza na kuendesha kilimo bora cha mwani 

kwa lengo la kuongeza uzalishaji na kupanua soko la zao 

hilo.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.