Mkuu wa mkoa wa Mjini magharibi Unguja, Mheshimiwa Ayoub Mohammed Mahmoud akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Bandari walipokuwa eneo la makontena
Mkuu wa mkoa wa Mjini magharibi Unguja, Mheshimiwa Ayoub Mohammed Mahmoud akikagua baadhi ya nyaraka za mizigo inayoingizwa bandarini
Mkuu wa mkoa wa Mjini magharibi Unguja, Mheshimiwa Ayoub Mohammed Mahmoud akiwa katika chumba cha kuscan mizigo pamoja na CCTV wakati alipokuwa akikagua Bandari ya Malindi
Mkuu wa mkoa wa Mjini magharibi Unguja, Mheshimiwa Ayoub Mohammed Mahmoud alipokuwa akizungumza na watendaji wa Shirika la Bandari baada ya kumaliza ziara yake ya ghafla bandarini hapo. Miongoni mwa mambo sugu mambo sugu aliyoyakuta hapo ni pamoja na ukwepaji kodi za serikali wa kiwango kikubwa,Udhaifu wa Ulinzi,mizigo kuingia,kutoka kiholela na utendaji kazi wa Mazoea.
Ameviagiza taasisi zote zinazosimamia huduma bandarini hapo kurekebisha dosari Hizo Mara Moja na pia kuimarisha ulinzi na usalama ikiwemo ukaguzi wa kina wa Mizigo yote iingiayo na kutoka kupitia bandari hiyo na pia ameagiza Mamlaka ya bandari kumaliza Mara moja Tatizo la ulanguzi wa ticket za boti.
Mkuu wa mkoa wa Mjini magharibi Unguja, Mheshimiwa Ayoub Mohammed Mahmoud akizungumza na mwakilishi wa madereva wa Teksi wanaofanya kazi Bandarini kusikiliza kero zao
No comments:
Post a Comment