Na Haji Nassor, Pemba
SEPTEMBA 2, mwaka huu rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Mhe: John Pombe Magufuli, alifika kisiwani Pemba na
kuzungumza na wananchi wa mikoa miwili ya kisiwani humo.
Lengo
hasa la mkutano huo uliofurika mamia ya wananchi, ilikuwa ni kuwashukuru kwa
kumuingiza Ikulu ya Tanzania, baada kinyang’anyiro kizito mbele ya wagombea
wenzake kutoka vyama vyengine.
Magufuli
anakumbuka vyema Oktoba 15 alipofika kwenye uwanja huo wa Gombani ya kale,
kuwaomba kura wananchi wa kisiwa cha Pemba, ingawa pia aliahidi kurudi kuja
kuwashukuru.
Naam,
ahadi yake hiyo ya kuja kuwapa neno la ahasante, shukuran, ‘thanks’ au kama
wanavyosema wachina ‘xie xie’ ilitimia Septemba 2, akijua kuwa muungwana ni
vitendo na sio maneno.
Kama
hivyo ndivyo, lazima kwa viongozi wengine wakumbuke kuwa vile viwanja
walivyovitumia usiku na mchana kuomba kura, sasa vigeuke kuwa viwanja vya
kuwapa neno la shukuran wananachi.
Viongozi
wetu wa majimbo, hatukumbuki pale tulipokuwa tukivivamia viwanja kwa saa na
dakika kadhaa, kwa kuwaomba kura wananchi, sasa kama twakumbuka tuje tena
kuwashukuru kwa kutimiza ahadi zao.
Mbona ilikuwa tunakutana Polisi kila mmoja akimueleza mgombea mwenzake kuwa yeye aliomba mwanzo uwanja fulani kwa ajili ya mkutano wa kuombea kura, sasa vipi tumesahau kwamba hatujawapa shukuran.
Wakati
huo wa kusaka Jimbo, ilikua hata waandishi wa habari nao hawakunywa maji,
kulikoni kuna mgombea anataka kuzungumza na wananchi tena wakati mwengine, hata
kiwanja kisicho na hadhi, mgombea huyoo wamkuta, sasa je wako wapi?
Jawabu
wapo majimboni, niwaulize? Je mmesahu sasa kuwaska tena waandishi wa habari na
vipaza sauti vyao, kufanya mikutano kama ile, kwa ajili ya kuwashukuru
wananchi?.
Waandishi
wala hawana haja ya kuwakusanywa kwa kuwapa neno la ahasante, lakini hawa
wapiga kura wetu, mbona sasa hatuoni shamra shamra za mikutano ya shukuran?
Wapo
wagombea ukiwauliza walifanya mikutano ya hadhara pengine nane, sita au zaidi
kwa ajili ya kusaka kura, sembuse ile mikutano ya ndani katika nyumba na
vijiwe, leo wamesahau kupita humo humo kutoa shukuran, he maajabu haya.
Naamini
hawajasahau kuwapa neneo la shukuran wapiga kura na wananchi wengine, pengine
wametingwa na kazi za kiinchi, si unajua wengine mawaziri na wengine manaibu,
lakini msijejisahau.
Maana
kuna baraka kubwa na zenye thawabu ndani yake, iwapo mtu atampa shukuran
mwenzake kwa kumfanyia wema, lakini sijui kinyume chake nini kwa kukosa kutoa
shukuran.
Yeye
rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe: John Pombe Magufuli, na hata
mwenzake wa Zanzibar, walishatimiza ahadi hiyo, maana septemba 2 alikuwa Pemba
na kisha siku ya pili mapema Unguja kwa kutoa shukuran.
Sisi
madiwani, wawakilishi na wabunge tumeshatoa shukuran kwa waliotuvisha suti,
makoti na mitandio ya bei, kama bado wakati ndio huu.
Nanyi
wananchi msisite kuwakumbusha viongozi wetu wote, kwamba walau kama walituwekea
mikutanio kumi ya kuomba kura, sasa watuwekee japo mitano ya kutushukuru, maana
hakuna kuna leo na kesho.
Lakini
nayi makatibu na wenyeviti wa vyama, lazima muwakumbushe viongozi wetu hawa,
kwamba wapite kurejesha fadhila kwa wananchi, maana miaka mitano mengine haiko
mbali hata kidogo.
Mimi
naamini kila jambo linawezekana, iwapo kila mmoja atafanya kazi zake kwa
kufuata sheria na kanuni, na rushwa kwake ikiwa ni mwiko.
No comments:
Post a Comment