Na Rajab Mkasaba
MKE wa Rais wa Zanzibar,
Mama Mwanamwema Shein ametoa pongezi kwa wanawake wote wa Unguja na Pemba kwa kujitokeza
kwa wingi kwenda kutumia haki yao ya msingi na ya kikatiba ya kupiga kura
katika uchaguzi uliopita, licha ya baadhi yao kukumbana na vitisho mbali mbali
mitaaani na hata katika familia zao.
Mama Mwanamwema Shein
alitoa pongezi hizo huko katika ukumbi wa Chuo cha Mafunzo ya Amali Vitongoji,
Chake Chake Pemba katika mkutano maalum kati yake na Wanachama na Viongozi wa
Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT).
Katika hotuba yake
Mama Shein, aliwapongeza akina mama hao kwa kusimama kidete katika kuitumia haki
yao hiyo bila ya woga na kusisitiza kuwa ujasiri wao ni wa kupigiwa mfano.
Alisema kuwa kazi
iloyopo mbele yao hivi sasa ni kuendeleza shughuli za ujenzi wa wa nchi kwa kushirikiana na UWT na kuhakikisha kwamba
wanawake hawaachwi nyuma.
Mama Shein alitumia
fursa hiyo kuwakumbusha wanawake na wananchi wote kwa ujumla kuongeza bidii
katika kuunga mkono juhudi za Serikali zenye lengo la kuwawezesha wananchi
kiuchumi, ili waweze kujiajiri wenyewe.
Alieleza kufarajika
kwake kwa kuwepo mwamko mkubwa wa kuanzisha vikundi vya Ushirika, SACCOS na
kuongeza nguvu katika kilimo hasa cha mboga mboga.
Katika mkutano huo
Mama Shein aliwakabidhi kadi wanachama wapya 30 wa Jumuiya ya UWT wa katika
Wilaya hiyo ya Mkoani.
Nae Mama Asha Balozi,
Mke wa Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar, aliwapongeza akina mama hao kwa
juhudi walizozichukua katika kuhakikisha chama chao cha CCM kinaendelea
kuongoza huku akiwasisitiza wanajumuiya hao kuwa kitu kimoja na kuondokana na
ubinafsi.
Mapema Mama Fatma
Karume, Mjane wa Marehemu Mzee Abeid Amani Karume aliwataka akina mama wasirudi
nyuma na badala yake wawe kitu kimoja na
washirikiane kama akina mama wenzao walivyoshiriki katika harakati za kudai
uhuru wa Zanzibar.
Nae Kaimu Katibu Mkuu,
alitumia fursa hiyo kuwahamasisha akina mama hao kuchukua fomu za kugombea
nafasi mbali mbali za uongozi katika Jumuiya hiyo katika uchaguzi ujao wa chama
na kuwaeleza kuwa wanachama wote wa chama hicho sifa za kuongoza.
Akiwahutubia viongozi na wanachama wa Jumuiya ya UWT,
Wilaya ya Wete, Mama Shein aliwaomba mashehe, walimu,
wanasiaasa na wale wote wenye nafasi za uongozi katika Taasisi na Jumuiya mbali
mbali wasimame kidete na kukemea vitendo vya udhalilishaji.
Alisema kuwa vitendo
vya udhalilishaji wa kijinsia na ukatili dhidi ya wanawake na watoto bado
vinaendelea kuriopotiwa katika Mkoa huo wa Kaskazini Pemba pamoja na Mikoa yote
ya Zanzibar.
Mama Shein alisisitiza
kuwa vita dhidi ya vitendo hivyo havitoweza kufanikiwa iwapo hawatochukua
nafasi yao katikajamii kwa kuelimishana na kuwaelimisha watoto juu ya madhara
ya udhalilishaji kwa kila mmoja kwa nafasi aliyonayo atakeleze wajibu wake.
Nao Viongozi wa UWT,
Wilaya ya Wete walimpongeza Mama Shein kwa utaratibu aliouchukua wa kwenda
kuwashukuru na kuwapongeza akina mama hao kwa kushiriki vyema katika uchaguzi
mkuu uliopita ambao umeendelea kuiweka CCM madarakani.
Viongozi hao
walitunmia fursa hiyo kueleza baadhi ya changamoto walizokumbana nazo ikiwa ni
pamoja na kususiwa kuuziwa bidhaa, misiba, harusi pamoja na kusisiwa katika masuala
mengine ya kijamii.
Walimpongeza Dk. Shein kwa
hatua anazozichukua za kusimamia mafisadi pamoja na jinsi anavyotekeleza Ilani
ya Uchaguzi ya CCM huku wakieleza kuwa umoja wao ndio ngao kubwa iliyosababisha
kupatikana kwa ushindi mkubwa wa uchaguzi uliopita katika Majimbo ya Wilaya na
Mkoa huo.
Nae Waziri wa Kazi,
Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Maudline Castico aliwaeleza akina
mama hao juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya uongozi wa Dk.
Shein katika kupambana na vitendo vya unyanyasaji, jinsi inavyowasaidia wazee,
vijana, pamoja na wanawake na watoto.
No comments:
Post a Comment