Habari za Punde

Miundo mbinu bado ni tatizo Pemba

Na Salmin Juma - PEMBA

Ubovu wa miundo mbinu rafiki kwa ajili ya wawekezaji  bado ni tatizo ambalo zinarudisha nyuma sekta ya uwekezaji kisiwani pemba .

Mkurugenzi mkaazi wa mamlaka ya uwekezaji zanzibar ( ZIPA) Fadhila Hassan Abdalla amesema mamlaka imekuwa ikijitahidi kuboresha huduma hizo lakini bado hawajafanikiwa akutokana na ubovu wa miundo mbinu .

Kauli hiyo ameitoa jana wakati akitoa taarifa kwa wajumbe wa kamati ya fedha , biashara na kilimo ya baraza la wawakilishi walipofanya ziara ya kuyatembelea maeneo huru ya uwekezaji yaliyoko maziwangombe wilaya ya micheweni mkoa  wa kaskazini pemba .

Amesema  kwamba kwa maeneo ya kiuchumi kisiwani pemba hayajaweza kufanya hivyo licha ya kwamba yametangazwa kwa muda mrefu .

Naye mwenyekiti wa kamati hiyo Yusssuf Hassan Idd ameishauri serikali kuimarisha huduma ya miundo mbinu katika maeneo huru yaliyotengwa kwa ajili ya uwezekezaji ili kusaidia pia kupatikana ajira kwa vijana.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.