Habari za Punde

Azam yatwaa kombe la Mapinduzi Cup yaifunga Simba 1-0 katika mchezo wa Fainali usiku huu

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein akimkabidhi kombe la Mapinduzi nahodha wa Timy ya Azam John Bocco 'Adebayor' baada ya kuwafunga timu ya Simba goli 1-0 katika mchezo wa fainali uliofanyika hivi usiku uwanja wa Amaan Zanzibar 
 Wachezaji wa timu ya Azam wakinyanyua juu kombe la ubingwa wa michuano ya Mapinduzi Cup baada ya kuwafunga Simba 1-0 katika mchezo wa fainali uliofanyika hivi usiku uwanja wa Amaan Zanzibar  
 Wachezaji wa Timu ya Azam wakishangiria mbele ya mwari wao Kombe la Mapinduzi
 Wachezaji wa Timu ya Azam wakimtembeza mwari wao baada ya ushindi mwembamba wa goli 1-0 dhidi ya Simba 

Wapenzi wa Timu ya Azam wakiwapa hongera wachezaji wa timu hiyo baada ya ushindi na kutwaa ubingwa wa kombe la Mapinduzi 2017

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.