Habari za Punde

Jumuia ya Ustawishaji wa zao la karafuu na viungo Pemba ‘JUKAVIPE’ laandaa mkutano kwa mabaraza ya vijana Mkoani

 MKURUGENZI wa Jumuia ya Ustawishaji wa zao la karafuu na viungo Pemba ‘JUKAVIPE’ Hassan Ali Bakar, akifungua mkutano ulioandaliwa na jumuia hiyo, kwa mabaraza ya vijana ya wilaya ya Mkoani, juu ya kuelewa namna ya migogoro inavyoweza kujitokeza ndani ya jamii, mkutano huo umefanyika skuli ya Maendeleo ya Ngwachani, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 MTOA mada Ali Yussuf Ali akiwasilisha mada juu ya dhana ya migogoro ndani ya jamii, kwenye mkutano uliowashirikisha mabaraza ya vijana ya wilaya ya Mkoani, mkutano huo, umefanyika skuli ya Maendeleo Ngwachani, uliotayarishwa na Jumuia ya wazalishaji na viungo Pemba, JUKAVIPE’ (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 WAJUMBE wa mabaraza ya vijana wa wilaya ya Mkoani Pemba, wakisikiliza mada dhana ya migogoro iliowasilishwa kwenye mkutano, uliotayarishwa na ‘JUKAVIPE’ ili kuyajengea uwezo mabaraza hayo, mkutano huo umefanyika skuli ya Mendeleo ya Ngwachani, (Picha na Haji Nassor, Pemba).


 WAJUMBE wa mabaraza ya vijana wa wilaya ya Mkoani Pemba, wakishiriki katika kazi za vikundi, kwenye mkutano wa kuyajengea uwezo kwa mabara hayo, uliotayarishwa na ‘JUKAVIPE’ na kufanyika skuli ya Mendeleo ya Ngwachani, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

AFISA vijana wilaya ya Chakechake Sara Khamis Salim, akielezea athari za rushwa kwa vijana wanapotafuta kazi, kwenye mkutano wa kuyajengea uwezo mabaraza ya vijana ya wilaya ya Mkoani, mkutano huo umeandaliwa na JUKAVIPE na kufanyika skuli ya Maendeleo Ngwachani, (Picha na Haji Nassor, Pemba). 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.