Habari za Punde

Vijana watakiwa kuendelea kutambua thamani ya Mapinduzi


STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar                                       5.2.2017
---
RAIS wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein leo amewasisitiza vijana kuendelea kutambua thamani ya Mapinduzi na wajibu wa kuyatetea na kuyalinda kwa kutambua kuwa ndio mkobozi wa taifa letu na  ndio chachu ya maendeleo yanayoendelea kupatikana hivi sasa

Akitoa neno la shukran mara baada ya chakula  alichowaandalia vijana  walioshiriki katika halaiki kwenye sherehe za maadhimisho Ya miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika hafla iliyofanyika huko katika viwanja vya vya Makao Makuu ya KVZ kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Haji  Ussi Gavu  alisema ni vyema kwa vijana kuendelea kuwa na mbegu za kizalendo ili kuendelea kunawirisha dhama ya Mapinduzi kwa miaka mingi zaidi ijayo

Alisema ushiriki wa vijana hao  uliojaa furaha  katika sherehe hizo umeendelea kumpa moyo na matumaini makubwa Dk. Shein na hivyo anaamini kuwa kutaendelea ya kujenga hamasa kwa kushiriki kwa wingi zaidi katika sherehe zijazo zinapofikia za kusherehekea Mapinduzi ya Zanzibar kwa miaka ijayo.

Hata hivyo Dk. Shein alitoa  pongezi maalum kwa vijana hao wa halaiki na makundi mengine yaliyoweza kushiriki vyema  na kufanikisha sherehe hizo ambazo zilikuwa kubwa na za aina yake.

Mapema Katibu wa uhamasishaji wa Halaiki Ali Mohamed Baraka SHASHA amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed kwa kuendeleza utaratibu wa kuyakutanisha makundi mbali mbali kwa ajili ya kupongezana kutokana na kazi nzuri zinazofanyika katika sherehe hizo.

Sherehe hizo pia zilihudhuriwa  na viongozi mbali mbali akiwemo Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid, Katibu Mkuu Kiongozi Abdulhamid Yahya Mzee, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Haji Omar Kheir, na viongozi wengine wa serikali.

Mwandishi Yunus Sose. Idara ya Mawasiliano (Ikulu)


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.