BODI
YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

WANAFUNZI
2,348 WASHINDA KATIKA RUFAA ZAO ZA MIKOPO YA ELIMU YA JUU
1.0
UTANGULIZI
Taratibu za upangaji na utoaji mikopo ya
wanafunzi wa elimu ya juu,zinatoa fursa kwa waombaji ambao ama hawakupata
mikopo au wamepata kiwango cha mikopo wanachoona hakikidhi mahitaji, kukata
rufaa. Kwa mujibu wa taratibu zilizopo,
waombaji hupewa siku tisini (90) kuanzia mwanzo wa mwaka wa masomo kuwasilisha
rufaa zao. Rufaa hizo huwasilishwa kwa njia
ya mtandao na vielelezo/viambatisho huwasilishwa kupitia madawati maalum ya
mikopo vyuoni. Katika mwaka wa masomo
2016/17, zoezi la kupokea rufaa lilianza rasmi tarehe 1 Novemba, 2016 na
kuhitimishwa tarehe 31 Januari, 2017.
2.0
MATOKEO
YA RUFAA
Katika kipindi cha kati ya tarehe 1 Novemba,
2016 na 31 Januari, 2017 jumla ya rufaa 20,020
ziliwasilishwa kwa njia ya mtandao. Kati ya hizo, jumla ya fomu za rufaa 17,020 zilipokelewa kutoka vyuoni
zikiwa na viambatisho muhimu. Mapitio ya
rufaa zilizowasilishwa yalifanywa kwa fomu zote zilizopokelewa na matokeo ya
rufaa hizo (zilizoshinda) kwa makundi ni kama ifuatavyo: Walemavu 61; Yatima 57; Wenye mzazi mmoja 570;
Familia zenye kipato duni 1,169 na
Waliosomeshwa na wahisani 491.
3.0
HITIMISHO
Bodi ya Mikopo tayari imetuma vyuoni majina
ya wanafunzi walioshinda rufaa zao na inaendelea kukamilisha malipo ya mikopo
yao. Aidha, Bodi inapenda kuwataarifu waombaji na umma kwa ujumla kuwa zoezi
hili limefungwa rasmi hadi hapo litakapotangazwa tena katika mwaka ujao wa
masomo.
Imetolewa
na:
MKURUGENZI
MTENDAJI
BODI
YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
28
Februari, 2017.
No comments:
Post a Comment