Habari za Punde

Chama cha Mpira wa Kikapu Zanzibar (BAZA) Taifa Kufanya Uchaguzi July 9, Wilaya ya July 1 na July 4.

Na: Abubakar Khatib Kisandu, Zanzibar.
Chama cha Mpira wa Kikapu Zanzibar (BAZA) kinatarajia kufanya Uchaguzi wake ambao umepangwa kufanyika July 9, 2017.

Katibu wa kamati ya Uchaguzi Kibabu Haji ametaja ratiba yote ya uchaguzi ambapo Uchaguzi huo unaanzia Wilayani na July 9 ukifanyika wa Taifa.

Ratiba ya uchaguzi wa BAZA ngazi ya Taifa na wilaya kama ifuatavyo:-
Kuanzia tarehe 14.6.2017 lilianza zoezi la Uchukuaji wa fomu ambapo tarehe 23.6.2017 ni siku ya mwisho ya urejeshaji wa fomu kwa wagombea wakati wa saa za kazi.

Tarehe 24.6.2017 ni usaili wa wagombea baada ya kuthibitishwa kuwa mgombea anaruhusiwa kuanza kampeni na pingamizi kwa mgombea.

Tarehe 01.7.2017 uchaguzi Wilaya Mjini  ambapo tarehe 04.7.207 ni uchaguzi Wilaya Chake .

Tarehe 09.7.2017 uchaguzi BAZA Taifa utafanyika Unguja.
Bei ya fomu kugombea nafasi za uongozi wilaya ni tsh 15,000/= na ngazi ya taifa tsh 40,000/=

NAFASI ZINAZOGOMBANIWA WILAYA NI:-
MWENYEKITI
MAKAMO MWENYEKITI
KATIBU
MSHIKA FEDHA
MSAIDIZI MSHIKA FEDHA

BAZA TAIFA
MWENYEKITI
MAKAMO MWENYEKITI-PBA
KATIBU MKUU
MSAIDIZI KATIBU-PBA
MSHIKA FEDHA
MSAIDIZI MSHIKA FEDHA-PBA

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.