Habari za Punde

Jang'ombe Boys yaaga mashindano ya Sportpesa Super cup yafungwa 2-0 na Gor Mahia ya Kenya

 Mshambuliaji wa Jang'ombe Boys, Juma Hafidh, akijaribu kumtoka beki wa Gor Mahia,Kagere Medie, wakati wa mchezo wa mashindano ya SportPesa Super Cup, yanayoendelea kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo uliomalizika hivi punde, Gor Mahia wameshinda mabao 2-0 yaliyofungwa na Medie Kagere katika dakika ya 63 na 84. Picha kwa hisani ya Montage Ltd.
 Kiungo wa Jang'ombe Boys, Abdi Kassim, akimiliki mpira mbele ya beki wa Gor Mahia, wakati wa 
mchezo wa mashindano ya SportPesa Super Cup, yanayoendelea kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. 
 Kipa wa Gor Mahia, Shakava Haron, akiruka kudaka mpira wa hatari langoni kwake, wakati wa mchezo wa mashindano ya SportPesa Super Cup, yanayoendelea kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. 
 Mchezaji wa Jang'ombe Boys, Abdallah Rashid, akimtoka Wafula Innocent, wakati wa mchezo wa 
mashindano ya SportPesa Super Cup, yanayoendelea kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
 Abdi Kassim akitawala dimba......
 Kikosi cha Gor Mahia
 Kikosi cha Jang'ombe......
 Makame Khamis wa Jang'mbe, akiruka kumiliki mpira....
 Mshambuliaji wa Jang'ombe Boys, Juma Hafidh, akijaribu kukatika katikati ya msitu wa wachezaji wa Gor Mahia.
Wachezaji wa Nakuru wakiwa jukwaani kabla ya mchezo wao.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.