Habari za Punde

Operation ya kwanza ya kisasa ya kutibu mifupa yafanywa Hospitali ya Abdulla Mzee Pemba, vifaa kwa Afrika vipo hapo pekee.

Na.Haji Nassor. Pemba.

MTOTO Mussa Khamis Abdalla (14) mkaazi wa Michezani wilaya ya Mkoani Pemba, amekuwa mtu wa kwanza kufanyia upasuaji mdogo na matibabu ya kuvinjika mguu bure, kupitia vifaa vya kisasa kutoka China, vilivyopo hospitali ya Mkoa ya Abdalla Mzee Mkoani.

Mtoto huyo alifikishwa hospitalini hapo, akiwa amevunjika mfupa wa mguu wa kushoto, baada ya kupata ajali akiwa kwenye shughuli zake za kawaida, na kupokelewa kisha kuanza kuandaliwa taratibu za matibabu kwa kutumia vifaa vya kisasa.

Vifaa hivyo ambavyo kwa Afrika Mashariki vipo kwenye hospitali hiyo pekee, kama sio kuwepo familia ya mtoto huyo ingelazimika kuvifuata India na kutumia zaidi ya shilingi milioni 15.

Daktari mkuu kutoka China wa kitengo cha Mifupa kwenye Hospitali ya Mkoa wa Abdalla Mzee Mkoani, dk Yang Xiao, alisema matibabu hayo yamechukua muda wa dakika 55 hadi kumalizika.

Alisema mfupa huo wa mguu wa kushoto, umepasuka na kama sio kuwepo kwa vifaa hivyo vya kisasa, engelazimika kufanyiwa upasuaji mkubwa wa kuondoa nyama za mguu, na kisha mfupa na kuanza kuutibu.

Dk Yang, alieleza kuwa utabibu huo wa zamani kwa sasa haupo tena kwenye hospitali hiyo, hasa baada ya serikali ya watu wa China, kukabidhi vifaa hivyo vya kisasa mwezi uliopita, mbapo kwa Afrika Mashariki, vipo hospitalini hapo pekee.

“Vifaa hivi vya kisasa ndio vya kwanza kwa Afrika Mashariki, na hapa matibabu yake ni bure, lakini India vipo na matibabu pamoja na usafiri wa mtu mmoja ni shilingi milioni 15”,alifafanua.

Hata hivyo alisema operesheni hiyo ambayo aliongoza yeye, alikuwa karibu sana na madaktari wazalendo, ambapo lengo la baadae ni kuhakikisha wanaweza kuvitumia mara watakapoondoka.

Aliongeza kuwa, mashine hiyo hata ikikaa zaidi ya mwaka kama haijapata mtu alievunjika, haiathiriki ingawa alisema uzoefu unaonyesha kila ifikapo msimu wa uvunaji wa zao la karafuu, waathirika huwa wengi.

Akizungumza na mwandishi w ahabari hizi motto huyo, alisema anashangaa kuona siku moja kabla baada ya matibabu anaweza kuunyanyua mguu wake.
“Leo (jana) niko adhali sana sina yale maumivu makali niliokuja nayo, maana kama nilietiwa mguu mpya, sihisi hasa kama nna athari ya ndani”,alisema.
Baba mzazi wa motto huyo Khamis Abdalla Haji, aliwapongeza madaktari hao kwa ujemedari wao mkubwa wa kuokoa mguu wa mtoto, ambapo hakutarajia kwamba ungezekena.

“Mimi nilijua mwanangu ameshapa ulemavu wa maisha, na wakati natoka nyumbani nilijua ni safari ya Muhimbili jinsi mguu ulivyokuwa, lakini nashukuru”,alisema.   

Daktari Makame Chirau anaefanyakazi kwenye kitengo cha mifupa hospitalini hapo, alisema matumizi ya vifaa hivyo vya kisasa, ni mazuri na yataepusha wanaovujika kwa kiaisi kikubwa kuwekewa piop ipo au vyuma.

“Zamani ilikuwa kila anaekuja amevunjika anawekewa vyuma ndani ya mwili au pio pio, lakini sasa baada ya kupata vifaa hivi, hali imekuwa ya kisasa zaidi”,alifafanua.

Mmoja kati ya wananchi waliozungumza na waandishi wa habari hizi, Haji Makame Hilali wa Mkoani, alisema hiyo ni hatua moja wapo kubwa ya kuimarisha huduma za afya kwenye hospitali hiyo ya Mkoa.

Nae Ashura Hija Yussuf, alisema hata baada ya kuondoka kwa madaktari hao kutoka China, vifaa hivyo ni vyema vikaendelea kutumika na kuondoa suala la fedha kidogo kabla ya huduma.

Vifaa hivyo vya kisasa ambavyo vinathamani ya shilingi milioni 60, vilitolewa mwezi uliopita na hospitali ya Wuxi no 2 ya watu wa China, ambapo vifaa hivyo kwa Afrika Mashiriki pekee, vipo hospitalini hapo.

1 comment:

  1. Tunapswa kumshukuru Allah kwa hatua hiyo. Ingawa bado najiuliza ikiwa vifaa hivyo vya kisasa kabisa gharama zake ni 60milioni, hivi kwa miaka yooooote hiyo Serikali yetu imeshindwa kabisa kupata fedha hizo ili kuwasaidia wanyonge sisi kupata huduma bora? Na hata kwa hospital nyengine za Zanzibar bado kama tuna nia njema khasa ya kuwasaidia wanyonge wa nchi hii million kama hizo tunao uwezo wa kuzipsta, la msingi kuwsjali wananchi

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.