Na Abdi
Shamnah
Wanachama wa
chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) wametakiwa kushirikiana na
serikali zilizoko madarakani, ili kufanikisha azma ya kuwaletea maendeleo ya
kiuchumi na kijamii wananchi.
Changamoto
hiyo imetolewa na mwanachama wa Chama hicho Mussa Jangwa Bohero katika hafla ya
kupokea na kukabidhi kadi mpya kwa wanachama 25 wa chama cha TADEA waliojiunga
na chama hicho, iliofanyika katika makao makuu ya ADC Bububu.
Miongoni mwa
waliokihama chama hicho, wapo viongozi watatu ambao walishiriki katika kugombea
nafasi za uongozi ngazi za tofauti, katika uchaguzi mkuu wa 2015.
Akizungmza katika hafla hiyo, mwanachama huyo
aliefika kwa madhumuni ya kushudia tukio hilo, alisema ni wajibu wa wanachama
wa chama hicho kushirikiana kikamilifu na serikali zilioko madarakani, kwa
kuelewa kuwa ndizo zenye jukumu la kuwahudumia wananchi na kuimarisha uchumi wa
Taifa.
Alisema
katika kufanikisha jambo hilo, wanachama wa ADC wana jukumu a kudumisha amani
na utulivu uliopo nchini pamoja na kujenga mshikamano na wanachama wa vyama
vyengine, ili kuleta ustawi wa Taifa.
‘‘ Tunapaswa
kuhirikiana na serikali zilizoko madarakani, hizi ndio zenye dhima ya kuongaza
Taifa hili hadi mwaka 2020, hivyo tuna wajibu wa kuzitii na kudumisha aman iliopo’’, alisema.
Nae Issa Ame
Issa, aliekuwa Katibu wa TADEA Mkoa wa Kusini Unguja, aliahidi kushirikiana an
wanachama wa chama hicho (ADC) katika kuendeleza harakati za kukiimarisha chama
hicho, ili kukiweka katika mazingira bora ya uchaguzi mkuu ujao .
Alisema yeye
pamoja na wanachama wengine 25, wameamuwa kwa hiari yao kujiunga na ADC baada
ya kuridhika na utendaji wake na kubaini kuwa ni chama chenye malengo ya kweli
na sera zinazotekelezeka.
Mapema Naibu Katibu Mkuu wa ADC Zanzibar,
Khamis Mohammed Kombo alipokea kadi 25
za wanachama hao kutoka TADEA, sambamba na kukabidhi kadi mpya za ADC.
Miongoni mwa
wanachama wapya wa ADC ambapo kabla walikuwa Viongozi wa TADEA na kugombea nafasi za
uongozi katika uchaguzi mkuu wa 2015 jimbo la Mtopepo ni pamoja na Hamad Rashid
Kombo(Ubunge), Amana (Uwakilishi) pamoja na Khadija nafasi ya Udiwani.
Katika siku
za hivi karibuni Chama cha TADEA kimekumbwa na jinamizi la kuondokewa na
viongozi pamoja na wanachama wake na kujiunga na ADC, ambapo Julai, 4 mwaka huu, kundi kubwa lilikihama chama hicho.
No comments:
Post a Comment