Habari za Punde

Mchezo wa Ng'ombe watia fora katika Tamasha la 22 la Mzanzibari kisiwani Pemba

 MCHEZAJI Ng'ombe maarufu Kisiwani Pemba, Mzee Azani Salim Suwedi kutoka Uwandani, mwenye flana ya mikono mirefu, akimpiga chenga Ng'ombe wakati wa mchezo wa ngombe, uliofanyika Pujini Wilaya ya Chake Chake ikiwa ni shamra shamra za Tamasha la 22 la Utamaduni wa Mzanzibari (PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.

WANANCHI mbali mbali Kisiwani Pemba, wamejitokeza kushuhudia mchezo wa Ng’ombe, ikiwa ni shamra shamra za Tamasha la 22 la Utamaduni wa Mzanzibari.

Mchezo huo uliofanyika katika kijiji cha Pujini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, huku ukihudhuriwa wananchi na Viongozi mbali mbali wa Serikali.

Mchezo huo ulianza saa kumi za Jioni na kumalizika saa 12 za jioni, huku ngombe watatu wakichezwa katika mchezo huo akiwemo Kiburungo kutoka Uwandani Vitongoji, Toba Roho yangu kutoka Pujini, Pua mbovu kutoka Vitongoji.

Akizungumza na wananchi mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Naibu Waziri Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Mmanga Mjengo Mjawiri, alisema ipo haja kwa wizara ya habari kurudisha utamaduni wa mchezo wa ng’ombe kama ulivyokuwa ukichezwa zamani.

Alisema mchezo wa Ng’ombe ni moja ya vivutio vikubwa vya kutangaza utalii wa Zanzibar, wareno wanautumia mchezo wa ngombe kwa kuitangaza nchi yao na ndio waanzilishi wa mchezo huo.

“mchezo huu ni mmoja kati ya michezo mashuhuri kwa Zanzibar, mchezo unapendwa na wananchi wengi hasa katika kisiwa cha Pemba, sasa ni wakati Serikali kuurudisha tena mchezo huu katika asili yake’alisema.

Alifahamisha ipo haja kwa michezo yote ya asili ya Zanzibar kurudishwa katika hadhi yake, ili vijana waweze kufahamu tamaduni zao.

Naibu Waziri huyo, alisema Serikali inapaswa kuwawezesha wananchi, kuimarisha mchezo huo wa ng’ombe ili vijana na waweze kufuata nyayo za mchezo huo.

Afisa mdhamini Wizara ya Habari Utalii, Utamaduni na Michezo Pemba, Khatib Juma Mjaja, alisema lengo la tamasha hilo ni kuzifanya shuhuli mbali mbali za Utamaduni na kuona zinapata nafasi kubwa.

Alisema tamasha hilo limeweza kuvuta hisia za wananchi wengi kuweza kujitokeza na kuangalia utamaduni wao ambao, vijana wameanza kuupa kisogo kwa kufuata tamaduni za kimagharibi

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.