Habari za Punde

Naibu Waziri Mhe Masauni Akagua Miradi ya Maendeleo ya Wizara Yake Mjini Babati Ahitimisha,Ziara Yake Mkoani Manyara.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wapili kulia) akionyeshwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Francis Massawe (kulia), jengo la Makao Makuu ya Jeshi la Polisi mkoani humo ambalo limekwama ujenzi wake, lililopo mjini Babati mkoani humo. Masauni amemaliza ziara yake ya siku mbili mkoani humo. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akimsikiliza Afisa Uhamiaji Mkoa wa Manyara, Naibu Kamishna, Juliette Sagamiko (kushoto) alipokua anatoa maelezo kuhusu Jengo la Makao Makuu ya Uhamiaji mkoani humo (linaloonekana nyuma ya viongozi hao), ambalo lipo katika hatua ya mwisho kukamilika lakini limekwama kuendelea na ujenzi wake. Katikati ni Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, Francis Massawe. Masauni amemaliza ziara yake ya siku mbili mkoani humo
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto), akipokea salamu ya heshima kutoka kwa Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Manyara. Watatu kulia ni Kamanda wa Jeshi hilo, mkoani humo, Heriel Kimaro.Masauni amemaliza ziara yake ya siku mbili mkoani humo kwa kutembelea ofisi mbalimbali zilizopo ndani ya Wizara yake
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akimsikiliza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Francis Massawe, wakati alipokua akitoa taarifa fupi ya utendaji wa Jeshi hilo,ofisini kwake mkoani humo. Masauni amemaliza ziara yake ya siku mbili mkoani humokwa kutembelea ofisi mbalimbali zilizopo ndani ya Wizara yake. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.