NA/ SAID ABDULRAHMAN ---- PEMBA
KATIKA kupambana na vitendo vya udhalilishaji,
Serikali imepiga marufuku uokotaji wa karafuu (mpeta) wakati wa zoezi la
uchumaji wa zao hilo litakapo anza rasmi Kisiwani Pemba.
Hii
itaondosha ile dhana ya ‘mali kwa mali’ ambapo katika kipindi kama hichi cha
msimu wa uchumaji wa zao hilo baadhi ya wananchi huitumia nafasi hiyo kufanya
vitendo visivyo na maadili.
Akizungumza
katika mkutano wa mapambano ya vitendo vya udhalilishaji na mapambano dhidi ya
ukimwi huko katika ukumbi wa mkutano katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini
Pemba,Ofisa tawala Mkoa huo, Ahmed Khalid Abdalla, alisema kwa
mwaka huu mikoa yote miwili imepeleka mapendekezo hayo Serikalini ili waokotaji
wasiruhusiwe.
Alisema
kuwa kwa mwaka huu mchumaji atalazimika kuokota karafuu zake mwenyewe au mtu
aliyemo katika familia hiyo ndie tu atayeweza kuachiliwa kuokota ili kuepusha
vitendo ambavyo vimekuwa vikitendeka.
‘Tayari
tumeshapitisha mapendekezo yetu sisi na wenzetu wa Mkoa wa Kusini na
tumeyapeleka Serikali kuu ili kuzuia mara moja wale wananchi wanaokota Karafuu kwa
msimu huu wasiruhusiwe kwani mara nyingi huwa kunajitokeza vitendo
viovu,”alisema Khalid.
Akiwasilisha
mada juu ya muongozo wa mwitiko wa jamii juu ya mapambano ya Ukumwi, Ofisa kutoka Tume
ya Ukimwi, Jokha Mohamed, alisema kuwa tume imeandaa muongozo mpya ambapo
umekamilika na lengo lake ni kusaidia kurahisisha utekelezaji wa mkakati wa
tatu (3) wa Ukimwi kwa wadau wanaofanya kazi katika ngazi ya jamii.
Alieleza kuwa mbali na hayo lakini pia
utaimarisha uwezo wa kamati na Uratibu,Halmashauri,Mabaraza ya miji, Wilaya na Shehia
katika kupanga,utekelezaji na kufuatilia na kutathmini muitiko wa jamii.
‘Lakini
pia utafanikisha upatikanaji wa taarifa za VVU na ukimwi katika ngazi ya
jamii,’alisema Jokha.
Hata
hivyo Ofisa huyo alieleza kwa sasa hatua mbazo zinahitajika kuchukuliwa kwa
haraka ni pamoja na kuharakisha uundaji wa kamati za uratibu katika ngazi zote
pamoja na kutoa mafunzo kwa kamati kuu ili nao wawafunze SHACCOM zao.
Kwa
upande wake Mkuu wa Wilaya ya Micheweni
Abeid Juma Ali, aliihakikishia kamati hiyo kuwa kwa upande wa Wilaya yake,
itachukua jitihada za makusudi ili kuhakikisha DACCOM na SHACCOM zinafufuliwa
na kufanya kazi zake.
“Niwahakikishie
kwa upande wa wilaya ya Micheweni kwa kushirikiana na viongozi wenzangu
tutazifufua daccom na shaccom zote kwani hapo awali tulikuwa hatuna bajeti hiyo ili kwa
sasa tunashukuru tumepata,”alisema Abeid.
Hivyo alisema kila mmoja anawajibu wakutekeleza majukumu juu ya mapambano ya VVU na Ukimwi bila ya kuoneana haya na mapambano ya udhalilishaji wa kijimsia ulioenea katika maeneo mbali mbali .
No comments:
Post a Comment