Habari za Punde

Waajiri sekrta binfasi wafikishwa mahakamni kisiwani Pemba

NA/ SAID ABDULRAHMAN PEMBA. 

 WAAJIRI wa sekta binafsi wapatao saba (7) wamefikishwa Mahakamani na mfuko wa hifadhi ya Jamii (Z.S.S.F) kutokana na makosa ya kutowasajili wafanyakazi wao katika mfuko huo pamoja na kutowalipia ada zao. 

 Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi huko Ofisini kwake Tibirinzi Chake Chake Pemba,Meneja wa Mfuko huo Tawi la Pemba, Rashid Mohamed Abdulla, alisema kwa mwaka 2016 – 2017 ni waajiri saba tu ndio waliyoweza kufikishwa katika vyombo vya sheria.

 Alieleza mfuko huo hauna nia ya kuwapeleka Waajiri Mahakamani ,bali kuna baadhi ya waajiri wanakwepa sheria ya kuzisajili taasisi zao pamoja na kuwasajili na kuwalipia wafanyazi wao waliowaajiri katika sekta zao.

 “Kuna baadhi ya waajiri ambao wanakwepa Sheria za kusajili taasisi zao hivyo kwa upande wetu tunatumia Sheria ya mwaka 2005, ambayo inatupa uwezo wa kuwapeleka Mahakamani ila tu kwa wale wakaidi ambao hawataki kufuata sheria lakini hatuna lengo la kufanya hivyo,”alieleza Meneja. Rashid, alifahamisha kwa sasa kesi ambazo zimeshafikia makubaliano ni kesi nne (4) ambapo tayari waajiri wa sekta hizo, wamekubali kuzisajili taasisi zao pamoja na wanyakazi wao na kuwalipia ada zao na kesi tatu (3) tu ndizo bado wanaendeleana nazo huko Mahakamani.

 “Kwa vile sisi mara nyingi huwa hatutaki kesi hivyo tunapofika kule mahakamani huwa tunajaribu kutafuta suluhu kwa upande wetu na kwa waajiri na anaekubali tu sisi tunaondosha shauri hilo Mahakamani,’alisema Meneja Rashid. 

 Meneja huyo, alisema kuwa endapo mwajiri huyo atakubali kulipia ada hizo hulazimika kulipa na faini japo kidogo kama ni adhabu yake. Hivyo alitoa wito kwa wenye taasisi binafsi kuzisajili taasisi zao pamoja na kuwalipia ada wafanyakazi wao na wasisubiri kusukumwa na kufikishana katika vyombo vya sheria kwani hilo sio zuri.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.