Na.Haji Nassor. Pemba.
KATIBU tawala wilaya ya Micheweni Pemba,
Hassan Abdalla Rashid, amesema lazima viongozi wa vyama vya wafanyakazi nchini,
wawe makini kufuatilia na kulilia haki za wafanyakazi, badala ya kuvifanya
vyama hivyo kama mtaji wa kujipatia fedha kwa maslahi yao binafsi.
Alisema,
vyama hivyo havikuanzishwa kwa ajili ya wachache kwenda kwenye mikutano,
makongamano na semina kujipatia fedha, bali ni kujenga misingi imara na endelevu
katika kuwatetea wanachama wao.
Katibu
tawala huyo, alieleza hayo alipokuwa akifungua mafunzo ya siku mbili ya haki za
binadamu, kwa wanachama wa vyama vya wafanyakazi, yalioandaliwa na kufanyika
Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba.
Alieleza
kuwa, wanfanyakazi hasa kwenye sekta binafsi, wamekuwa wakikoseshwa haki zao na
wakati mwengine kufanya kazi zao bila ya kuagalia usalama wao, hivyo ni nafasi
kwa viongozi hao kuyafuatilia hayo.
“Mimi
naamini vyama vya wafanyakazi kama vikiwa makini kweli kweli na kufanya kazi
zao kwa kuangalia misingi ya haki na sheria zinavyotaka, basi vitawasaidia sana
wanachama wao”,alieleza.
Katika hatua
nyengine, Katibu tawala huyo wa Wilaya ya Micheweni amewakumbusha washiriki wa
mafunzo hayo, kuifanyia kazi elimu watakayopewa, ili wapunguze manung’uniko
miongoni mwao.
Mapema
Mratibu wa mafunzo hayo Siti Habib Mohamed, alisema ZLSC, iliamua kuwapatia
mafunzo hayo wanachama wa vyama vya wafanyakazi, ili kuwajengea uwelewa zaidi.
“Kituo chetu
kimekuwa kikitoa mafunzo kwa makundi mbali mbali, lakini na wanachama wa vyama
vya wafanyakazi nao tukaona umuhimu wa kukutanao nao”,alifafanua.
Mratibu wa Kituo
cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, ZLSC Fatma Khamis Hemed,
alisema kituo kimekuwa kikihakikisha kila kundi ndani ya jamii, linapata
uwelewa wa masuala ya kisheria, ili wafanye kazi zao kwa ufanisi.
Wakichangia
mada hizo, washiriki hao walisema bado vyama vya wafanyakazi havijatekeleza
wajibu wake ipasavyo kwa wananchama wake, ikiwemo kuwaelimisha.
Makame
Suleiman alisema bado vyama hivyo vinahitaji ushawishi wa hali ya juu, ili kwa
wale ambao hawajajiunga waone umuhimu wake na faida.
Nae Marzuku
Khamis Sharif, alisema lazima hata kwa wananchama wenyewe waone umuhimu wa
kujisomea sheria mbali mbali kwa faida yao.
Katika
mafunzo hayo mada sita zilijadiliwa ikiwa ni pamoja na ufafanuzi wa sheria ya
mahusiano kazini no 1 ya mwaka 2005, sheria ya mfuko wa hifadhi ya jamii ZSSF
no 2 ya mwaka 2005, sheria ya fidia, sheria ya afya na usalama kazini no 8 ya
mwaka 2005 na sheria ya uajiri no 11 ya mwaka 2005.
No comments:
Post a Comment