Na.Haji Nassor. Pemba.
WAZAZI na walezi wenye watoto wao
skuli ya sekondari ya Mauwani Kiwani wilaya ya Mkoani Pemba, walioweka kambi
kwa jili ya matayarisho ya mitihani, wametolewa hofu na uongozi wa skuli hiyo,
na kusema lengo ni kuongeza ufaulu na sio vyenginevyo.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi skulini hapo, Kaimu Mwalimu Mkuu wa skuli hiyo
Mussa Mohamed Abass, alisema wazazi waondowe wasiwasi juu ya kambi hiyo, kwani
uongozi wa skuli, una lengo zuri na sio vyengine kama baadhi ya watu
wanavyofikiria.
Alisema,
anachokiomba kwa wazazi na walezi hao, ni kuendelea kushirikiana na uongozi wa
skuli hiyo na kamati yake, ikiwa ni pamoja na kufikisha michango yao
waliokubaliana kwa wakati.
Kaimu Mwalimu
Mkuu huyo, alisema baada ya kumaliza kikao na wazazi hao, na kukubaliana kuweka
kambi, sasa wasiwe tayari kusikiliza maneno ya nje yasio kuwa na hoja, na
badala yake wawaamini juu hilo.
“Wazazi
wasikubali kupotoshwa juu ya uwepo wa kambi hii, ambayo sio mara ya kwanza, na
badala yake wao waendelee kutoa michango na hata wakati mwengine watutembelea
kutushauri, kutukumbusha na kutupa nguvu”,alifafanua Mwalimu mkuu huyo.
Katika hatua
nyengine Kaimu huyo, aliwataka wanafunzi hao wanaojitayarisha na mitihani ya
taifa, kufahamu malengo ya wao kuwepo kwenye kambi hiyo, ambayo hasa
inawategenezea mazingira yao mema ya baadae.
“Niwatake
wananfunzi waelewa kuwa, wazazi na walezi wanatumia nguvu na fedha nyingi
kuidumisha kambi hiyo, sasa wasikubali kucheza cheza, maana mitihani
imekaribia, na hata waalimu wenyewe wa baadhi ya masomo ya sayansi hatuna”, alifafanua.
Baadhi ya
wanafunzi wasiopenda majina yao yachapishwe, walisema kambi hiyo ni muhimu na
hasa kama yengeanza tokea mwanzoni mwa mwaka huu wa mitihani ya taifa.
Walisema,
linalohitaji kwa wizara husika ni kuhakikisha inawapatia waalimu wa masomo ya
sayansi, ambapo kwa sasa mwalimu wao tegemeo anadaharura ya kibinadamu.
Hata hivyo
wanafunzi hao wa madarasa ya kumi na kumi na mbili, wameahidi kuongeza idadi ya
ufuulu, ikilinganishwa na miaka mengine, hasa kwa moyo na ari walionao wa
kusoma kwa ushindani.
Skuli hiyo
ya Mauwani iliopo Kiwani wilaya ya Mkoani, ambayo ilioasisiwa mwaka 2013, kwa
mwaka huo ilitokezea ya mwisho kwa Zanzibar kwenye mitihani ya darasa la kumi
(FII).
Ingawa mwaka
2015 ilishika nafasi ya pili kwa Zanzibar kwa kupasisisha wanafunzi wote
waliokubali kukaa kambini, ambapo kwa mwaka huo walipata wanafunzi 19 waliokosa
vyeti wa darasa la kumi na mbili na mwaka 2016 walipunguza na kuwa na wanafunzi
wanne pekee.
Wilaya ya
Mkoani kwa sasa imeanzisha utaratibu wa kambi nne kuu za pamoja ikiwa ni
Kengeja ufundi, Maendeleo Mngwachani, Mauwani na skuli ya Juma Khamis Pindua,
kwa kuungana skuli tano tano na kuwatumia vijana waliomaliza, kuendesha kambi
hizo na waalimu wengine.
No comments:
Post a Comment