Na.Haji Nassor. Pemba.
WANANCHI wanayoyatunza mashamba ya mikarafuu ya serikali, wamependekeza kuwepo
kwa utaratibu wa kuyafanyia tathimini mashamba hayo kila msimu wa uvunaji, na
kisha kuwaelezwa wao, iwapo wanauwezo wa kuyakodi, kabla ya kuitisha minda ya
hadhara kama ilivyo sasa.
Walisema
kuitisha minada hiyo, huwa ni kikwazo kwao kutokana na ukosefu wa fedha za
kukodia mashamba hayo, ambapo kama wakiyafanyai tathimini na kisha kukodisha
kwa bei isiokuwa ya mnada, wanaweza kuyamudu.
Wakizungumza
na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati taifauti, wananchi hao wanaoyatunza
mashamba hayo walisema, lazima kwa serikali iwape kipaumbele cha pekee kwenye
kuyakodi mashamba na sio kupitia minada ya hadhara kama ilivyo sasa.
Walieleza
kuwa, wengi wao wanaoyatunza mashamba hayo, ni wanyonge kifedha na hutumia
fedha nyingi kwa kuyafanyia usafi na wengine kupanda mikarafuu mipya, hivyo
lazima kuwe na fungu la huruma, wakati wa azoezi la uvunaji unapofika.
Mmoja kati wananchi
hao anaelitunza shamba lililokuwa la Suleiman Riyami lililopo shehia ya Chonga,
Kombo Abdalla Kombo, alisema yeye amepanda mikarafuu mipya 100 kwenye shamba
hilo, ambalo amekabidhiwa zaidi ya miaka 15 sasa.
Kombo,
alieleza kuwa pamoja na kupanda mikarafuu hiyo, pia ametumia shilingi 600,000
kulifanyia usafi shamba hilo lenye mikarafuu mikongwe isiozidi 80.
“Mimi
nimetumia gharama kwanza kulitunza, pia kupanda mengine na nimeweka watu hapa
shamba walilinde, sasa ukiniambia nitoe shilingi milioni 18.1 ili nilikodi kama
mnada ulivyofika ni kunionea”,alifafanua.
Nae Is-mail
Haji Chuma wa Mizingani alisema kwa vile mashamba hayo, serikali ilikaa kwa
muda mrefu bila ya kuyafuatilia, lazima wawaangalie kwa jicho la huruma hasa
kufuatia msimu huu kuwa mkubwa.
“Sio vyema
sisi tunaoyatunza mashamba haya, kutuunganisha kwenye minada wa jumla jumla, ingependeza
kwanza yakafanyia tathimini na wizara husika na kisha tukagepewa bei na
tukishindwa ikiitishwa minada”,alishauri.
Kwa upande
wake Mmanga Makame Mmanga wa Wete, alisema kinyume chake cha kuwaweka kwenye minada,
inaweza kusababisha manun’guniko kwao na hatimae mashamba hayo, kukosa
washughulikiaji hapoa baadae.
Said Juma
Ali akizungumza kwa niaba ya Afisa Mdhamini wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo
na Uvuvi, alisema taratibu zinataka mashamba hayo kabla ya kukodishwa kuitishwa
mnada wa hadhara na kipaumbele kwa bei
itakayofikiwa, huulizwa anaelitunza shamba na sio vyenginevyo.
Afisa
Mdhamini huyo alisema, wanaoyatunza mashamba hayo iwe wamekubali kuyakodi wenyewe
kwenye mnada huo wa hadhara au yamekodiwa na mtu mwengine, hupewa asilimi
40 ya bei iliofikiwa.
“Bei
inayofikiwa kwenye mnada wa hadhara iwe anaelitunza kakubali yeye kulikodi au
mtu mwengine, asilimia yake 40 kama kifuta jasho iko pale pale, lakini sio
kuyakodisha siri siri”,alifafanua.
Wakuu wa
wilaya za Mkoani na Chake chake wakizungumza kwa nyakati tofauti, walisema
serikali haifanyia zoezi hilo kwa kumuonea mtu, bali ni kuhakikisha mali yale
haishii kwenye mikono ya wachache.
“Zipo eka
tatu tatu ambazo zilitolewa na rais wa kwanza wa Zanzibar au zile hati
zilizotolewa na rais Aboud Jumbe Mwinyi, kwa walionazo, wala zoezi hili
haliwagusi, lakini hati nyengine kwenye eka tatu haziotambuliki”,alisema Mkuu
wa wilaya ya Mkoani Hemed Suleiman.
Nae Mkuu wa
wilaya ya Chakechake Salama Mbarouk Khatib, alisema anaamini zoezi hilo,
linaweza kuyaibua mashamba kadhaa ya serikali, yaliokuwa mikononi mwa wananchi
kinyume na sheria.
Wakati zoezi
la ukodishaji wa mashamba ya mikarafuu ya serikali ukiendelea, tayari zaidi ya
mashamba 580 yameshagundulika, ambayo mengi yao yalikuwa mikononi mwa wananchi
kinyume na tataribu, huku wilaya ya Mkoani ikigundua zaidi ya 80 pekee.
No comments:
Post a Comment